Vijana wengi wamekuwa wakijiingiza katika matumizi ya aina tofauti tofauti za vichochoe vya ulevi pamoja na madawa ya kulevya!
Hivi sasa kuna wimbi kubwa la vijana ambao wamejiingiza katika matumizi ya ugoro kiasi kwamba wamepata uraibu mkubwa, na wamefikia hatua ya kuwa mateja kabisa!
Ugoro una athari nyingi kiafya, ikiwemo kusababisha magonjwa kama kansa ya koo, kuharibika kwa mdomo na kutema mate hovyo ambapo ni kero kwa wasiotumia kwani hupata kinyaa!
Matumizi haya ya ugoro yameongezeka hasa baada ya serikali kupiga marufuku matumizi ya viroba, pia baada ya bei ya sigara za kawaida kuongezeka bei!
Ni ajabu sana kuwakuta vijana wadogo, na smart kabisa wakiwa wanabwia ugoro, mbaya zaidi ugoro huo huwa unaongezewa baadhi ya vitu ili kuuongezea ulevi!
Wapo wanafunzi, wengine ni wafanyakazi kwenye ofisi za umma, wafanyabiashara, makondakta n.k kwa ujumla wapo vijana wengi sana ambao huu uraibu umewakamata!
Bila shaka huu ni wakati wa kutoa elimu ya kutosha juu ya matumizi ya ugoro na ikibidi serikali ipige marufuku matumizi yake na uuzwaji holela wa kilevi hiki!