Ofisi ya waziri mkuu yageuka kuwa mahakama kuu katika sakata la madaktari

hapo patamu sijui maana ya sheria nini na ukweli utaonekana sio muda mrefu. haki ya mtu haipotei itapatikana tu na huu ndio mwanzo wa safari tu
 
hivi JK una waziri mkuu ana matakataka ya jalalani? huyu waziri mkuu gani anafanya mambo ya kipumbafuu..unatuaibisha bana..aghhhh wazungu wanatucheka ofisini hapa kwa ajili ya mautumbo ya Pinda
 
hakuna serikali iliyowahi kutia aibu katika historia ya tanzania kama hii!kauli zao zinapishana kila siku,kila mtu msemaji,sasa kila mtu mwandishi,.hili wazo lazima alilitoa lusinde kupitia kwa wassira...
 
yani serikali yetu ni aibu tupu mimi nahisi tunaonekana kituko kwa jirani zetu na walioko mbali.
Raisi yeye kila siku anapaa tu wakati kwake matatizo mengi, waziri mkuu baadala afanye kazi kwa kufuata misingi ya uongozi yeye anaanza mambo ya vijiweni ya kuoneana huruma na mambo ya kijinga. Yani ananiboa huyu pinda ananiboa to the maximum.
Sijawahi ona serikali ya kipumbavu na kijinga na ya wahuni wazandiki wasio jua nini wanafanya kama serikali yetu ya tanzania.
 
Dont tell me hata saini hawakuiona kwamba ni ya waziri mkuu...
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mahakama Kuu, Divisheni ya Kazi, leo (*Alhamisi Machi 8, 2012) *imetoa
... uamuzi wa kusitishwa mara moja kwa mgomo wa Madaktari ulioitishwa nchi
nzima tangu jana (*Jumatano Machi 7, 2012).

Katika amri yake ya pili, Mahakama Kuu pia imekitaka Chama cha Madaktari
Tanzania na Jumuiya ya Madaktari kuwatangazia wanachama wao mara moja kupitia
Vyombo vya Habari kusitishwa kwa mgomo huo nchi nzima kama
walivyowatangazia wakati wanauitisha mgomo wenyewe.

Mahakama Kuu pia imeamuru pande zote mbili, yaani Serikali kwa upande mmoja
na Chama cha Madaktari na Jumuiya ya Madaktari, kwa upande mwingine,
kutumia fursa zilizopo katika kutatua mgogoro wa kikazi uliopo kati yao kwa
haraka.


Uamuzi huo wa Mahakama Kuu imetolewa na Jaji R.M. Rweyemamu, baada ya
kusikiliza ombi la Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi ya Chama cha
Madaktari na Jumuiya ya Madaktari kuitaka itoe zuio kwa mgomo huo.

Akitoa uamuzi huo, Jaji Rweyemamu alisema anazingatia madhara ambayo mgomo
huo ungeleta kwa jamii kwa vile huduma za tiba ambazo madaktari walitaka
kugoma kuzitoa ni miongoni mwa huduma muhimu zilizotajwa kwenye Sheria ya
Ajira na Mahusiano Kazini, Namba 6 ya Mwaka 2004.

Uamuzi huo, ni kama ifuatavyo:

Leo, tarehe 8, Machi 2012, Mahakama Kuu, Divisheni ya Kazi, mbele ya Jaji
R.M. Rweyemamu
, baada ya kusikiliza Ombi No. 24 la 2012 lililowasilishwa na
Mwanasheria Mkuu wa Serikali (Mwombaji) dhidi ya Chama cha Madaktari
Tanzania na Jumuiya ya Madaktari (Walalamikiwa), imetoa uamuzi ufuatao:

i) Chama cha Madaktari Tanzania na Jumuiya ya Madaktari
pamoja na Wanachama wao, kusitisha Mgomo waliouanzisha rasmi tarehe 7 Machi
2012 nchi nzima na kurejea kazini mara moja kwa kuendelea na kazi zao kama
kawaida, mara tu Amri hii itakapowafikia. Aidha, waombaji watatakiwa kutoa
Kiapo cha kuthibitisha kwamba wamewasilisha Amri hiyo kwa Walalamikiwa na
kuwasilisha Kiapo hicho Mahakama Kuu – Divisheni ya Kazi kesho tarehe 9,
Mach 2012.

ii) Mara baada ya Amri hii kuwasilishwa kwa Walalamikiwa
(Chama cha Madaktari Tanzania na Jumuiya ya Madaktari) watatakiwa
kuwatangazia Wanachama wao kupitia Vyombo vya Habari kusitishwa kwa Mgomo
huo Nchi nzima kama walivyowatangazia wakati wa kuitisha Mgomo huo;

iii) Mahakama inaamuru pande zote mbili (Serikali na Chama
cha Madaktari Tanzania pamoja na Jumuiya ya Madaktari) kutumia fursa za
Kisheria zilizopo katika kutatua Mgogoro wa Kikazi uliopo kati yao kwa
haraka.
(mwisho)
Imetolewa na:

Ofisi ya Waziri Mkuu,
S.L.P. 3021
DAR ES SALAAM.
Alhamisi Machi 8, 2012


Siku hizi kazi za ofisi ya PM zimekuwa za kimahakama au ndio kuzuia PM asiachie madaraka,pinda jiuzulu umeiabisha.

Jamani hii HUKUMU ama ZUIO lime serviwa kwa nani? Hakuna hukumu inatolewa hewani ama kwenye vyomboo vya habari. Hapa naona tunaambiwa wadaiwa ni MAT na Jumuiya ya Madaktari na mdai ni Serikali kwa hiyo uamuzi huu/amri hii ungepelekwa kwa Viongozi hivyo vyama ili kutekeleza amri ya mahakama. Na uamuzi huo ulitakiwa utolewe na mahakama ukiwa na seal ya mahakama ili uweze kuheshimiwa na siyo Ofisi ya Waziri Mkuu (Mdai) kutoa amri kwa Mdaiwa. Tungepata tamko lenyewe la mahakama tuone linasemaje. Kwa hiyo hapo juu hakuna tamko wa hukumu ya mahakama ni maneno tu yameandikwa na hiyo Ofisi (kama ni kweli).
 
Hii thread mi nawasiwasi nayo sana maana hiyo mahakama imekaa saa ngapi?jana usiku?km usiku basi hiyo si mahakama maana hakuna mahakama inayofanya kazi usiku,anwani nilitegemea kuwa ingekua ya mahakama ss cha ajabu ni kinyume au huyu jaji ni rweyamamu yule wa ikulu?i dont believe this scrap ngoja nimsubiri kiongozi wa nchi jioni saa kumi akiongea na wazee wa dar atatoa tamko gani
 
something is wrong...


I agree, something is very very very wrong. Mgomo haukuanza jana, kwa nini hukumu itolewe usiku usiku, tena na ofisi ya Waziri mkuu? separation of powers ... in reverse!
 
Tanzania yangu Ee Mungu!
Kwanini Unayaruhusu?
Yatusononeshe moyoni
Kwani umeyaruhusu?

Kwakuwa mmekuwa mkiaminishwa kwamba serikali hii imetokana na ninyi wananchi, kwamba ni waajiriwa wenu, inakuwaje tena muajiriwa anakuwa na nguvu kuliko mwajiri?? hii bila shaka ipo Tanzania tu katika hii sayari.

Kwamba serikali iko tayari kuona maelfu ya watanzania wanakufa ili tu haji mponda na lucy nkya waendelee kulamba posho za uwaziri.

Nilishasema tangu mapema kwamba, kwanini kikwete asiwahamishie wizara nyengine mponda na nkya ili mazungumzo baina yao yaendelee ili kuepusha madhara kwa wagonjwa, lakini hakuna anayesikia na bahati mbaya sana wananchi nao wamelala huku serikali ikichezea maisha yao.
 
Ikiwa tangazo hili halijaeditiwa basi madaktari wanayo haki ya kuishitaki mahakama pamoja na waziri mkuu kwa kuwahadaaa wananchi pamoja na madaktari. What a shame................. Kwanza haina hana nembo.

halijakaa vyema tangazo lao............tusubiri wachambuzi
 
Imetolewa na ofisi ya Waziri Mkuu!!! duuu......nchi hii bana.
 
Jamani hii HUKUMU ama ZUIO lime serviwa kwa nani? Hakuna hukumu inatolewa hewani ama kwenye vyomboo vya habari. Hapa naona tunaambiwa wadaiwa ni MAT na Jumuiya ya Madaktari na mdai ni Serikali kwa hiyo uamuzi huu/amri hii ungepelekwa kwa Viongozi hivyo vyama ili kutekeleza amri ya mahakama. Na uamuzi huo ulitakiwa utolewe na mahakama ukiwa na seal ya mahakama ili uweze kuheshimiwa na siyo Ofisi ya Waziri Mkuu (Mdai) kutoa amri kwa Mdaiwa. Tungepata tamko lenyewe la mahakama tuone linasemaje. Kwa hiyo hapo juu hakuna tamko wa hukumu ya mahakama ni maneno tu yameandikwa na hiyo Ofisi (kama ni kweli).

Kama wanavyodai kwamba kikwete ni mzuri isipokuwa watendaji wake ndio wanamuangusha, basi katika muktadha huo huo tuseme waziri mkuu ni mtendaji mzuri isipokuwa wasaidizi wake ndio wanamuangusha?

Kwamba hiyo "hukumu" kutoka "mahakama kuu divisheni ya kazi ofisi ya waziri mkuu", waziri mkuu mwenyewe hakushirikishwa katika kuiandaa, wala hakuiona na wala hakushirikishwa katika kufikia uamuzi wa kuitengeneza na namna ya kuitoa kwa public pamoja na watuhumiwa madaktari!!??

This is simply a sign of "frustrated government".
 
Hii notice isije ikawa kama posho za wabunge ifikie sehemu kila mmoja aseme hakuiandika yeye.

Nasikia leo Mkuu wa Kijiji ameandaa mkutano ahutubie wale wacheza bao wa mwebe yanga kuhusu mgomo wa madaktari. He is now seeking public sympathy. Hivyo vibabu si sehemu ya mgogoro sioni sababu ya kuacha kuwahutubia madaktari badala yake ahutubie vibabu.
 
Kama wanavyodai kwamba kikwete ni mzuri isipokuwa watendaji wake ndio wanamuangusha, basi katika muktadha huo huo tuseme waziri mkuu ni mtendaji mzuri isipokuwa wasaidizi wake ndio wanamuangusha?

Kwamba hiyo "hukumu" kutoka "mahakama kuu divisheni ya kazi ofisi ya waziri mkuu", waziri mkuu mwenyewe hakushirikishwa katika kuiandaa, wala hakuiona na wala hakushirikishwa katika kufikia uamuzi wa kuitengeneza na namna ya kuitoa kwa public pamoja na watuhumiwa madaktari!!??

This is simply a sign of "frustrated government".

Mkuu Mwita mimi nachelea kuiongelea kwa undani hii taarifa; sijui inaenda kwa nani na ati imetolewa na ofisi ya waziri mkuu. Kitu kingine ambach huwa sitaki kukubaliana nacho ni hicho cha kwamba mtu fulani ni mzuri lakini wasaidizi wake ndio hawamsaidii! Kama hawamsaidii si awafute kazi mara moja kwa kuwa huwa halazimishwi kuwa nao.

Radio One wanatoa taarifa kama ya Vimon. Ila hawajasema taarifa imesainiwa na nani. Tusubiri tuone
 
Back
Top Bottom