Nyota yako leo Jumapili juni 22/2025

Nyota yako leo Jumapili juni 22/2025

Dogoli kinyamkela

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2024
Posts
2,144
Reaction score
3,459
NYOTA YAKO LEO JUMAPILI JUNI 22/2025:

UKIWA NA SHIDA YOYOTE YA KINYOTA NA TIBA, NIPO MOROGORO MJINI NAPATIKANA KILA SIKU OFISINI KWANGU FOREST KILREKA KUANZIA SAA 12 ASUBUHI MPAKA SAA 12 JIONI.
IMG-20250620-WA0132(1).jpg


MAALIM ANAPATIKANA MUDA WOTE.


★MAPACHA– GEMINI ♊ (May 21– Juni 20)

Utafutaji wako wa pesa ambao ulikwama utafaulu Pamoja na kwamba umekuwa katika hali mbaya sana kimawazo na kifikra hasa kuhusiana na familia yako jitahidi uwe na mawazo chanya na utaona faida yake.

•Utapata maudhi makubwa leo na siku yako itakuwa nzito pia haja zako leo itakuwa ngumu kutimia.

★KAA– CANCER 🦀 (Juni 21– Julai 22)

Huu ndio hasa muda wa wewe kubadili kazi au jambo unalolifanya kwa sababu unatumika bure na hakuna faida unayipata fanya juu chini ukamilishe mambo yako muhimu mapema iwezekanavyo.

•Safari zako sio nzuri utapoteza kitu muhimu ila utafika salama na kurudi salama.

★SIMBA LEO 🦁 (Julai 23– Agosti 22)

Leo tumia akili inaonekana usipokuwa makini kunaweza kukazuka ubishini mkali sana kati yako na mtu wako wa karibu jaribu kujiepusha na hayo magomvi.

•Mahusiano yako yatakuwa na kutokuelewana ila yote yanapita.

★MASHUKE– VIRGO ♍ (Agosti 23– September 23)

Leo Jiepushe na maamuzi yoyote unayotarajia kuyafanya unaweza kujikuta ukiamua mambo hovyo na kupelekea kuharibika kwa mipango yako kuwa muangalifu sana.

•Utapata bahati nzuri na habari nzuri nyingi zitakufikia leo.

★MIZANI– LIBRA ⚖️ (September 24– Oktoba 23)

Jumapili ya leo ni njema na nzuri kwako Biashara au kazi utakayoifanya ikakusukuma mbele au kupata mafanikio Hali hii ya mafanikio na kufaulu isikufanye ulegeze juhudi zako ulizoanza nazo mwanzoni mwa wiki hii.

•Utapata heshima na nguvu kubwa ya watu kukusikiliza.

★NG'E– SCORPION 🦂 (Oktoba 24– November 21)

Siku ya leo Masuala ya pesa yasikuletee khofu kwako shughuli ambazo umezipanga zifanikiwa hakuna hitilafu yoyote ila rekebisha mambo machache na utaona mafanikio makubwa.

•Safari zako ni nzuri tegemea kheri ndani yake.

★MSHALE– SAGITTARIUS 🏹 (November 22– December 21)

Hii ni jumapili njema sana kwako ila unahitajika kuwa mnyenyekevu kwa kila kitu na kila mtu watu walio karibu na wewe wanakuhitaji sana jaribu kujikurubisha kwao ili kuondokana na mikosi na mabalaa.

•Mahusiano yako yatajaa neema na utulivu pia kuna kitu kizuri mno kitakutokea ndani yake.

★MBUZI– CAPRICORN 🐐 (December 22– January 20)

Kwa hakika Leo itakuwa ni siku nzuri murua kushughulikia mambo ambayo yana manufaa kwako mwenyewe na jamii nzima inayokuzunguka leo utapata marafiki wapya.

•Kazi zako zitakuwa nzito kwa kila kitu na watu watakuudhi kwenye shughuli zako leo vumilia yanapita.

★NDOO– AQUARIUS 🏺 (January 21– February 19)

Jitahidi kuyashughulikia na mambo ambayo yanakukabili hasa kwa wakati huu bila ya kuanzisha mambo mapya hili litakuwa jambo la busara zaidi kwako na kwa wanaokutegemea.

•Mahusiano yako pia yatakuwa na usaliti wa wazi hivyo usijiamini sana hakuna kheri katika mahusiano mapya leo yatakufa ghafla.

Safari zako leo sio nzuri.

★SAMAKI– PISCES 🐟 (February 20– March 20)

Siku ya leo itakuwa nyepesi sana kwako mambo nayo yatakuwa mepesi ila jiepushe na magomvi hasa yanayohusiana na masuala ya kimapenzi Mambo yako yatakamilika na kukuacha ukiwa na furaha.

•Utapata matumaini makubwa na mazuri kwenye mambo yako yote kwa ujumla na utafarijika kwa mengi.

★PUNDA– ARIES 🐏 (March 21– Aprili 20)

Siku ya leo ni nzuri na tumia muda mwingi katika kupanga mambo yako kwa sababu ukifanya mambo kwa haraka na pupa unaweza kujiletea matatizo au ukaijiingiza katika balaa kubwa hapo baadae.

•Tegemea kufunguka zaidi biashara zako na kazi zako zitaenda vizuri.

★NG'OMBE– TAURUS 🐂 (Aprili 21– May 20)

Leo siyo siku njema sana kuwa kuwa na tahadhari inaonekana utakabiliwa na upinzani mkubwa katika mambo yako hakikisha kwamba umejikinga na jambo lolote kabla hujapata matatizo vinginevyo maisha yako yatakuwa mtegoni.

•Mahusiano yako yatakuwa na utulivu na amani itatawala katika nyumba yako.

Safari zako ni nzuri.

★★★★★★★★★★★★★★★
Kwa ushauri na mengineyo wasiliana na maalim niwatakie siku njema na mafanikio mema

MAALIM DOGOLI KINYAMKELA 💀☠️ 🌳🌱 MTABIRI WA NYOTA NA MTAALAM WA MAMBO MBALI MBALI YANAYO HUSIANA NA NYOTA ZENU.
 
IJUE NYOTA YAKO Taurus ♉
sehemu ya pili

Dr DOGOLI KINYAMKELA 💀☠️

MAELEZO YA NYOTA YA NG’OMBE (TAURUS ♉)

Hii ni nyota ya pili katika mlolongo wa nyota 12.

Nyota hii ni kwa watu waliozaliwa kati ya Tarehe 21 Aprili hadi 20 Mei

Siku yao ya bahati ni Ijumaa .
Namba yao ya bahati ni 6 .
Rangi yao ya bahati ni Kijani .
Asili yao ni Udongo.
Sayari yao ni Venus (Zuhra).

Malaika wake anaitwa Anael au An-yaeel na Jini anayetawala siku hii anaitwa Hagith au Al abyadh au jina la utani anaitwa Abú Hassan Zoob’aa.

Rangi zao ni Rangi ya, Kijani, udongo, njano na Rangi ya machungwa.
Wenye nyota hii wanashauriwa kinyota wapake au watumie rangi za Kijani au rangi za Pinki au rangi ya Bluu ambayo haijakoza katika nyumba zao au sehemu zao ya biashara ili kuleta mvuto wa kinyota.

Rangi zinazowapa uwezo wa mapenzi, mahaba na furaha ya kujumuika na watu ni rangi za zambarau (Violet) na Nyekundu

Kito (Jiwe) ni Emarald.
Madini yao ni Shaba
Manukato yao ni Lozi chungu, Waridi na vanila

MAMBO MUHIMU:-

Ubora unaohitajika kusawazisha mambo yao ni kuwa wenye uwezo wa kubadilika kwa urahisi katika maamuzi yao.

Maadili yao ni Uvumilivu, Utiifu, Ustaamilivu, kuwa Imara, amani na kuelewana.

Matakwa yao ni Maliwazo, Urahisi wa vitu na mali.

Tabia za kujiepusha nazo ni kutoshawishika au kutobadilika, kuwa mbishi, mng’ang’anizi na kuwa yakinifu.

USHIRIKIANE NA NANI?

⭐Nyota za watu ambao anaelewana nao ni nyota za Mashuke na Mbuzi

⭐Nyota za watu ambao haelewani nao ni nyota za Simba, Nge na Ndoo.

⭐Nyota inayomsaidia kikazi ni nyota ya Ndoo

⭐Nyota inayomsaidia kihisia ni nyota ya Simba

⭐Nyota inayomsaidia kipesa ni nyota ya Mapacha

⭐Nyota inayomsaidia katika ubunifu ni nyota ya Mashuke

⭐Nyota bora ya Mapenzi, Ndoa na Ushirikiano ni nyota ya Nge

⭐Nyota bora ya kujifurahisha ni nyota ya Mashuke

⭐Nyota ambazo zinamsaidia katika mambo ya kidini na kiroho ni nyota za Punda na Mbuzi.

KIPAJI CHA NGOMBE .

Wenye nyota hii wana kipaji kikubwa kilicho ndani ya mwili wao (Body centred) ambacho kinawasidia kuelewa mambo kabla hayajatokea. Vile vile wana kipaji cha hesabu, kipaji cha kuponya kwa kutumia mikono.
Wanaweza kuyaombea maji na kumwagia mwenye matatizo na matatizo yake yakamalizika.

TABIA ZAO KIMAUMBILE NA KIMAPENZI.

Ngombe ni watu wanaopenda kujishughulisha katika shughuli nyingi. Ni wakarimu na wanaopenda kusaidia watu, ni wavumilivu na wenye subira katika jambo lolote wanalolifanya.

Ni watu wenye malengo na wenye msimamo thabiti, wasiopenda kupindishwa na wana tabia ya ubishi na ukaidi hasa katika jambo lao wanalolitaka.

Kwenye Mapenzi ni waaminifu sana lakini wanahitaji uhakika katika mapenzi na njia au mwenendo unaoeleweka.
Ni wenye mahaba na mapenzi makubwa kwa wapenzi wao.Uhakika wa mapenzi ndio jambo kubwa ambalo wenye nyota hii huangalia kwanza na baadae Penzi hilo liwe lenye hisia na mpangilio.

Pamoja na hisia kali walizonazo, wao ni watu imara na wasiobadilika hivyo kuwafanya watu wenye shauku kutovutiwa nao.Uaminifu ni jambo la pili ambalo wenye nyota hii wanalo hivyo kuwafanya wao wawe watu wenye kuaminika na hiyo inasababisha wawe wenye wivu kupindukia.

Wanachotakiwa kufanya ni kujitahidi kuwapa nafasi wapenzi wao la sivyo watajikuta wako peke yao. Ndoa kwao ndio uamuzi mzuri kuliko kuishi na wapenzi. Tabia yao ni ya kudumisha jambo fulani wanaloliamini au walilolianzisha na hawapendi kubadilishwa.

KAZI NA BIASHARA ZA NGOMBE:

Kazi na biashara zao zinakuwa za muziki, biashara zinazohusiana na chakula, hoteli, migahawa, kazi za ujenzi, kazi za mashamba, kazi za uhasibu, na kazi au biashara za sanaa hasa uchoraji au uchongaji vinyago.

MAVAZI NA MITINDO:

Ngombe wavae nguo zenye mitindo mizuri iliyo nakishiwa na yenye Mvuto wa kimapenzi, (Sexy Outfits). Rangi ziwe za kijani au Pinki na rangi zilizo laini, Vitambaa viwe vya Pamba vilivyo chorwa au vyenye picha. Mavazi yaambatane na mishipi, au maua na skafu.

MAGONJWA YA NGOMBE:

Nyota hii inatawala shingo, Koo, Koromeo, Kidevu na sehemu ya chini ya taya. Maradhi yao mara nyingi yanakuwa matatizo ya mvutano na misuli hasa katika sehemu zilizotajwa.

VYAKULA, NCHI, NA MIJI YA NGOMBE :

Wenye nyota hii wanashauriwa wapende kula vyakula vifuatavyo ambavyo ndivyo vinavyotawaliwa na nyota yao; Tofaa (Apple), Chaza (Oysters), Viazi Mbatata (Potatoes), na Dover sole (samaki).
Ili kupata mafanikio ya kinyota, kwa wale wenye uwezo wanashauriwa aidha kuishi au kutembelea nchi au miji ifuatayo ambayo inatawaliwa na nyota yao; baadhi ya nchi hizo ni Urusi, Ireland, St louis,na Lucerne (Switzerland).

MADINI, VITO NA MAFUSHO:

Madini ya Ngombe ni Shaba. Vito vyao vya kuvaa katika pete ni kama vilivyoonyeshwa katika picha hapa chini.

Mafusho yao yanaitwa Mustaka, mafusho haya yako kama vijiwe vidogo vyenye vumbi kama jeupe na vina rangi ya kijivu, ambavyo wenye nyota hii wanatakiwa kuchoma siku yao ya Ijumaa kati ya saa 12 mpaka saa 1 au saa 7 mchana mpaka saa 8. kuchoma mafusho ya nyota yako kunakusaidia kusafisha nyota yako na kukuongezea bahati.

Kwa msaada wa tiba ya nyota, maisha, uchumi, mahusiano na magonjwa, wasiliana nasi

By Dr dogoli kinyamkela 💀☠️ , mtafiti na mkufunzi wa maswala ya kiroho
 
IJUE NYOTA YAKO Taurus ♉
sehemu ya pili

Dr DOGOLI KINYAMKELA 💀☠️

MAELEZO YA NYOTA YA NG’OMBE (TAURUS ♉)

Hii ni nyota ya pili katika mlolongo wa nyota 12.

Nyota hii ni kwa watu waliozaliwa kati ya Tarehe 21 Aprili hadi 20 Mei

Siku yao ya bahati ni Ijumaa .
Namba yao ya bahati ni 6 .
Rangi yao ya bahati ni Kijani .
Asili yao ni Udongo.
Sayari yao ni Venus (Zuhra).

Malaika wake anaitwa Anael au An-yaeel na Jini anayetawala siku hii anaitwa Hagith au Al abyadh au jina la utani anaitwa Abú Hassan Zoob’aa.

Rangi zao ni Rangi ya, Kijani, udongo, njano na Rangi ya machungwa.
Wenye nyota hii wanashauriwa kinyota wapake au watumie rangi za Kijani au rangi za Pinki au rangi ya Bluu ambayo haijakoza katika nyumba zao au sehemu zao ya biashara ili kuleta mvuto wa kinyota.

Rangi zinazowapa uwezo wa mapenzi, mahaba na furaha ya kujumuika na watu ni rangi za zambarau (Violet) na Nyekundu

Kito (Jiwe) ni Emarald.
Madini yao ni Shaba
Manukato yao ni Lozi chungu, Waridi na vanila

MAMBO MUHIMU:-

Ubora unaohitajika kusawazisha mambo yao ni kuwa wenye uwezo wa kubadilika kwa urahisi katika maamuzi yao.

Maadili yao ni Uvumilivu, Utiifu, Ustaamilivu, kuwa Imara, amani na kuelewana.

Matakwa yao ni Maliwazo, Urahisi wa vitu na mali.

Tabia za kujiepusha nazo ni kutoshawishika au kutobadilika, kuwa mbishi, mng’ang’anizi na kuwa yakinifu.

USHIRIKIANE NA NANI?

⭐Nyota za watu ambao anaelewana nao ni nyota za Mashuke na Mbuzi

⭐Nyota za watu ambao haelewani nao ni nyota za Simba, Nge na Ndoo.

⭐Nyota inayomsaidia kikazi ni nyota ya Ndoo

⭐Nyota inayomsaidia kihisia ni nyota ya Simba

⭐Nyota inayomsaidia kipesa ni nyota ya Mapacha

⭐Nyota inayomsaidia katika ubunifu ni nyota ya Mashuke

⭐Nyota bora ya Mapenzi, Ndoa na Ushirikiano ni nyota ya Nge

⭐Nyota bora ya kujifurahisha ni nyota ya Mashuke

⭐Nyota ambazo zinamsaidia katika mambo ya kidini na kiroho ni nyota za Punda na Mbuzi.

KIPAJI CHA NGOMBE .

Wenye nyota hii wana kipaji kikubwa kilicho ndani ya mwili wao (Body centred) ambacho kinawasidia kuelewa mambo kabla hayajatokea. Vile vile wana kipaji cha hesabu, kipaji cha kuponya kwa kutumia mikono.
Wanaweza kuyaombea maji na kumwagia mwenye matatizo na matatizo yake yakamalizika.

TABIA ZAO KIMAUMBILE NA KIMAPENZI.

Ngombe ni watu wanaopenda kujishughulisha katika shughuli nyingi. Ni wakarimu na wanaopenda kusaidia watu, ni wavumilivu na wenye subira katika jambo lolote wanalolifanya.

Ni watu wenye malengo na wenye msimamo thabiti, wasiopenda kupindishwa na wana tabia ya ubishi na ukaidi hasa katika jambo lao wanalolitaka.

Kwenye Mapenzi ni waaminifu sana lakini wanahitaji uhakika katika mapenzi na njia au mwenendo unaoeleweka.
Ni wenye mahaba na mapenzi makubwa kwa wapenzi wao.Uhakika wa mapenzi ndio jambo kubwa ambalo wenye nyota hii huangalia kwanza na baadae Penzi hilo liwe lenye hisia na mpangilio.

Pamoja na hisia kali walizonazo, wao ni watu imara na wasiobadilika hivyo kuwafanya watu wenye shauku kutovutiwa nao.Uaminifu ni jambo la pili ambalo wenye nyota hii wanalo hivyo kuwafanya wao wawe watu wenye kuaminika na hiyo inasababisha wawe wenye wivu kupindukia.

Wanachotakiwa kufanya ni kujitahidi kuwapa nafasi wapenzi wao la sivyo watajikuta wako peke yao. Ndoa kwao ndio uamuzi mzuri kuliko kuishi na wapenzi. Tabia yao ni ya kudumisha jambo fulani wanaloliamini au walilolianzisha na hawapendi kubadilishwa.

KAZI NA BIASHARA ZA NGOMBE:

Kazi na biashara zao zinakuwa za muziki, biashara zinazohusiana na chakula, hoteli, migahawa, kazi za ujenzi, kazi za mashamba, kazi za uhasibu, na kazi au biashara za sanaa hasa uchoraji au uchongaji vinyago.

MAVAZI NA MITINDO:

Ngombe wavae nguo zenye mitindo mizuri iliyo nakishiwa na yenye Mvuto wa kimapenzi, (Sexy Outfits). Rangi ziwe za kijani au Pinki na rangi zilizo laini, Vitambaa viwe vya Pamba vilivyo chorwa au vyenye picha. Mavazi yaambatane na mishipi, au maua na skafu.

MAGONJWA YA NGOMBE:

Nyota hii inatawala shingo, Koo, Koromeo, Kidevu na sehemu ya chini ya taya. Maradhi yao mara nyingi yanakuwa matatizo ya mvutano na misuli hasa katika sehemu zilizotajwa.

VYAKULA, NCHI, NA MIJI YA NGOMBE :

Wenye nyota hii wanashauriwa wapende kula vyakula vifuatavyo ambavyo ndivyo vinavyotawaliwa na nyota yao; Tofaa (Apple), Chaza (Oysters), Viazi Mbatata (Potatoes), na Dover sole (samaki).
Ili kupata mafanikio ya kinyota, kwa wale wenye uwezo wanashauriwa aidha kuishi au kutembelea nchi au miji ifuatayo ambayo inatawaliwa na nyota yao; baadhi ya nchi hizo ni Urusi, Ireland, St louis,na Lucerne (Switzerland).

MADINI, VITO NA MAFUSHO:

Madini ya Ngombe ni Shaba. Vito vyao vya kuvaa katika pete ni kama vilivyoonyeshwa katika picha hapa chini.

Mafusho yao yanaitwa Mustaka, mafusho haya yako kama vijiwe vidogo vyenye vumbi kama jeupe na vina rangi ya kijivu, ambavyo wenye nyota hii wanatakiwa kuchoma siku yao ya Ijumaa kati ya saa 12 mpaka saa 1 au saa 7 mchana mpaka saa 8. kuchoma mafusho ya nyota yako kunakusaidia kusafisha nyota yako na kukuongezea bahati.

Kwa msaada wa tiba ya nyota, maisha, uchumi, mahusiano na magonjwa, wasiliana nasi

By Dr dogoli kinyamkela 💀☠️ , mtafiti na mkufunzi wa maswala ya kiroho
Majuzi kwenye Uzi wako ulisema tuulize chochote wewe utajibu nikauliza lakin sikuona umejibu
 
Pamoja sana kaka mchawi ,ila mwenzio ile njia ya kuwatimua majirani nimefanikiwa na nimewatimua wengi ila sasa nawaza unipe dawa nipate majirani ninaoendana nao hasa wenye kujua haki zangu za msingi kuwa haziingiliwi hasa kulewa na kukoma kunishitaki kwa mwenyekiti wa kitongoji eti nawapigia kelele usiku wa manane nikirudi zangu batani.

Msaada jamaa yangu wa ukweli
 
Pamoja sana kaka mchawi ,ila mwenzio ile njia ya kuwatimua majirani nimefanikiwa na nimewatimua wengi ila sasa nawaza unipe dawa nipate majirani ninaoendana nao hasa wenye kujua haki zangu za msingi kuwa haziingiliwi hasa kulewa na kukoma kunishitaki kwa mwenyekiti wa kitongoji eti nawapigia kelele usiku wa manane nikirudi zangu batani.

Msaada jamaa yangu wa ukweli
Si wawashe sabufa asiskie kelele zako,au nao wanataka mifumo ya ubaya ubwela 🤷🏽‍♂️🤷🏽‍♂️ kaka mchawi 😂😂
 
😂😂😂 Umetumia Ile trick ya ubaya ubwela🤷🏽‍♂️🤷🏽‍♂️ kaka mchawi😂😂😂
Mapema sana kaka ,hakuna jirani mwenye kiburi aliyebaki karibu na mimi ,wote nimewatimulia mbali ,wanajikuta wanahama kwa kusema eti mtaa wetu umejaa watu waswahili waswahili wasijue nimeshamaliza kazi kaka
 
Nilikuliza mtu aliyechizika kwasabab ya mizimu anasaidiwaje?
Hii inategemea iyo mizim iliyo mfanya ivyo n ya kher au shali na je shida n nN ad imfanye ivyo,apo Kuna uchunguz wa kina ufanyike ndo niweze kuona kama nakusaidiaje au nakushaurije 👂🏽
 
Mapema sana kaka ,hakuna jirani mwenye kiburi aliyebaki karibu na mimi ,wote nimewatimulia mbali ,wanajikuta wanahama kwa kusema eti mtaa wetu umejaa watu waswahili waswahili wasijue nimeshamaliza kazi kaka
Soon nakusajili kwenye chama letu la wababe asili ukiifata ina Raha yake jamani utumii nguvu nyiiingi kufanya jambo lako😂😂
 
Si wawashe sabufa asiskie kelele zako,au nao wanataka mifumo ya ubaya ubwela 🤷🏽‍♂️🤷🏽‍♂️ kaka mchawi 😂😂
Mimi napenda nikitoka batani usiku lazima niweke disco langu mwenyewe getini kwangu niruke rumba walau masaa mawili ikiwa sehemu ya mazoezi lakini pia kumshukuru baba kwa kunisomesha .

Hivyo nina mziki mnene kwenye corola yangu na pia sound system kali ndani kwangu hivyo mida ya saa nane nikofika lazima niunganishe wimbo mmoja kwenye corolla unaoendana na ule wa kwenye vyombo vya mziki ndani ili niweze kuruka rumba ni hapo wanadai nawapigia kelele ila nikajua ni wivu wa maisha tu ,nikaamua kuwaamisha kwa nyogoli mapema sana
 
Understood
Kutafuta mganga wa jadi au mtaalamu wa tiba za asili

Mganga wa kweli anaweza kufanya tambiko (sadaka, matoleo) kwa mizimu ili kutuliza roho zinazomsumbua.

Anaweza kutumia dawa za asili (miti shamba, mafusho, maji ya dawa).


Kufanya matambiko ya kupatanisha na mizimu

Wazee wa ukoo au wanandugu hufanya sherehe ndogo kwa mizimu kama chanzo ni roho za mababu waliokasirika.


3️ Kufukiza na kunyunyizia maji yenye dawa

Mafusho ya miti maalum.

Ukiitaj msaada zaidi kalibu🙏🏽
 
Mimi napenda nikitoka batani usiku lazima niweke disco langu mwenyewe getini kwangu niruke rumba walau masaa mawili ikiwa sehemu ya mazoezi lakini pia kumshukuru baba kwa kunisomesha .

Hivyo nina mziki mnene kwenye corola yangu na pia sound system kali ndani kwangu hivyo mida ya saa nane nikofika lazima niunganishe wimbo mmoja kwenye corolla unaoendana na ule wa kwenye vyombo vya mziki ndani ili niweze kuruka rumba ni hapo wanadai nawapigia kelele ila nikajua ni wivu wa maisha tu ,nikaamua kuwaamisha kwa nyogoli mapema sana
Sio nyogoli bhana n dogoli😂😂
 
Mimi napenda nikitoka batani usiku lazima niweke disco langu mwenyewe getini kwangu niruke rumba walau masaa mawili ikiwa sehemu ya mazoezi lakini pia kumshukuru baba kwa kunisomesha .

Hivyo nina mziki mnene kwenye corola yangu na pia sound system kali ndani kwangu hivyo mida ya saa nane nikofika lazima niunganishe wimbo mmoja kwenye corolla unaoendana na ule wa kwenye vyombo vya mziki ndani ili niweze kuruka rumba ni hapo wanadai nawapigia kelele ila nikajua ni wivu wa maisha tu ,nikaamua kuwaamisha kwa nyogoli mapema sana
😂😂😂 Kwaiyo unataka niwaweke kikaangaoni kaka mchawi 😂🤷🏽‍♂️
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom