Chief Isike
JF-Expert Member
- Jan 17, 2010
- 445
- 462
Wakuu ingawa mawasiliano na makamanda walioko field huko Tabora katika Operesheni Chukua Igunga (OCI), si mazuri sana, bado tumeweza kupata walau taarifa kidogo juu ya kinachoendelea. Taarifa zilizopo ambazo zilipatikana kabla mawasiliano hayajakatika kabisa zilikuwa zinaonesha maendeleo mazuri kwa OCI. Jana (katika siku ya pili) makamanda hao, baadhi yao kutoka makao makuu wakisaidiana na makamanda wa huko, waligawanyika katika timu kama nane hivi, wakishambulia tarafa kadhaa kwa mpigo.Mathalani katika katika vijiji vya Mwamashimba na Mwamakona, kulikuwa na mikutano mizuri sana. Naambiwa na mtoa taarifa kuwa wanavijiji wengine wanatoa machozi kila wanapopigwa dozi juu ya local issues zinazowasumbua na jinsi zilivyo na uhusiano na utawala mbovu wa CCM kwa miaka 50 baada ya uhuru. Wakuu hii ya kuwatoa machozi wahudhuriaji mkutano nimeishuhudia sana katika mikutano ya hawa jamaa. Mara ya mwisho nilimwona Mkurugenzi wa Bunge na Halmashauri, Bw. John Mrema niliwashuhudia akiwatoa machozi akina mama pale Mzumbe, Morogoro. Taarifa zinaongeza kuwa OCI pale Mwamashimba ni kama vile ilichukua kijiji kizima, kwa jinsi walivyopigania kadi wakitaka kujiunga katika course for change kupitia people's power. Nitaendelea kuwapatia vitu kadri ya muda...