Nyumba yenye thamani ya Tshs. Trillion 1 hapa bongo

Nyumba yenye thamani ya Tshs. Trillion 1 hapa bongo

Kwanza nitoe pole kwa watanzania kwa msiba mzito uliotukuta.
Hivi kuna nyumba yenye thamani ya tshs. Trillion 1 hapa Tanzania?
Tunabishana hapa baada ya tajiri mkubwa India kumiliki mjengo wa ghorofa 7 wenye thamani ya trillion 2.3 za kobongo.
Kuna jamaa anadai posta na k.koo kuna mijengo ya thamani hiyo.
Wanaojua ukweli watujuze. Ikibidi watupe pia orodha ya majengo ya gharama zaidi duniani na bongo pia. Karibuni.
Huyo anayekuambia dar kuna nyumba ya trillion moja hana uelewa wa hela ansfikiria trillion moja ni hela ya mchezo
 
Yah trillioni 1 sio mchezo. Ni zaidi ya budget za wizara kadhaa Tanzania. Hichi kitita ukila kila siku 1M utaitumbua kwa miaka zaidi 2,000 na ushee.

Kuwa billionaire $ ni kipaji.
Kwa mwaka 2019/2020 budget za baadhi ya wizara zilikua:

Wizara ya Habari,Utamaduni Sanaa na Michezo=Tsh. 30.88bil

Wizara ya madini=Tsh 49.46bil

Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake=TshSh148.8bil

Viwanda na biashara=Tsh 100.38bil

Wizara ya sheria=Tsh 55.18bil

Mambo ya nje=Tsh 166bil

Wizara ya Kilimo= Tsh 253.85 bilioni

Ukijumlisha hizo budget za hizo wizara 7 unapata Tsh. Bil 805 na bado zinabaki chenchi kama bil. 195 za kula bata.

Tsh.Trilioni 1 ni pesa nyingi sana mzee.
 
Huyo anayekuambia dar kuna nyumba ya trillion moja hana uelewa wa hela ansfikiria trillion moja ni hela ya mchezo

Hahah kweli mkuu hio pesa ni nyingi sana,hata ikiwa converted kwenda currency yoyote ile.

Wamarekani wenyewe uki invest kati $500,000-$1,000,000 na ukazalisha ajira za watu 10 wanakupa u-kaazi and eventually uraia utapata.,sembuse hio Tsh 1 tril(into usd).
 
Daah na sijui itakua lini hio mkuu,ila tutafika mdogo mdogo.

Burundi wenyewe Total budget yao 2019/2020 ni $824.84 million,hapo na hela za misaada+mikopo zimejumlishwa.,hahah.

Hapo ndo hua najua kweli bado tunazungukwa na nchi maskini sana mkuu.

Anyway,tusifanye mchezo na Tsh tril. 1 ni pesa nyingi sana mkuu.
Safi sana kwa kuleta data. Upo vizuri. Nchi yetu bado maskini sanaaaaa. Siku tajiri namba 1 wetu akifika trillion 20 au 30 kama nchi tutaingia uchumi wa kati.
 
Hahah mzee baba hakuamini bongo hii hii kuna hotel ya 8mil/day pamoja na kubana kote hahah,kuna hotel flani iko kule Serengeti minimum room rate ni $2100/day na through out the year iko booked kwa 90% na sio hata wazungu ndo wanaijaza karibu 40% ni wabongo tu wanaenda zao kula good time.

Maisha haya yana ma-gap kinyama.
Mi nasemaga kila siku vyuma havijakaza kwa wote
 
Tunabishana hapa baada ya tajiri mkubwa India kumiliki mjengo wa ghorofa 7 wenye thamani ya trillion 2.3 za kobongo.
Kuna jamaa anadai posta na k.koo kuna mijengo ya thamani hiyo.
MATAJIRI: Huku juu kuna view nzuri kweli!, nimeipenda design yako!.
MASIKINI: Ukipewa bil 1 utaruka toka juu ya lile jengo!?..
 
Back
Top Bottom