Vilevi vingine ni upumbavu% .kuna vitu vingine huwa hata kuviwazia siwezi,
Nilifanya kazi kwenye mambo ya utarii ,nilikuwa nakutana na wazungu wananipa sigara zao navuta kama kujistarehesha,napewa pakiti lakini havikuwahi kunikolea,nilikuwa nakaa na sigara hadi najikuta nazifuria kwenye suruali yani sipati hamu hadi nimuone mtu anavuta na mimi ndo nakumbuka kuvuta.
Siku moja najivutia sigara barazani akaja mrembo mmoja akaanza kunikejeri
"hee! na wewe unavuta sigara? Loh hufanani bora uache tu"
Tangu siku zile nikaachana na tabia za kufata mkumbo ,sivuti sigara na siujui ugoro wala radha yake.
Mambo mengine ni kujipa mzigo tu,pombe wewe,ugoro wewe,sigara wewe,aaah,haina mana kabsa,bora bia mbili tatu si mbaya ukiwa umetulia zako maeneo,hata sigara for fun unaweza kuvuta ila siyo miugoro,
Sent using
Jamii Forums mobile app