Operation korosho na hasira za mkizi

Operation korosho na hasira za mkizi

Kuna mdau amesema serikali imejipanga tu kununua korosho za mkulima mtanzania tu
Kuna tatizo, hapo biashara ina kanuni zake, ukizikiuka undhoofisha mfumo mzima wa biashara
Hivi unawezaje kukutaa kuchukua (dhahabu) bidhaa kwa wingi na kwa bei nzuri ili ukiuza update faida kubwa?

Au selikari haijajipanga kupata faida??
 
Yes maana sot kwa korosho za Tandahimba na Newala ni kati ya 50-53 na Masasi ni kati ya 48-50 jambo ambalo siyo la kawaida kwenye first crop
Kweli kabisa, nilikuwepo katika ule mnada wa kwanza na kupita Tandahimba kwenye godown moja pale na hata Mtwara town
 
Kwa mjasiliamali wakweli hawezi kataa kuchukua korosho to nchi jirani kama anaongozwa na kanuni sahihi za biashashara, .

Labda mnunuzi( jiwe) ameisha give up kuwa hawrzi pata soko akauza kwa faida.

Huenda ananunua korosho kwa kukwepa aibu ya ubabe wake siyo kuingia sokoni kupata faida
 
Miaka yote ambayo zao la korosho limekuwa bei yake ipo juu na kuliingizia taifa mapato ya kujivunia sehemu kubwa ya korosho ilikuwa inavushwa mpaka kutoka msumbiji na kuingizwa Tanzania na inauzwa bila tatizo lolote,na ubora wake unalingana na zile za Tanzania yaani wastani wa sot 51-54 na nuts count zao ni kati ya 160-190.

Lakini leo hii wakubwa wa operation hii wanazizuia hizo korosho zisiingie tena nchini mwetu kwa kigezo kisicho julikana ni jambo la kushangaza sana na sijui wanamkomoa nani kati ya Tanzania na Mozambique?wilaya za Tandahimba na Newala zilikuwa zinanufaika na korosho nyingi kutoka Mozambique kwani tozo zote zilikuwa zinaingia kwenye wilaya hizo sasa hali imekuwa kinyume kabisa.kweli nimeamini ule usemi wa hasira za mkizi!!!
Kuruhusu korosho za Msumbiji kuingia nchini ni kuiongezea mzigo serikali. Mzigo wa kununua korosho zilizododa. Otherwise, washauri wale waliojiorodhesha kwa waziri mkuu, wakazifuate wao huku Msumbiji na kuzi export. Hakuna haja ya kuzileta Tanzania. Kwani huko Msumbiji hakuna bandari?
 
Hilo la faida nafikiri ashalifuta kichwani kama kweli alikuwa nalo maana mwezi February msimu wa korosho wa west Africa unaanza
Kwa mjasiliamali wakweli hawezi kataa kuchukua korosho to nchi jirani kama anaongozwa na kanuni sahihi za biashashara, .

Labda mnunuzi( jiwe) ameisha give up kuwa hawrzi pata soko akauza kwa faida.

Huenda ananunua korosho kwa kukwepa aibu ya ubabe wake siyo kuingia sokoni kupata faida
 
Una uhakika kulikwa na cartel katika korosho?
Cartel inafanyaje kazi ukiwa na bodi ya korosho inayotoa bei elekezi na korosho kuuzwa mnadani pia?
Achana na wafanyabiashara wa mazao mkuu, wana syndicate ya ajabu na wewe kama hujui wala huwezi shtukia lolote

Miaka yote kwenye minada sio ya korosho tu hata ya mazao mengine ya ku export wanunuzi ni hao hao. Hakuna player mwengine mpya anayeweza kuingia kwenye biashara hiyo bila consent yao na ukijaribu unaangushwa na kufilisika kibiashara kwa kufanyiwa umafia wa hali ya juu

Kwa ufupi watu hawa wana control kila kitu ikiwemo uzalishaji, masoko na bei na hakuna anayeweza kuwaingilia kirahisi, na hata serikali haiwezi na inalijua hilo. Lakini wakipambana wataweza kama ilivyo kwa ZSTC ya Zanzibar na karafuu yake

Kwanza entry qualifications za world market kwenye hii syndicate ziko katika namna ambayo hata kama ni serikali lazima ifanye kazi kwelikweli ili kuingia. Ndio maana serikali bado haijajua itafanya nini na hizo korosho inazozinunua ingawa itawezekana kuziuza kwa njia nyingine japo kwa hasara

Bodi ya korosho kwanini imevunjwa? Ni kwasababu wamekua outsmarted na hii cartel mkuu,jamaa wana akili nyingi na network kubwa sana. Sasa kuja kushtuka maskini kina Anna Abdallah kamailivyokua kwa kina Marehemu Kitwana Kondo hawana cha kufanya kwa sababu hawana wajualo
 
Naweza kukubaliana na wewe na kutokubaliana na wewe mkuu kwa kuwa dunia ya sasa ni sawa ipo uchi au wazi maana kama ni soko la zao lolote ukihitaji kuliona unaliona tu,ndiyo maana siku magu alipo kutana na wanunuzi pale mwl Nyerere alikiri bei halisi iliyopo duniani
Achana na wafanyabiashara wa mazao mkuu, wana syndicate ya ajabu na wewe kama hujui wala huwezi shtukia lolote

Miaka yote kwenye minada sio ya korosho tu hata ya mazao mengine ya ku export wanunuzi ni hao hao. Hakuna player mwengine mpya anayeweza kuingia kwenye biashara hiyo bila consent yao na ukijaribu unaangushwa na kufilisika kibiashara kwa kufanyiwa umafia wa hali ya juu

Kwa ufupi watu hawa wana control kila kitu ikiwemo uzalishaji, masoko na bei na hakuna anayeweza kuwaingilia kirahisi, na hata serikali haiwezi na inalijua hilo. Lakini wakipambana wataweza kama ilivyo kwa ZSTC ya Zanzibar na karafuu yake

Kwanza entry qualifications za world market kwenye hii syndicate ziko katika namna ambayo hata kama ni serikali lazima ifanye kazi kwelikweli ili kuingia. Ndio maana serikali bado haijajua itafanya nini na hizo korosho inazozinunua ingawa itawezekana kuziuza kwa njia nyingine japo kwa hasara

Bodi ya korosho kwanini imevunjwa? Ni kwasababu wamekua outsmarted na hii cartel mkuu,jamaa wana akili nyingi na network kubwa sana. Sasa kuja kushtuka maskini kina Anna Abdallah kamailivyokua kwa kina Marehemu Kitwana Kondo hawana cha kufanya kwa sababu hawana wajualo
 
Mkizi ni Tanzania maana sisi ndiyo tunakosa hayo mazao ambayo kimsingi miaka yote huwa tunayapata na kuyauza na kuingiza kodi kibao
(Mkizi) huruka juu kwa "hasira" akitoke ndani ya maji na kujikuta ametumbukia kwenye mtumbwi ikawa "furaha ya mvuvi"

Katika uzi wako umegusia hasira za mkizi lakini umeshindwa kabisaaaaa kuzioanisha kanakwamba zimeletaje furaha kwa mvuvi?

Tiririka na kuserereka tafadhali.
 
Mkuu tayari ashaanza kuwapigia magoti WB. Wewe subiri atawapigia magiti
Hiyo haina ubishi wowote lazima afanye hivyo ili korosho ziuzwe vinginevyo hayo maneno mengine ni siasa tu,kuziprocess korosho zaidi ya tani 200 000 siyo jambo la kuamka na kuamua tu zinahitaji matayarisho ya miaka
 
Tufanye umeshinda wewe kulingana na ulivyo elewa
(Mkizi) huruka juu kwa "hasira" akitoke ndani ya maji na kujikuta ametumbukia kwenye mtumbwi ikawa "furaha ya mvuvi"

Katika uzi wako umegusia hasira za mkizi lakini umeshindwa kabisaaaaa kuzioanisha kanakwamba zimeletaje furaha kwa mvuvi?

Tiririka na kuserereka tafadhali.
 
Back
Top Bottom