Operation Jicho la Paka na dakika za Mwisho(with Wolf rules )

Operation Jicho la Paka na dakika za Mwisho(with Wolf rules )

RIWAYA :: OPERATION JICHO LA PAKA
Na BAHATI MWAMBA
0758573660

Sauti ya mziki ilikuwa inaenda sawa na mapigo ya gitaa lake huku sauti yenye uzito kidogo ikiwa inapokewa na kinasa sauti kisha bugizi zilizokuwa zimefungwa kila kona ya ukumbi ule wa kisasa zikitoa mchamganyiko wa sauti na gitaa kwa namna ya kipekee kabisa na kufanya watu waliokuwa mle ndani kupiga makelele ya shangwe kwa utaalamu wa mwimbaji yule aliekuwa akiimba pikavu au waingereza walioharibu lugha za wenyewe wakiita Laivu.

Vidole vyake vilizidi kulitekenya gitaa kwa umaridadi sana huku sauti ikipaa sawa na mtekenyo ule

“Naililia Afrika,afrika yangu mpya,Afrika ilionipokonya mke mama wee
Mke mzuri kama darubi,akakimbilia dasalama,wajanja wakampa ramani ya Afrika..Afrika ooh Afrika eeh…”

Ilikuwa mistari kuntu kutoka kwa mwimbaji yule na hapo watu wakashindwa kujizuia wakapiga makeleke huku baadhi wakinyanyuka na kwenda kumtuza mwimbaji yule mahiri ndani ya Tembo bar.

Miongoni mwa walionyanyuka kumtuza alikuwa ni mbunge wa viti maalumu bi Kaisa,alicheza huku akitupia elfu kumikumi nyingi tu na punde akanyanyuka mmewe bwana Makoye aliekuwa waziri wa mambo ya ndani ndani ya serikali ya Zanzibar.

Umati ulishangilia kuwaona bibi na bwana wanavyoserebuka kwa utamu wa muziki wa gitaa lililokuwa linacharazwa kiufundi kabisa na bwana aliekuwa amefunika kichwa chake kwa kofia kubwa la pama hivyo kufanya asionekane usoni.

Ilikuwa ni kawaida kwa mwimbaji yule kuimba kwenye bar usiku na ni wachache waliofanikiwa kuiona sura yake na kwa kuwa watu walimpenda bila kujua hivyo wakajikuta wakimoachika jina la a night singer,yaani mwimba usiku.

Ndani ya moyo wa night singer si kuburudisha bali alikuwa anapitia maumivu makubwa hasa alipoona watu wanatumbua pesa wakati huko nje wengine wametopea kwenye umasikini na watu wamakufa kila uchwao kwa vifo visivyo na kichwa wala miguu.
***
Katikati ya usiku mnene a night singer akatangaza kusitisha muziki na hapo akasikia malalamo kutoka kwa watu waliokuwa wamekolea kwa vilevi huku wakicheza bila mpango maalumu.

Night singer akalalamika koo linamuuma hivyo karuhusu doka joka asugue sahani za mzungu kwenye santuli.

Akasimama na kuchukua begi la gitaa na kuihifadhi humo kisha akalitia mgongoni na kuanza kutoka nje na huko akaona watu wakiwa wanakokotana huku na huko akatabasamu ila lilikuwa tabasamu la maumivu.

Akaiendea pikipiki yake na kuiwasha akatia gia.

Kabla hajaachia kifyatua mwendo,akasikia sauti za watu Kama wanarumbana,akaizima tukutuku yake akatega sikio.

Mabishano yaliendelea baina ya watu wale waliokuwa karibu kabisa na gari la kisasa kabisa v8.

A night singer akavutika na maongezi yale akashuka kwenye pikipiki na kuambaa na kivuli cha miti hadi karibu na magari mengi yaliokuwa yamepaki karibu na v8 ile.

Akawasha kidekoda chake kilichokuwa kwenye mfuko wa mbele wa shati lake kisha akatulia.

Mabishano hayakudumu zaidi ya dakika tano,a night singer akaona kitu mbele ya watu wale.

Alikuwa ni mtu aliejiziba uso na bastola mkononi na alipowafikia watu wale akafyatua risasi kadhaa kumwendea mwanamke yule aliekuwa anabishana na mumewe.

Ajabu alioona mwimba usiku ni kuwa baada ya mauaji,muuaji akabaki anapiga soga na mume wa alieuliwa kisha mume akapiga simu polisi na sehemu nyingine akatoa maelezo na kisha akaanza kupiga mayowe ya kuomba msaada.

Yote yalionwa na night singer na wakati watu wakianza kujaa yeye akatoka alipo na kuelekea kwenye pikipiki yake kisha akaitia moto na kuondoka.
****

Vyombo vya habari Zanzibar havikuwa na habari njema ahsubuhi ile.

Kila habari ilikuwa ni kuhusu mauji ya bi Kaisa,mbunge wa viti maalumu aliekuwa na msimamo mkali kuhusu muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Mara nyingi hoja zake zilikuwa ni kusimamia kuto vunjwa kwa muungano ule.

Mji wa Jang’ombe ulikuwa si mji tena,watu walikuwa wanauwana kama filamu.

Lakini waliopata taabu ni watu wa bara,walifukuzwa na wengine kuchomewa nyumba zao,walipigwa wengine walibakwa na waandamanaji.
Ilikuwa Jang’ombe,sasa ikashika pemba nzima,kisha ikafuatia unguja na Mafia,kote hakukalika,watu walikufa kama mchezo wa kuigiza.
 
Riwaya:Op.Jicho la paka

Sehemu ya pili


Ilikuwa Jang’ombe,sasa ikashika pemba nzima,kisha ikafuatia unguja na Mafia,kote hakukalika,watu walikufa kama mchezo wa kuigiza.
Na hii ilikuwa ni habari mbaya kwa wapenda amani wa Afrika na dunia kiujumla.
*****
Night singer ahsubuhi hiyo ilimkuta akiwa kakaa kwenye tarakilishi yake na kazi aliokuwa akifanya ni kuhifadhi sauti aliorekodi usiku wa tukio la mauji ya mbunge wa viti maalumu Bi Kaisa.

Akaifunga tarakilishi yake na kisha akasimama na kujinyoosha viungo vya mwili wake kisha akaruhusu mwayo mkubwa umtoke.

Alipojirishisha na sayansi yake hiyo ya kujiondolea uchovu akayatwaa mavazi yake ya kiheshima,ilikuwa ni suti ya kisasa kabisa,kisha akakisogelea kioo chake kilichokuwa kimewekwa ukutani akajitizama.

Dakika tano baadae zilimkuta akiwa amesimama nje ya nyumba yake na alikuwa anatia ufunguo kwenye gari yake corola mbovumbovu,kisha akakamata barabara ambayo haikuwa mbali na nyumba yake kisha akaanza safari yake.

Gari yake ilisimama nje ya uzio wa geti la gereza Kuruso,kisha akashuka na kujitizama mbele ya kioo cha corola yake kilichokuwa kimepasuka katikati,kwa mbali akatabasamu baada ya kuiona sura yake ilivyobadilika na moyoni alikiri ya kuwa asingelikuwa ni yeye mwenyewe basi angejisahau.

Akataka kupiga hatua kuingia ndani ya lango kuu,lakini kabla hajapiga hatua zaidi akatokea askari magereza mwenye nembo maalumu ilioonesha yeye ni kutoka kikosi maalumu cha magereza au wenyewe huitwa makomando wa gereza.

“Mzee hujasikia tangazo huko ulikotoka!?”

“Sijasikia kiongozi!?”

“ok kifupi ni kuwa hamtakiwi kukanyaga hapa kwa wiki yote hii kwa raia wote wenye ndugu zao hapa na wageni wa aina yoyote”

“Kwanini kiongozi!”

Askari yule akaona kama anadhihakiwa kwa maswali mengi wakati mgeni huyo anajua kabisa nchi imechafuka na pengine kubwa hakujua ya kuwa kuna mfungwa katoroka,mfungwa hatari kuliko hatari yenyewe na ndio maana hadi kikosi maalumu cha askari magereza kipo pale.

Askari yule akaona anadhihakiwa akataka kujiandaa kumshambulia night singer ambae alikuwa amejibadilisha pakubwa sana .

Night singer aliona mienendo ya askari yule na hivyo akajipanga kumkabiri japo aliamini halikuwa jambo la busara kumkabiri eneo kama lile.

Kabla askari yule mwenye gadhabu za nyegere hajatimiza adhima yake,wote masikio yao yakanasa sauti ya king’ora cha tahadhari kutoka kwenye vipaza sauti vilivyokuwa vimefungww kila kona ya gereza lile.

Askari yule kama alieona Simba jike akakimbia kuelekea ndani ya lango la kuingilia mle ndani na hapo ndipo Night singer akapanda corola yake na kupotea eneo lile huku nyuma akiacha kimbembe ndani ya gereza lile.

Hakwenda mbali sana,akapaki pembeni mwa barabara na kujiunga na baadhi ya raia kushangaa moshi mkubwa uliokuwa ukitoka ndani ya gereza lile.

Penye wengi hapakosi jambo,Night singer akasikia wamama wakiteta kuhusu kinachoendelalea ndani ya gereza lile.

“Mwanaisha nasikia usiku wa kuamkia leo kuna mfungwa katoroka gerezani”

“ Na mimi nimesikia hivyo” alieitwa Mwanaisha akajibu lakini mwingine nae akadakia

“Jamani sasa kigereza kidogo hivi kwanini katoroka,si nasikia hapa wanaletwaga wanaomalizia kifungo chao?!”alimaliza kuongea na kutupia kiswali.

Night singer akatabasamu na kisha akainyoshea serikali mikono kwa kuwahadaa watu kuhusu gereza lile la Kuruso.

Kitu ambacho wakazi wa eneo lile hawakufahamu na hawajawahi kuambiwa kuhusu gereza lile ni kuwa,pale hawakufungwa wafungwa wa kawaida tu,kulikuwa na wafungwa wa maisha pale,wafungwa ambao serikali haitaki watu wajue sehemu walikofungwa,wafungwa wengi walikuwa ni makomamdo au majasusi walionekana wanatishia usalama wa nchi.
Gereza hili la Kuruso lilikuwa na sehemu mbili na aina mbili za wafungwa.

Sehemu ya kwanza ilikuwa ni juu ambako walifungwa wafungwa wanaomaliza kifungo chao hivi karibuni lakini sehemu ya pili ilikuwa ni sehemu ambayo ilikuwa imejengwa chini ya ardhi na huko ndiko walikofungwa watu wenye makosa ya ajabu au waliwekwa watu waliokuwa wanahatarisha usalama wa nchi.

Ajabu ni kuwa hata wafungwa wajuu hawakujua kama chini ya vyumba vyao kuna watu wanaishi huko na hata baadhi ya askari magereza hawakujua ya kama kuna sehemu ndio njia hasa ya kuingilia huko chini.

Night singer alikuwa ameenda pale kwa nia ya kuangalia usalama na mazingira yalivyokaa,kuna mtu akihitaji kukutana nae au kumuokoa na alijua ni miongoni mwa wafungwa walitangazwa ya kuwa ni adui wa taifa na wakaamua kumfungia pale.

Itaendelea
 
Asante kudo sasa story mbili uzi mmoja sio utatuchanganya ni wazo langu tu hilo
 
Asante kudo sasa story mbili uzi mmoja sio utatuchanganya ni wazo langu tu hilo
Hahaaa basi sawa maoni yakiwa mengi basi tutaenda na moja kwanza but kwa sasa ngoja niziweke zote afu mtaamua wenyewe tuendelee na ipi
 
Mkuu kila hadithi ungeiweka kwenye 'siredi' yake, hapa unatupa taabu sana...
 
Karibu tena katika uwanja mwingine wa maandiko ya Kudo na sasa ni Riwaya mbili ndani ya uzi mmoja

Riwaya😱peration jicho la paka
Riwaya😀akika za mwisho(with wolf rules)

Karibuni
Hii ni mupyaa?katag basi wakuu..
 
Karibu tena katika uwanja mwingine wa maandiko ya Kudo na sasa ni Riwaya mbili ndani ya uzi mmoja

Riwaya😱peration jicho la paka
Riwaya😀akika za mwisho(with wolf rules)

Karibuni
Hizi riwaya za JF hazifikagi mwisho, zote huishia njiani.
 
Op.Jicho la Paka


Sehemu ya tatu


Night singer alikuwa ameenda pale kwa nia ya kuangalia usalama na mazingira yalivyokaa,kuna mtu akihitaji kukutana nae au kumuokoa na alijua ni miongoni mwa wafungwa walitangazwa ya kuwa ni adui wa taifa na wakaamua kumfungia pale.

Night singer alitumia zaidi ya miaka mitatu kupeleleza kuhusu usiri wa gereza lile na mtu aliekuwa akimtafuta.

Hakutaka kuamini ya kuwa mtu anaeza kutoroka kienyeji ndani ya gereza lile kwa jinsi alivyolifahamu na kwakuwa alitaka kujua basi wakati askari yule alipokuwa akigeuka kuingia ndani alimrushia kifaa kidogo mithili ya punje ya mchanga lakini chenye uwezo wa kusafirisha mawimbi ya simu kuliko hata umaridadi wa simu.

Night singer kama watu walivyopenda kumuita akaiwasha corola yake na kuitia moto huku nyuma akiacha moshi ukiwa unawatesa watu.

Alitembeza gari yake hadi mitaa ya Jang’ombe sekondari na hapo kifaa kile alichokipachika kwenye mgongo wa askari magereza kikasikika tena ila safari hii kwa taarifa nzuri iliomfanya asimamishe gari na kusikiliza vyema.

“ C09 kavunja jungu na kutoroka…..mheshimiwa hata nashindwa kuelewa katokaje huko kuzimu….eeh ndio…tunajitahidi.”
Kisha akasikika akatoa amri ya kufanyika jambo flani na hapo Night singer akaamini aliekuwa akiongea ni kamishina wa magereza na aliekuwa akizungumziwa ni ni mtu huyo aliekuwa akimtafuta kwa udi na uvumba,lakini akabaki na swali moja tu,ni nani alikuwa anaongea na kamishina na pia ni vipi C09 ameweza kutoroka huko kuzimu?.

Akawasha gari yake na kutimka eneo lile na akaikamata barabara ya felixmoumie kisha akafanya mzunguko na kurudi kuikamata barabara ya Nyerere ndani na kisha akapiga breki mbele ya jengo refu kidogo na mbele lilipambwa na neno KILIMANI PLAZA,akataka kupaki pale ila akasita na akapitiliza mbele kidogo akaenda kupaki mbele ya maduka ya Fahud famas,kisha akashuka na kurudi nyuma kwa mguu.

Safari yake hiyo ikaishia kwenye duka za nguo zilizokuwa mle Plaza na akavuka milango kadhaa hadi alipofika kwenye mlango uliokuwa na maandishi ya kuwaka “MWAMVITA COLLECTION” akausukuma mlango na kuingia ndani.

Mapokezi kulikuwa na binti mrembo aliekuwa amejipamba kwa hijabu na alimlaki kwa bashasha la karibu mteja.

Baada ya salamu na utani wa hapa na pale Night singer akaamua kuuliza.

“binti wa kamishina Marwa yupo?”

Yule binti akafikiria kidogo kisha akajibu

“hapana katoka ahsubhi kaenda bandari kupokea mzigo”

“Naeza kupata namba ya baba yake ?!”

Aah unamaanisha kamishina Marwa?”

“Haswaa mrembo wangu..” Night singer alisema huku akiachia tabasamu chokozi na yule binti akainama chini ya droo na kutoka na simu yake kisha akamtajia zile namba bila kuhoji mzihitaji alizihitajia nini ,yaezekana ilikuwa ni jambo la kawaida watu kuja pale na kuomba kupewa namba za mheshimiwa yule.

Night singer akageuka na kuondoka eneo lile kwa kasi kidogo.
Dakika kumi baadae zilimkuta ndani ya uzio wa nyumba yake.

Kwa uharaka aliokuwa nao akaacha korola yake ikiunguruma muungurumo mbaya wa kuonesha imechoka kwa kilomita chache ilizotembea hakujali.

Alikimbilia tarakilishi yake kisha akafanya anavyojua na punde akayanasa mawasiliano ya kamishina na mtu aliekuwa anampa taarifa ya kukimbia kwa C09,akaifutilia namba ya aliekuwa anapewa taarifa ile alikuwa ni waziri wa mambo ya ndani Zanzibar bwana Makoye.

Night singer akaona kuna uhusika mkubwa sana wa waziri yule na matukio yanayotokea lakini kikubwa alijiuliza,Waziri huyo anahusika vipi na kutoroka kwa C09 maana taarifa ilivyokuwa inatolewa ni kama mtu anaempa taarifa mwanamipango mwenzie.

Hakutaka kufikiria sana akaona inatosha kwa siku hiyo,akatoka nje akazima corola yake kisha akarudi ndani na kuchukua gitaa lake na kuanza kupiga mazoezi maana usiku tena alikuwa anaenda kutumbuiza ndani ya bar nyingine ni kama hakujali machafuko yanayoendelea huko mitaani.

Itaendelea
 
Op.Jicho LA Paka

Sehemu ya nne


Hakutaka kufikiria sana akaona inatosha kwa siku hiyo,akatoka nje akazima corola yake kisha akarudi ndani na kuchukua gitaa lake na kuanza kupiga mazoezi maana usiku tena alikuwa anaenda kutumbuiza ndani ya bar nyingine ni kama hakujali machafuko yanayoendelea huko mitaani.

***

Alikuwa amesimama huku akiwa anatazama nje kupitia vioo vya dirisha pana vya jengo la Ikulu,huku simu yake ikiwa sikioni na ilikuwa imeshikwa kwa mkono wa kushoto.

Sio kama alikuwa anazungumza na simu,la aliekuwa amempigia alikuwa ameshakata simu dakika kadhaa zilizopita,na hadi wakati huo alikuwa bado anaipima taarifa aliopewa na ni vipi anaweza kuikabili na vipi raia watachukulia vipi taarifa hiyo.

Akawa bado anapima kisasi kinavyokuja kujijenga baina ya watu WA bara na Zanzibar,akaona madhara yatakayofanywa na watu wa bara baada ya ndugu zao kuuwawa visiwani.

Taratibu akageuka na kukutana na vijana wa cobra squad wakimtizama bila kusema neno.

Akaona vile hawa vijana waliochaguliwa kumlinda watakavyopata tabu ya kuhakikisha usalama wake hapo baadae.

Akanyanyua simu yake na punde akaja mmoja wa vijana wale na kuichukua kisha akaiweka mahali salama.

Rais akapiga hatua na kuongoza kuelekea ukumbi wa mikutano na nyuma walifuatia vijana sita na alipoingia ndani vijana watatu wakabaki nje ya mlango wa chumba kile.

Hakukaa kwenye viti vilivyokuwa mle ndani,ila akaagiza vijana wote watoke nje kisha akaomba aitiwe ADC(aide de camp) au mpambe kwa lugha rahisi na iliozoeleka na wengi.

Mpambe wa rais wa jamuhuri ya muungano aliitwa na akaacha shuguli zake zote alizokuwa anazifanya kwa muda huo na kwenda kusikia wito wa mnene wake.

Mpambe alishangaa kukuta chumba kizima akiwa amesimama rais pekee na kwa jinsi alivyomkuta alijua kabisa kutakuwa na jambo halipo sawa.

“Taarifa za huko nje unazo?” aliuliza rais bwana Mwenda Mpya.

“Nimesikia mheshimiwa” alijibu kanali Lucas Nsonde.

“Nimekuita hapa naomba uandae hotuba kwa kushirikiana na katibu,usimwache aandae peke yake”

“Sawa mheshimiwa”alijibu kanal Lucas Nsonde huku akipiga saluti na kutoka nje ambapo alipishana na vijana wa cobra squad wakiingia ndani na kuendelea na jukumu la ulinzi kwa rais wa nchi.

Rais Mwenda Mpya alikuwa anawaza kufanya jambo flani na hilo alijua kabisa linaeza kuwa ni salama ya maisha ya familia yake maana alijua ni wapi mstakabali wa nchi unaelekea na alijua kabisa lengo ni yeye na si hicho wanachopigia kelele wazanzibar na alikubali ya kuwa watanzania wamekubali kutumika.

Akaomba simu na akapewa akazitafuta namba za kiongozi wa cobra squad na kupiga.

“ndio mheshimiwa !”

“Nakuomba kwenye chumba cha mkutano sasa hivi”

“Nimefika mheshimiwa”alijibu kiongozi yule mwenye dhamana ya kuhakikisha usalama wa rais na familia yake muda wote ndani na nje ya ikulu.

Rais huwa anatabia moja ambayo hakujua ataiacha lini.

Alikuwa akimaliza kuongea na simu basi hataiondoa sikioni ndani ya dakika nzima.

Na ndicho kilichotokea hata wakati anamaliza kuagiza kiongozi wa walinzi wake akabaki akiwa ameacha mkono wa simu bila kuushusha kutoka sikioni na hapo akapata jambo jipya lililoibua hisia ambazo hakuwa na hakika nazo.

Wakati mkurugenzi wa kikosi cha ulinzi wa rais au Cobra squad kama walivyokiita akikata simu,Rais alisikia tena kuna mkato wa simu nyingine mbali na simu ya kiongozi aliempigia.

Akatabasamu kisha akaishusha chini na muda huo bwana Juma Twete akaingia ndani ya chumba cha mkutano na kupokea salamu ya kitiifu kutoka kwa vijana wake.

Kisha akasogea hadi alipo Rais na kumpa heshima kisha akakaa kimya kusikiliza wito.

“Kuna jambo moja naomba unisaidie japo lilikuwa nje ya utaratibu na ratiba za ofisi.”aliweka kituo bwana Mwenda Mpya Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kisha akaendelea baada ya kuona anasikilizwa.

“… najua wewe ndie unaeongoza jopo la vijana wanaolinda usalama wangu hivyo naomba uwapange vijana unaowaamini waende na familia yangu mapumzikoni nchini Uganda” alimaliza kusema rais na hapo bwana Juma Twetwe akasema

“Lakini mheshimiwa kuipeleka familia nje ya nchi bila nchi husika kuwa na taarifa si inaeza kuwa si…”hakumaliza kusema na rais akadakia

“Najua rais wa Uganda hana taarifa na ni singependa ajue au mtu yeyote tofauti na wewe ajue…”

“Lakini mheshimiwa.” Alitaka kusema kitu mkurugenzi yule wa cobra squad ila rais akaingilia

“Juma fanya ninavyokuomba na safari hiyo iwe leo na mtu asijue.”

“Sawa mheshimiwa”
Alijibu kisha akaanza kutoka ndani ya chumba kile na alipofika nje akasimama na kufikiria kuhusu maamuzi ya rais ya kupeleka familia yake nje ya nchi,maswali kadhaa yalipita kichwani pake lakini hakupata majibu yeye akabaki msikilizaji tu na mtekelezaji.

Itaendelea
 
Back
Top Bottom