Ombi: Ili haki itendeke Joseph Mkundi aondolewe kwenye Kamati ya kuchunguza Ajali ya MV Nyerere

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,651
218,131
Baada ya ajali ya MV NYERERE na hasa baada ya kukamilika kwa shughuli za ukusanyaji maiti na uokozi , Waziri Mkuu Mh Kasimu Majaliwa aliunda tume ya kuchunguza chanzo cha ajali hiii mbaya kabisa iliyoua namia ya wananchi , naogopa kuweka idadi halisi ya waliokufa kwa ajili ya kuheshimu SHERIA YA TAKWIMU , Mungu aziweke roho za marehemu wote mahali pema peponi , Amina .

Mmoja wa wajumbe wa tume hii anaitwa JOSEPH MKUNDI , ambaye Waziri Mkuu alizitaja sababu za kuteuliwa kwake ndani ya kamati hii kuwa ni pamoja na yeye kuwa mkazi wa eneo hilo na pia ni Mwakilishi wa wananchi , kwa maana ya mbunge wa eneo la ajali na kwamba bila ya shaka uwepo wake utaleta imani ya wananchi kwa tume husika , amekuwa akilipigia kelele suala la kivuko hicho ndani na nje ya bunge kwa muda mrefu .

Kwa bahati mbaya kabla hata ya kazi ya tume kushika kasi Ndugu JOSEPH MKUNDI ameamua kujiuzulu ubunge na hivyo KUPOTEZA sifa kuu ambayo ilimfanya Waziri Mkuu amteue kuwa mjumbe ndani ya kamati , na katika taarifa yake kwa vyombo vya habari pamoja na kujivua ubunge ametaja pia kujivua vyeo vyote alivyokuwa navyo awali , ninao uhakika kwamba moja ya vyeo alivyokuwa navyo ni pamoja na ujumbe wa tume hii , nashauri aondolewe.

Naomba kuwasilisha .
 
Baada ya ajali ya MV NYERERE na hasa baada ya kukamilika kwa shughuli za ukusanyaji maiti na uokozi , Waziri Mkuu Mh Kasimu Majaliwa aliunda tume ya kuchunguza chanzo cha ajali hiii mbaya kabisa iliyoua namia ya wananchi , naogopa kuweka idadi halisi ya waliokufa kwa ajili ya kuheshimu SHERIA YA TAKWIMU , Mungu aziweke roho za marehemu wote mahali pema peponi , Amina .

Mmoja wa wajumbe wa tume hii anaitwa JOSEPH MKUNDI , ambaye Waziri Mkuu alizitaja sababu za kuteuliwa kwake ndani ya kamati hii kuwa ni pamoja na yeye kuwa mkazi wa eneo hilo na pia ni Mwakilishi wa wananchi , kwa maana ya mbunge wa eneo la ajali na kwamba bila ya shaka uwepo wake utaleta imani ya wananchi kwa tume husika , amekuwa akilipigia kelele suala la kivuko hicho ndani na nje ya bunge kwa muda mrefu .

Kwa bahati mbaya kabla hata ya kazi ya tume kushika kasi Ndugu JOSEPH MKUNDI ameamua kujiuzulu ubunge na hivyo KUPOTEZA sifa kuu ambayo ilimfanya Waziri Mkuu amteue kuwa mjumbe ndani ya kamati , na katika taarifa yake kwa vyombo vya habari pamoja na kujivua ubunge ametaja pia kujivua vyeo vyote alivyokuwa navyo awali , ninao uhakika kwamba moja ya vyeo alivyokuwa navyo ni pamoja na ujumbe wa tume hii , nashauri aondolewe.

Naomba kuwasilisha .
naunga mkono hoja
cc: Pascal Mayalla
 
Napingana na wewe kwa sababu, iwapo ataondolewa tutachafua ule uchunguzi ambao tiyari ushaanzwa pindi tukileta tena mgeni ambaye hatukuanza naye. Kumbuka, aliingia ka mwakilishi wa wananchi sifa aliyoiacha kwa kitambo kifupi tu kwani twajua kuwa,ATARUDI TENA KWA KISHINDO. Je, utakuja hapa pia kusema; Mrudisheni kwa kuwa sasa anazo sifa?? Je unataka wananchi wawakilishwe na nani?? Aendelee na CV hiyo hiyo ya "Mwakilishi wa wananchi". Amejivua ubunge na uchama sio uananchi wa huko jimboni mwake.
 
Kwa hiyo ujumbe wa tume ni lazima uwe mwanachama wa CDM, akili za ki nyumbxxx kabisa.

Hilo ni wazo lake, hata wewe unaruhusiwa kuja na wazo lako. Yeye kasema sifa iliyomuingiza kwenye hiyo kamati ni kwakuwa ni muwakilishi wa wananchi mbunge na diwani. Kwa sasa kajivua hizo nafasi zote kiasi kwamba anakosa sifa hizo. Sasa wewe unamtusi kisha mkitukanwa mnapiga kelele. Huwezi matusi hivyo kuwa mvumilivu wa hoja kinzani, lakini ukileta matusi jiandae kupewa matusi mazito na usipige kelele.
 
Napingana na wewe kwa sababu, iwapo ataondolewa tutachafua ule uchunguzi ambao tiyari ushaanzwa pindi tukileta tena mgeni ambaye hatukuanza naye. Kumbuka, aliingia ka mwakilishi wa wananchi sifa aliyoiacha kwa kitambo kifupi tu kwani twajua kuwa,ATARUDI TENA KWA KISHINDO. Je, utakuja hapa pia kusema; Mrudisheni kwa kuwa sasa anazo sifa?? Je unataka wananchi wawakilishwe na nani?? Aendelee na CV hiyo hiyo ya "Mwakilishi wa wananchi". Amejivua ubunge na uchama sio uananchi wa huko jimboni mwake.
unajua tume imepewa muda gani kukamilisha kazi ?
 
Napingana na wewe kwa sababu, iwapo ataondolewa tutachafua ule uchunguzi ambao tiyari ushaanzwa pindi tukileta tena mgeni ambaye hatukuanza naye. Kumbuka, aliingia ka mwakilishi wa wananchi sifa aliyoiacha kwa kitambo kifupi tu kwani twajua kuwa,ATARUDI TENA KWA KISHINDO. Je, utakuja hapa pia kusema; Mrudisheni kwa kuwa sasa anazo sifa?? Je unataka wananchi wawakilishwe na nani?? Aendelee na CV hiyo hiyo ya "Mwakilishi wa wananchi". Amejivua ubunge na uchama sio uananchi wa huko jimboni mwake.
wapo wanainchi wengi sio lazima yeye. vigezo na masharti kuzingatiwa.
wewe utakuwa huna tofauti na HAPI kavurunda kino kapewa mbeleko kubwaa.
kufika huko alikobebwa kaamua kutaka sifa kama wewe kwa kumuweka ndani meya kisa kamvuruga kada wenu.
shwain kweli nyie

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
Baada ya ajali ya MV NYERERE na hasa baada ya kukamilika kwa shughuli za ukusanyaji maiti na uokozi , Waziri Mkuu Mh Kasimu Majaliwa aliunda tume ya kuchunguza chanzo cha ajali hiii mbaya kabisa iliyoua namia ya wananchi , naogopa kuweka idadi halisi ya waliokufa kwa ajili ya kuheshimu SHERIA YA TAKWIMU , Mungu aziweke roho za marehemu wote mahali pema peponi , Amina .

Mmoja wa wajumbe wa tume hii anaitwa JOSEPH MKUNDI , ambaye Waziri Mkuu alizitaja sababu za kuteuliwa kwake ndani ya kamati hii kuwa ni pamoja na yeye kuwa mkazi wa eneo hilo na pia ni Mwakilishi wa wananchi , kwa maana ya mbunge wa eneo la ajali na kwamba bila ya shaka uwepo wake utaleta imani ya wananchi kwa tume husika , amekuwa akilipigia kelele suala la kivuko hicho ndani na nje ya bunge kwa muda mrefu .

Kwa bahati mbaya kabla hata ya kazi ya tume kushika kasi Ndugu JOSEPH MKUNDI ameamua kujiuzulu ubunge na hivyo KUPOTEZA sifa kuu ambayo ilimfanya Waziri Mkuu amteue kuwa mjumbe ndani ya kamati , na katika taarifa yake kwa vyombo vya habari pamoja na kujivua ubunge ametaja pia kujivua vyeo vyote alivyokuwa navyo awali , ninao uhakika kwamba moja ya vyeo alivyokuwa navyo ni pamoja na ujumbe wa tume hii , nashauri aondolewe.

Naomba kuwasilisha .
Upo sahihi
 
Hilo ni wazo lake, hata wewe unaruhusiwa kuja na wazo lako. Yeye kasema sifa iliyomuingiza kwenye hiyo kamati ni kwakuwa ni muwakilishi wa wananchi mbunge na diwani. Kwa sasa kajivua hizo nafasi zote kiasi kwamba anakosa sifa hizo. Sasa wewe unamtusi kisha mkitukanwa mnapiga kelele. Huwezi matusi hivyo kuwa mvumilivu wa hoja kinzani, lakini ukileta matusi jiandae kupewa matusi mazito na usipige kelele.

Hamna hoja yoyote hapa zaidi ya siasa majitaka, mnamuonea wivu hadi kuwa kwenye tume tu ? Ukerewe hakuna Mbunge, yeye ndio mwakilishi mstaafu wa karibuni, je hiyo ni dhambi akiwakilisha wana Ukerewe au mnataka aje Mbowe au mwana CDM ?
 
Hoja yako dhaifu. Wananchi hawabadili imani yao kwa yule waliyekuwa wamemchagua awali hasa nyakati za awamu hii ya Tano hata baada ya kubadili msimamo wake na uanachama wake kisiasa. Ushahidi upo. Tumeyaona Moduli, Ukonga na kwingineko!!
Huyo ndugu aendelee kuwemo kwenye tume
 
Huyo amepumzika tu ubunge kwa muda, anarudi tena muda sio mrefu ila itakuwa kwa tiketi ya CCM
 
Hamna hoja yoyote hapa zaidi ya siasa majitaka, mnamuonea wivu hadi kuwa kwenye tume tu ? Ukerewe hakuna Mbunge, yeye ndio mwakilishi mstaafu wa karibuni, je hiyo ni dhambi akiwakilisha wana Ukerewe au mnataka aje Mbowe au mwana CDM ?

Kichwa cha habari ya uzi wake kasema kabisa ni ombi. Sasa unaposema kwamba ni siasa majitaka sijui unataka atumie lugha gani. Hakuna popote alipolazimisha, hata ukitaka kwenye hiyo kamati awepo huyo jamaa pamoja na mke wake ni sawa. Lakini sifa iliyomuingiza kwenye hiyo kamati ni kwakuwa yeye alikuwa mbunge na diwani wa eneo hilo na ndio mwakilishi wao. Sifa hizo kwa sasa hana tena? Kuna mahali popote kapendekeza mjumbe mbadala huyo Mbowe au mwingine, achia mbali kuwa ni wa cdm au la? Je ubaya wa mleta uzi kutoa ombi lake kuendana na sifa ya sasa ya huyo mjumbe ni ipi tena kwa lugha kistaarabu? Jifunze kuvumilia hoja usizozipenda kwani hiyo ndio demokrasia.
 
Hoja yako dhaifu. Wananchi hawabadili imani yao kwa yule waliyekuwa wamemchagua awali hasa nyakati za awamu hii ya Tano hata baada ya kubadili msimamo wake na uanachama wake kisiasa. Ushahidi upo. Tumeyaona Moduli, Ukonga na kwingineko!!
Huyo ndugu aendelee kuwemo kwenye tume

Kilichofanyika kwenye hayo majimbo uliyotaja wakati wa uchaguzi ni aibu kwa mwanaume mzima kutumia kama sehemu ya utetezi wa hoja zako.
 
Kateuliwa Kwa Kuwa kwake Mwakilishi wa Wananchi wakati Ajali inatokea sio wakati wa Uchunguzi!
 
Back
Top Bottom