Ongezeko la vijana kula ugoro

Ongezeko la vijana kula ugoro

Wazee mnatabu sana, kila starehe ambayo vijana wakifanya au wakihamia, kwenu ni nongwa.

Virobo, marufuku.

Shisha, marufuku.

Bar, mwisho saa 6.

Mirungi, marufuku.

Gongo, marufuku.

Kuberi, marufuku.

Malaya, marufuku.

Sasa mnataka wakataze mpaka ugoro. Acheni uchawi wenu. Au mnataka vijana waanze kuvaa sketi na blauzi??? Waacheni vijana wapunguze stress za ugumu wa maisha.
 
Nikiwa mdogo nilidhani ugoro unatumiwa na kina Bibi pekee, maana ndio tuliowaona wakitumia na kututuma tukawanunulie.

Siku hizi ni kila rika la kila jinsia lazima ukutane na wanaotumia ugoro.
 
Mtoa mada fata maisha Yako,kwani vijana wakila ugoro akaunti Yako inapungukiwa ela?au unakosa kula wewe na familia Yako?fuata mambo yanayokuhusu uishi miaka mingi na na kheri duniani,dunia imeumbwa na kila mtu tofauti ili maisha yabalance Kama mtu anakula ugoro wake na hakuwashi,wala haungilii maisha Yako just keep on with your life
 
Mtoa mada fata maisha Yako,kwani vijana wakila ugoro akaunti Yako inapungukiwa ela?au unakosa kula wewe na familia Yako?fuata mambo yanayokuhusu uishi miaka mingi na na kheri duniani,dunia imeumbwa na kila mtu tofauti ili maisha yabalance Kama mtu anakula ugoro wake na hakuwashi,wala haungilii maisha Yako just keep on with your life

Kiongozi, bila shaka wewe ni mmoja wapo wa watumiaji wa ugoro!
Watumiaji ugoro ni tabu sana, nakumbuka ipo siku nilikuwa nasafiri kumbe nimekaa na kijana mmoja mbwia ugoro, akabwia sasa kuna wakati ikawa inamlazimu ateme mate, kwa kuwa mimi nilikuwa nimekaa dirishani akawa ananiegemea ili afungue kioo ateme! But nikaamua kumpisha akae upande wa dirishani ikawa kila saa ni kutema mate tu, kwa kuwa ile safari ilikuwa ya mbali ilifika mahali a.c za gari ziliwashwa hivyo madirisha hayakuruhusiwa kufunguliwa, akaaanza kutema mate kwenye kapeti, aisee aliboa sana plus harufu iliyokuwa inatoka mdomoni mhh, nilitamani nimzabe kibao bahati abiria alishukua akaacha sit wazi nikaenda kuikalia!

Btw sambamba na kero kama hizo, ugoro unaathari kubwa sana kiafya, kama wewe ni mbwia ugoro wewe endelea tu lakini ipo siku utaleta uzi huku wa kuomba ushauri wa kutibu madonda koo, yaliyosababishwa na ubwiaji ugoro!
IMG_3838.jpg


IMG_3837.jpg

IMG_3836.jpg
 
Kwa wadau wenzangu wa kula dawa,dongo,kidonge,kigwati ongeza jina ukipenda! Hii kitu umeshika hatamu awamu hii...! Zamani walikua wanakula wazeee, sahivi vijana watanashati tunabwia. Leo nakupa raha zake.

1. Asubuhi ukienda kukata gogo na ugoro mdomoni unajihisi upo kwa Joe Biden.

2. Kwa sisi walevi ukipiga plisiner kubwa 3 ukishushia na ugoro unawaka zaidi ya jua kwahiyo unapunguza matumizi ya kulewa.

3. Kabla ya kulala usiku lazima upige ugoro ulale vizuri, bila hivyo misuri ya kichwa itakusimama na kuuma Sana.

4. Ukipata alosto na hauna mwingine tafuna kikaratasi Cha juzi au Jana maana kipo na akiba.

Mwisho...' Ugoro hatunyimani Kama wavuta Sigara tu,ndio maaana kwa muuzaji hukosi wa kuonja.
 
MKUU JANA NIMEKAA NAE KWENYE DALADALA ANATEMA MATE BALAA AFU ANAWEKA UGORO TENA

Hint:Sina gari wakuu ndo mana napanda daladala
 
Ugolo kwetu tunadabia wale wanyama wanaojiona wajanja sana halafu wanapenda vitu vitamu vitamu kama ndizi.
 
Ugoro umeshamiri baada ya kuberi kupigwa marufuku na serikali nilikuwa mlevi wa kuberi ila ugoro sijawai hata kuonja
 
MI KUMI TENAA,

Hongera sana kwa serikaki ya CCM
 
Back
Top Bottom