Nyimbo za Dini sehemu za Starehe

Nyimbo za Dini sehemu za Starehe

Binadamu ni muelewa ndo maana watu wanatubu ..
Mtu akishakunywa anatoka kwenye hali yake ya uelewa wa kawaida. Na ndio maana kuna wengine ili watende dhambi wanakunywa kwanza ndio wanapata ujasiri wa kutenda.
 
Sijasema dini ninkanisani tu! Umenisingizia hapo, sitaja jila la sehemu yoyote ya ibada. Najua dini na ibada inaweza kufanyika popote kwa sharti pawe pasafi. Nakataa Bar si sehemu mojawapo.
Mwamposa yule unaemuona historia yake alianzia kuhubiri Bar pale Sinza Kumekucha akakimbiwa na mkewe ambae ana mtoto mmoja kwa kukudokezea tu usiyoyajua, kwa hio angalia unaposema Bar sio sehemu ya ibada
 
Mtu akishakunywa anatoka kwenye hali yake ya uelewa wa kawaida. Na ndio maana kuna wengine ili watende dhambi wanakunywa kwanza ndio wanapata ujasiri wa kutenda.
Injili inahubiriwa popote penye watu wanaohitaji chakula Cha kiroho, unajua mfumo wa Roho unavyofanya kazi ukiondoa mfumo wa Mwili na Nafsi ?
 
Inanikumbusha Swami Vivekananda alipoambiwa ,ukitazama Hekalu la mwalimu wako,Ramakrishna, siku hizi hali inasikitisha sana ,lile Hekalu sasa limekuwa danguro.
Akasema,wacha liwe danguro,Ramakrishna alikuja(Duniani) kwa ajili ya makahaba pia.
 
Mwamposa yule unaemuona historia yake alianzia kuhubiri Bar pale Sinza Kumekucha akakimbiwa na mkewe ambae ana mtoto mmoja kwa kukudokezea tu usiyoyajua, kwa hio angalia unaposema Bar sio sehemu ya ibada
Bado nakataa Bar si sehemu ya ibada. Nenda kaulize kwenye ile bar aliyokuwa anahubiri, wateja walikuwa wanalalamika kuwa jamaa walikuwa anawarusha stimu, na hata wakaanza kupungua.

Na kuna utofauti wa kupigwa nyimbo na kwenda kuhubiri. Nyimbo zikipigwa mtu hana habari kusikiliza maneno, ni ule mdundo tu na vibe, na ndio maana naona ninkama kuzidhalilisha hizi nyimbo.

Mahibiri yanamtaka mtu atulie asikilize, sasa wewe uende bar na washkaji zako, muache kupiga story zenu mkae kimya kusikilza mahubiri?

Wahubiri wapo sehemu nyingi, hata ukienda vituo vya daladala na ndani ya madaladala wanakuwepo pia. Kwa hiyo si ajabu.
 
Injili inahubiriwa popote penye watu wanaohitaji chakula Cha kiroho, unajua mfumo wa Roho unavyofanya kazi ukiondoa mfumo wa Mwili na Nafsi ?
Basi na watu wa Jumuiya waanze kuweka vikao vyao kwenye bar za jirani na wanapoishi, wapeane neno huku wanapata moja mbili.
 
Akuna nyimbo za dini zote ni nyimbo za kidunia na zmeimbwa na wahuni na maraya tu
Waimbaji wanavaa modo wanavaa vimini na wao wanacharge mtu kuangalia shoo yao na bado kuna wengne wanalilia pesa za mirabaha za basata kwaiyo hao ni wasanii km walivyo wasanii wengne na ndo maana wanamatendo km ya wasanii wengne mnaowaitwa wa kidunia
 
Nani alikwambia bar ni sehem ya shetani na jeshi lake kufanya kazi? Na kama ni sehemu kweli ya shetani na jeshi lake kufanya kazi, huyo shetani anawezaje kufanya kazi huku akisikiliza nyimbo za kumsifu Mungu, hasimu wake?.
 
Akuna nyimbo za dini zote ni nyimbo za kidunia na zmeimbwa na wahuni na maraya tu
Waimbaji wanavaa modo wanavaa vimini na wao wanacharge mtu kuangalia shoo yao na bado kuna wengne wanalilia pesa za mirabaha za basata kwaiyo hao ni wasanii km walivyo wasanii wengne na ndo maana wanamatendo km ya wasanii wengne mnaowaitwa wa kidunia
Shida ni kuwa kwa uwelewa wetu ikipigwa Kaswida inahusishwa na Uisilam na Ikipigwa kwanya/gospel inahusishwa na ukristo, inakuwa kama alama isiyo rasmi ya dini hiyo. Ndio maana kama ulisikia Mufti aloyoa tamko kukataza wanapiga kaswida na kucheza kama miziki mingine.

Haijalishi hao waimbaji wanafanya nini, ule wimbo utabaki kuitambulisha dini.

Napia si waimbaji wote wana sifa ulizozitaja, usihukumu wote kwa sababu ya wachache.
 
Nani alikwambia bar ni sehem ya shetani na jeshi lake kufanya kazi? Na kama ni sehemu kweli ya shetani na jeshi lake kufanya kazi, huyo shetani anawezaje kufanya kazi huku akisikiliza nyimbo za kumsifu Mungu, hasimu wake?.
Narudia nukta yangu kuwa Pombe ni moja ya zana za shetani kumuingiza mtu katika uasi, na huwezi kukataa kuwa bar ni sehemu moja pana mambo mengi ya dhambi hata umalaya unafanyika sana Bar. (Ila si sehemu pekee panakofanyika umalaya). Na ndio hukuti muuza bar amevaa kiheshima, lazima wavae nguo taiti na wenye bar wanatafuta wadada wenye sura na shepu zao kama wahudumu.

Hukuona zile karatasi za meseji za wahudumu wa bar kwa wateja wao, wanwaandikia namba zao za simu?

Hukusikia malalamiko ya wahudumu wa bar kushikwashikwa makalio na wateja?

Sijui kama kuna cha kutetea hapo, hata kama bar ni kiwanja chako.
 
Kusema ukweli huwa nakereka sana kusikia nyimbo za dini, zinapigwa kwenye sehemu za starehe, hasa Bar. Sehemu hizi ni sehemu Shetani na jeshi lake wanafanya kazi zao kwa ufanisi, na anaona ni kama kuikosea heshima dhana ya kuwa nyimbo za dini ni sehemu ya kuabudu.

Kwenye hizi Bar, zinapopigwa nyimbo hizi wakati watu wamelewa, naona ni kama kumkebehi Mungu.

Na pia ni kuzikosesha heshima nyimbo hizi, ambazo zilipaswa kuzikumbusha nyoyo Utukufu wa Mungu.

Yesu mwenyewe alikaa katikati ya starehe kwa Malengo, unakereka nini? Amekuwa kwa waliopotea, wako humo.
 
Kusema ukweli huwa nakereka sana kusikia nyimbo za dini, zinapigwa kwenye sehemu za starehe, hasa Bar. Sehemu hizi ni sehemu Shetani na jeshi lake wanafanya kazi zao kwa ufanisi, na anaona ni kama kuikosea heshima dhana ya kuwa nyimbo za dini ni sehemu ya kuabudu.

Kwenye hizi Bar, zinapopigwa nyimbo hizi wakati watu wamelewa, naona ni kama kumkebehi Mungu.

Na pia ni kuzikosesha heshima nyimbo hizi, ambazo zilipaswa kuzikumbusha nyoyo Utukufu wa Mungu.
Ndugu muandishi.. unaumia ukiwa wapi?
 
Yesu mwenyewe alikaa katikati ya starehe kwa Malengo, unakereka nini? Amekuwa kwa waliopotea, wako humo.
Mbona hukuti kaswida zinapigwa Bar, au hakuna waislamu walevi????

nilichomaanisha ni kuwa hizi nyimbo hazijalishi zinaimbwq na nani, zinasimama kama alama mojawapo ya dini husika, zinapopigwa sehemu zile ni kama kudhalilisha dini husika na kufanya vya dini husika kuonekana si ya maana.
 
Basi na watu wa Jumuiya waanze kuweka vikao vyao kwenye bar za jirani na wanapoishi, wapeane neno huku wanapata moja mbili.
Tembea uone kuna baadhi ya Bar na Pub hufanywa sehemu ya Jumuiya na watu wa madhehebu hususani hawa wa Lutheri km sijakosea waprotestant nimeona mara kadhaa wakiendesha Jumuiya kwenye Bar na Pub fulani asubuhi maana pana kaukumbu na viti vya kutosha,
 
Kusema ukweli huwa nakereka sana kusikia nyimbo za dini, zinapigwa kwenye sehemu za starehe, hasa Bar. Sehemu hizi ni sehemu Shetani na jeshi lake wanafanya kazi zao kwa ufanisi, na anaona ni kama kuikosea heshima dhana ya kuwa nyimbo za dini ni sehemu ya kuabudu.

Kwenye hizi Bar, zinapopigwa nyimbo hizi wakati watu wamelewa, naona ni kama kumkebehi Mungu.

Na pia ni kuzikosesha heshima nyimbo hizi, ambazo zilipaswa kuzikumbusha nyoyo Utukufu wa Mungu.
Usijali kumbuka yesu hakutususbiri mbinguni ili atuokoe bali alishuku kwenye dunia ya djambi akaishi kula na kunywa na wadhambi
 
Tembea uone kuna baadhi ya Bar na Pub hufanywa sehemu ya Jumuiya na watu wa madhehebu hususani hawa wa Lutheri km sijakosea waprotestant nimeona mara kadhaa wakiendesha Jumuiya kwenye Bar na Pub fulani asubuhi maana pana kaukumbu na viti vya kutosha,
Muda huo shughuli za bar zinakuwa zimesimama.... na wanapofuata hapo ni venue tu, sasa waende jioni, mida ya saa moja hadi saa tatu usiku, itatosha.
 
Back
Top Bottom