Nyota ya Punda na character zake

Nyota ya Punda na character zake

Naomba nifafanulie nyota ya MBUZI

MBUZI.jpg


NYOTA YA MBUZI (CAPRICON)
  • Hii ni nyota ya kumi katika mlolongo wa nyota 12.
  • Wenye nyota hii ni wale waliozaliwa kati ya tarehe 22 Dec na 19 Jan ya mwaka wowote.
  • Sayari yao ni SATURN (ZOHAL)
  • Siku yao ya bahati ni Jumamosi.
  • Namba yao ya bahati ni 8.
  • Rangi yao ya bahati ni rangi ya Kijivu au Nyeusi.
  • Asili yao ni Udongo.
KIPAJI CHA MBUZI(GRADUAL)
Wenye nyota hii wana kipaji cha kuchambua mambo kidogo kidogo au kufuatilia kitu bila watu kujua na kupata ufumbuzi wa uhakika mwishoni.

TABIA ZA MBUZI

Wale wote waliozaliwa katika nyota hii ni watu ambao wanapenda kuwajibika, ni wenye bidii ya kazi, katika kazi yeyote watakayofanya hata kama ikiwa ni ya kipuuzi.
Ni viumbe waaminifu sana na ni watu wastahamilivu na wenye kuweza kuvumilia matatizo yeyote.
Kwa upande mwingine ni watu wenye tamaa kubwa ya kimaisha na kimaendeleo, na kwa sababu ya kutekeleza malengo yao basi huwa wanakuwa wabinafsi na wenye uroho na uchu.

TABIA YA MBUZI KATIKA MAPENZI
Watu wenye nyota hii wanakuwa ni watu wenye aibu sana kwa wapenzi wao lakini aibu ikishawaondoka huwa ni wapenzi wa kutisha, kwa maana ya kwamba kwa vile wao ni waaminifu wanataka wapenzi wao wawaunge mkono katika hisia zao za kimapenzi.
Ni watu wanaoogopa sana kuachwa na wapenzi wao hivyo basi huwa wanakuwa waangalifu sana katika kuchagua wapenzi.
Jambo jingine ni kuwa huwa wao wenyewe hawajiamini kimapenzi, mara nyingi wanashindwa kuingia katika mapenzi kwa woga tu hivyo kukosa nafasi nzuri ya kupendwa.
Kwa ujumla ni wapenzi makini na huwa hawaoi mpaka wapate uhakika wa kutosha kutoka kwa wapenzi wao. Ni wapenzi makini, waaminifu na wanaoweza kuaminiwa. Lengo lao katika mapenzi ni usalama.

TABIA YA MBUZI KATIKA FEDHA
Kwa watu wenye nyota hii fedha ni kitu muhimu sana katika maisha.
Watu wa Mbuzi wanaamini kabisa kwamba fedha ndio zitawapa uwezo wa kuweza kupambana au kukabiliana na mazingira ya Dunia, hivyo basi suala lolote la fedha na mali wanalichukulia kwa uzito mkubwa sana.
Inawachukua muda mrefu kutekeleza malengo yao ya kifedha lakini wakishazipata basi huwa hawatetereki tena. Wana uwezo wa kuhifadhi walichonacho.
Ni watu wabahili sana na hata kama wakiwa na fedha nyingi utaona wanaishi maisha ya kawaida na wala huwezi kuwajua.
Fedha zao zinatoka kwa sababu maalum ya dharura na wala siyo katika starehe au vinginevyo na hiyo ni kwa sababu hupenda kukumbuka walikotoka katika hali ya umasikini au ufukara.

MAVAZI YA MBUZI
Wenye nyota ya Mbuzi wanatakiwa wavae nguo za mitindo, zilizoshonwa kwa ustadi.
Nguo hizo ziwe za rangi ya kijivu au Kijani iliyoiva au hudhurungi nzito.
Kitambaa kiwe cha kitani (Linen) au cha ngozi.
Nguo ziwe ni suti na ziambatane na saa za mikononi.

MATATIZO YA KIAFYA
Nyota hii inatawala Mifupa, Magoti na Ngozi.
Matatizo yao makubwa ya kiafya huwa yanasababishwa na muda mrefu ambao wanafanya kazi au kujishughulisha.
Hii ni kwa sababu hawamwamini mtu mwingine afanye shughuli zao ambazo zina mipangilio ya muda mrefu, nguvu nyingi, na akili hutumika.
Shughuli zao nyingi za mizunguko na kufikiria huwaletea maradhi kama Baridi Yabisi (rheumatism).
Maradhi yao mengine makubwa ni ugonjwa wa ngozi, matatizo ya Magoti na maradhi ya mifupa.

KAZI ZA MBUZI
Wenye nyota ya Mbuzi kitu muhimu katika maisha yao ni kazi na maisha mazuri na yanayoeleweka ambayo yako katika mpangilio wanaoutaka wao.
Ni watu ambao wanazingatia sana muda wa maisha na wana mpangilio maalum kwamba katika umri fulani awe amepata nini au awe na fedha kiasi gani.
Ni wenye kupenda utekelezaji wa kazi wa hali ya juu na wao wanapoagizwa hufanya hivyo.
Kazi zao zinazowafaa ni zile za kutumia akili, Uhandisi, Usanifu Majengo, Saveya, kazi za Serikali, Siasa na Daktari wa Meno.

FAMILIA ZA MBUZI
Wazazi wenye nyota ya Mbuzi ni watu ambao wamepangilia kabisa mipango ya watoto wao kabla hawajazaa.
Ni wazazi ambao wanayachukulia kwa uzito mkubwa majukumu yao ya kulea na hawakubali kabisa watoto wao kufanya michezo michezo ya kipuuzi. Wanapenda kuwahimiza watoto wao kuwa na malengo ya maana.
Wanapenda sana nidhamu katika familia zao.
Mara nyingi wazazi wa kiume huwa hawapati muda kuwa na watoto wao kutokana na kazi nyingi walizonazo lakini kwa wazazi wa kike wanakuwa wanatumia akili ya hali ya juu katika kutatua matatizo au hisia za watoto wao.

MADINI YA MBUZI
Wenye nyota hii wanatakiwa wavae vito vinayoitwa Black Jet.
Jiwe hili inaaminiwa lina uwezo wa kuongeza ujasiri na kumletea mvaaji mafanikio ya kibishara.

UHUSIANO WA KIMAPENZI (MBUZI NA KAA)
Tabia ya Mbuzi ya ubahili na kutopenda anasa hulainishwa na tabia ya Kaa ya upendo, mapenzi na huruma.

VYAKULA VYA MBUZI
Wenye nyota ya Mbuzi wanashauriwa wapende kula vyakula au matunda yafuatayo. Ambayo ndio yanatawaliwa na nyota yao.
Wapende sana vyakula vya Nazi na Nyama yeyote.
Vile vile wapendelee kula Viazi Vitamu na Samaki Gamba (Shellfish).

NCHI ZA MBUZI
Ili kupata mafanikio ya kinyota kwa watu wenye uwezo wanashauriwa aidha waishi au watembelee miji au nchi zifuatazo ambayo inatawaliwa na nyota ya Mbuzi.
Miji hiyo ni Brussels (Ubelgiji) na Oxford (Uingereza) au nchi za Mexico na India.

RANGI ZA MBUZI
Wenye nyota hii wanashauriwa wapake rangi zifuatazo kwenye nyumba zao, rangi ya Kahawia (Brown) Rangi ya Kijivu (Grey) au Nyeusi
 
MziziMkavu mkuu hapo kwenye cancer number 9 kama kuna kijikosa.

Aquarius tuko na matatizo gani? Yan najiona mie nina tatizo la kutopenda kuchanganyikana na watu, napenda kukaa mwenyewe tu na kama ni nyumbani basi nitulie na family mates sio mambo za majirani nk ( kama kuna zile shughuli za kkijamii za ulazima hapo naweza changamana nao otherwise naonaga tabu sana.
Ase uko kama mimi sipendi kabisa hadi Kuna najilazimisha kukaa na watu ila napenda sana kukaa mwenyewe
 
Back
Top Bottom