dong yi
JF-Expert Member
- Jan 31, 2016
- 5,470
- 7,443
alafu mwenye nyumba hanunui umeme wala halipi bili ya majiShida ya nyumba za hivyo ni kwenye umeme ukikatika usumbufu wa kununua mwingine ni mkubwa sana
alafu mwenye nyumba hanunui umeme wala halipi bili ya majiShida ya nyumba za hivyo ni kwenye umeme ukikatika usumbufu wa kununua mwingine ni mkubwa sana
Taulo anavaa baba mwenye nyumba tu wengine mlitie begani
chupi kujaa kamba. LolUkiibiwa hawajui aliyeiba ila ingiza mwanamke atajulikana mtaa mzima
yule jirani yangu wa kufua chupi tu na kujaza kamba bado yupo
bado nawakomesha kwa kuchoma viungo vya pilau kila ninapopata nafasi
Njoo Tandale
Wiki ijayo naachia chumba
Hapa umeme raundi ni 1000 kila mtu,
Tupo 9 na mwenye nyumba ni wa 10,
Maji tunanunua kwa mwenye nyumba ndoo 150
Usafi haubagui unafagia mpaka uwani kwa mwenye nyumba,
Ukipika chakula unagawa nyumba kubwa
Ukipendeza uwe tayari kwa interview,ukipauka ujiandae kwa madongo
Karibu Tandale, nahamia komakoma
LolUnywe bia huku unadeni la Kodi ya nyumba??? My God!?
tanga nako kuna balaa ila sio km dar!Mi niliishi maandazi Rd msasani nyumba yote wapemba tupu kasoro Mimi, nikirudi mida yangu saa 5 Hadi 7 usiku nikifika najiandaa kuoga bafu halikuwa na paa unaingia bafuni mlangoni bonge la paka nyuma ya nyumba makaburi kibao ukiweka sabun ukigusa ukuta tu unapigwa shoti ya umeme balaa, chumbani kwangu kumbe faza hausi was urithi huwa Ana funguo wake akitoka chanika anakuja kulala mchana chumbani kwangu na kusikilizia mziki nilikuwa na Sony music double speaker akaiba spika moja nikamdai akapotezea akaleta friza yake ndani yaani akaanza kunifukuza pole pole nikaamua kuhama na redio yangu na spika 1 iliyobaki na friji lake nikabeba ngoma ikawa droo...***** hapa nilipo Nina PHD ya nyumba za kupanga dar, mza na tanga
hii mbaya mkuuNilipanga nyumba moja maeneo ya Argentina sasa mwenye nyumba ni mmama anaishi na mwanae wa kike na mdogo wake kila siku vitimbi aisee Mara kufagia mara oooh mbona hatumuoni wifi Mara mkwe yote ilikuwa zuga nikaona ushenzi huu nikachapa kuanzia mama,mtoto,na mdogo wa mama mwenye nyumba siku sikia tena hata kudaiwa kodi mwisho wa siku nikahamia kimara nikaona watashtuka sinaga mazoea ya kijinga
Uwwwiii hiyo nyama unaipika kwenye sufuria ya nani ???na utaitoa WAP???hapo utakuwa unajikomoa mkaa unapotea bure kuchemsha nyama ya pakaNaoika nyama ya paka tuu, halafu najifanya nipo bussy na mambo mengine, nawaacha wadokoe wakimaliza ndio nawaambia hiyo nyama ya nini
Leo Jumamosi nimelala hadi saa mbili ile nashtuka toka kwenye usingizi mzito namsikia baba mwenye nyumba " Hivi inawezekana mpaka saa hizi mtu hajaamka?" kisa sijazima taa za nje, yaani kanikera! yaani nisilale kisa taa? usipowasha maneno anakugongea, jamani, nyumba za kupanga sio.
kwa maendeleo ya kiteknolojia yaliyofikiwa vyote vinawezekanaunataka kuoa au kuolewa ?
😁😁Mshua alipangaga mahali hivi,mama mwenye nyumba ni bahili mno alikuwa anaachiwa pesa ya mboga na mmewe lakini yeye mboga hapiki. Ikifika tu mida ya saa saba saba utasikia "shiimboni, utakua na akiba ya mchuzi kidogo baba angu ?". Nyumba ilikua inawapangaji wengi sana zaidi ya kumi, akikuomba mboga leo ,kesho haji tena anaenda kwa mwingine. Wiki ijayo anaanza tena na yule aliyemuomba mwanzo wa wiki iliyoisha. Kuna watu hawajaumbwa na aibu asee,daily anazunguka na bakuli lake kuomba mboga kwa wapangaji. Mumewe alipokuja kupata taarifa,mwanamke alipigwa mikanda ya maana wachaga wanakung'uta sio poa. Tangu siku hiyo hakurudia tena tabia yake ya kuzunguka na bakuli kwa wapangaji
Mgambo boy umepanga lini wewe?Nyumba yenye wapangaji zaidi ya 4 sio Nyumbaaa ya kupanga aisee....Nyumba ambayo mwenye nyumba anaishi hapo hapo Sio nyumba ya kupanga....Nyumba ambayo kuna wapangaji au mpangaji wa kirangi mdada ukipanga jiandae Kwa vita na maneno kama huwezi usipange......
Nimepanga mbona kitambo..Mgambo boy umepanga lini wewe?
SawaNimepanga mbona kitambo..
Leo Jumamosi nimelala hadi saa mbili ile nashtuka toka kwenye usingizi mzito namsikia baba mwenye nyumba " Hivi inawezekana mpaka saa hizi mtu hajaamka?" kisa sijazima taa za nje, yaani kanikera! yaani nisilale kisa taa? usipowasha maneno anakugongea, jamani, nyumba za kupanga sio.
kunakua na foleni kabisa mkuu....Sojui mtu wa mwisho anaenda kuoga saa ngapi? Nadhani wana upatu wa kuoga kuwa wa kwanza kwa ratiba