Old Soviet Missile Destroys US M1 Abrams Tank (VIDEO)

Old Soviet Missile Destroys US M1 Abrams Tank (VIDEO)

Acha ushabiki baba mkwe, AK47 huwezi kulinganisha na hiyo silaha nyingine. Urusi bado haijapata upinzani kwenye hii sekta.

Huyo Mrusi alifurushwa huko Afghanistan na akina Osama halafu wewe hapa unaimba nyimbo za kumtukuza?

Umelewa kool-aid ya MRusi wewe.
 
Hapa ni mpambano kati ya Iran na Saudia arabia.Iran mfadhili wao ni Russia na Marekani inafadhili Saudia arabia,kwamaana waasi wa houthi wanasaidiwa kila kitu na Iran kwa kupewa wanajeshi,washauri,mafunzo,zana za vita,pesa nk
Vita ya yemen imeshawashika pabaya wa saudia na ni lazima wapigane kwani yemen ni jirani yake lolote linaweza kutokea ikiwemo kusambaratishwa kwa ufalme wa saudia,mwanzoni walitumia ndege za kivita kushambulia na mwishowe matokeo mazuri hayakupatikana wakatangaza kupeleka majeshi ya ardhini na sasa wamepata mapigo makubwa wanajeshi wao wanakufa na zana za vita zinateketea kwahivyo matokeo sio mazuri.
Imebidi viongozi wa ngazi za juu akiwemo mfalme wa saudia waende kumuomba Putin aokoe jahazi.
Putin anawaambia wa saudia waache michezo yao michafu ya kuwapa silaha islamic jihadist wakiwemo isis ili kuisambaratisha nchi ya syria,kuwapa silaha vikundi vilivyoasi chechnya na kusapoti America kwa kuzalisha mafuta kwa wingi kwa bei ya chini ktk soko la dunia ili mafuta ya Russia yapungue soko na kupelekea ela ya Russia Rouble kupungua dhamani ambapo uchumi wa Russia utaporomoka.
Saudi arabia imebidi iungane kisiri na Israel ktk kupinga Iran iondolewe vikwazo.Marekani hasikii la kuambiwa anamezea mate mafuta ya Iran.
Middle east ni uwanja wa mapambano yasiyoisha ila mshindi atakuwa Israel kwani hata kwenye vitabu vitakatifu imeandikwa.
 
jaman mbona mnapend san vibaya.mmesahau kiichotokea ktk vita vya yugoslavia F117 stealth attack aircraft ambayo wamarekan walisem hii kitu haionekan kwenye rada na pia ni ngumu kui target.lakin kilichotokea ilikuwa na aibu kubw ambayo ni ngum kufutik.mfumo ambao uko urusi watot wanatumia kuchezea kombolela ndio uliotumik kuangush ndege iyo
 
Mbona speed ndogo sana hii..!!?
Haichagui. Ni sawa na risasi ya tembo si inaua hata binadamu? Abrams M1 ni special armor platwd tank ambayo ilitakiwa isidhurike na hizo missiles pamoja na IPDs. Ina spidi mpaka 72kph
 
Kwani are those tanks designed to withstand strikes from old missiles (from Russia) or what?
If that is the case, then we should only assume that the tank was damaged only bcos the missile managed to trigger the explosives within the vehicle. Therefore, it is the tank's own ordnances, rather than the supposed missile's superiority (or the tank's inferiority, whichever's your perspective) that are responsible for it destruction.
 
comrade kwa ninafaham hasa nyakati hizi sidhani kama nchi zilizoendelea wanazi umia sana, ikiwa na maana kwa sasa kuna vifaru vinachanja mbu mbuga kwa high speed..!
 
comrade kwa ninafaham hasa nyakati hizi sidhani kama nchi zilizoendelea wanazi umia sana, ikiwa na maana kwa sasa kuna vifaru vinachanja mbu mbuga kwa high speed..!
kifaru ili kichanje mbuga itabidi kiwe chepesi sana. kikiwa chepesi sana hakiwezi fanya kazi ya kifaru. labda unazungumzia humvees.
 
comrade kwa ninafaham hasa nyakati hizi sidhani kama nchi zilizoendelea wanazi umia sana, ikiwa na maana kwa sasa kuna vifaru vinachanja mbu mbuga kwa high speed..!

Hebu kitaje hicho kifaru. Kwa marekani hivi ndio latest na havivuki 72kph
 
Hapa nimejifunza mengi kuhusu uwezo wa silaha za mataifa mengi - asanteni sana wachangaiji.

Tatizo langu ni kuwa:
Hivi haya malumbano (postures) ya haya mataifa makubwa ya kivita (USA, Russia, EU, China, Israel, Pakistan, India, N. Korea, etc.) yanatusaidia nini sisi walalahoi wa mataifa mengine duniani na sisi wa Bongo tu - (au kama sio vikaragosi au wategemea wakuu wa haya mataifa makubwa?)

Nina tatizo kubwa sana kwa Marekani kuikwaza Urusi kiuchumi eti tu kwa sababu Urusi inawapinga Marekani kuhimilishwa na kuhujumiwa na NATO.

(Kumbuka kuwa - Reagan na Gobachev walikubaliana kuwa NATO haitajisogeza hata mita moja mashariki kuihujumu Urusi walipovunja ukuta wa Berlin).

Hiki kitu cha Urusi kuihimili Crimea ni sababu tu. Crimea walijichagulia wenyewe kuhamia Urusi baada ya mapinduzi ya raisi Yanukovych yaliyotokea February 2014. Kinacholeta huu mtafaruku sasa ni kuwa NATO wanajikusanyia nchi nyingi ndani ya NATO ambazo katika makubaliano ya awali ya Reagan na Gobachev walikubaliana kuwa hayatatokea.

Kwa sasa Marekani (NATO) wanasema kuwa eti enzi hizo "Gobachev na Reagan hawakuyafanya haya makubaliano kimaadishi" - really?.

Mkuu Nyani Ngabu (na wengine pia - nitawanukuu hapa chini), kwa kuwa wewe (nyie) natumai una(mna) historia nzuri ya "the cold war", u(m)naweza kunisahihisha vizuri.

Ushauri:
Tusishabikie haya malumbano ya hizi SUPER au superior powers hata kidogo. Kwa nini?

SISI SOTE NI MAJERUHI TU WA HAWA MAFAHARI WANAOGOMBANA!!

Tukatafute MIHOGO na MAHARAGE yetu tu tule!! Au vipi? Tupo Njia panda.

cc. Dotworld Safari_ni-Safari Maziku Masunga Jr. kui Somi mohamedidris789 TODAYS INConoclastes malcolm Lumumba Njooni huku bwana Bukyanagandi elingata TUJITEGEMEE Red Giant
 
M1A1_HA_sideLOS.jpg
 
Back
Top Bottom