Nyimbo zenye ujumbe mzito sana

Nyimbo zenye ujumbe mzito sana

Nakusalimu mwafrika nakusalimu habari gani, nikaribishe tuketi niseme yaliyo ndani../
Umesahau kuhusu hadithi za kale za upendo wako nataka leo tukae tuijadili kesho yako.../

Kutoka kupiga ramli na kutii mizimu, umeanza kufata amri za tv na simu.../

Na ubaya ni kwamba umeanza kuikacha sanaa, na kufata siasa ambayo inakulaza na njaa.../

Na kila unachokiona unataka kubeba, vichache vimekushinda na unataka kuongeza..../

Juzuu katekisimu mpaka novena, sio zako zako ilikua ni kutamba ngonjera..../

Umezubaa majirani wameanza kufika kwako, na unaamini kua watakubebea shida zako..../

Kwasababu ujinga umezidi umasikini, unamjengea jirani kwako unachimba unabaki chini.../

Zamani ulikua unasembe ya kusaza, uliabudu kazi uliweka jembe kwenye shamba.../

Ghafla ukauza panga ukapanga jembe kwenye kabati, ukanunua kioo ujirembe ili uende na wakati.../

Umechagua urembo umetupa werevu, unauza mifugo unafuga kucha na ndevu.../

Familia ife mwafrika uzame mitini, au uombe msaada wakati unakufa na fashion mwilini.../

Mwafrika unamzigo mkubwa wa madeni, hauna mali ardhi yako ni future ya wageni.../

Unalala ndani kungoja hisani ya wenye nguvu, nyumba iko wazi we uko ibadani unaabudu..../

Ujasiri ni kujimudu mwafrika haujui hili, umejaliwa nguvu na unashindwa kuzihimili.../

Unavamia diplomasia unatunga hotuba, na hakuna mwenye hisia kua upo nyuma ya muda.../
 
Umepewa karatasi ukaipa jina pesa, ukasubiri ikuletee furaha ikakutesa.../

Ukauza umoja ukauza amani ukauza utu, ukashusha mashujaa wako ukamuinua yesu wa kizungu.../

Unakucha ndefu kushika chungu matusi, hauwezi kuandika history haumudu herufi.../

Ume-bleach nywele mdomo mwekundu umebusu baruti, nikuite nani mwafrika mzungu au mzungu mweusi.../

Unadanganywa rangi yako sio nzuri, ili ukatafute pesa ukawaungishe vipuli.../

Ume-switch kutoka mama african mpaka drama queen, umenunua tv ili uone africa ikizama chini..../

Mwafrika umekosa mipango, unajua kuchonga ngega badala ya kuchonga vinyago...Unaacha wanyama mikumi serengeti unaenda kushangaa ghorofa chicago..../

Unarudi unajikuta mmarekani eti real nigga, real nigga mbona haulipi bill nigga?

jAsiri haiachi asili, real nigga kamwe usijiite G nigga..../

hauwezi kuwa warrior, unajua majina ya wasanii kushinda historia.../
 
Je utanipenda? Diamond platnumz
binadamu wabaya Diamond platnumz
Mwana kiba
Kanyaga
 
Kwa heshima na taadhima unautunza msaafu, unatupa kitenge kisha unafunga hijabu.../

Na ubaya ni kwamba haujajua sababu, unapewa zaburi utafakari huku wenyewe wakichukua dhahabu.../

Ufeli majibu uishie kubuni, ushindane nani msafi aingie mbinguni..../

mhanga wewe rudi uzipitie kanuni, umeshikishwa kitabu wenzio wakushikie uchumi.../
 
Kwa heshima na taadhima unautunza msaafu, unatupa kitenge kisha unafunga hijabu.../

Na ubaya ni kwamba haujajua sababu, unapewa zaburi utafakari huku wenyewe wakichukua dhahabu.../

Ufeli majibu uishie kubuni, ushindane nani msafi aingie mbinguni..../

mhanga wewe rudi uzipitie kanuni, umeshikishwa kitabu wenzio wakushikie uchumi.../
mzee inaonekana unamuelewa sana dizasta
 
Eti manabii wanavyeti, kanisa lina account ya mitandao ya kijamii mpaka bank.../

Wahubiri wanavutana kinguvu, kanisa unajitangaza kutafuta umaarufu?.../

Unapishana na muda hakika, unachojua pekee ni kufa kuzika.../

Unanishauri nije kwako ndoa ikiyumba kanisa, kichekesho ni kwamba wewe ndo umeyumba kabisa.../

Aaah kanisa nilikuja uniongoze nimpende mungu we ukanifunza nimuogope, Jua kali lilinifunza kukaba nikakupa maisha na cha ajabu hujanifunza chochote..../

naskia unapande mbili za sarafu, upande mzuri na upande unaingia dili mpaka na wafu.../

Na unanifundisha baya haliwi na thawabu, nilikua mjinga sasa nabashiri majawabu.../

Tunahitaji mafunzo halisia, wakati mbinu zako zimejaa mafumbo na sheria.../

Kanisa tunaishi na wanafki kudadadeki, unajifanya rafiki sababu ya ulafi wa chenchi.../

Ikiwa huruma ya jah haina kipimo, basi kati ya wanaoomba msamaha nami nimo..../

Dhambi zako sawa tumezidiana kimo, mungu aliyehai akuepushie shimo.../

Kanisa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom