Nyumba imejengwa juu ya kaburi la Abushiri bin Salim al Harith

JUU YA KABURI LA BUSHIRI BIN SALIM PAMEJENGWA NYUMBA

Nimesoma historia ya Bushiri nikiwa shule ya msingi miaka ya 1960 pamoja na historia ya Vita Vya Maji Maji vilivyopewa jina la, "Maji Maji Rebellion."

Walioandika historia hii waliwaona Abushiri bin Salim, Abdulrauf Songea Mbano na Bi. Khadija Mkomanile, Mtwa Abdallah Mkwawa kwa kutoa mfano kutoka kundi la viongozi walioongoza vita dhidi ya Wajerumani si chochote ila waasi.

Kama waasi hukumu ya wao kunyongwa ilikuwa stahili yao.

Bushiri alitembezwa nusu uchi katika barabara za Pangani wakati anapelekwa kunyòngwa na huko alikotolewa alipokuwa amefungiwa Bushiri aliwekwa ndani ya chumba akiwa hana nguo.

Bushiri alikuwa kiongozi katika jamii yake aliyoishi na mtu aliyestahika kwa hiyo kumvua nguo hadharani kulikusudiwa kumwondolea heshima yake.

Kiasi cha miaka 20 iliyopita nilifika Pangani kwa nia ya kuzuru kaburi la Abushiri, kuutembelea msikiti ulioingizwa mbwa, kuona msikiti uliong'olewa mlango wa Kizanzibari uliokuwa na aya za Qur'an ukenda kufungwa bar panapouzwa ulevi na mwisho kutafuta baadhi ya nyumba walizoishi wazee wetu tuliopokea historia zao baada ya wao kufariki yapata miaka 100 nyuma.

Hakuna aliyekuwa anajua ni msikiti upi ulioingizwa mbwa enzi za Bushiri lakini nilionyeshwa na nilisali dhuhur katika msikiti uliong'olewa mlango.

Wala sikuwa na haja ya kuuliza kwani ule mlango mpya uliowekwa ulikuwa unachusha kama vile unasema, "Ning'oeni mahali hapa."

Nilifahamishwa na kiongozi mmoja mkuu wa serikali kuwa serikali ilikuwa ipo katika mchakato wa kulitafuta kaburi la Abushiri lakini bado hawajafanikiwa.

Kiongozi huyu wa serikali alinifahamisha kuwa serikali imeamua kulitafuta kaburi la Abushiri kwa sababu watu wengi kutoka nje ya Tanzania wamekuwa wakifika Pangani kwa nia ya kuliona kaburi lake.

Nilifahamishwa kuwa si mbali na Pangani sehemu inayoitwa Mahiwa kuna sehemu Bushiri alikuwa na makazi yake hapo na sehemu hiyo anaishi Mholanzi mmoja.

Nilikwenda hadi Mahiwa na nilipokelewa na huyo Mzungu.

Huyu Muholanzi alikuwa amejenga nyumba yake ya ghorofa moja pembeni ya Mto Pangani na aliniambia kuwa yeye amesikia kutoka kwa wenyeji kuwa Bushiri alipata kuishi hapo ambapo yeye alipojenga.

Sehemu hii imejitenga sana hakuna nyumba yeyote jirani.

Huyu Mzungu hakuwa anajua lolote kuhusu Abushiri ila hili la kunyongwa na Wajerumani.

Inawezekana hapa ndani msituni ndipo Bushiri alipojenga ngome yake na kuweka kambi wakati wa vita ile dhidi ya Wajerumani.

Lakini zipo taarifa kuwa hadi miaka ya 1960 wakati mimi nikiwa mwanafunzi wa shule ya msingi na nikifundishwa historia ya "uasi," wa Abushiri dhidi ya Wajerumani watu wa Pangani walikuwa wanajua wapi alipozikwa Bushiri.

Watu walikuwa wanajua sehemu kaburi la Abushiri lilipo ingawa kaburi lenyewe lilikuwa halionekani kwa kukosa matunzo.

Alipozikwa Abushiri kwa kwa wakati ule mwaka wa 1889 hapo palikuwa pori.

Wajerumani walimzika Abushiri porini pasipokuwa na watu wala makaburi akiwa kijana wa miaka 36.

Wajerumani walimzika Bushiri msituni kutokana na chuki waliyokuwa nayo dhidi yake na kwao wao walichukulia kitendo kile sawa na kufukia kitu kinachoudhi.

Wajerumani wakati wakimzika Bushiri porini, maiti za Wajerumani askari waliouawa na askari wa Bushiri zilizikwa katika viwanja makhsusi vya makaburi kwa heshima zote.

Makaburi haya ya Wajerumani yapo Pangani hadi leo na historia ya vifo vyao inafahamika.

Ukiingia Pangani kwa mara ya kwanza utapigwa na butwaa na utajiri wa historia iliyoko bayana mbele ya macho yako.

Halikadhalika utasikitishwa na magofu ya nyumba zilozojengwa zaidi ya karne mbili zikiachiwa zibomoke hadi zitoweke.

Watu niliowakuta Pangani miaka 20 iliyopita hakuna hata mmoja aliyekuwa anajua historia ya Bushiri kwa ukamilifu wake wala kujua katika nyumba zile zilizobaki magofu Bushiri alikuwa akiishi nyumba ipi.

Lakini nilifanikiwa kuona msikiti wa Ibadh ukiwa bado umesimama katika hali yake ile ilivyokuwa wakati Bushiri katika uhai akisali.

Nilifarajika sana mwenyeji wangu kutoka Tanga aliyenisindikiza Pangani aliponionyesha gofu la nyumba iliyokuwa ya Suleiman Nasr el Lemki aliyekuwa Liwali wa Pangani wakati Bushiri na jeshi lake walipoamua kunyanyua silaha dhidi ya Wajerumani.

Taarifa ni kuwa kaburi la Bushiri bin Salim Al Harith lipo Pangani na sasa kaburi hili halipo tena porini.

Palipimwa kiwanja na mnunuzi wa kiwanja hiki amejenga nyumba yake juu ya kaburi la Abushiri.

Mengi yameandikwa kuhusu Wajerumani walioshiriki katika vita hivi lakini hakuna chochote kilichoandikwa kuhusu askari Waafrika walioletwa Pangani na Hermann von Wissman kutoka Sudan na Mozambique.

Kama Kleist Sykes asingeandika maisha yake na kueleza historia ya baba yake Sykes Mbuwane aliyepigana vita vile Bagamoyo dhidi ya Bushiri historia hii kwa upande wa Waafrika ingekuwa imepunjika pakubww.

Kutokana na kalamu ya Kleist ndipo leo tumefahamu kuwa von Wissman alipoamua kushambulia kambi ya Bushiri iliyokuwa Nzole nje ya Bagamoyo pamojanae alikuwapo Chief Mohosh (Affande Plantan), Sykes Mbuwane Chakulan na Machakaomo kwa kuwataja Wazulu wachache katika Wazulu 400 waliokuwa askari mamluki.

Wissman alishambulia kambi ya Abushiri tarehe 8 May 1889.

Haya majina ya hawa Wazulu waliopigana vita vyao vya kwanza Bagamoyo yapo katika mswada wa kitabu alioandika Kleist kabla hajafa mwaka wa 1949.

Na historia hii yote Kleist aliisikia kutoka kwenye kinywa cha mlezi wake Affande Plantan baba yao Thomas Plantan, Schneider Plantan na Mashado Plantan akaiandika kabla hajafa mwaka wa 1949.

Sishangai kwa nini wanahistoria hawampi Abushiri hapewi heshima sawa na ile anayopewa Mtwa Mkwawa na wala sistaajabu kwa nini jina lake la Abdallah halitosis katika maandishi yao kama vile yalivyokwepwa majina ya Abdulrauf Songea Mbao na Khadija Mkomanile.

Baada vita dhidi ya Bushiri na Mkwawa kumalizika Chief Mohosh sasa akijulikana kama Affande Plantan akafanywa kuwa mkuu wa Germany Constabulary katika Tanganyika.

Affande Plantan alifariki 1914 Vita Vya Pili Vya Dunia vikiwa tayari vimeshaanza na majeshi ya Uingereza yapo ndani ya ardhi iliyokuja kujulikana baada ya vita kama Tanganyika.

Kila ninapokwenda kumsalimu Mwalimu Maunda Plantan mjukuu wa Chief Mohosh, bint ya Mwalimu Thomas Plantan huondoka na jipya ambalo sikupata kulijua kabla.

Picha: Picha ya kitabu kinachoeleza kwa ufupi hali ilivyokuwa Bagamoyo wakati wa mapambano, gofu la nyumba ya Suleiman Nasr el Lemki na mtaa wa biashara Pangani kama ulivyokuwa mwaka wa 1910.

View attachment 1931587

View attachment 1931593

View attachment 1931604
Mwaka 1914 ulikuwa mwanzo wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, na si ya Pili kama ulivyoandika. Pia nashauri uwe unaandika ulivyovipata, kisha maoni yako yawe mwishoni.
 
Mwaka 1914 ulikuwa mwanzo wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, na si ya Pili kama ulivyoandika. Pia nashauri uwe unaandika ulivyovipata, kisha maoni yako yawe mwishoni.
James,
Ahsante sana nimekosea tarehe nitasahihisha.

Kuhusu maoni.

Hupenda kuunganisha hapo kwa hapo ili nisimwache nyuma msomaji.
 
Maandiko yako ni elimishi lakini mara zote huwa yana mlengo wa kidini! Siku zote unaandika kwa namna ya kulalamika.
Trace...
Umesema kweli kabisa.

Wakoloni waliwachukua Waislam kama maadui zao na wakafanya kila hila kuwahujumu.

Hii ndiyo sababu Wajerumani katika Vita Vya Maji Maji waliwanyonga makamanda zaidi ya 60.

Makaburi yao yapo Mahenge, Songea.

Walipokuja Waingereza hali haikubadilika na Waislam wakaunda African Association kuwakusanya Waafrika kwenye umoja ulikuja kuzaa TANU.

Historia hii ilipokuja kuandikwa ilifanyiwa hujuma kubwa.

Nimenyanyua kalamu kusahihisha historia hii kwa kueleza nafasi ya Uislam na Waislam katika kupambana na ukoloni.
 
Mohamed Said, siku moja tuandikie lolote kuhusu Mchungaji Mtilia Christopher
Kiranja,

Screenshot_20210911-161220_Opera.jpg
 
JUU YA KABURI LA BUSHIRI BIN SALIM PAMEJENGWA NYUMBA

Nimesoma historia ya Bushiri nikiwa shule ya msingi miaka ya 1960 pamoja na historia ya Vita Vya Maji Maji vilivyopewa jina la, "Maji Maji Rebellion."

Walioandika historia hii waliwaona Abushiri bin Salim, Abdulrauf Songea Mbano na Bi. Khadija Mkomanile, Mtwa Abdallah Mkwawa kwa kutoa mfano kutoka kundi la viongozi walioongoza vita dhidi ya Wajerumani si chochote ila waasi.

Kama waasi hukumu ya wao kunyongwa ilikuwa stahili yao.

Bushiri alitembezwa nusu uchi katika barabara za Pangani wakati anapelekwa kunyòngwa na huko alikotolewa alipokuwa amefungiwa Bushiri aliwekwa ndani ya chumba akiwa hana nguo.

Bushiri alikuwa kiongozi katika jamii yake aliyoishi na mtu aliyestahika kwa hiyo kumvua nguo hadharani kulikusudiwa kumwondolea heshima yake.

Kiasi cha miaka 20 iliyopita nilifika Pangani kwa nia ya kuzuru kaburi la Abushiri, kuutembelea msikiti ulioingizwa mbwa, kuona msikiti uliong'olewa mlango wa Kizanzibari uliokuwa na aya za Qur'an ukenda kufungwa bar panapouzwa ulevi na mwisho kutafuta baadhi ya nyumba walizoishi wazee wetu tuliopokea historia zao baada ya wao kufariki yapata miaka 100 nyuma.

Hakuna aliyekuwa anajua ni msikiti upi ulioingizwa mbwa enzi za Bushiri lakini nilionyeshwa na nilisali dhuhur katika msikiti uliong'olewa mlango.

Wala sikuwa na haja ya kuuliza kwani ule mlango mpya uliowekwa ulikuwa unachusha kama vile unasema, "Ning'oeni mahali hapa."

Nilifahamishwa na kiongozi mmoja mkuu wa serikali kuwa serikali ilikuwa ipo katika mchakato wa kulitafuta kaburi la Abushiri lakini bado hawajafanikiwa.

Kiongozi huyu wa serikali alinifahamisha kuwa serikali imeamua kulitafuta kaburi la Abushiri kwa sababu watu wengi kutoka nje ya Tanzania wamekuwa wakifika Pangani kwa nia ya kuliona kaburi lake.

Nilifahamishwa kuwa si mbali na Pangani sehemu inayoitwa Mahiwa kuna sehemu Bushiri alikuwa na makazi yake hapo na sehemu hiyo anaishi Mholanzi mmoja.

Nilikwenda hadi Mahiwa na nilipokelewa na huyo Mzungu.

Huyu Muholanzi alikuwa amejenga nyumba yake ya ghorofa moja pembeni ya Mto Pangani na aliniambia kuwa yeye amesikia kutoka kwa wenyeji kuwa Bushiri alipata kuishi hapo ambapo yeye alipojenga.

Sehemu hii imejitenga sana hakuna nyumba yeyote jirani.

Huyu Mzungu hakuwa anajua lolote kuhusu Abushiri ila hili la kunyongwa na Wajerumani.

Inawezekana hapa ndani msituni ndipo Bushiri alipojenga ngome yake na kuweka kambi wakati wa vita ile dhidi ya Wajerumani.

Lakini zipo taarifa kuwa hadi miaka ya 1960 wakati mimi nikiwa mwanafunzi wa shule ya msingi na nikifundishwa historia ya "uasi," wa Abushiri dhidi ya Wajerumani watu wa Pangani walikuwa wanajua wapi alipozikwa Bushiri.

Watu walikuwa wanajua sehemu kaburi la Abushiri lilipo ingawa kaburi lenyewe lilikuwa halionekani kwa kukosa matunzo.

Alipozikwa Abushiri kwa kwa wakati ule mwaka wa 1889 hapo palikuwa pori.

Wajerumani walimzika Abushiri porini pasipokuwa na watu wala makaburi akiwa kijana wa miaka 36.

Wajerumani walimzika Bushiri msituni kutokana na chuki waliyokuwa nayo dhidi yake na kwao wao walichukulia kitendo kile sawa na kufukia kitu kinachoudhi.

Wajerumani wakati wakimzika Bushiri porini, maiti za Wajerumani askari waliouawa na askari wa Bushiri zilizikwa katika viwanja makhsusi vya makaburi kwa heshima zote.

Makaburi haya ya Wajerumani yapo Pangani hadi leo na historia ya vifo vyao inafahamika.

Ukiingia Pangani kwa mara ya kwanza utapigwa na butwaa na utajiri wa historia iliyoko bayana mbele ya macho yako.

Halikadhalika utasikitishwa na magofu ya nyumba zilozojengwa zaidi ya karne mbili zikiachiwa zibomoke hadi zitoweke.

Watu niliowakuta Pangani miaka 20 iliyopita hakuna hata mmoja aliyekuwa anajua historia ya Bushiri kwa ukamilifu wake wala kujua katika nyumba zile zilizobaki magofu Bushiri alikuwa akiishi nyumba ipi.

Lakini nilifanikiwa kuona msikiti wa Ibadh ukiwa bado umesimama katika hali yake ile ilivyokuwa wakati Bushiri katika uhai akisali.

Nilifarajika sana mwenyeji wangu kutoka Tanga aliyenisindikiza Pangani aliponionyesha gofu la nyumba iliyokuwa ya Suleiman Nasr el Lemki aliyekuwa Liwali wa Pangani wakati Bushiri na jeshi lake walipoamua kunyanyua silaha dhidi ya Wajerumani.

Taarifa ni kuwa kaburi la Bushiri bin Salim Al Harith lipo Pangani na sasa kaburi hili halipo tena porini.

Palipimwa kiwanja na mnunuzi wa kiwanja hiki amejenga nyumba yake juu ya kaburi la Abushiri.

Mengi yameandikwa kuhusu Wajerumani walioshiriki katika vita hivi lakini hakuna chochote kilichoandikwa kuhusu askari Waafrika walioletwa Pangani na Hermann von Wissman kutoka Sudan na Mozambique.

Kama Kleist Sykes asingeandika maisha yake na kueleza historia ya baba yake Sykes Mbuwane aliyepigana vita vile Bagamoyo dhidi ya Bushiri historia hii kwa upande wa Waafrika ingekuwa imepunjika pakubww.

Kutokana na kalamu ya Kleist ndipo leo tumefahamu kuwa von Wissman alipoamua kushambulia kambi ya Bushiri iliyokuwa Nzole nje ya Bagamoyo pamojanae alikuwapo Chief Mohosh (Affande Plantan), Sykes Mbuwane Chakulan na Machakaomo kwa kuwataja Wazulu wachache katika Wazulu 400 waliokuwa askari mamluki.

Wissman alishambulia kambi ya Abushiri tarehe 8 May 1889.

Haya majina ya hawa Wazulu waliopigana vita vyao vya kwanza Bagamoyo yapo katika mswada wa kitabu alioandika Kleist kabla hajafa mwaka wa 1949.

Na historia hii yote Kleist aliisikia kutoka kwenye kinywa cha mlezi wake Affande Plantan baba yao Thomas Plantan, Schneider Plantan na Mashado Plantan akaiandika kabla hajafa mwaka wa 1949.

Sishangai kwa nini wanahistoria hawampi Abushiri hapewi heshima sawa na ile anayopewa Mtwa Mkwawa na wala sistaajabu kwa nini jina lake la Abdallah halitosis katika maandishi yao kama vile yalivyokwepwa majina ya Abdulrauf Songea Mbao na Khadija Mkomanile.

Baada vita dhidi ya Bushiri na Mkwawa kumalizika Chief Mohosh sasa akijulikana kama Affande Plantan akafanywa kuwa mkuu wa Germany Constabulary katika Tanganyika.

Affande Plantan alifariki 1914 Vita Vya Kwanza Vya Dunia vikiwa tayari vimeshaanza na majeshi ya Uingereza yapo ndani ya ardhi iliyokuja kujulikana baada ya vita kama Tanganyika.

Kila ninapokwenda kumsalimu Mwalimu Maunda Plantan mjukuu wa Chief Mohosh, bint ya Mwalimu Thomas Plantan huondoka na jipya ambalo sikupata kulijua kabla.

Picha: Picha ya kitabu kinachoeleza kwa ufupi hali ilivyokuwa Bagamoyo wakati wa mapambano, gofu la nyumba ya Suleiman Nasr el Lemki na mtaa wa biashara Pangani kama ulivyokuwa mwaka wa 1910.

View attachment 1931587

View attachment 1931593

View attachment 1931604
Japo huwa napingana na mlengo wako, hakuna shaka. Abushiri alikuwa shujaa na bado ni shujaa wetu. Historia mara nyingi, kama alivyowahi kusema Winston Churchill, huandikwa na washindi. Hivyo, hupotosha mambo mengi ya msingi. Adui yako anapoandika historia yako, lazima atakudhoofisha na kukusingizia. Hii ndiyo maana historia hufanyiwa marejeo, marekebisho hata kuandikwa upya inapobidi.RIP SHUJAA ABUSHIRI BIN SALUM
 
Mzee Mohamad Said, asante kwa taarifa yako. Nimesoma sasa hivi taarifa tofauti. Kuna kitabu cha Kijerumani kilichoandikwa na H.F. von Behr, luteni katika kikosi cha Wissmann kilichokandamiza upinzani wa watu wa pwani manmo 1888/1889. Kitabu ni "Kriegsbilder aus dem Araberaufstand in Deutsch-Ostafrika, Leipzig 1891", pamoja utangulizi uliotungwa na Wissmann. (yaani "Kumbukumbu ya vita wakati wa uasi wa Waarabu katika Afrika ya Mashariki ya Kijerumani)
Kinapatikana kupitia google-books.
Mlango wa 15 na wa mwisho unaitwa "Kukamatwa na kifo cha Bushiri". (uk. 329-336)
Kufuatana na taarifa hiyo, kwenye Disemba 1889 kombania mbili za askari chini ya kapteni Schmidt kilimfuata Abushiri hadi "Muenda" kwenye eneo la "Nguru" (yaani Ungulu) . Hapa walishambulia kambi la Abushiri aliyeweza kukimbia. Tarehe 7 Disemba Schmidt alipata ujumbe kutoka jumbe Magaya kuwa Bushiri alikamatwa mahali panapoitwa "Quamkoro" ; kufuatana na taarifa ya Behr maili 20 za Kijerumani, yaani kilomita 140 kutoka "Muenda".
(Kwenye ramani ya google naona eneo la msitu wa Kwamkoro, kati ya Muheza na Korogwe; "Muenda" sijakuta; "majumbe" walikuwa ama machifu wadogo au viongozi ya eneo dogo waliopewa nafasi yao na Sultani )

Walimkuta Abushiri katika nyumba moja alipofungwa. Behr alieleza alikuwa nusu-uchi, akivaa kikoi pekee, mikono na miguu ikifungwa kwa nyoro za chuma; kichwa kilifungwa katzika uma ya mti jinsi ilivyokuwa kawaida kwa watumwa waliosafirishwa. Walimpeleka Pangani wakimweka juu ya punda (Behr aliandika Abushiri alikuwa na miguu iliyovimba ).
Behr anasimulia jinsi Abushiri alihojiwa na Wissmann aliyefika na jinsi alivyonyongwa mnamo saa 10 tarehe 15 Disemba. Baada ya kifo walifika ndugu zake wakapewa mwili wakazika usiku uleule.
Naongeza picha iliyopo baada ya ukurasa 331. Maelezo yake ni "Buschiri's Gefangennahma" (Kukamatwa kwa Abushiri). Kitabu hakina maelezo picha zilichorwa na nani; kama ni kweli, walimpa blanketi avae baada ya kumtoa kutoka kitanda alipofungwa, akisimama pamoja na afande na askari Wanubi.
1631454585954.png
 
Mzee Mohamad Said, asante kwa taarifa yako. Nimesoma sasa hivi taarifa tofauti. Kuna kitabu cha Kijerumani kilichoandikwa na H.F. von Behr, luteni katika kikosi cha Wissmann kilichokandamiza upinzani wa watu wa pwani manmo 1888/1889. Kitabu ni "Kriegsbilder aus dem Araberaufstand in Deutsch-Ostafrika, Leipzig 1891", pamoja utangulizi uliotungwa na Wissmann.
Kinapatikana kupitia google-books.
Mlango wa 15 unaitwa "Kukamatwa na kifo cha Bushiri". (uk. 329-336)
Kufuatana na taarifa hiyo, kwenye Disemba 1889 kombania mbili za askari chini ya kapteni Schmidt kilimfuata Abushiri hadi Muenda kwenye eneo la "Nguru" (yaani Ungulu) . Hapa walishambulia kambi la Abushiri aliyeweza kukimbia. Tarehe 7 Disemba Schmidt alipata ujumbe kutoka jumbe Magaya kuwa Bushiri alikamatwa mahali panapoitwa "Quamkoro" ; kufuatana na taarifa ya Behr maili 20 za Kijerumani, yaani kilomita 140 kutoka Muenda.
(Kwenye ramani ya google naona eneo la msitu wa Kwamkoro, kati ya Muheza na Korogwe)

Walimkuta Abushiri katika nyumba moja alipofungwa. Behr alieleza alikuwa nusu-uchi, akivaa kikoi pekee, mikono na miguu ikifungwa kwa nyoro za chuma; kichwa kilifungwa katzika uma ya mti jinsi ilivyokuwa kawaida kwa watumwa waliosafirishwa. Walimpeleka Pangani wakimweka juu ya punda (Behr aliandika Abushiri alikuwa na miguu iliyovimba ).
Behr anasimulia jinsi Abushiri alihojiwa na Wissmann aliyefika na jinsi alivyonyonyongwa mnamo saa 10 tarehe 15 Disemba. Baada ya kifo walifika ndugu zake wakapewa mwili wakazika usiku uleule.
Naongeza picha iliyopo baada ya ukurasa 331. Maelezo yake ni "Buschiri's Gefangennahma" (Kukamatwa kwa Abushiri). Kitabu hakina maelezo picha zilichorwa na nani; kama ni kweli, walimpa blanketi avae baada ya kumtoa kutoka kitanda alipofungwa.
Mwana...
Nakushukuru sana kwa taarifa hii yako.
Kuna baadhi nilikuwa nimeyasikia lakini yamepotoshwa kidogo.

Kukamatwa kwake nimesoma ni kuwa alisalitiwa na jamaa mmoja kabila Mzigua.

Wakati huo Bushiri aliwekewa dau la rupia nyingi kwa mtu atakaemkamata.

Bushiri taarifa hiyo alikuwa yuko njiani akijaribu kukimbilia Mombasa.

Iko picha ninayo mahali ya Bushiri kavaa blanketing.

Ahsante sana.
 
Mwana...
Nakushukuru sana kwa taarifa hii yako.
Kuna baadhi nilikuwa nimeyasikia lakini yamepotoshwa kidogo.

Kukamatwa kwake nimesoma ni kuwa alisalitiwa na jamaa mmoja kabila Mzigua.

Wakati huo Bushiri aliwekewa dau la rupia nyingi kwa mtu atakaemkamata.

Bushiri taarifa hiyo alikuwa yuko njiani akijaribu kukimbilia Mombasa.

Iko picha ninayo mahali ya Bushiri kavaa blanketing.

Ahsante sana.
Huyu Magaya aliyemkamata kuwa Mzigua nimesoma kwa Iliffe, Modern History of Tanganyika, uk.96f.
Ile uliyoandika juu kuwa Wajerumani walitaka kuficha kaburi lake sijaona uthibitisho; kufuatana na Behr ndugu zake walimzika.
Behr mwenyewe katiba kitabu chake anampa heshima kiasi akisifu uwezo wake kama kiongozi wa pekee aliyewapa Wajerumani matatizo makubwa.
Binafsi sijaelewa bado kwa nini walitaka kumnyonga wakati walimsamehe Bwana Heri bin Juma kiongozi wa Saadani. Labda kwa sababu walipaswa kufuata propaganda yao (maana walipata kibali cha bunge la Ujerumani tu kwa kudai, eti hapa ni vita ya kupambana na Waarabu wafanyabiashara wa watumwa) ? Au kwa sababu Wissmann alikumbuka msaada wa Bwana Heri aliopata miaka ya nyuma? Au kwa sababu hakumwona Bwana Heri kama "Mwarabu"? Labda kwa sababu Abushiri hakuwa tena na wafuasi wengi lakini Bwana Heri alikuwa na kundi kubwa hivyo waliona afadhali wapatane naye?(ona zaidi hapa Bwana Heri - Wikipedia, kamusi elezo huru)
 
Nimenyanyua kalamu kusahihisha historia hii kwa kueleza nafasi ya Uislam na Waislam katika kupambana na ukoloni.
Kwani mkuu kuna hujuma zozote zinafanywa kuonesha kua waislamu hawakupambania uhuru??

Mimi naona hostoria zinaelezea utaifa zaidi na sio udini zaidi, mfano hao wapigania uhuru na kama hao kina bushir, mkwawa wanatajwa tu majina yao na sio dini zao labda tu watatajwa kanda wanazotoka.

Imekuaje unalalama hivi kuhusu hiyo diji mkuu, kuna namna yoyote mnahujumiwa kwenye historia??
Au unataka dini ipewe heshima na isomwe mashuleni kua ni dini iliyoahiriki kupigania uhuru, naomba nieleweleshe hapo ndgu.
 
Maandiko yako ni elimishi lakini mara zote huwa yana mlengo wa kidini! Siku zote unaandika kwa namna ya kulalamika.
Kweli hii ni changamoto kubwa kwa Mzee wetu halafu ulalamishi wenyewe mm sioni mantiki maana Wote Abushiri tumemsoma mashuleni ila hapa Mzee anakwambia majina yao yamekwepwa ila kwa upande wangu leo ndio nimesikia kuwa kumbe Mutwa Mukwava mukwavinyika Akiitwa Abdalah kiukweli nilikua sijapata kulisikia jina hili kabla
 
😍😍😍😍😍😍😍😍 Nami huwa namuona hivyo. Mohamed ni mwandishi anayependa udini na kuutelekeza utaifa.
Ulitaka asiipende dini? Wewe huna dini?
Mji wa Pangani umetekelezwa..uchumi wake haukui. Umedumaa mno.Majengo yake bado ni ya kizamani.
darcity nadhani ulitaka kuandika "umetelekezwa".

Kuhusu majengo ya kizamani, ni vyema wakayaacha lakini wawe wanayakarabati, ndio historia yenyewe hiyo.

Naona wenyewe wanyeji wa Pangani wamezubaa, mashamba ya nazi wanayauza badala ya kuuza nazi, na fukwe zao zote wanauwauzia wageni. Pesa wanaolea wake na kulia pilau.


Mwisho itakuwa kama Unguja, mpaka sasa nadhani 80% ya fukwe zake inamilikiwa na Wataliano,(nahi ni Vatikano au mawakala wake). Kama si wao vile, wanashambulia kimkakati.

Si Pangani tu, tufunge vibwebwe, pwani yote ya Afrika Mashariki, kwenye chimbuko la Uislam, tunaipoteza kwa Wataliano, kidogo kidogo. Historia njema ya Waislam inafutwa.
 
Back
Top Bottom