Osaka Raha, Bukoba to Dar siyo gari la kupanda

Maisha pesa

JF-Expert Member
Nov 6, 2015
681
630
Wasalaam wanaJF kama ilivyo kawaida huwa tunapeana taarifa na habari mbalimbali zenye lengo la kujenga. Jana nilisafiri kutoka Bukoba kuja Dar na nikapanda gari la Osaka Raha niliyoyashuhudia ndiyo yamenisukuma kuleta uzi hapa.

Kiukweli ni gari mpya wala haina tatizo lolote la kiufundi au kwa lugha nyingine niseme gari haijachakaa wala haliharibiki hovyo njiani mwendo wake wa kawaida tu hamna shida.

Tatizo linakuja kwenye tabia za madereva na wafanyakazi wa hilo gari kwanza hawana ustaarabu ukishakata tiketi basi unaonekana huna maana tena wana lugha chafu kama makonda wa daladala.

Shughuli imeanza asubuhi wakati wa abiria kupanda wanalipisha mizigo kama hawana akili nzuri mzigo wako ukizidi 20kg basi wanachaji elfu moja kwa kila kilo iliyozidi na wala hawana punguzo basi abiria kakata tiketi 60,000/= analipishwa na mzigo elfu20, 15, 30. Kibaya zaidi hawatoi risiti ya hizo hela za mizigo. Mimi niliwakomalia nijue kwanza hiyo rate ya 1,000/= kwa kila kilo imepangwa na nani? Na pili nikilipa nipewe risiti lakini waligoma almanusura niachwe stendi huku nikipewa matusi ya kila aina na kuambiwa nitarudishiwa nauli ofisini wakati gari limeshaondoka nilisaidiwa na askari aliyewaamuru kama wananiacha basi wanirudishie nauli yangu kabla hawajaondoka nipande gari nyingine. Hapo wakaona pagumu kurudisha nauli ikabidi wanipakie tu kumbe walitaka wanitapeli ionekane nimechelewa gari imeniacha.

Baada ya sereka hiyo safari ikaanza kisanga kingine kikaja kwenye kuchimba dawa duh hawa jamaa ukizubaa wanakuacha na hawajali watu wanalikimbilia gari wakati linaondoka. Tumepiga mwendo kutoka Kahama hadi Singida 302km masaa matano bila kuchimba dawa wakati magari mengine tunaona wanachimba dawa sisi ni mwendo tu hadi abiria tukaomba watusaidie lakini wapi wanajidai eti wana haraka wao wakipata kinafasi kidogo cha kupakia abiria wanaenda kuchimba dawa wanatuacha sisi abiria.

Mziki ukaja pale mtoto alipolilia kujisaidia wakamshusha halafu wakampandisha kabla hajajisaidia eti wana haraka mwishoe dogo akaaharisha kwenye gari na harufu ikasambaa gari zima lakini hawakujali kama abiria tunapata shida wakaendelea na safari hadi kelele za abiria zilivyozidi ndo wakasimamisha kwa kutupa dk5 tu almanusura tuwaache baadhi ya abiria. Aisee sipandi tena hili gari.
 
k
Wasalaam wanaJF kama ilivyo kawaida huwa tunapeana taarifa na habari mbalimbali zenye lengo la kujenga. Jana nilisafiri kutoka Bukoba kuja Dar na nikapanda gari la Osaka Raha niliyoyashuhudia ndiyo yamenisukuma kuleta uzi hapa.

Kiukweli ni gari mpya wala haina tatizo lolote la kiufundi au kwa lugha nyingine niseme gari haijachakaa wala haliharibiki hovyo njiani mwendo wake wa kawaida tu hamna shida.

Tatizo linakuja kwenye tabia za madereva na wafanyakazi wa hilo gari kwanza hawana ustaarabu ukishakata tiketi basi unaonekana huna maana tena wana lugha chafu kama makonda wa daladala.

Shughuli imeanza asubuhi wakati wa abiria kupanda wanalipisha mizigo kama hawana akili nzuri mzigo wako ukizidi 20kg basi wanachaji elfu moja kwa kila kilo iliyozidi na wala hawana punguzo basi abiria kakata tiketi 60,000/= analipishwa na mzigo elfu20, 15, 30. Kibaya zaidi hawatoi risiti ya hizo hela za mizigo. Mimi niliwakomalia nijue kwanza hiyo rate ya 1,000/= kwa kila kilo imepangwa na nani? Na pili nikilipa nipewe risiti lakini waligoma almanusura niachwe stendi huku nikipewa matusi ya kila aina na kuambiwa nitarudishiwa nauli ofisini wakati gari limeshaondoka nilisaidiwa na askari aliyewaamuru kama wananiacha basi wanirudishie nauli yangu kabla hawajaondoka nipande gari nyingine. Hapo wakaona pagumu kurudisha nauli ikabidi wanipakie tu kumbe walitaka wanitapeli ionekane nimechelewa gari imeniacha.

Baada ya sereka hiyo safari ikaanza kisanga kingine kikaja kwenye kuchimba dawa duh hawa jamaa ukizubaa wanakuacha na hawajali watu wanalikimbilia gari wakati linaondoka. Tumepiga mwendo kutoka Kahama hadi Singida 302km masaa matano bila kuchimba dawa wakati magari mengine tunaona wanachimba dawa sisi ni mwendo tu hadi abiria tukaomba watusaidie lakini wapi wanajidai eti wana haraka wao wakipata kinafasi kidogo cha kupakia abiria wanaenda kuchimba dawa wanatuacha sisi abiria.

Mziki ukaja pale mtoto alipolilia kujisaidia wakamshusha halafu wakampandisha kabla hajajisaidia eti wana haraka mwishoe dogo akaaharisha kwenye gari na harufu ikasambaa gari zima lakini hawakujali kama abiria tunapata shida wakaendelea na safari hadi kelele za abiria zilivyozidi ndo wakasimamisha kwa kutupa dk5 tu almanusura tuwaache baadhi ya abiria. Aisee sipandi tena hili gari.



sie watanzania ni watu wapole sana mwarabu angeshatoa jambia
 
Usinamizi wa viongozi barabarani ni mbovu sana mkuu,hawafikirii kuwa ile ni long safari?,pole sana mkuu
 
Mngekunya basi zima humo humo ndani ya basi lao, wangeipata fresh.

By the way, Sumatra walikataza watu kusimamishwa porini kuchimba dawa, wakisimama wanafanya kosa.
Unataka kusema kahama to singapoo ninpori tuuh.. !
 
Kwani hao wafanyakazi ni wangapi ?na nyinyi abiria ni wangapi mpaka mnashindwa kuwapa kichapo ?
 
Watu karibia 60......mlikubalije kunyanyaswa hivyo na watu 4/5.....?.......mlishindwa kuwazaba vibao.....?.......
Watanzania bado tuna asili ya woga mpaka maji yafike shingoni ndo tunareact
 
Mngekunya basi zima humo humo ndani ya basi lao, wangeipata fresh.

By the way, Sumatra walikataza watu kusimamishwa porini kuchimba dawa, wakisimama wanafanya kosa.
Sehemu za kusimama ni nyingi siyo lazima porini kuna sehemu tu za kulipia ata kwenye masheli wangesimama tu
 
Wasalaam wanaJF kama ilivyo kawaida huwa tunapeana taarifa na habari mbalimbali zenye lengo la kujenga. Jana nilisafiri kutoka Bukoba kuja Dar na nikapanda gari la Osaka Raha niliyoyashuhudia ndiyo yamenisukuma kuleta uzi hapa.

Kiukweli ni gari mpya wala haina tatizo lolote la kiufundi au kwa lugha nyingine niseme gari haijachakaa wala haliharibiki hovyo njiani mwendo wake wa kawaida tu hamna shida.

Tatizo linakuja kwenye tabia za madereva na wafanyakazi wa hilo gari kwanza hawana ustaarabu ukishakata tiketi basi unaonekana huna maana tena wana lugha chafu kama makonda wa daladala.

Shughuli imeanza asubuhi wakati wa abiria kupanda wanalipisha mizigo kama hawana akili nzuri mzigo wako ukizidi 20kg basi wanachaji elfu moja kwa kila kilo iliyozidi na wala hawana punguzo basi abiria kakata tiketi 60,000/= analipishwa na mzigo elfu20, 15, 30. Kibaya zaidi hawatoi risiti ya hizo hela za mizigo. Mimi niliwakomalia nijue kwanza hiyo rate ya 1,000/= kwa kila kilo imepangwa na nani? Na pili nikilipa nipewe risiti lakini waligoma almanusura niachwe stendi huku nikipewa matusi ya kila aina na kuambiwa nitarudishiwa nauli ofisini wakati gari limeshaondoka nilisaidiwa na askari aliyewaamuru kama wananiacha basi wanirudishie nauli yangu kabla hawajaondoka nipande gari nyingine. Hapo wakaona pagumu kurudisha nauli ikabidi wanipakie tu kumbe walitaka wanitapeli ionekane nimechelewa gari imeniacha.

Baada ya sereka hiyo safari ikaanza kisanga kingine kikaja kwenye kuchimba dawa duh hawa jamaa ukizubaa wanakuacha na hawajali watu wanalikimbilia gari wakati linaondoka. Tumepiga mwendo kutoka Kahama hadi Singida 302km masaa matano bila kuchimba dawa wakati magari mengine tunaona wanachimba dawa sisi ni mwendo tu hadi abiria tukaomba watusaidie lakini wapi wanajidai eti wana haraka wao wakipata kinafasi kidogo cha kupakia abiria wanaenda kuchimba dawa wanatuacha sisi abiria.

Mziki ukaja pale mtoto alipolilia kujisaidia wakamshusha halafu wakampandisha kabla hajajisaidia eti wana haraka mwishoe dogo akaaharisha kwenye gari na harufu ikasambaa gari zima lakini hawakujali kama abiria tunapata shida wakaendelea na safari hadi kelele za abiria zilivyozidi ndo wakasimamisha kwa kutupa dk5 tu almanusura tuwaache baadhi ya abiria. Aisee sipandi tena hili gari.

Hapo kwenye mizigo ni sawa hawajakuonea coz seria ni kilo 20 free.
Ila hapo kwenye kuchimba dawa waliwaomea sana sizani kama toka mtoke kahama mpaka singida kama hakuna sehemu mlikuta au mlisimamishwa na trafic maana najua sehumu ni nyingi sana lazima msimamishwe na angeeleza hizo shida na hata singida wakati wa ukaguzi mngeleza hayo matatizo na mngeweza saidiwa.
Nilishapanda hilo basi tokea singida sikupata shida yoyote ile. Pia ndani ya mabasi kuna namba za sumatra na namba za polisi kwanini hamkupiga hizo.

Mda mwingine badala ya kulalamika inabidi kuwajibika.

All in all pole sana misukosuko ya safari
 
Kwa kweli wangewapasua vibofu vya haja ndogo maana kuna mji kidogo mingi kutoka Kahama -Singida mgeweza kujisaidia. Kuna kagongwa,Isaka,Tinde,Nzega,Nziba,Ibologelo, Igunga &Sheluwi kabla ya kupandisha Sekenke.
 
Last edited:
Kwa kweli wangewapasua vibovu vya haja ndogo maana kuna mji kidogo mingi kutoka Kahama -Singida mgeweza kujisaidia. Kuna kagongwa,Isaka,Tinde,Nzega,Nziba,Ibologelo, Igunga &Sheluwi kabla ya kupandisha Sekenke.


Fa Fe Fi Fo Fu
Vibofu..
 
I wish uzi ungekuja like "Abiria tulivyowachapa watumishi wa basi la Osaka" ... Kisha unaeleza hayo yaliyotokea kwenye ile mood ya "kiburi cha ushindi" afu unamalizia na kauli kama ; washenzi sana wale jamaa au 'pumbavu zao, watakuwa wamekoma'
 
Back
Top Bottom