Baada ya kutuhumiwa na Tundu lisu wa chadema kuwa alipokea rushwa ili kukwamisha bajeti ya wizara ya nishati na madini,Mbunge wa Simanjiro Olesendeka alikua jana jimboni kwake ktk kijiji cha Kimotorok kuhudhuria mkutano mkuu wa kijiji kilichokua kinajadili mgogoro wa ardhi na hifadhi ya Tarangire. Mara baada ya sendeka kuwasili ktk eneo hilo nusra wamasai wenzie wampige kwasababu kuu Tatu: 1.kwa kitendo cha yeye kupoke rushwa,maana wamesema hiyo ni kawaida yake kupokea na kutoa rushwa 2.kwamba;sendeka ni msaliti na kigeugeu km kinyonga na pia hana msimamo na hivyo kuudhalilisha umaasai wao na umma ya wanasimanjiro 3. Kwamba; alihusika kushirikiana na Tarangire kuhujumu eneo lao kuchukuliwa kuwa sehemu ya hifadhi huku yeye akijifanya yupo na jamii kumbe ni unafki mtupu!! Sendeka alijitahidi kuomba msamaha huku akipiga magoti na kuongea lugha ya kwao akichanganya na kiswhli lakini aliambulia matusi,kejeli na mwisho akafukuzwa! Hajulikani ametokomea wapi, labda wenye taarifa watujuze alipo maana mpk jana taarifa zinasema hali yake ilikuwa mbaya sana......