Operation Jicho la Paka na dakika za Mwisho(with Wolf rules )

Operation Jicho la Paka na dakika za Mwisho(with Wolf rules )

Op.Jicho la Paka

Sehemu ya sita


Makomando wenzie walikuwa wapo makini kungojea amri kutoka kwake na kila mmoja alikuwa na ari na jambo walilokuwa wanataka kulifnya ndani ya kisiwa hicho usiku huo.

Luten kanali Mwinyi Kisoda aliwapa maagizo vijana wake waliounda kikosi cha 309 unit.

“Kila kitakachoonekana tofauti na lengo ni kuua na kuwakomboa mateka wote ndani ya ndege,kuna mateka zaidi ya ishirini na sita akiwamo rubani wa ndege ya AirZanzibar,na kwa mujibu wa taarifa zinasema mateka wote wamewekwa upande wa mashariki mwa ngome.” Alimaliza kuwapa maelekezo muhimu na kabla hajaendelea akawatazama wenzie waliokuwa kimya wakimsikiliza na walikuwa wamengojea amri yake tu ili vijana wasonge mbele.

“Koboko mtaelekea upande wa kusini na mtangojea amri kutoka kwetu endapo tutahitaji usaidizi na Luten Zaza utaongoza huko mimi na wengine saba tutaenda kufanya wokozi kwa kupitia mbele,idadi ya watekaji ni chini ya kumi na tano” alimaliza kusema na kuanza kuondoka huku vijana saba wakiwa wanamfuata nyuma na kikundi cha koboko kilichoongozwa na komando Luten Zaza nacho kilifuata uelekeo walioaelekezwa.

Ulikuwa ni mwendo wa kukimbia katikati ya msitu wa miti mifupi ndani ya kisiwa cha Kome.

Luten kanali Mwinyi Kisoda alikuwa mbele huku mwili wake uliojaa kimazoezi ukionekana kila radi ilipopiga na hivyo makomando wenzie walikuwa wakiona kiwiliwili chake vile kilikuwa kinakata giza usiku ule huku bunduki yake ikiwa mkononi tayari kwa lolote.

Ngome ya kikundi cha waasi wa LRA ilikuwa tulivu usiku huo na kutokana na mvua kuwa kubwa walinzi wa nje wengi waliamua kwenda kwenye mahema na kujihifadhi huku akili zao zikiwaza mabilioni ya fedha walioyahitaji kutoka kwa serikali ya Tanzania ili waweze kuwachia mateka zaidi ya Ishirini na tano wa timu ya mpira ya Zanzibar iliokuwa inaenda kushiriki michezo ya kirafiki nchini Uganda.

Kiongozi wa waasi wale bwana Mangazeni Nkunda ndie alikuwa anajua kitakachojiri usiku ule hivyo kila mara alikuwa anatazama saa yake ya mkononi na ilipofika majira ya saa tano na nusu usiku akachukua simu yake iliokuwa mezani akapiga pahali na kusikiliza upande wa pili kisha maongezi yakaendelea

“Chopa ipo upande gani…ok vikosi vingapi..ok..”kisha akakata simu na moja kwa moja akawageukia vijana wake aliowaamini na kuwambia “Kumekucha wapo hapa”hakungoja swali akachukua koti lake la baridi na kulivaa kisha akachukua bastola zake tatu na kuzisunda maeneo tofauti ya mwili wake kisha akachukua na mabomu mawili ya kutupa kwa mkono na kuyaweka mifukoni na haraka akaamuru vijana wake wapitie njia ya magaribi kutoka ndani ya ngome ile na kweli hiyo ndio ilikuwa salama yake maana vijana wa 309unit walikuwa upande wa mashariki na wengine kusini wakiikaribia ngome ile.

Nchini Tanzania usiku huo.

Waziri wa ulinzi na waziri wa mambo ya ndani wa Zanzibar walikuwa wapo ndani ya kikao usiku ule na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania bwana Mwenda Mpya.

“mheshimiwa C. D. F anangoja sahihi yako ili operation hii ikamilike na watu wetu wakombolewe”alisema waziri wa ulinzi

“Au kwa kuwa waliotekwa ni wazanzibar basi Rais hutaki kusaini operation hii..”alizungumza waziri wa mambo ya ndani wa Zanzibar aliekuwa ndie mwakilishi wa Rais wa Zanzibar ambae alikuwa nje ya nchi kikazi.

Rais alimtazama waziri wa mambo ya ndani wa Zanzibar kisha akamuuliza kiupole kama ilivyodesturi yake hasa anapokuwa amekwazika

“Wazanzibar sio watanzania?”

“ila mhe…” hakumaliza kuongea waziri yule na haraka Rais akaendelea

“bwana Makoye naona unataka kufanya haya mambo kwa mihemko na sasa unaleta ubara na visiwani,mimi ni Rais wa wote na kabla sijafanya maamuzi inatakiwa nijue madhara na faida ya uamzi huo na sijaona sababu ya kupeleka wokozi wakati watekaji wanafanya mazungumzo ya kumaliza hili jambo bila ya kumwaga damu na sioni sababu ya kuharakisha jambo hili,Makoye kumbuka wale ni waasi na hawana cha kupoteza.

Alizungumza Rais na Waziri wa ulinzi akatikisa kichwa kukubaliana na jambo lile huku Waziri wa mambo ya ndani akiwa amenuna kwa kuona mawazo yake hayajaafikiwa.

Rais aliagiza wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama waingie katika kikao kile na hapo CDF,IGP,na DG walijumuika katika kikao kile ndani ya ikulu.

Ni katika utoaji wa taarifa ndipo mkuu wa majeshi alipokutana na ripoti ya kumstua ambayo hakuwa ameona katika nyaraka zake huko mwanzo.

Kulikua na ripoti kutoka kwa Major jeneral Kambi Kibeyo aliekuwa na jukumu la kusimamia kambi zote upande wa Zanzibar.

Ripoti hiyo ilikuwa inatoa taarifa ya kuruhusiwa kikosi cha makomando cha 309 kilichokuwa kimekwenda Kome usiku huo kufanya wokozi.

Taarifa hiyo iliibua tafrani ndani ya Kikao kile huku Waziri wa mambo ya ndani Zanzibar akichelea moyoni.

Itaendelea
 
Kuu je unatunga mwenyewe au unatusaidia kutukopia toka Kwa mwingine? Ili nijiandae kuanza kusubiri endapo mtunzi akivurugwa nae anavuruga wasomaji wa JF
Kudo ndio mtunzi mwenyewe mkuu hakopi sehemu yoyote kwa hiyo ondoa shaka
 
Oparation Jicho la Paka

Sehemu ya saba
Na Bahati Mwamba

Taarifa hiyo iliibua tafrani ndani ya Kikao kile huku Waziri wa mambo ya ndani Zanzibar akichelea moyoni.
****

Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania bwana Mwenda Mpya alichanganyikiwa kwa taarifa ile na alibaki akiwatizama wakuu wa idara za usalama bila kutia neno.
CDF alikuwa haamini macho yake na pia aliona ni kama kudharauliwa kwa kiasi kikubwa na meja jeneral Kambi kibeyo mnadhimu wa jeshi Zanzibar.

“Inawezekanaje hii CDF!” Rais alijikuta akiuliza bila kutaka

“Sielewi mheshimiwa Rais”alijibu CDF.

“Huelewi nini?! Inamaana hadi kikosi cha 309 kinaondoka wewe hujui na kwanini usijue ikiwa wewe ndie final say kwenye Idara yako?!” alihoji kwa ukali Rais Mwenda Mpya.

Mkuu wa majeshi Jeneral Tasi Kinoga hakuwa na la kusema zaidi alijiinamia na kushindwa atoe maamuzi au jibu gani wakati huo.

Ndani ya kikao kile watu wote walikuwa kimya wakijaribu kuwaza hili na lile,wapo waliowaza vyema na wapo waliokuwa wanafurahia mitego yao juu ya Rais wao.

Jeneral Tasi kinoga akanyanyua uso wake na kumtazama Rais kisha akayahamishia macho yake kwa waziri wa mambo ya ndani Zanzibar ndugu makoye kisha akaamua kumuuliza

“Kikao chenu ndo kilimshinikiza Meja jenaral Kambi Kibeyo kuhusu kufanya Operation Jicho la Paka nyingine tena?”

Waziri wa ulinzi na wakuu wengine wa Idara za usalama walitumbua macho baada ya kusikia swali lile lakini kati ya wote ni Rais aliechanganyikiwa zaidi hasa baada ya kusikia jina waliloipa operation hiyo ya kuwakomboa wachezaji wale wa mpira.

“Kwanini mnajiamulia nyinyi wenyewe siku hizi!?”aliuliza Rais ambae muda huo jasho lilikuwa linamtoka mwili mzima.

Waziri wa mambo ya ndani Zanzibar alibabaika kujibu.

SIKU MOJA KABLA

“Haiwezekani tuendelee kungojea tamko la Rais ambae naonekana wazi hahitaji kuwakomboa Wachezaji wetu”aliunguruma kwa jaziba makamu wa Rais Zanzibar Mwinjuma Tariq.

“Lazima tufanye jambo ndani ya siku hizi mbili bila kungojea amri kutoka serikali kuu”alikazia hoja waziri wa mambo ya ndani Zanzibar bwana Makoye.

“Hebu tupe taarifa ya uchunguzi wa mwanzo kuhusu kisiwa cha Kome”aliuliza makamu wa Rais huku akimgeukia mkurugenzi wa usalama kanda ya visiwa vya Zanzibar ambae alikuwa amepewa jukumu la kuhakikisha taarifa zinapatikana haraka kabla hakujapambazuka.

“taarifa za mwanzo zinasema vijana waliondoka wenyewe ndani ya uwanja na ndani ya ndege hakukuwa na abiria mwingine yeyote tofauti na marubani wawili waliokuwa wanaiongoza ndege hiyo”Mkurugenzi mwandamizi wa Idara ya Usalama wa Taifa alizungumza kisha akatulia na kumeza mate kisha akaendelea

“…kwa makadirio inaonekana ndege hii ilitekwa wakati ikiwa angani lakini swali la msingi ambalo hatujapata jibu lake ni kuwa kama waliondoka peke yao nani alieiteka ndege ile ?! Mwanzo tulidhani yaezekana waasi walitumia ndege nyingine lakini picha za setilite na kumbukumbu za kuongoza ndege zinaonesha hakukua na ndege nyingine kwenye njia iliokuwa inapita Airzanzibar,isipokuwa ilibadilisha uelekeo wa Entebe na kuelekea Kisiwa cha Kome ndani ya dakika kumi tangu itoke katika uwanja wa ndege wa Mwanza,kinachotushangaza ni kuwa ndege ile haikutakiwa kutua mwanza ilitakiwa kuendelea na safari hadi Entebe.uongozi wa uwanja wa Mwanza wanadai ilitua kwa dharura baada ya rubani kuhisi kuna kunguru aliejigonga kwenye bawa moja la ndege na walipoikagua hawakukuta hitilafu wakairuhusu iondoke.
Baada ya kutekwa ilibidi tuwasiliane na majasusi wetu walioko kule Uganda wametupa ramani nzima ya kisiwa kile na hadi ilipo hiyo ngome ya waasi wa LRA na hata uelekeo wa simu inayopigwa na kiongozi wao Mangazeni Nkunda imesaidia sisi kupata picha za eneo la ngome yao”alimaliza kueleza mkurugenzi wa usalama wa Taifa Zanzibar.

Meja jeneral Kambi Kibeyo alikuwa amekaa kimya muda wote akiwasikiliza mara akasikia akitajwa na makamu wa Rais Mwinjuma Tariq

“Meja inabidi uandae kikosi kizuri cha makomando na hadi kufikia kesho tujue hatima ya vijana wetu”

“Maagizo hayatolewi na kutekelezwa vile unavyodhani mheshimwa makamu jeshi linautaratibu wake na mambo Kama haya lazima yaamuliwe na serikali kuu na Kama unavyojua rais wa jamhuri hajataka sisi kutumia nguvu anataka tutumie demokrasia ya maelewano na isimwagike damu.”alimaliza kufafanua vyema meja jeneral Kambi.

“Tatizo nyinyi wabara mnayadharau maamuzi yetu, hivi tutawangojea hadi lini hao unaowaita wa serikali kuu? Lazima tufanye maamuzi na sisi tuna jeshi na linajitosheleza”alizungumza kwa jaziba waziri Makoye.

“Lazima tufanye kitu meja na mimi nasaini faili hili lenye kukutaka uteuee kikosi cha nguvu kiwakomboe vijana ifikapo usiku wa kesho kinyume na hapo utakuwa unagomea maamuzi ya jamhuri”alimaliza kusema makamu wa rais huku akisaini faili la kuruhusu operation hiyo kufanyika na aligonga muhuri kisha akawapa wahudhuriaji wote wa kikao hicho wasaini.

Walisaini wote ila meja jeneral akastuka baada ya kuona jina la faili lile na operation ilivyokuwa imewekwa katika maandishi makubwa “OPERATION JICHO LA PAKA”alamu ya tahadhari ikalia kichwani pake na hapo akakumbuka miaka zaidi ya Tisa nyuma paliwahi kutumika jina hilo katika mpango fulani uliozaa taharuki kwenye nchi na sasa anakutana na jina Kama hilo akajua kuna namna ila hakuwa na budi kusaini kisha kwenda kutekeleza jambo hilo na kuacha faili lile lihifadhiwe kama classified.

Meja jeneral alipotoka kwenye kikao kile akaamua kumpigia simu Jeneral Tasi kinoga na kusema nae mambo machache tu

“Ya mwaka 97 yanajirudia tena ila kwa tofauti Jeneral,nchi inaserikali mbili bila serikali kuu kuwa na taarifa”alipomaliza kusema hakutaka kusikia mkuu wake atajibu nini yeye akaamua kukata simu na kisha akaanza safari ya kwenda kukipanga kikosi kazi kikosi namba 309 unit au Gost Recon Alpha.
*****

Ikulu usiku

“zuieni operation hiyo na vijana warudi huku mara moja”alizungumza rais

Haraka Jeneral akapiga simu kwenda kwa Meja jeneral lakini simu ikawa inaita tu bila kupokelewa na baada ya dakika mbili simu ya Jeneral ikaita na alipoishusha chini hakuwa na cha kusema mbele ya kikao kile na hata ulimi wake ukawa mzito akabaki kujisemea mwenyewe tu
“Haiwezekani hii..”
Maneno yale yalisikiwa na kila mtu ndani ya chumba kile cha mikutano na hakuna aliemsemesha kila mtu akabaki akimshangaa vile alivyozubaa na kupigwa na mshangao.

Lakini hatimae akaipata kauli

“Meja jeneral Kambi Kibeyo amejiua kwa sumu usiku huu”

Kila mtu hakuamini si rais tu hata IGP alishangaa DG alishangaa pia waziri wa ulinzi yeye alianza na kulia kabisa maana meja alikuwa ni kama kaka yake waliezoeana sana.

Rais akakuna kichwa na kumtazama waziri wa mambo ya ndani Zanzibar kisha hakusema neno akaomba kikao kiishe na kesho alimtaka CDF akutane nae wajadiri upya suala hilo lakini hawakujua kuchanganyikiwa kwao na kuahirisha kikao ilikuwa ni pigo jingine ndani ya idara ya jeshi la kujenga taifa na taifa kiujumla.

Hawakujua!!!

Itaendelea
 
Op.Jicho la paka

Na Bahati Mwamba

Sehemu ya nane




Rais akakuna kichwa na kumtazama waziri wa mambo ya ndani Zanzibar kisha hakusema neno akaomba kikao kiishe na kesho alimtaka CDF akutane nae wajadiri upya suala hilo lakini hawakujua kuchanganyikiwa kwao na kuahirisha kikao ilikuwa ni pigo jingine ndani ya idara ya jeshi la kujenga taifa na taifa kiujumla.

Hawakujua!!!

Katika kisiwa cha Kome tayari makomando walikuwa wamenza kukaribia kambi ya waasi wa Uganda huku Luteni kanali Mwinyi Kisoda akiwa mbele akikimbia huku nyuma kukiwa na vijana kama sita hivi waliokuwa wakifuata kila hatua aliopiga Luten kanali .

Walikuwa wametumia zaidi ya dakika kumi na tatu tangu walipotua na chopa.

Kwa umbali wa mita tisini waliweza kuona majengo ya kambi ya waasi kwa kutumia mawani waliokuwa wemevaa ili kuwarahisishia kuona kizani.

Luteni Mwinyi Kisoda akatoa ishara ya kukunja ngumi na kuipunga hewani hapo vijana wote walisimama huku wakitweta kwa mbio walizokimbia usiku huo

“Alfa 01 pass right Alfa 03 left….”luteni aliwagawa wawili wawili ili kuizunguka kambi ile na kila Alfa moja ilikuwa na komando wawili waliofiatana namba.

Makomando wote wakatawanyika akabaki Luteni peke yake amesimama

“Koboko nipe uelekeo wako”aliongea Luteni huku kidole kikiwa kimebana sikioni.

“Tupo hatua hamsini kutoka kwenye point”alijibu komando Koboko.

“Tunamzungukia mwali”alijibu luteni kanali Mwinyi Kisoda huku akianza kupiga hatua za taratibu kuelekea kwenye kibanda cha mlinzi aliekuwa amekaa akivuta sigara.

“Bravo Alfa”alijibu koboko.

Luteni Kanali Mwinyi Kisoda alichomoa kisu chake na kuanza kutambaa chini na alipobakiza hatua nne tu kutoka alipokuwa mlinzi yule akasimama gafla na kurusha kisu chake kikaenda kutua kifuani mwa mlinzi yule na na hakusubiri kelele imtoke akaruka juu Kama mruka viunzi na goti lake likatua kichwani mwa mlinzi yule ambae alikufa kwa shambulio lile la gafla huku akiacha moshi wa sigara aliokuwa akivuta ukipepea hewani bila kuvutwa na mapafu.

Luteni kanali Mwinyi Kisoda akatazama kushoto na kulia akaona kuko kimya bila kuwa na kelele ama mjongeo wa waasi wengine.

Jambo hilo likamtia shaka kidogo akatulia huku akijaribu kuangaza macho zaidi.

“Alfa 03left nasema hakuna mwali hata mmoja upande huu”sauti hiyo ikafika sikioni mwa Luteni Kanali na akajua kuna shida au basi hiyo itakuwa sio kambi halisi wanaliopaswa kuivamia

“Bravo Alfa be care Mwali anamachale”akajibu Luteni kanali.

Kisha akateremka kutoka kwenye kibanda kile na kuanza kunyata na kuelekea mbele huku akiwa hajasikia lolote kutoka kwa Alfa 01.

“Nahisi anakata viuno nyuma ya jabali”ilikuwa ni ripoti ya Alfa 01 na luteni Kanali Mwinyi Kisoda alielewa ya kuwa wanahisi kuna mtu anawataza.

“hameni kigodoro tumieni kamba ya kusini”alizungumza kwa mafumbo kuelekea kwa Alfa 01 ambae alielewa ya kuwa wanatakiwa kurudi nyuma kwa tahadhari na waache kusonga mbele.

Luteni kanali mwinyi kisoda alijipunguzia ulinzi kwa kutokutaka kuwapoteza vijana wake na aliheshimu mawazo yao hivyo alivyowaomba warudi nyuma alimaanisha waende kukutana na kikosi cha koboko wapange namna nyingine ya kukutana tena.

Luteni mwinyi kisoda aliona mtu mwingine akiwa amevaa koti la mvua akikojoa nyuma ya hema.

Haraka akaruka mruko unaotumiwa sana na makomando wawapo wanakimbia mlipuko wa bomu na kutua chini kama paka na aliposimama tayari mikono yake ilikuwa imeinasa shingo ya mtu yule na kuivunja.

Akatazama usalama alipojihakikishia yupo salama akalizunguka hema lile na kupata pahali pa kuingilia na kwa mwendo wa taratibu akanyata na kuzama ndani huku bunduki ikiwa tayari kwa lolote.

Ajabu hakukuwa na mtu licha ya kuona vitanda vikiwa vimetandikwa magodoro kumaanisha ni makazi ya kuhifadhi watu nyakati za usiku.

Mwinyi kisoda akiwa ameanza kuingiwa na mashaka na operation hiyo akatoka na kujaribu kuatazama kushoto na kulia huku akiamini kabisa wanachezewa mchezo na waasi wale mara kwa mbele yake akaona ishara maalumu kutoka kwa upande walikokuwa Alfa 03 na 04.

Akakimbia kikomando bila kutoa kishindo chini licha ya viatu vizito alivyokuwa amevaa ila kabla hajawafikia akasikia mlio wa kitu kikipita karibu na sikio lake na muda huohuo akashuhudia Alfa 03 akipiga kelele ya uchungu kisha akajibwaga chini na wakati Alfa 04 akijiuliza kulikoni akashangaa kichwa kikisambaratika na kmwenda chini bila walao kupiga kelele.

Luteni kanali Mwinyi kisoda akajitupa pembeni kwa kasi na kuamgukia viroba vya mchanga vilivyokuwa vimepangwa kiustadi huku kukiwa na waya au senyenge zilizomchoma mwilini,lakini hakujali akajiweka pembeni huku akijaribu kutazama upande alikohisi risasi imetokea lakini hakuona kitu.

“Sniper”akajisemea Mwinyi

Luteni kanali mwinyi Kisoda akataka kuwapa wenzie taarifa ila kabla hajabana sikio lake yeye ndie akapata taarifa tena

“we are in trouble Luteni”ilisikika sauti ambayo alijua kabisa ni kutoka kwa koboko.

Akarekebisha mawani yake akaanza kutambaa ili atoke ndani ya uzio wa kambi ile ikibidi afanye msaada kwa koboko na vijana wengine maana kwa uzoefu wa kazi hizo za kuokoa alijua tayari adui amewazidi ujanja hivyo mateka hawawezi kuwa eneo hilo hiyo itakuwa ni trap kwa lugha ya wenyewe.

“Luteni chopa imepigwa bomu we are in trouble sir”ilikuwani ni sauti ya rubani luteni Makame ambae alikuwa amepaki umbali wa kilomita mbili kutoka usawa wa kisiwa

Luteni kanali Mwinyi Kisoda akapagawa na alipojaribu kuwasiliana na upande wa Koboko aliishia kusikia miruzi sikioni kwake kumaanisha hawako na mawasilano tena

Luteni kanali Mwinyi Kisoda komando mzoefu alikuwa ndani ya matatizo katika uwanja wa Vita huku akiwa hajui adui yupo upande gani

Alichoka!!!!


Itaendelea
 
Back
Top Bottom