TANMO
JF-Expert Member
- Apr 12, 2008
- 11,514
- 11,277
Mwanafunzi wa Afrika aliyemaliza digrii yake na kulowea nchini Urusi akifanya biashara ya kuuza matikiti maji anataka kufuata nyayo za Barack Obama kwa kufanya vitu ambavyo haviwezekani kwakuwa mweusi wa kwanza kuingia kwenye siasa za nchini Urusi nchi ambayo ina kiwango kikubwa cha ubaguzi wa rangi.
Mkulima aliyezaliwa barani Arfrika anataka kufanya miujiza ya kuwa mweusi wa kwanza kuingia kwenye siasa ya nchini Urusi baada ya kupata changamato ya Barack Obama kuwa rais wa kwanza wa Marekani.
Joaquim Crima mwenye umri wa miaka 37, alizaliwa nchini Guinea Bissau na baadae kuanzisha makazi yake kusini mwa Urusi baada ya kumaliza digrii yake ya kwanza nchini humo na kuoa mwanamke wa Urusi.
Crima ana nia ya kuwaletea maendeleo watu wa wilaya yake na kutokomeza rushwa kwenye wilaya hiyo iliyopo kwenye ukanda wa mto Volga.
Kutokana na ndoto zake za kuleta mabadiliko kwenye nchi hiyo ambayo ina kiwango kikubwa cha ubaguzi wa rangi, Crima amebatizwa jina la "Obama wa Urusi".
"Nampenda Obama kama mwanasiasa ambaye amethibitisha kuwa hakuna kitu kigumu duniani" alisema Crima na kuongeza "Nafikiri naweza kujifunza baadhi ya vitu kutoka kwake".
Crima ambaye pamoja na kuwa na digrii yake alikuwa akiuza matikiti maji kabla ya kuingia kwenye siasa, amefanikiwa kuwavutia watu wengi hata hivyo bado ana kazi kubwa ya kuwabadilisha mawazo warusi ambao hawataki kuwa na kiongozi mweusi.
"Alikuwa akiuza matikiti maji na ghafla sasa anataka kuwa kiongozi wetu, Urusi ina wageni wengi hatutaki wageni zaidi, Urusi haiko tayari kuwa na viongozi weusi" alisema mkazi mmoja wa wilaya hiyo.
"Ni bora akarudi Afrika akauze matikiti maji yake, hana nafasi nchini Urusi, hatuhitaji Obama mwingine hapa" alisema mkazi mwingine wa wilaya hiyo.
Crima ambaye analonga kirusi kama kazaliwa Urusi vile, ni vigumu sana kwake kuchaguliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Srednyaya Akhtuba yenye wakazi 55,000 sio tu kutokana na upeo wake mdogo kwenye siasa bali pia kutokana na kwamba yeye ni mweusi na lazima atakabiliwa na ubaguzi wa rangi.
Mwezi disemba mwaka jana, mwanafunzi mmoja mweusi toka Marekani aliyekuwa akisoma nchini humo, aliuliwa kwa kuchomwa kisu katika mji wa Volgograd katika kile kinachoaminika kuwa ni chuki za ubaguzi wa rangi.
Crima kwa upande wake ili kujiweka salama, wakati wote wa kampeni zake hutembea na kaka wa mke wake mzungu mwenye asili ya Armenia ambaye ni baunsa kama mlinzi wake.
Crima ana shamba la eka 55 nchini humo ambalo amelima matikiti maji. Amewaajiri jumla ya watu 20 kumsaidia kazi za shambani. Mkewe ndiye anayeuza matikiti maji hayo.
"Kiongozi wa wilaya hii yuko madarakani kwa miaka 10 sasa lakini hajafanya chochote cha maendeleo. Familia nyingi zinahitaji makazi, maji na barabara hakuna" alisema Crima na kuongeza "Mabadiliko yanahitajika katika wilaya hii na Urusi kwa ujumla".
Crima alimalizia kampeni zake kwa kusema "Yes We Can" akiiga kibwatizo cha rais wa Marekani Barack Obama.
Chanzo cha habari Nifahamishe
Mkulima aliyezaliwa barani Arfrika anataka kufanya miujiza ya kuwa mweusi wa kwanza kuingia kwenye siasa ya nchini Urusi baada ya kupata changamato ya Barack Obama kuwa rais wa kwanza wa Marekani.
Joaquim Crima mwenye umri wa miaka 37, alizaliwa nchini Guinea Bissau na baadae kuanzisha makazi yake kusini mwa Urusi baada ya kumaliza digrii yake ya kwanza nchini humo na kuoa mwanamke wa Urusi.
Crima ana nia ya kuwaletea maendeleo watu wa wilaya yake na kutokomeza rushwa kwenye wilaya hiyo iliyopo kwenye ukanda wa mto Volga.
Kutokana na ndoto zake za kuleta mabadiliko kwenye nchi hiyo ambayo ina kiwango kikubwa cha ubaguzi wa rangi, Crima amebatizwa jina la "Obama wa Urusi".
"Nampenda Obama kama mwanasiasa ambaye amethibitisha kuwa hakuna kitu kigumu duniani" alisema Crima na kuongeza "Nafikiri naweza kujifunza baadhi ya vitu kutoka kwake".
Crima ambaye pamoja na kuwa na digrii yake alikuwa akiuza matikiti maji kabla ya kuingia kwenye siasa, amefanikiwa kuwavutia watu wengi hata hivyo bado ana kazi kubwa ya kuwabadilisha mawazo warusi ambao hawataki kuwa na kiongozi mweusi.
"Alikuwa akiuza matikiti maji na ghafla sasa anataka kuwa kiongozi wetu, Urusi ina wageni wengi hatutaki wageni zaidi, Urusi haiko tayari kuwa na viongozi weusi" alisema mkazi mmoja wa wilaya hiyo.
"Ni bora akarudi Afrika akauze matikiti maji yake, hana nafasi nchini Urusi, hatuhitaji Obama mwingine hapa" alisema mkazi mwingine wa wilaya hiyo.
Crima ambaye analonga kirusi kama kazaliwa Urusi vile, ni vigumu sana kwake kuchaguliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Srednyaya Akhtuba yenye wakazi 55,000 sio tu kutokana na upeo wake mdogo kwenye siasa bali pia kutokana na kwamba yeye ni mweusi na lazima atakabiliwa na ubaguzi wa rangi.
Mwezi disemba mwaka jana, mwanafunzi mmoja mweusi toka Marekani aliyekuwa akisoma nchini humo, aliuliwa kwa kuchomwa kisu katika mji wa Volgograd katika kile kinachoaminika kuwa ni chuki za ubaguzi wa rangi.
Crima kwa upande wake ili kujiweka salama, wakati wote wa kampeni zake hutembea na kaka wa mke wake mzungu mwenye asili ya Armenia ambaye ni baunsa kama mlinzi wake.
Crima ana shamba la eka 55 nchini humo ambalo amelima matikiti maji. Amewaajiri jumla ya watu 20 kumsaidia kazi za shambani. Mkewe ndiye anayeuza matikiti maji hayo.
"Kiongozi wa wilaya hii yuko madarakani kwa miaka 10 sasa lakini hajafanya chochote cha maendeleo. Familia nyingi zinahitaji makazi, maji na barabara hakuna" alisema Crima na kuongeza "Mabadiliko yanahitajika katika wilaya hii na Urusi kwa ujumla".
Crima alimalizia kampeni zake kwa kusema "Yes We Can" akiiga kibwatizo cha rais wa Marekani Barack Obama.
Chanzo cha habari Nifahamishe