Nyimbo za Dini sehemu za Starehe

Nyimbo za Dini sehemu za Starehe

Mbona hukuti kaswida zinapigwa Bar, au hakuna waislamu walevi????

nilichomaanisha ni kuwa hizi nyimbo hazijalishi zinaimbwq na nani, zinasimama kama alama mojawapo ya dini husika, zinapopigwa sehemu zile ni kama kudhalilisha dini husika na kufanya vya dini husika kuonekana si ya maana.
Pia kuna sehemu ntakupa na direction km upo Dar maeneo ya Airport upande wa Pili wa barabara kuna Bar & Guest House moja nyuma ya Sheri kila JUMAMOSI wanajumuiya hufanya ibada hapo kila JUMAMOSI na Jumapili pia hua kuna ibada ndogo hufanyika asubuhi kwenye ukumbi wa hio Bar watu hukusanyika na kufanya maombi
 
Muda huo shughuli za bar zinakuwa zimesimama.... na wanapofuata hapo ni venue tu, sasa waende jioni, mida ya saa moja hadi saa tatu usiku, itatosha.
Wewe umesema Bar hapafai kufanya ibada kwa hio unajipinga mwenyewe ?
 
Wewe umesema Bar hapafai kufanya ibada kwa hio unajipinga mwenyewe ?
Shida ni kuwa huelewi point ninayoiongelea, rudi kwenye suala la msingi, kuwa Nyimbo za dini zinapigwa wakati wa usiku watu wanalewa. Sikuzungumzia Bar kama jengo bali kwanile shughuli ya unywaji na uuzwaji wa pombe unaofanyolika, hasa nyakati.za usiku.

Pole kama hukuwa umeelewa.
 
Usijali kwa hilo! Nyimbo za Injili ni sehemu ya kuhubiri wenye dhambi.
Ukimwona Mlevi anaimba nyimbo za dini mpongeze kabisa.
Huwezi kujua kuna Walevi ambao wanaweza kukutana na Yesu kwa njia ya nyimbo.
 
Mara ya mwisho hili songi nimepigiwa pale mianzini A town december mwaka jana sijui baa gani ile....aseee vyombo vimekolea yani niliinuka kwa utamu niliinjoi mnoo halafu akamalizia na mkono wa bwana alooooo acha tu.
Zabron singers ya umenitoa chini chini Mara ya kwanza nimesikilia pale picnic na wale mabaamedi wenye matakio makubwa wakawa wanaocheza kwa mduara
 
Usijali kwa hilo! Nyimbo za Injili ni sehemu ya kuhubiri wenye dhambi.
Ukimwona Mlevi anaimba nyimbo za dini mpongeze kabisa.
Huwezi kujua kuna Walevi ambao wanaweza kukutana na Yesu kwa njia ya nyimbo.
kweli sidhani kama neno la mungu lina mipaka
 
Kusema ukweli huwa nakereka sana kusikia nyimbo za dini, zinapigwa kwenye sehemu za starehe, hasa Bar. Sehemu hizi ni sehemu Shetani na jeshi lake wanafanya kazi zao kwa ufanisi, na anaona ni kama kuikosea heshima dhana ya kuwa nyimbo za dini ni sehemu ya kuabudu.

Kwenye hizi Bar, zinapopigwa nyimbo hizi wakati watu wamelewa, naona ni kama kumkebehi Mungu.

Na pia ni kuzikosesha heshima nyimbo hizi, ambazo zilipaswa kuzikumbusha nyoyo Utukufu wa Mungu.
Sheteni yupo makanisani na misikitini kuliko kwenye nyumba za starehe
 
Ni bora hizo nyimbo zipigwe kwenye kumbi za starehe Na sisi walevi tumkumbuke mungu kuliko kukaa kanisanii kuwaza pombe
 
Back
Top Bottom