Zitto
Former MP Kigoma Urban
- Mar 2, 2007
- 1,562
- 10,890
Ndugu wana JF,
Kwa muda mrefu na hasa siku za hivi za karibuni kumekuwa na threads nyingi sana humu ndani kuhusu Zitto na kuhusu Chama cha ACT Wazalendo. Kumekuwa na tuhuma kwamba chama cha ACT Wazalendo kinashambulia vyama vingine vya upinzani hapa nchini. Napenda kusema mambo machache sana
Chama cha ACT Wazalendo ni chama cha siasa chenye mrengo wa kushoto na kinajitanabaisha na siasa ya Ujamaa iliyoasisiwa na Azimio la Arusha. Lengo letu ni kueneza siasa zetu zenye mrengo huo.
1. Chama cha ACT Wazalendo kwa sasa ni chama cha upinzani nchini. Kimekuja kuhuisha zaidi siasa za upinzani ili kuiondoa CCM madarakani. Chama cha ACT Wazalendo hakina lengo hata kidogo kuzorotesha upinzani nchini. Tofauti zetu tulizokuwa nazo katika chama tulichokuwamo wengine tumeshazifuta, tumepiga mstari na kutazama mbele.
Ndio maana hutasikia kiongozi hata mmoja wa ACT Wazalendo akihangaika na vyama vingine vya upinzani. Hata tukichokozwa namna gani tumefanya maamuzi kwamba hatutajibizana na chama kingine chochote cha upinzani hapa nchini. Tutapambana na chama tawala ili kubomoa mfumo wa uchumi unaonyonya wengi na kufaidisha wachache. Tutapigania uwajibikaji wa viongozi kwa wananchi. Tutapambana na ufisadi kwa nguvu zetu zote. Hizo ndizo kazi tulizo nazo.
2. Tunasisitiza, tunayo vita moja lakini una njia nyingi za kupigana dhidi ya adui. Huko tulipokuwa tulitofautiana mbinu hizo. Sasa tumepata jukwaa la kutumia mbinu hizo. Wenzetu watumie mbinu zao pia. Hatimaye kila mmoja alenge shabaha kwa adui mmoja. Tunasema One Struggle, Many Fronts
3. Kuitana mamluki, wasaliti nk ni siasa za framing tu. Sio mara ya kwanza siasa hizi kutumika nchini katika kujaribu ku frame watu. Mwaka 1995 Mrema wa NCCR aliita CHADEMA chama cha mashushu kutoka Benki Kuu na kila mtu alimwamini. Leo Mrema yupo wapi na CHADEMA ipo wapi? Mwaka 2000 mpaka 2005 CUF ndio ilikuwa chama kikuu cha upinzani na kuidharau CHADEMA. Mwaka 2013 CHADEMA iliita CUF chama cha mashoga.
Miaka yote Mbatia amekuwa akiitwa pandikizi nk. Yote haya hayajazuia vyama hivi kufanya kazi pamoja hivi sasa. Ni vizuri sana wanasiasa kuweka akiba ya maneno. Hakuna sababu ya kutukanana na kuitana majina mabaya. Tunachohitaji ni kila mmoja kumlenga adui ili kumshinda. Tulishindwa kufanya kazi ndani ya moja, tunaweza kufanya kazi tukiwa majirani. Adui bado ni yule yule.
4. Sisi ACT Wazalendo tutachochea kuni kuwasha moto wa mapinduzi nchini kwa kuendesha siasa za masuala (issues). Tumeanza ziara yetu mkoa wa Ruvuma kwa sababu ni mkoa ambao wabunge wake wote ni CCM. Tutaweka nguvu sana maeneo hayo badala ya maeneo ambayo tayari vyama vingine vya upinzani vina nguvu. Sisi katika ACT wazalendo tunataka kuona uchumi unarudi kwa wananchi wenyewe badala ya uchumi kushikiliwa na watu wachache.
Tunataka kuona Miiko ya Uongozi inarudi ili kurejesha imani ya wananchi kwa viongozi wao. Tunataka kuona mfumo madhubuti wa uwajibikaji nchini. Hayo ndio mapambano yetu. Hayo ndio maelekezo yetu kwa wanachama wetu; Kupambana na adui mmoja tu - CCM.
Kwa muda mrefu na hasa siku za hivi za karibuni kumekuwa na threads nyingi sana humu ndani kuhusu Zitto na kuhusu Chama cha ACT Wazalendo. Kumekuwa na tuhuma kwamba chama cha ACT Wazalendo kinashambulia vyama vingine vya upinzani hapa nchini. Napenda kusema mambo machache sana
Chama cha ACT Wazalendo ni chama cha siasa chenye mrengo wa kushoto na kinajitanabaisha na siasa ya Ujamaa iliyoasisiwa na Azimio la Arusha. Lengo letu ni kueneza siasa zetu zenye mrengo huo.
1. Chama cha ACT Wazalendo kwa sasa ni chama cha upinzani nchini. Kimekuja kuhuisha zaidi siasa za upinzani ili kuiondoa CCM madarakani. Chama cha ACT Wazalendo hakina lengo hata kidogo kuzorotesha upinzani nchini. Tofauti zetu tulizokuwa nazo katika chama tulichokuwamo wengine tumeshazifuta, tumepiga mstari na kutazama mbele.
Ndio maana hutasikia kiongozi hata mmoja wa ACT Wazalendo akihangaika na vyama vingine vya upinzani. Hata tukichokozwa namna gani tumefanya maamuzi kwamba hatutajibizana na chama kingine chochote cha upinzani hapa nchini. Tutapambana na chama tawala ili kubomoa mfumo wa uchumi unaonyonya wengi na kufaidisha wachache. Tutapigania uwajibikaji wa viongozi kwa wananchi. Tutapambana na ufisadi kwa nguvu zetu zote. Hizo ndizo kazi tulizo nazo.
2. Tunasisitiza, tunayo vita moja lakini una njia nyingi za kupigana dhidi ya adui. Huko tulipokuwa tulitofautiana mbinu hizo. Sasa tumepata jukwaa la kutumia mbinu hizo. Wenzetu watumie mbinu zao pia. Hatimaye kila mmoja alenge shabaha kwa adui mmoja. Tunasema One Struggle, Many Fronts
3. Kuitana mamluki, wasaliti nk ni siasa za framing tu. Sio mara ya kwanza siasa hizi kutumika nchini katika kujaribu ku frame watu. Mwaka 1995 Mrema wa NCCR aliita CHADEMA chama cha mashushu kutoka Benki Kuu na kila mtu alimwamini. Leo Mrema yupo wapi na CHADEMA ipo wapi? Mwaka 2000 mpaka 2005 CUF ndio ilikuwa chama kikuu cha upinzani na kuidharau CHADEMA. Mwaka 2013 CHADEMA iliita CUF chama cha mashoga.
Miaka yote Mbatia amekuwa akiitwa pandikizi nk. Yote haya hayajazuia vyama hivi kufanya kazi pamoja hivi sasa. Ni vizuri sana wanasiasa kuweka akiba ya maneno. Hakuna sababu ya kutukanana na kuitana majina mabaya. Tunachohitaji ni kila mmoja kumlenga adui ili kumshinda. Tulishindwa kufanya kazi ndani ya moja, tunaweza kufanya kazi tukiwa majirani. Adui bado ni yule yule.
4. Sisi ACT Wazalendo tutachochea kuni kuwasha moto wa mapinduzi nchini kwa kuendesha siasa za masuala (issues). Tumeanza ziara yetu mkoa wa Ruvuma kwa sababu ni mkoa ambao wabunge wake wote ni CCM. Tutaweka nguvu sana maeneo hayo badala ya maeneo ambayo tayari vyama vingine vya upinzani vina nguvu. Sisi katika ACT wazalendo tunataka kuona uchumi unarudi kwa wananchi wenyewe badala ya uchumi kushikiliwa na watu wachache.
Tunataka kuona Miiko ya Uongozi inarudi ili kurejesha imani ya wananchi kwa viongozi wao. Tunataka kuona mfumo madhubuti wa uwajibikaji nchini. Hayo ndio mapambano yetu. Hayo ndio maelekezo yetu kwa wanachama wetu; Kupambana na adui mmoja tu - CCM.