Ombi/Rai kwa viongozi wa CHADEMA, tuanzishe Siku ya Mashujaa wetu!

Kiwi

JF-Expert Member
Sep 30, 2009
1,054
990
Heshima kwenu wanajamvi,

Nina ombi ama rai ambayo ningependa ifanyiwe utafiti na ikiwezekana iwekwe kwenye historia ya mapambano yetu ya ukombozi.

Ninapendekeza CHADEMA iweke siku maalum kwenye kalenda zetu, iwe siku ya kuwakumbuka wote wale waliopoteza maisha yao kwenye harakati za kumkomboa maskini wa Tanzania kutoka kwenye makucha ya wakoloni hawa weusi wadhalimu wanaotuangamiza kila kukicha. Ni wazo tu naomba muwe huru kulijadili na hata kuliacha kama mnaona halina tija. Ili kufanikisha hili ningeomba iwekwe orodha ya wote waliotangulia mbele ya haki na kama inawezekana hata picha zao na historia fupi za maisha yao. Tunao wengi, na kwa jinsi serikali yetu inavyoendelea kubanwa na badala ya kutafuta ufumbuzi inavyoendeleza vitisho na ubabe ninafikiri bado hatujafika mwisho wa safari yetu, ingawa tunakaribia...

Wapumzike kwa Amani mashujaa wetu! Tunaweza kuapa tu ya kuwa tutawaenzi, na damu yao itakuwa chachu itakayoongeza vuguvugu la mabadiliko katika nchi yetu!
 
Heshima kwenu wanajamvi,

Nina ombi ama rai ambayo ningependa ifanyiwe utafiti na ikiwezekana iwekwe kwenye historia ya mapambano yetu ya ukombozi.

Ninapendekeza CHADEMA iweke siku maalum kwenye kalenda zetu, iwe siku ya kuwakumbuka wote wale waliopoteza maisha yao kwenye harakati za kumkomboa maskini wa Tanzania kutoka kwenye makucha ya wakoloni hawa weusi wadhalimu wanaotuangamiza kila kukicha. Ni wazo tu naomba muwe huru kulijadili na hata kuliacha kama mnaona halina tija. Ili kufanikisha hili ningeomba iwekwe orodha ya wote waliotangulia mbele ya haki na kama inawezekana hata picha zao na historia fupi za maisha yao. Tunao wengi, na kwa jinsi serikali yetu inavyoendelea kubanwa na badala ya kutafuta ufumbuzi inavyoendeleza vitisho na ubabe ninafikiri bado hatujafika mwisho wa safari yetu, ingawa tunakaribia...

Wapumzike kwa Amani mashujaa wetu! Tunaweza kuapa tu ya kuwa tutawaenzi, na damu yao itakuwa chachu itakayoongeza vuguvugu la mabadiliko katika nchi yetu!

Poa iwe tarehe ngapi?
 
Ombi lako ni zuri ila naomba ukapitie vyema maana ya neno SHUJAA. hasa uliangalie neno hilo katika ulingo wa siasa lina maana gani
 
Poa iwe tarehe ngapi?

Mkuu, hilo nawaachia wana CHADEMA wenzangu walijadili kwa pamoja na kuamua. Inaweza hata kuwa tarehe 15.6 kila mwaka, lakini mimi siwezi kuamua kwa niaba ya wana CHADEMA. Ningependa sana demokrasia ya wengi ifanye uamuzi kuhusu jambo hili, tarehe yoyote itakayokubalika na wengi ni sawa. Cha muhimu ni ile dhana!
 
Back
Top Bottom