Ukweli ndio huo!
Shell kama sheli haina matatizo!Tatizo ni wafanyakazi wa hiyo shell.Na si kwamba ni wafanyakazi wa shell hiyo,ni shell nyingi hapa mjini wenye tabia ya namna hiyo!
Mie nilienda kuweka mafuta sheli moja ya pale Ubungo external nikampa 10000/- mdada aniwekee mafuta, nikamuacha aendelee kuniwekea.
Baadae nikasikia akigonga gari kwenye ubavu akimaanisha ameshamaliza kuweka!Nikamuuliza mbona amechukua muda mfupi kuweka mafuta?Akanambia ndiyo hivyo ameshaweka!!
Ikanibidi nishuke kuangalia kwenye mita ya sheli,nikakuta 5000/- kwenye sheli moja na nyingine 7000/-!Nikamuambia mbona mita inayosoma 10000/- siioni?Akanambia hizo ni gharama za mafuta ya pikipiki ambazo ameweka baada ya kuniwekea mimi!!!
Wakati kwa muda niliokaa pale ni ndoto kuwawekea wateja watatu!!
Nikajilaumu kwa kuwa mzembe kwa kutoshuka kwenye gari alipokuwa akiweka mafuta!
Nikawa nimeshaibiwa tayari!
Tahadhari:
Hakikisha unapoweka mafuta kwenye gari unashuka kabisa na kusogelea mita kuhakikisha kuwa kiasi cha mafuta unayoweka ni ya gharama uliyolipia!