OPERATION GOTHIC SERPENT: Nguvu ya Itikadi, Imani na Ushujaa uliotukuka

Habibu B. Anga

JF-Expert Member
May 7, 2013
6,557
25,671
OPERATION GOTHIC SERPENT: NGUVU YA ITIKADI, IMANI NA USHUJAA ULIOTUKUKA


Sasa, unaweza kupata nakala za Kitabu changu cha "NYUMA YA ULIMWENGU WA SIRI NA UJASUSI".
kitabu kina kurasa 442 na ndani yake kuna makala 17.
Bei ya kitabu hiki ni Tsh 50,000/-

Pia waweza kupata kitabu changu cha "OPARESHENI ZA KIJASUSI ZILIZOFANIKIWA ZAIDI"
Kitabu hiki kina kurasa 214 na ndani yake nimechambua Oparesheni 6 tofauti.
Bei ya kitabu hiki ni Tsh 15,000/-

Wasiliana nami kwa namba 0759 181 457

Au bofya link hapa chini kunitumia ujumbe moja kwa moja whatsApp



images+%2816%29.jpeg


Tarehe fulani isiyojulikana mwaka 1993 - Sudan

"…ndugu zangu nyote katika imani, popote mlipo dunia. Wote tumeshuhudia udhaifu wa adui yetu. Wote tumeshuhudia kudhalilika kwa Marekani. Hili ni onyo, na huu ni ujumbe kwao. Kwamba tutawapiga tena, na tena na tena mpaka siku tutakapowafuta juu ya uso wa dunia au siku watakapo ongoka na kumuamini Mwenyezi Mungu. Huu ni ushindi kwetu sote na ishara ya kwamba adui yetu ni dhaifu. Nawataka wapigania imani wote, popote mlipo duniani, endeleeni kuwa na moyo mkuu. Adui yetu ni dhaifu, tumpige tena na tena na tena.."

- Sauti ya Osama Bin Laden katika moja ya rekodi zilizokuwa zinasambazwa kwa vikundi vya wapiganaji wenye msimamo mkali.




Nchini Marekani mwaka huo huo 1993

Wananchi wa Marekani walikua wamemka na habari ya kushtua. Vyombo vyote vya habari vilikuwa vimetawaliwa na habari juu ya kujiuzulu kwa Waziri wa Ulinzi wa Marekani Bw. Les Aspin.

Ilikuwa ni habari ya kushitusha kuzingatia kwamba nchi bado ilikuwa imefunikwa na giza kutokana na kifo cha idadi kubwa ya wanajeshi wake barani Afrika.

Wakati huo huo rais Bill Clinton alikuwa kwenye mvutano mkubwa na Umoja wa Mataifa juu ya muelekea wa hali ya amani nchini Somalia. Bill Clinton akitaka kuondoa wanajeshi wake haraka huku Umoja wa Mataifa wakitaka Marekani kusubiri kidogo ili kuongoza oparesheni ya kuondoa wanajeshi wengine wote wa UN waliopo nchini humo.



Mogadishu, Somalia - Pembe ya Afrika

Mamia ya wananchi walikuwa wameandamana. Si kwamba walikuwa wameandamana kupinga jambo fulani au kuhamasisha suala fulani, la hasha… maandamano haya yalikuwa ni ya kusheherekea. Walikuwa wanasheherekea huku wakiwa na 'trophy' mbele yao. Mwili wa binadamu aliyekufa ambao walikuwa wameufunga kamba wakiuburuza mitaani wakiwa wameuvua nguo zote mwili huo. Tofauti na muonekano wa waandamanaji hawa ambao wengi walikuwa wembamba na weusi na sura za kuchongoka, mwili huu waliokuwa wanauburuza ulikuwa ni wa mtu mweupe, mzungu. Ulikuwa ni mwili wa mwanajeshi wa Marekani, mmoja wa mwanajeshi wa weledi ambaye alikuwa kwenye chopa ya kivita ya 'Super Six Four'.


Ulimwengu wote ulikuwa kana kwamba umesimama na macho na masikio yote yalikuwa yameelekezwa nchini Somalia. Hakuna ambaye alikuwa anaamini kilichotokea. Hata Marekani wenyewe hawakutegemea kutokea kitu ambacho walikuwa wanakishuhudia.

Siku hii imeingia katika historia ya jeshi la Marekani kama moja ya siku chungu zaidi ambazo waliwahi kupitia. Ni siku ambayo kwa mara ya kwanza tangu kuisha kwa vita ya Vietnam, wanajeshi wa Marekani ndipo walipokabiliwa na mapigano mazito ya ana kwa ana na adui.

Lakini pia siku hii itufundisha kitu adhimu sana… kwamba hasira, imani na itikadi inauwezo wa kupambana dhidi ya weledi na ushujaa wa hali ya juu na ikashinda.

Screenshot_20180331-084944.jpeg


_46400881_10_somalia_afp.jpeg



Genesis

Katika miaka ya 1986 Rais wa Somalia wa kipindi hicho, Mohammed Siad Barre alipata ajali ya gari katikati ya mji wa Mogadishu. Ajali hii ilitokana na upepo mkali ulioambatana na mvua kubwa ambao ulisababisha gari ambayo ilikuwa inatumika kumsafirisha kwenda kujibamiza nyuma ya gari kubwa la usafiri wa umma. Rais Barre alipata majeraha makubwa sana, hasa hasa kichwani na pia alivunjika mbavu kadhaa. Ilibidi asafirishwe kwenda kutibiwa nchini Saudi Arabia kwa ajili ya matibabu.

Kwa miezi kadhaa ambayo Rais Barre alikuwa kwenye matibabu nchini Saudi Arabia, Jenerali Mohamed Ali Samatar ambaye alikuwa makamu wa Rais ilibidi akaimu nafasi yake na kuongoza nchi kama Rais wa Somalia.

Katika nyanja za siasa na masuala ya madaraka nchini humo kukaanza kuibuka minong'ono ya kutaka apatikane mrithi wa Urais wa Somalia. Barre alikuwa ameitawala Somalia kwa kipindi kirefu sana, umri wake ulikuwa umeenda mno na pia watu walikuwa na shaka na uimara wa afya yake.

Hata kipindi ambacho Rais Barre alitibiwa na kurejea kwenye afya njema na kurudi nyumbani Somalia, bado minong'ono iliendelea ya kutaka apatikane mrithi wake.
Ili kuonyesha kwamba yuko ngangari, Rais Barre aligombea tena Urais mwaka 1986, Mwezi desemba na kushinda ikimaakisha kwamba alipata muhula mwingine wa miaka saba wa kuendelea kuwa Rais wa somalia.

Lakini minong'ono haikuisha. Watu walitaka mrithi apatikane. Walitaka sura mpya kwenye uongozi wa nchi.

Na katika minong'ono hii kuliibuka majina mawili ambayo yalikuwa yanatajwa tajwa sana. Jina la kwanza lilikuwa la Jenerali Mohamed Ali Samatar, makamu wake wa Rais. Jina la pili lilikuwa la waziri wa Mambo ya Ndani Jenerali Ahmed Suleiman Abdille ambaye alikuwa ni mkwewe Rais Barre aliyemuoa moja ya binti yake.

Lakini kama ilivyo kwa madikteata wote duniani, kunapotokea tishio la madaraka yao kupokwa ni kana kwamba wanapata wehu. Rais Barre alianza kuwa dikteta katili akiwafunga na kuua wapinzani wake na wote ambao walikuwa wanaonekana kuwa na mwelekeo wa kumpinga.

Rais Barre woga wa madaraka kumponyoka ulioanda kwenye akili yake. Aliacha mpaka kusikiliza ushauri wa baraza lake la Mawaziri na badala yake aliongoza nchi kwa kuhusisha watu wachache sana ambao alikuwa anawaamini.

Kama ilivyo ada, watawala wakizidisha ukatili ndivyo navyo moto wa upinzani dhidi yao unavyozidi kukolea. Kwa hiyo Rais Barre sasa alikuwa anapingwa wazi wazi, ndani na nje ya Somalia.

Lakini kama tujuavyo kwamba nchi ya Somalia ina mgawanyiko mkubwa sana wa koo. Kwamba kuna uadui wa miaka mingi sana baina ya koo tofauti nchini humo. Rais Barre alianza kutumia mwanya huu wa uadui wa koo ili kuwaweka baadhi ya koo upande wake na wengine akiwapambanua kama koo adui kwa Taifa la Somalia.

Tunafahamu kwamba katika kipindi hiki 'Derg' ilikuwa na ushawishi mkubwa sana katika nchi zilizoko kwenye pembe ya Afrika. Derg ni kamati ya uongozi wa kijeshi ambao walisimamia kuondolewa madarakani kwa Mfalme Haile Selassie. Wao ndio waliokomesha utawala wa Kifalme nchini Ethiopia.

Japokuwa Rais Barre alikuwa anafanya uovu nchini kwake Somalia, lakini Mengistu Haile Mariam, kiongozi wa Derg huko Ethiopia alichukizwa mno. Ndipo hapa akaanza kuunga mkono vikundi vya wapiganaji wa kisomali ambao walikuwa wanataka Rais Barre aondoke madarakani.

Rais Barre hakuwa na simile… alitumua jeshi na silaha nzito kupambana na adui zake. Kufumba na kufumbua maeneo ya kaskazini mwa Somalia ambao ndiko hasa upinzani dhidi yake ulikuwa mkubwa, kuligeuka uwanja wa vita.

images+%2813%29.jpeg


images+%2814%29.jpeg


Hali hii ya nchi kuingia kwenye machafuko iliwahuzunisha sana watu wengi wazalendo na wenye ushawishi ndani ya Somalia akiwemo Rais wa kwanza wa nchi hiyo Aden Abdullah Osman Daar. Osman Daar aliongoza wanasiasa wengine wapatao mia moja wenye ushawishi mkubwa nchini humo kusaini waraka maalumu wenye kumtaka Rais Barre afanye suluhu na vikundi vya wapiganaji.

Kama wasemavyo kwamba sikio la kufa halisikii dawa. Rais Barre hakutaka kusikiliza rai hii ya wanasiasa wenzake wakongwe. Aliendeleza ukatili dhidi ya wote ambao walikuwa wanampinga na mapambano dhidi ya vikundi vya wapiganaji yalipamba moto.


Mapambano haya kati ya majeshi ya serikali na vikundi vya waasi yalidumu kwa miaka kadhaa.

Kadiri muda ulivyokuwa unaendelea ndivyo ambavyo majeshi ya Rais Barre yalikuwa yanazidiwa nguvu.
Mpaka kufikia katikati ya mwaka 1990 majeshi ya serikali yalikuwa yamezidiwa nguvu kwa kiasi kikubwa sana. Waasi walikuwa wametwaa sehemu kubwa ya vijiji na mitaa inayozunguka mji mkuu wa Mogadishu. Ndipo hapa ambapo watu walimbatiza jina la utani Rais Barre kwamba ni 'Meya wa Mogadishu', wakimanisha kwamba ni eneo la Mogadishu ndilo pekee ambalo Barre alikuwa na mamlaka nalo na maamuzi kutokana na vikundi vya waasi kutawala maeneo mengine yote ya nchi na Raias alikuwa hawezi hata kutoka nje ya mji huo.

Mwezi desemmba mwaka huo 1990 waasi wa USC (United Somali Congress) waliingia ndani ya mji wa Mogadishu wakiingozwa na Jenerali Mohamed Farah Aidid. Baada ya kuingia zilifuata wiki nne za mapigano makali kati ya USC na jeshi la rais Barre.
Mpaka kufikia mwezi January, wapiganaji wa USC walikuwa wamefanikiwa kuyashinda majeshi ya Rais Barre na hatimaye kumuondoa Barre mwenyewe madarakani.

Shida nyingine ikaibuka…

Nilieleza hapo nyuma kidogo kwamba Somalia wana mgawanyiko mkubwa na uadui wa koo. Kwa hiyo hata baada ya vikosi vya USC kumshinda Rais Barre na kumuondoa madarakani, koo nyingine zilikataa kumtambua Jenerali Farah Aidid kama kiongozi mpya wa Somalia. Matokeo yake vikundi hivi vya waasi vikaanza kupigana wenyewe kwa wenyewe. Kila kikundi kikipigania kutawala eneo fulani.

Kwa mfano, kikundi kingine cha waasi wa SNM walijiamulia kutangaza moja ya eneo la nchi ya Somalia kama nchi huru na kuibatiza jina jipya la Somaliland na kiongozi wao Abdirahman Ahmed Ali Tuur kuwa Rais wa nchi hiyo mpya. Mgogoro huu bado ungalipo mpaka leo hii wananchi wa eneo hilo wakitaka kutambulika eneo lao kama nchi huru.

Hata kikundi cha USC chenyewe nacho kiligawanyika baada ya makamanda wake wakuu Farah Aidid na Ali Mahdi Mohamed kutofautiana wakigombea madaraka na utawala wa mji wa Mogadishu.

Wapiganaji wa USC waliokuwa wanamuunga mkono Aidid na upande mwingine ambao walikuwa wanamuunga mkono Mahdi walianza kupigana wenyewe kwa wenyewe kugombea kutawala mji mkuu wa mogadishu.

Baada ya miezi kadhaa ya mapigano makali, mwaka 1992 ilibidi Aidid na Mahdi wakubaliane kuugawanya mji wa Mogadishu katika pande mbili… kusinu na kaskazini. Ukawekwa mpaka katikati ambao hakuna upande ulikuwa unaruhusiwa kuvuka.

Nchi ya Somalia ilikuwa imefikia kuwa kiroja cha namna hiyo. Ikiwa imegawanyika vipande vipande. Kila ukoo ukitawala eneo fulani. Kwa maneno mengine nchi haikuwa na serikali wala jeshi la pamoja bali kila ukoo ulkkuwa na lwake.


Ndipo hapa ambapo mwaka 1992 Baraza la Usalama la Umoja wa mataifa walipitisha resolution namba 733 kuunda UNOSOM I (United Nations Operation in Somali I) kwa lengo la kusaidia kupeleka misaada ya kiutu nchini Somalia.

Mwezi desemba tarehe 3 mwaka huo 1992 Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa walipitisha resolution nyingine namba 794 kuunda kikosi maalumu cha UNITAF (United Task Force) kwa ajili ya kulinda watoa huduma za kiutu na kulinda amani nchini Somalia.

Mwezi January mwaka 1993 vikosi hivi vya umoja wa mataifa kwa ajili ya kazi hii maalumu. Hakuna ambaye alikuwa na hofu au shaka juu ya utekelezaji wa oparesheni hii. Ilikuwa inategemewa kwenda sawia na murua kabisa na amani kurejea nchini Somalia.

Jambo moja la msingi ambalo hawakuliangalia au hawakuling'amua mwanzoni ni kwamba… hakuna weledi au ushujaa unaotosha kupambana na wananchi wenye hasira au imani. Na kama waswahili wasemavyo, "usiingile ugovi wa ndugu… wakipatana watakurarua wewe". Ndicho kinachofanana kabisa na aambacho kilikuwa kinaelekea kutokea nchini Somalia.

Ni kweli nchi ilikuwa imemegeka vipande vipande… na vita vilipiganwa hovyo baina ya ukoo na ukoo kugombea utawala wa maeneo. Lakini kitendo cha Umoja wa Mataifa kuingiza majeshi nchinu Somalia ilikuwa ni kana kwamba kuwapa koo hizo adui mmoja wa wote kupigana nae.

Lilikuwa ni suala la muda tu kabla ya vikosi vya Umoja wa Mataifa vikiongozwa na Marekani kugundua kosa kubwa ambalo walikuwa wamelifanya. Kosa ambalo lilikuja kupelekea kufanyika kwa moja oparesheni ya za kijeshi hatari zaidi kwenye historia… Operation Gothic Serpent. Operation ambayo imeacha vidonda kwa pande zote mbili… Marekani na Somalia. Na kuchangia Somalia kutotengamaa mpaka leo hii.


Tuwe pamoja kuichambua mpaka mwisho.


Jiunge na Group langu la WhatsApp kusoma simulizi mpya kila siku. Kuna malipo ya 5,000/- kwa mwezi. Wasiliana nami 0759 181 457




Habibu B. Anga 'The bold' - 0718 096 811
To Infinity and Beyond
 

Attachments

  • 2d9900357-2013-12-10t235424z_1_cbre9b91kt400_rtroptp_3_madoff.jpg
    2d9900357-2013-12-10t235424z_1_cbre9b91kt400_rtroptp_3_madoff.jpg
    33.8 KB · Views: 436
Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi @Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM @Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu The Certified DON SINYORI mij adden


bwii ONTARIO Kobe The Vein Mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya Sitaki ukuda Domhome Mpatanishi MKANDAHARI mtugani wa wapi huyo wealthier cluecell Toyota escudo mgumu2 troublemaker Linamo shedede kamtu33 SteveMollel ngushi Donald stewart Mshuza2 Glycel mnonje Ochuanilove SingleFather Santi DEOD 360 ngushi anatory antony ukhuty chris van chicha auxillius Goma Son Hubeb pes KING DUBU VILLAIN mwayena donbeny Aleppo JipuKubwa shoo61 BOMBAY John mungo Nyakageni bato Dogo 1 sufra chamlungu painscott wegman Bravo Engliash MOSELBAY wa stendi FaizaFoxy bigmind cadabraa Internal Kelvin mwalukas mnonje Kelvin X Somoche Wgr30 Miiku Poise Jabman kalamuyamwalimu BOMBAY the say juxhb witnessj Gide MK Mmanyema mgogoone Mnongane Mandingo koncho77 afsa ngaboru Paradoxer Heavy Metal KIMBURU 06 Raaj kichekoh ngumba njeche kikale DullahTza Goodluck Mshana julius Darcy Denis Kasekenya mashonga kitalembwa Khaleed Shaban middle east SirChief jiwe jeusi Mkambarani mansakankanmusa gambada ynwa ney kush[/USER
 
Shukrani sana mkuu.
Binafsi nakufuatilia sana kimya kimya, na nimepata mambo mengi sana.
Mungu akubariki mno.

Story ya Vipepeo Weusi Part 2:From Zurich with principles imeishia hewani, tunaomba utumalizie vipande vilivyo baki.
Maana hata kwenye web yako imeishia part 16 tu.

Kwa sasa bado nafuatilia tena kwa mara ya pili Black Wednesday maana kuna vitu imenifungua sana macho baada ya kuisoma kwa mara ya kwanza.

Kitabu kikitoka nitakuunga mkono.

Ubarikiwe mno.
 
Shukrani sana mkuu.
Binafsi nakufuatilia sana kimya kimya, na nimepata mambo mengi sana.
Mungu akubariki mno.

Story ya Vipepeo Weusi Part 2:From Zurich with principles imeishia hewani, tunaomba utumalizie vipande vilivyo baki.
Maana hata kwenye web yako imeishia part 16 tu.

Kwa sasa bado nafuatilia tena kwa mara ya pili Black Wednesday maana kuna vitu imenifungua sana macho baada ya kuisoma kwa mara ya kwanza.

Kitabu kikitoka nitakuunga mkono.

Ubarikiwe mno.
Pamoja sana chief...

Vipepeo Weusi Season 2 leo jioni kitaweka mwendeleza. Pamoja na mwendelezo wa TOH
 
Kuna muvi inaitwa somalia, hicho kipengele ulichosema wananchi walimburuza askari. kwenye hiyo muvi kipo.

Ahsanteh kwa darasa murua mkuu The Bold
 
Baada ya kutapeli watu Forex umeamua kurudi kwenye hadithi za uongo na kweli
 
Back
Top Bottom