Hii ndio historia ya familia ya Sykes

Magical power

JF-Expert Member
Sep 27, 2022
356
1,605
HII NDIO HISTORIA YA FAMILIA YA SYKES.

Historia hii inaanzia kwa MZEE SYKES MBUWANE KLEIST. Huyu ndiye baba yake KLEIST SYKES.

MZEE SYKES MBUWANE KLEIST ni nani?
Sykes Mbuwane ni mamluki wa KIZULU aliyechukuliwa yeye na vijana wenzake wa kizulu kutoka kijiji cha LIKUNYI MSUMBIJI.

Walifikaje Tanganyika?
Kipindi cha UTAWALA wa kikoloni wa kijerumani chini ya HERMANN VON WISSMAN aliwachukuwa kwa meli ya kivita kama askari mamluki mpaka Pangani Tanga, Tanganyika kuja kupigana na ABUSHIRI BIN SALIM AL HARITH NA MTWA MKWAWA WA IRINGA.

KLEIST SYKES ALIZALIWA WAPI?

KLEIST SYKES alizaliwa mwaka 1894, Pangani Tanga kwa baba yake SYKES MBUWANE KLEIST na MAMA yake ni Mnyatulu, baada ya baba yake kufariki Kleist Sykes baadae alikuja Dar es salaam.

MAISHA YA KLEIST SYKES BAADA YA KUJA DAR.

KLEIST SYKES alimuoa Bi MLUGURU BINT MUSSA, na alibahatika kupata watoto watatu wa kiume.

(1) ABDULWAHEED KLEIST SYKES. (1924__1968).

(2) ALLY KLEIST SYKES. (1926__2013).

(3) ABBAS KLEIST SYKES. (1929__2021).

Kama inavyoonekana katika Picha namba (1). Waliosimama kutoka kulia ni Abdulwaheed Kleist Sykes, na Ally Kleist Sykes. Aliyekaa kutoka kulia ni Abbas Kleist Sykes na Baba yao mzazi Mzee Kleist Sykes.

Picha hii ilipigwa 1942, kipindi Abdulwaheed Kleist Sykes alipokuja kumuaga baba yake akitokea LOWER KABETE KENYA mafunzoni kabla ya kwenda BURMA kama Askari wa KAR BURMA INFANTRY. Na picha namba 2, ni MZEE ALLY KLEIST SYKES kipindi cha uhai wake.

Vile vile MZEE KLEIST SYKES ALIKUWA NA WAJUKUU.
Wafuatao ni baadhi ya wajukuu wake:

(1) EBRAHIM (EBBY) ABDULWAHEED KLEIST SYKES. 1952__2015). Kama anavyoonekana katika picha namba 3. Huyu ndiye Baba yake mzazi DULL SYKES msanii wa bongofleva.

(2) MUSSA ABBAS KLEIST SYKES.

(3) KLEIST ABDULWAHEED SYKES. Alifariki 22 novemba 2017.

(4) ABRAHAM ALLY KLEIST SYKES.

ASANTENI:

1686750949151.jpg
1686750950786.jpg
1686750952579.jpg
 
HII NDIO HISTORIA YA FAMILIA YA SYKES.

Historia hii inaanzia kwa MZEE SYKES MBUWANE KLEIST. Huyu ndiye baba yake KLEIST SYKES.

MZEE SYKES MBUWANE KLEIST ni nani?
Sykes Mbuwane ni mamluki wa KIZULU aliyechukuliwa yeye na vijana wenzake wa kizulu kutoka kijiji cha LIKUNYI MSUMBIJI.

Walifikaje Tanganyika?
Kipindi cha UTAWALA wa kikoloni wa kijerumani chini ya HERMANN VON WISSMAN aliwachukuwa kwa meli ya kivita kama askari mamluki mpaka Pangani Tanga, Tanganyika kuja kupigana na ABUSHIRI BIN SALIM AL HARITH NA MTWA MKWAWA WA IRINGA.

KLEIST SYKES ALIZALIWA WAPI?

KLEIST SYKES alizaliwa mwaka 1894, Pangani Tanga kwa baba yake SYKES MBUWANE KLEIST na MAMA yake ni Mnyatulu, baada ya baba yake kufariki Kleist Sykes baadae alikuja Dar es salaam.

MAISHA YA KLEIST SYKES BAADA YA KUJA DAR.

KLEIST SYKES alimuoa Bi MLUGURU BINT MUSSA, na alibahatika kupata watoto watatu wa kiume.

(1) ABDULWAHEED KLEIST SYKES. (1924__1968).

(2) ALLY KLEIST SYKES. (1926__2013).

(3) ABBAS KLEIST SYKES. (1929__2021).

Kama inavyoonekana katika Picha namba (1). Waliosimama kutoka kulia ni Abdulwaheed Kleist Sykes, na Ally Kleist Sykes. Aliyekaa kutoka kulia ni Abbas Kleist Sykes na Baba yao mzazi Mzee Kleist Sykes.

Picha hii ilipigwa 1942, kipindi Abdulwaheed Kleist Sykes alipokuja kumuaga baba yake akitokea LOWER KABETE KENYA mafunzoni kabla ya kwenda BURMA kama Askari wa KAR BURMA INFANTRY. Na picha namba 2, ni MZEE ALLY KLEIST SYKES kipindi cha uhai wake.

Vile vile MZEE KLEIST SYKES ALIKUWA NA WAJUKUU.
Wafuatao ni baadhi ya wajukuu wake:

(1) EBRAHIM (EBBY) ABDULWAHEED KLEIST SYKES. 1952__2015). Kama anavyoonekana katika picha namba 3. Huyu ndiye Baba yake mzazi DULL SYKES msanii wa bongofleva.

(2) MUSSA ABBAS KLEIST SYKES.

(3) KLEIST ABDULWAHEED SYKES. Alifariki 22 novemba 2017.

(4) ABRAHAM ALLY KLEIST SYKES.

ASANTENI:

View attachment 2657367View attachment 2657369View attachment 2657370
Wajukuu mbona umetaja wachache?

Abraham ndo alikuja kuwa Mayor?
 
Hawa kina sykes mbona wanaimbwa sana humu kunanini behind?
Hilo jina Sykes ndio lilifanya Nyerere awatenge, hapakuwahi kuwa na mtanganyika mwingine anayeitwa Sykes wala kleist, mpaka leo, hao ni wahamiaji haramu
Afro...
Mimi ndiye nilyeieleza historia ya ukoo wa Sykes kwa kuandika kitabu cha maisha yao Tanganyika kwa kutumia nyaraka zao zinazokwenda nyuma kuanzia miaka ya mwanzoni karne ya ishirini.

Hizi nyaraka zipo na wamenimefungulia nikazisoma zote.

Hizi ni nyaraka za Kleist Sykes Mbuwane alizotumia kuandika kitabu cha maisha yake.

Kwa simulizi alizopokea kwa wazee wake ambao ndiyo mamluki wenyewe walioingia Tanganyika wakiongozana na Hermann von Wissmann historia ya ukoo wao inaanza na Chaka alipoanza vita kutokea Kwa Bulawayo mwaka 1828 akiteka majirani zake.

Katika kukimbia vita hivi Ukoo wa Sykes wakahamia Kwa Likunyi, Imhambane ambayo sasa ni Mozambique.

Hapo ndipo walipochukuliwa na Wissmann kuja kuwasaidia Wajerumani kuituliza Germany Ostafrika.

Wazulu waliwashinda Bushiri bin Salim Al Harith na rafiki yake Mtwa Abdallah Mkwawa.

Yapo mengi vipi ukoo huu ukaja kuwa mashuhuri hata wakaasisi African Association 1929, Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) 1933 na TANU 1954.

Sasa hakika historia hii ilikuwa haijulikani na zilifanyika juhudi kubwa kuwafuta katika historia ya kuasisi African Association na TANU na harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.
 
Afro...
Mimi ndiye nilyeieleza historia ya ukoo wa Sykes kwa kuandika kitabu cha maisha yao Tanganyika kwa kutumia nyaraka zao zinazokwenda nyuma kuanzia miaka ya mwanzoni karne ya ishirini.

Hizi nyaraka zipo na wamenimefungulia nikazisoma zote.

Hizi ni nyaraka za Kleist Sykes Mbuwane alizotumia kuandika kitabu cha maisha yake.

Kwa simulizi alizopokea kwa wazee wake ambao ndiyo mamluki wenyewe walioingia Tanganyika wakiongozana na Hermann von Wissmann historia ya ukoo wao inaanza na Chaka alipoanza vita kutokea Kwa Bulawayo mwaka 1828 akiteka majirani zake.

Katika kukimbia vita hivi Ukoo wa Sykes wakahamia Kwa Likunyi, Imhambane ambayo sasa ni Mozambique.

Hapo ndipo walipochukuliwa na Wissmann kuja kuwasaidia Wajerumani kuituliza Germany Ostafrika.

Wazulu waliwashinda Bushiri bin Salim Al Harith na rafiki yake Mtwa Abdallah Mkwawa.

Yapo mengi vipi ukoo huu ukaja kuwa mashuhuri hata wakaasisi African Association 1929, Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) 1933 na TANU 1954.

Sasa hakika historia hii ilikuwa haijulikani na zilifanyika juhudi kubwa kuwafuta katika historia ya kuasisi African Association na TANU na harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.
Haya yote yanatusaidia nini kwa sasa?
 
Tukishajua then what?
I think kuna vitu vya maana zaidi kufocus kwa sasa
Afro...

Then what ni hayo hapo chini:

Sijui ni kitu gani khasa kinakukera lakini umuhimu kwa historia hii ni kuwa baada ya mimi kuandika kitabu hiki: ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism,'' Minerva Press, London 1998 mabingwa wa historia ya Africa John Iliffe, Jonathon Glassman na James Brennan walifanya pitio la kitabu na mapitio yao yalichapwa katika Cambridge Journal of African History.

Gazeti la The East African walifanya serialisation tatu la kitabu mwezi December 1998.

Oxford University Press Nairobi wakanitia katika mradi wa kuandika vitabu vya historia na wanafunzi kujifunza lugha ya Kiingereza kupitia vitabu hivyo.

Oxford wakachapa kitabu changu , ''The Torch on Kilimanjaro,'' (2007).

Harvard na Oxford University Press wakanitia katika mradi wa kuandika Dictionary of African Biography (DAB) wakanipa kazi ya kuandika historia ya Kleist Sykes.

Nikaalikwa kuzungumza University of Iowa, Iowa City na Northwestern University, Evanston Chicago.

1686854967809.png
 
Afro...

Then what ni hayo hapo chini:

Sijui ni kitu gani khasa kinakukera lakini umuhimu kwa historia hii ni kuwa baada ya mimi kuandika kitabu hiki: ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism,'' Minerva Press, London 1998 mabingwa wa historia ya Africa John Iliffe, Jonathon Glassman na James Brennan walifanya pitio la kitabu na mapitio yao yalichapwa katika Cambridge Journal of African History.

Gazeti la The East African walifanya serialisation tatu la kitabu mwezi December 1998.

Oxford University Press Nairobi wakanitia katika mradi wa kuandika vitabu vya historia na wanafunzi kujifunza lugha ya Kiingereza kupitia vitabu hivyo.

Oxford wakachapa kitabu changu , ''The Torch on Kilimanjaro,'' (2007).

Harvard na Oxford University Press wakanitia katika mradi wa kuandika Dictionary of African Biography (DAB) wakanipa kazi ya kuandika historia ya Kleist Sykes.

Nikaalikwa kuzungumza University of Iowa, Iowa City na Northwestern University, Evanston Chicago.

Anhaa kumbe wewe ndiye unaefaidika.
Wewe unapata faida ya kuuza vitabu na hayo madili.

ila sisi jamii ya watanzania hautusaidii chochote,unatupotezea tu muda. Usitake kutuektia hapa eti hizo historia zina umuhimu sana kwetu ili utuuzie hivyo vitabu..Wewe ni kama dalali au tapeli fulan.
 
Hilo jina Sykes ndio lilifanya Nyerere awatenge, hapakuwahi kuwa na mtanganyika mwingine anayeitwa Sykes wala kleist, mpaka leo, hao ni wahamiaji haramu. HATA NYERERE NI MHAMIAJI. JAMII YAO INATOKEA UGANDA. WALIKUWA WANAKUJA NA KUONDOKA, WAKILETA BIDHAA TOFAUTI KUUZA HAPA BIHARAMULO. MARA MAHINDI, MARA MAHARAGE AU NDIZI KAMA SIYO ASALI BASI HATA NGUO WALIKUJA KUUZA TZ. WENYEJI WA BIHARAMULO, IKAWA WANAULIZA HAO . (WAZANAKI?) HAO WAMEKUJA NA NINI?. NDIPO LILIZALIWA NENO AU KABILA MNAOWAITA WAZANAKI. KAMA ILIVYO KWA WAZARAMO. ZARAMO SIYO KABILA KIASILI. KABILA LA ASILI NI "SHOMVI" ZARAMU NI NENO KATIKA MANENO YA KISHOVI. WAPEMBA SIYO KABILA KIASILI. NENO PEMBA LIMEPELEKWA ZANZIBAR NA WAMAKONDE TOKEA PEMBA MSUMBIJI. KAMA ILIVYO LEO HAWA TUNAOWAITA WAMACHINGA. BAADA YA MIAKA 50 MPK 100 HAPO BAADAE, NENO AU KABILA MAKONDE LITAKUFA, LITASIMAMA NENO MACHINGA.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom