Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 85,784
- 145,596
Samia kaongea kwa kuelewa kuwa Tanzania ishasaini mikataba ya kimataifa ya haki za binadamu. Labda watu ambao hamjatoka Tanzania, au hamjafuatilia hili jambo kwa karibu kimataifa, mnaweza kuwa na ugumu wa kuelewa hili jambo kutokana na muktadha wa kimataifa. Kimataifa, haki za mashoga ni sehemu ya haki za binadamu. Yani ni sawa na haki za watu weusi kutotaka kubaguliwa kwa rangi ya ngozi zao.Na nukuu maneno haya amesema hivi “Msiwalegeze watoto wetu fanyaneni wakubwa kwa wakubwa watoto waache”
Chawa nawasubiri muandamane kuunga mkono au kumpongeza mama yenu karuhusu fanyaneni wakubwa lazima tutaelewana tu dhambi tulioifanya itaturudiaView attachment 2581271
Ndiyo maana hata kabla Samia hajawa rais,Makonda aliwaandama mashoga, halafu ikabidi Waziri wa Mambo ya Nje Marehemu Balozi Dr. Mahiga aje kusawazisha mambo na kusema maneno yale yalikuwa ni ya Makonda binafsi. Si ya serikali. Na jibaba mwenyewe anayependa kuwasema mabeberu (Jiwe) alikaa kimya. Kwa sababu alijua mziki ule ni wa kimataifa hatauweza.
Samia hana ubavu wa kulianzisha kwenye ushoga wakati kila siku anaongea na kina Kamala Harris wanampa somo, na yeye misaada anaitaka.
Zaidi, suala la ushoga kwa watu wazima ni jambo la kulindwa ki faragha za kikatiba , nchi za kidemokrasia hazibagui watu kwa dini, rangi, kabila, umri wala sexual orientation. Mkianza kubagua watu kwa sexual orientation kwa sababu ni minorities tu, basi hakuna sababu ya kutobagua minorities wengine wowote.
Samia kasema exactly alichotakiwa kusema katika ulimwengu huu.
Watu wazima wana haki ya kufanyana wanavyotaka, si kazi ya serikali wala kazi yako kuwaingilia.
Watoto wadogo hawatakiwi kuingiliwa kivyovyote vile, bila kujali ushoga au straight.
Ila, naelewa Watanzania wengi sana bado hawaelewi suala la autonomy.
Yani ni hivi, kama wewe usivyopenda ushoga na ukaachiwa kuwa na haki zako uwe na mtu wa different sex, kuna watu hawataki kuwa na mtu wa different sex wanataka kuwa na mtu wa same sex. Kama wewe usivyitaka kulazimishwa ufanye usichotaka, na wao pia hawataki kulazimishwa wafanye wasichotaka.
As long as ni watu wazima, hawajalazimishwa, wewe kinachokuwasha ni nini?
Serikali iache kufukuzana na wezi aliowataja CAG ije kuangalia nani anamfira nani? Kwa watu wazima wenye akili zao na walioamua wenyewe kufanyana wanachotaka?
Na nyie watu wazima mnaona sawa hilo?
Mimi si mshabiki wa Samia, lakini katika hili namuunga mkono.
Zaidi ya argument za kidini, ambazo ni mufilisi katika nchi secular, hakuna argument dhidi ya ushoga kwa watu wazima waliokubaliana katika nchi inayothamini uhuru wa watu binafsi inayoweza kusimama.
Ila, Watanzania wengi hatuelewi uhuru binafsi ni nini, ndiyo maana watu wanapinga ushoga kwa mkumbo.
Wakati matatizo yao mengi makubwa ni ya kiuchumi, na wanayakubali tu bila ya kuyapinga.
Ni kama vile dini zime short circuit akili za watu wawe wana prioritize mambo yasiyo na priority, wakati mambo ya priority yanaachwa.

