GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,542
- 108,877
Naona Watu wengi (Members) hapa tunawasema, tunawacheka, tunawadhihaki hadi kuwatukana huku tukiwaambia sijui wamenunuliwa na wana Njaa sana. Sitaki Kuwakatalia au Kupinga haya Maneno yenu Kwao hawa Wabunge Viti Maalum CHADEMA kutokea BAWACHA, ila GENTAMYCINE nina Ombi moja Maalum tu Kwenu na nitafurahi mkilitekeleza haraka tu hapa Jamvini.
Nawaombeni wale Wote ambao mnawacheka, mnawadhihaki na kuwaambia akina Mdee, Bulaya na Wenzake kuwa wana Njaa na wamenunuliwa au kuahidiwa Vyeo nanyi mtuwekee hapa Majina yenu halisia (siyo haya Fake na hizi ID's zetu) ili na Sisi wanaotujua vyema waweze kusema kama tuna njaa au hatuna ili tuweze pia Kuwatendea Haki hawa Wabunge Viti Maalum CHADEMA.
Kitu pekee tu ninachoweza kusema na tena nina uhakika nacho kwa 99.999% ni kwamba kwa hali ya Msoto ( Maisha Magumu ) hasa ya Kipato tuliyonayo Watanzania wengi wengi Wetu Zali hili au Mchongo huu wa kwenda Bungeni na Kupata Pesa pamoja n kile Kiinua Mgongo wala tusingekiacha na tungesalitiana tu. Cheza na Vitu vyote ila siyo Njaa. Tuacheni Unafiki katika hili.
Wabunge wote wa Viti Maalum CHADEMA kutokea CHADEMA hata Mimi GENTAMYCINE ningewashangaa mno kama mngeziachia Pesa za Bwerere kisha muanze Kusota na Kupigiana tu Miayo hapo Biafra Kinondoni na Mwenyekiti wenu Taifa Mbowe huku Tundu Lissu akipumzika zake tu huko Ulaya na Wazungu wakimlisha, wakimlipa na wakimtunza vile vile.
Watanzania (Waswahili) tumekuwa wepesi sana Kulaumu na Kuhukumu mno wakati tumesahau kuwa kwenye Njaa Unafiki na Usaliti hushirikiana.
Nawaombeni wale Wote ambao mnawacheka, mnawadhihaki na kuwaambia akina Mdee, Bulaya na Wenzake kuwa wana Njaa na wamenunuliwa au kuahidiwa Vyeo nanyi mtuwekee hapa Majina yenu halisia (siyo haya Fake na hizi ID's zetu) ili na Sisi wanaotujua vyema waweze kusema kama tuna njaa au hatuna ili tuweze pia Kuwatendea Haki hawa Wabunge Viti Maalum CHADEMA.
Kitu pekee tu ninachoweza kusema na tena nina uhakika nacho kwa 99.999% ni kwamba kwa hali ya Msoto ( Maisha Magumu ) hasa ya Kipato tuliyonayo Watanzania wengi wengi Wetu Zali hili au Mchongo huu wa kwenda Bungeni na Kupata Pesa pamoja n kile Kiinua Mgongo wala tusingekiacha na tungesalitiana tu. Cheza na Vitu vyote ila siyo Njaa. Tuacheni Unafiki katika hili.
Wabunge wote wa Viti Maalum CHADEMA kutokea CHADEMA hata Mimi GENTAMYCINE ningewashangaa mno kama mngeziachia Pesa za Bwerere kisha muanze Kusota na Kupigiana tu Miayo hapo Biafra Kinondoni na Mwenyekiti wenu Taifa Mbowe huku Tundu Lissu akipumzika zake tu huko Ulaya na Wazungu wakimlisha, wakimlipa na wakimtunza vile vile.
Watanzania (Waswahili) tumekuwa wepesi sana Kulaumu na Kuhukumu mno wakati tumesahau kuwa kwenye Njaa Unafiki na Usaliti hushirikiana.