Nyumba ya Mh. Mariam Kassembe sh. 400mil

Nyumba ya Mh. Mariam Kassembe sh. 400mil

Thamani za nyumba zetu sinema tupu!..........milioni 400? Masasi?

VURUGU+MTWARA+NA+MASASI+%25281%2529.jpg

Ungeliweka na nyumba za majirani zake tuzione
 
kwa kipindi cha muda mfupi aliokaa bungeni anwaeza kusema mali hizo amezitoa wapi. haono kuwa tifauti ni kubwa sana wale walichoma nyumba hiyo, si ajabu walikuwa wanashangaa kuwa mali hizo amezitoa wapi.


Kaka we ni mtu wa mmahenge - tifauti
 
" .... kama wewe (mtangazaji) ulivyo huna kitu hata mimi nimebaki sina kitu chochote sasa" aliongeza kusema Mh. Kassembe... Mwiso wa kunukuu..

Kwa kauli hiyo , huyo Mheshimiwa anaonyesha kuwa kumbe ana dharau kupita maelezo ! Ni Mbunge wa Jimbo au ni wale wa vile Viti Maalum , unawezaje kujua umasikini wa mtu kwa Dk 5 ? Dah! Hizi nyumba ndogo za watu kweli ni balaa .
 
Tuchambue mambo kwa makini. Hivi ni ajabu mbunge kumiliki nyumba ya mil400? Mshahara wake kwa miaka mitano ni mil420 na bado wanachukua mikopo. Kwa hiyo kuwa na vitu hivyo si ajabu. Bodaboda wajue adui yao ni nani, si mbunge wala nyumba wala matrekta ni mfumo. Tupigane kuondoa mfumo si kuharibu mali.

Huyu kilichomponza ni kutochukua hatua yoyote pale bodaboda walipomfikishia kilio chao cha udhalimu na udhalilishaji wanaofanyiwa na polisi. Amepelekewa malalamiko ya hao vijana zaidi ya mara tatu yeye akawaona wajinga akakauka.
 
Milioni mia nne unajenga mjengo wa ghorofa hata tatu,hiyo nyumba yake kama imekula m100, basi mafundi walimchakachua

Ametaka kujikweza tu. Nyumba yenyewe sio kivileeee, kalikuwa kabanda ndo anakamodoa modoa siku hizi. Mashauzi tu. Yatamdhuru.
 
Nadhani tutakujashudia watumishi wetu siku zijazo wakitendewa vitendo vibaya zaidi kama kubakwa n.k na vijana wetu ambao wako irritable kwa kila jambo. Hawaoni nafuu yoyote wala hope ya maisha yao. Hata hizi bodaboda wanazoendesha huwa zinawaletea matatizo makubwa kiafya (fractures, vifua kuuma, kutekwa) huku wakikimbizana kupata kodi za matajiri wao, TRA, matumizi yao na rushwa za polisi barabarani. Iko siku waendesha bodaboda kote nchini watakuja kuungana dhidi ya jambo fulani!!!!!!

Nakubaliana na wewe hapo kwenye RED japo siungi mkono yanayoendelea. Ni haya haya alozungumza Lowasa halafu Kabaka akambeza... Kuna bomu linatengenezwa sasa limeanza kulipuka...Haya ni matokeo ya kuchoshwa ni matokeo ya kukosa ajira...Sinema inaendelea..
 
Mafisadi wenzao wanajenga dsm tuh,huko mwakwao wanajenga viota tuh kuhofia mambo kama hayo,
fanya uhame huko,usikute saiz plan yaoni mkukuchoma hadi nawewe mwenyewe kasembe.
 
Ulianza vyema taarifa yako, lakini baadaye umeharibu kwa kuonyesha wivu wako wazi wazi na siyo hata wa hao bodaboda, uandishi wako unasadifu kuwa unafurahia kuchomwa kwa nyumba na mali nyingine za waheshimiwa hawa. Kuwa na nyumba ya Sh.400ml. kwa Tanzania katika maisha ya leo bado ni maskini, ninaimani kuwa wapo wengi huko mtwara ambao wana nyumba zenye dhamnai maradufu ya hiyo ya 400mill. Ni ajabu kwa msomi kuwa na maono mafinyu hivi na ya kivuvu yaliyojaa wivu.

Nani anajua nyumba hiyo alijenga kwa miaka mingapi? je ulishajiuliza umaskini wako wewe unatokana na nini, je unajituma na kutumia muda wako na akili na maarifa yako kufikiria maendeleo yako au umekalia majungu na taarifa za kimbeya na kichonganishi kama hii. Acha uvivu na wivu usikuwa na mpango tumia muda wako na akili uliyojaliwa kujifunza kwa hao wenye nyumba za 400ml. ili nawe siku moja uweze kuwa na mali nyingi zaidi kuliko zako. Hatuwezi kuacha kujenga Mtwara eti kwa sababu wengi ni maskini. Kwanza nakataa siyo kweli wengi ni maskini bali wameridhika na hali waliyonayo. Maana kama siyo kuridhika wangejituma kufanya kazi kwa bidii ikiwa ni pamoja na kulima kuliko kutaka utajiri bila kufanya kazi.

Katika sakata la vurugu za bodaboda dhidi ya polisi (tigo) kule Masasi watu wameshuhudia vurugu zikibadilisha mwelekeo kutoka kwa polisi hadi viongozi wa CCM na serikali yake Wilayani Masasi kulikopelekea nyumba na majengo yanayomilikiwa na baadhi ya wabunge wa CCM na ofisi za chama cha CCM chenyewe kuchomwa moto na wananchi wenye hasira kutokana na sababu mbalimbali. Miongoni mwa nyumba zilizochomwa moto ni pamoja na za wah. Mariam Kassembe na Ana Abdallah.

"... ndugu mtangazaji, ukiondoa samani za ndani ambazo zote zimeungua, yumba yangu ilikuwa na thamani ya sh. 400mil"
alisikika akisema Mh. Mariam Kasembe wakati akihojiwa na mtangazaji wa kipindi cha patapata cha WAPO redio. Kassembe alivitaja vitu vingine vilivyoharibiwa ni pamoja na matrekta 2, gari na mifugo. " .... kama wewe (mtangazaji) ulivyo huna kitu hata mimi nimebaki sina kitu chochote sasa" aliongeza kusema Mh. Kassembe. Mh. Kasembe anaonekana na yeye hajui kwanini nyumba yake imelengwa pia katika vurugu hizi.

Maswali niliyokuwa najiuliza kuhusu Mh. Kasembe ni kwamba:

1.Wakati yeye akimiliki nyumba hiyo ya 400milioni, matrekta 2 na gari amewafanyia nini vijana (waliochoma nyumba yake) wa Masasi na majirani zake wanaomzunguuza katika kuwaondolea kero zao mabalimbali?

2. Wakati mikoa ya kusini ikilalamikia kutelekezwa na serikali kiuchumi viongozi wao mnamiliki mali kubwa katikati ya watu maskini, hii ni haki? mbona Nyerere hakufanya hivyo kule kwake Mara, Butiama na Msasani?

3. Ina maana kasembe hafahamu kwamba mikoa ya kusini iko nyuma kimaendeleo ikiwa chini ya Serikali inayoongozwa na chama chake tangu tupate uhuru?

4. Ina maana Kassembe hajui kama polisi ni chombo cha dola inayoongozwa na chama chake?

5. Ina maana Kassembe anashindwa kuona uhusiano uliopo kati ya waendesha bodaboda nchini, rushwa ya polisi, umaskini, serikali, wabunge wa chama tawala na chama tawala?

Nadhani tutakujashudia watumishi wetu siku zijazo wakitendewa vitendo vibaya zaidi kama kubakwa n.k na vijana wetu ambao wako irritable kwa kila jambo. Hawaoni nafuu yoyote wala hope ya maisha yao. Hata hizi bodaboda wanazoendesha huwa zinawaletea matatizo makubwa kiafya (fractures, vifua kuuma, kutekwa) huku wakikimbizana kupata kodi za matajiri wao, TRA, matumizi yao na rushwa za polisi barabarani. Iko siku waendesha bodaboda kote nchini watakuja kuungana dhidi ya jambo fulani!!!!!!
 
Wangewachoma moto hawa wanaowatapeli na kuwatumia ingependeza. Maana wamekuwa kimya wanapoona vibaka wakichomwa moto. Heri sasa wananchi wageukie mibaka huenda tutapata ukombozi. Anyways, huenda huu ni mwanzo wa mapinduzi ya kweli ya kurejesha hadhi ya taifa letu.
Katika sakata la vurugu za bodaboda dhidi ya polisi (tigo) kule Masasi watu wameshuhudia vurugu zikibadilisha mwelekeo kutoka kwa polisi hadi viongozi wa CCM na serikali yake Wilayani Masasi kulikopelekea nyumba na majengo yanayomilikiwa na baadhi ya wabunge wa CCM na ofisi za chama cha CCM chenyewe kuchomwa moto na wananchi wenye hasira kutokana na sababu mbalimbali. Miongoni mwa nyumba zilizochomwa moto ni pamoja na za wah. Mariam Kassembe na Ana Abdallah.

"... ndugu mtangazaji, ukiondoa samani za ndani ambazo zote zimeungua, yumba yangu ilikuwa na thamani ya sh. 400mil"
alisikika akisema Mh. Mariam Kasembe wakati akihojiwa na mtangazaji wa kipindi cha patapata cha WAPO redio. Kassembe alivitaja vitu vingine vilivyoharibiwa ni pamoja na matrekta 2, gari na mifugo. " .... kama wewe (mtangazaji) ulivyo huna kitu hata mimi nimebaki sina kitu chochote sasa" aliongeza kusema Mh. Kassembe. Mh. Kasembe anaonekana na yeye hajui kwanini nyumba yake imelengwa pia katika vurugu hizi.

Maswali niliyokuwa najiuliza kuhusu Mh. Kasembe ni kwamba:

1.Wakati yeye akimiliki nyumba hiyo ya 400milioni, matrekta 2 na gari amewafanyia nini vijana (waliochoma nyumba yake) wa Masasi na majirani zake wanaomzunguuza katika kuwaondolea kero zao mabalimbali?

2. Wakati mikoa ya kusini ikilalamikia kutelekezwa na serikali kiuchumi viongozi wao mnamiliki mali kubwa katikati ya watu maskini, hii ni haki? mbona Nyerere hakufanya hivyo kule kwake Mara, Butiama na Msasani?

3. Ina maana kasembe hafahamu kwamba mikoa ya kusini iko nyuma kimaendeleo ikiwa chini ya Serikali inayoongozwa na chama chake tangu tupate uhuru?

4. Ina maana Kassembe hajui kama polisi ni chombo cha dola inayoongozwa na chama chake?

5. Ina maana Kassembe anashindwa kuona uhusiano uliopo kati ya waendesha bodaboda nchini, rushwa ya polisi, umaskini, serikali, wabunge wa chama tawala na chama tawala?

Nadhani tutakujashudia watumishi wetu siku zijazo wakitendewa vitendo vibaya zaidi kama kubakwa n.k na vijana wetu ambao wako irritable kwa kila jambo. Hawaoni nafuu yoyote wala hope ya maisha yao. Hata hizi bodaboda wanazoendesha huwa zinawaletea matatizo makubwa kiafya (fractures, vifua kuuma, kutekwa) huku wakikimbizana kupata kodi za matajiri wao, TRA, matumizi yao na rushwa za polisi barabarani. Iko siku waendesha bodaboda kote nchini watakuja kuungana dhidi ya jambo fulani!!!!!!
 
Jamani huyu Mbunge alikuwa anapa fursa ya kukupa na ushahidi tunao matrekta yote mawili kakopa SUMA JKT na alikuwa mkulima hivi kupata mali kwa njia ya kilimo ni ufisadi? Hapana na cha kusikitisha zaidi vitu vingi viliporwa na tayari vishaanza kuuzwa hadharani sijuwi km hili ni miongoni mwa matakwa ya wanamtw? Gas na uporoji wapi na wapi?

Ndugu zangu wa mkuti,wapiwapi, mkomaindo, nyasa etc kama kilio gas isiondoke basi fanyeni maandamano yaliyoya kiuungwana ili lengo kuu lisipotee naogopa tusije tukajiingiza katika vita ya chartism na luddism maana nao walishindwa kutambua nani ni mbaya wao is t a system or industries? Mwisho wa ck walichoma moto viwanda lakini mabepari wakaendelea kujenga viwanda vingine ikala KWAO!!!!!!!

Naamini wengi walikuwa wanawaunga mkono kwa maandamano ya amani lakini baada ya kuanza kupora mali, samani za ofc na nk. hapo tunaanza kupata shida.Jiulize swali kwanini mtwara vijijini ambako gas inatoka kule msimbati hawajafanya fujo wala kuchoma halmashauri yao? Why masasi zaidi ya km 240 toka msimbati mumeamua kuchoma halmashauri na magari na kupora computer ambazo zimezagaa mtaani km njugu tena zikiwa na kumbukumbu muhimu sana kwetu.

Leo hii tutaonekana mashujaa ati ukombozi wa kweli unaanzia mtw lakini jana na juzi walikuwa wanatudharau na kutubeza.Hawa wanaotussuport leo kesho watatusaliti. They dont have parmanent friendship, they have permanent interest...tafakari!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kuna ndugu yangu zangu wanasema masasi imegeuka KEKO sasa maama vifaa vya magari, samani mbalimbali hususan computer zilikuwa zinauzwa shs 20000 hadi 5000 tena mali nyingi zikiwa na nembo ya halmashauri na vifaa vingine vimetupwa barabani kupoteza ushahidi. KUMBUKUMBU zote za idara ya elimu msingi na sec hazipo.Kwa bahati nzuri moja ya comp complete imetupwa wapi wapi karibia na LULINDI guest house imeokotwa asb hii na inadata baadhi ya idara ya elimu.

Jamani chonde chonde tusipoteze maana ya hoja muhimu ya maandamano. Our key issue is gas na sio uporaji.
 
Huyu Mbunge ajiulize "ni nyumba ngapi katika jimbo lake zenye thamani kama yake"? Je hilo jumba alijenga kabla ya kupata Ubunge? Je amewasaidiaje wananchi wake kujikwam ua kutoka hali ngumu za maisha?

Huijuwi Masasi wee acha kuandika vitu usivyovijua kuna nyumba nyingi sana tena bora zaidi ya 10000 ukilinganisha na ya mbunge, masasi is a hub of mtwara corriddor na southern corridor. KWA UFUPI Masasi ni miongoni mwa mji bora sana kusini yote. Uliza waliofika Masasi watakujuza peleka umbeya wako FB
 
Kwani kuwa kiongozi ni laana?? Ni kweli baba wa taifa hakuwa na nyumba kwa matashi yake,;-lakini gavana na waziri wake edwin mtei:-alijenga nyumba bora na akaweka misingi yake ya biashara ,hili unalisemeaje???mariam kasembe kafanya kazi ipi ya umma hata leo umsemee nyongo ya kwamba ni heri achomewe nyumba?? By being mbunge kaiba cha nani au kafisadi shirika lipi mpaka ushabikie yeye kuchomewa nyumba??binafsi ningejadili thamani ya hiyo nyumba ya milioni mia nne kwa masasi na muonekano wa nyumba yenyewe,but vyovyote iwavyo waliochoma makazi au nyumba za watu,ni watu wa kulaaniwa,sii watu wa kushabikiwa kupongezwa,ukiwa kama mwanajamii kemea matendo ovu ya aina hii.
 
Nenda masasi na uitishe mkutano wa hadhara na uzungumze haya

Waswahili tuna msemo kuwa "ukweli unauma". Kuna watu wanaweza wakajifanya hawaelewi huu ukweli kuwa kila mwananchi bila kujali nafasi yake katika jamii ana haki ya kuhakikishiwa usalama wa maisha na mali zake. Lakini nakuhakikishia kuwa huko masasi kuna watu wengi hawakubaliani na huu utamaduni wa vikundi vya watu kupora na kuharibu mali za watu wengine kwa kisingizio cha kudai haki zako. Huwezi kupata haki yako kwa kuingilia na kumnyang'anya haki mwenzako. Tutaishia kuwa na jamii kama ya wanyama inayoamini katika dhana ya "mwenye nguvu mpishe" au ile sheria ya porini ya "survival of the fittest".
 
Na wewe unakubaliana na sababu hii?

soma habari kwa makini. bei ya nyumba imefahamika baada ya kuchomwa....wazalendo walichoma kwa kuwa walikuwa na hasira....hata kama ingekuwa ya makuti bado wangechoma coz ni ya gamba ambalo halijawafanyia chochote zaid ya kujilimbikizia...

........
 
Ndo wachome? Sababu ya bei tu?[/QUOTE]

"Ostentation in the midst of destitution"

The late US presdent John F. Kennedy made a remark during his innaguration on january 20th 1961.

"If society can not help the many who are poor; then it can it protect the few who are rich"

TAFAKARI!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

 
Back
Top Bottom