Umeongea kitu ambacho mchana huu kimenifikirisha sana.
Nimetoka Airport naelekea Kariakoo huko aisee barabarani ni noma, kila mstimu wa taa una bango lake.
Sasa nikawa najiuliza
Kama bango moja linagharimu hata Tsh 50,000 kwa uchapishaji, usafirishaji, na usimikaji na kuna mabango zaidi ya 500 tu kwenye Nyerere Road—tunazungumzia zaidi ya milioni 25 kwa kipande kimoja cha barabara.
Ukiongeza Kigamboni, Morogoro Road, na maeneo mengine ya jiji, huwezi kuepuka kufikiria kuwa huu ni mradi wa mabilioni unaofanywa kwa jina la “kampeni” lakini bila uwazi wa bajeti wala tija ya moja kwa moja kwa mwananchi.
Na hapo bila kuhesabia yale mabango ya kwenye Big Screen kama ambalo lipo Tazara getini na lile la mbele karibu na Sigara. Na bado kuna yale ya ziada ambayo yamebandikwa kwenye flyover chini.
Mwanzo niliamini huwenda ile michango waliyopitisha kwa wafanyabiashara kwa ajili ya ku fund kampeni ndio inayotumika kwenye haya mabango. Lakini mazingira yanaonesha huwenda sio kweli.
Kwasababu tunaona TRA na watu wa Halmashauri wamekuwa na root nyingi siku hizi mitaani kama mashahidi wa Yehova kuliko kivindi vyote vilivyopita.
TRA na Halmashauri wanazidi kuwa wakali kwa wafanyabiashara wadogo, huku mamilioni yakitumika kwa mabango yasiyoleta tija ya moja kwa moja.