Nyoka avuruga date yangu na habiba

Habari wanajamvi!

Baada ya kumfukuzia mdada mmoja wa kichaga(habiba) mwenye umbo namba nane na sura nzuri ya kuvutia kwa takribani miezi mitatu bila mafanikio.

Nilipokea message ya uyo dada akinitaka tufanye evening walk huku akinipa nafasi ya kujaribu kushawishi mtima wake.

Mwanaume bila kuchelewa nikafika eneo la tukio, lakini kabla ya kuanza evening walk yetu.

Nilizama dukani kwa mangi na kununua chocolate, soft drinks pamoja na PK (maana niliamini kwa asilimia mia moja kuwa ninge pata denda kwa siku hiyo).

Evening walk yetu ikaanza nikampanga Mtoto akapangika vizuri, na mwisho kabisa kuna swali akaniuliza:-

Habiba: "hivi worldboss unaniambia unanipenda je upo tayari kunilinda?"

Worldboss:"mama usihofu yani nitakulinda, nitakutunza pia kukupenda maisha yangu yote"

Basi Habiba kusikia ivyo akanikumbatia, nakunijibu "nakupenda pia".Baada ya hapo tukakunja kona ili turudi mtaani.

Mara paap binti kaona kitu kama nyoka kaanza kupiga kelele huku akirukaruka na kunishikilia shati.

Mzee nikala mita kama Hussein bolt , manzi kang'ang'ania shati nika msukuma kulekule kwenye nyoka akaanguka Mzee nikauchana mpaka nyumbani huku nikihema juu juu kama funza.

Baada kama ya nusu saa naona text akiniambia hauwezi tena kuendelea na Mimi kwakuwa sitoweza kumlinda kama nilivyoahidi.

Aisee imeniuma sana, naombeni ushauri wanajamvi ntampataje habiba wangu.
Kama unataka kutunga tumia uhalisia hase hamna mwanaume anaweza kukimbia nyoka kiasi hicho unachosema ww kama ni mwoga ataenda mita kadhaa tu lakin sio mpaka nyumbani
 
tafuta toy la nyoka nenda nalo kwake mwambie usiku ule ule ulifanya uchunguzi wa kina na kugundua ilikuwa ni toy tuu.
(akikuulza kwahy we unaogopa toy la nyoka..? hapo jiongeze mwenyewe)
 
tafuta toy la nyoka nenda nalo kwake mwambie usiku ule ule ulifanya uchunguzi wa kina na kugundua ilikuwa ni toy tuu.
(akikuulza kwahy we unaogopa toy la nyoka..? hapo jiongeze mwenyewe)
Asante mkuu ushauri mzuri
 
Back
Top Bottom