Emma Shimano
Member
- Dec 3, 2012
- 11
- 0
Mh. Lowasa alishasema, tatizo la ajira kwa vijana ni ...........................Mungu saidia watanzania tupate visional leaders.
Thamani za nyumba zetu sinema tupu!..........milioni 400? Masasi?
![]()
Ndo wachome? Sababu ya bei tu?
Ninachokiona hapo ni chuki ya wananchi juu ya baadhi ya wana siasa. Haiwezekani upigane na polisi halafu ukachome nyumba ya mheshimiwa fulani.
Ina maana wananchi hawako pamoja na wana siasa katika mitazamo ya maisha ya kila siku.
Kongosho, ni ndugu yako huyo kasembe
Katika sakata la vurugu za bodaboda dhidi ya polisi (tigo) kule Masasi watu wameshuhudia vurugu zikibadilisha mwelekeo kutoka kwa polisi hadi viongozi wa CCM na serikali yake Wilayani Masasi kulikopelekea nyumba na majengo yanayomilikiwa na baadhi ya wabunge wa CCM na ofisi za chama cha CCM chenyewe kuchomwa moto na wananchi wenye hasira kutokana na sababu mbalimbali. Miongoni mwa nyumba zilizochomwa moto ni pamoja na za wah. Mariam Kassembe na Ana Abdallah.
"... ndugu mtangazaji, ukiondoa samani za ndani ambazo zote zimeungua, yumba yangu ilikuwa na thamani ya sh. 400mil"
alisikika akisema Mh. Mariam Kasembe wakati akihojiwa na mtangazaji wa kipindi cha patapata cha WAPO redio. Kassembe alivitaja vitu vingine vilivyoharibiwa ni pamoja na matrekta 2, gari na mifugo. " .... kama wewe (mtangazaji) ulivyo huna kitu hata mimi nimebaki sina kitu chochote sasa" aliongeza kusema Mh. Kassembe. Mh. Kasembe anaonekana na yeye hajui kwanini nyumba yake imelengwa pia katika vurugu hizi.
Maswali niliyokuwa najiuliza kuhusu Mh. Kasembe ni kwamba:
1.Wakati yeye akimiliki nyumba hiyo ya 400milioni, matrekta 2 na gari amewafanyia nini vijana (waliochoma nyumba yake) wa Masasi na majirani zake wanaomzunguuza katika kuwaondolea kero zao mabalimbali?
2. Wakati mikoa ya kusini ikilalamikia kutelekezwa na serikali kiuchumi viongozi wao mnamiliki mali kubwa katikati ya watu maskini, hii ni haki? mbona Nyerere hakufanya hivyo kule kwake Mara, Butiama na Msasani?
3. Ina maana kasembe hafahamu kwamba mikoa ya kusini iko nyuma kimaendeleo ikiwa chini ya Serikali inayoongozwa na chama chake tangu tupate uhuru?
4. Ina maana Kassembe hajui kama polisi ni chombo cha dola inayoongozwa na chama chake?
5. Ina maana Kassembe anashindwa kuona uhusiano uliopo kati ya waendesha bodaboda nchini, rushwa ya polisi, umaskini, serikali, wabunge wa chama tawala na chama tawala?
Nadhani tutakujashudia watumishi wetu siku zijazo wakitendewa vitendo vibaya zaidi kama kubakwa n.k na vijana wetu ambao wako irritable kwa kila jambo. Hawaoni nafuu yoyote wala hope ya maisha yao. Hata hizi bodaboda wanazoendesha huwa zinawaletea matatizo makubwa kiafya (fractures, vifua kuuma, kutekwa) huku wakikimbizana kupata kodi za matajiri wao, TRA, matumizi yao na rushwa za polisi barabarani. Iko siku waendesha bodaboda kote nchini watakuja kuungana dhidi ya jambo fulani!!!!!!
Sio ndugu, lakini wangeweza kumwajibisha kwa kumnyima kura na si kuchoma nyumba
Huu ni 'uharamia' kama uharamia mwingine tu
Ndo wachome? Sababu ya bei tu?
Million 400/ ahahahaha, hii ni Isidingo
Million 400/ ahahahaha, hii ni Isidingo
ukiona mtu anamtetea mwalifu ujue ananufaika na uhalifu unaofanyika na mhusika!!!
Tatizo sio bei ya nyumba, ila hali ya watu waliochoma hiyo nyumba ukilinganisha na maisha ya Mmiliki wa nyumba hiyo.
Sio ndugu, lakini wangeweza kumwajibisha kwa kumnyima kura na si kuchoma nyumba
Huu ni 'uharamia' kama uharamia mwingine tu
Yaani watunze hasira mpaka 2015?
Kupanga ni kuchagua
Hivi wamefaidika sasa?
Unadhani hawa akina mama walipolia walikuwa wanalilia nyumba zao? La hasha bima italipa......wao walikuwa wanalilia uhai wao wa kisiasa ambao umetoweka!
Kunufaika ama kutonifaika na mhalifu ni pointless hapa
Mmh, kama unaamini hivyo, good for you
Wachomaji walikuwa na yao tu, hata walolaumiwa kwa makanisa walikuwa akina fulani, lakini ukweli ni kundi dogo tu
Siamini katika masuluhisho ya aina hii