Nyerere hakuwahi kupata tunzo ya Nobel

Hapa Tunazungumzia Tuzo Ya Aman Ya Nobel. Hii Tuzo Watu Wengi Wanao Amini Amani Katika Mapigo Akiwemo George Bush Na Pinda Miaka 1000, Hawawezi Kuipokea! Kwa Case Ya Mwalimu Ni Kwamba Alikuwa Nauwezo Mkubwa Wa Kusorve Matatizo Kwa Mdomo, Lakini Aliamini Katika Mapigo! Wakati Furani Nilisikia Watanzania 3000, Waliuawa Na Mreno Mozambique, Kuficha Aibu Kombe Likafunikwa Hadi Miili Ilivyo Rudishwa Hv Karibuni! Watanzania Waliuawa Angola Na Zimbabwe, Uganda - Kiko Akatangaza WATANZANIA WANA KUFA KAMA KUKU, / KAMA MITI IMELAZWA! Ikabidi Arudishwe Aje Anae Tangaza Bara~bara! Kwa Tathmini Hii, Anastahili Tuzo Ya Amani?
Ni Kiko au Jacob Tesha? Anyway, De klerk naye alikuwa mbaguzi na dikteta. Yeye alibagua, aliua na kufunga weusi na dunia ilitambua. Mwisho wa siku alipewa tuzo pamoja na mzee Mandela. Kwa maoni yangu wala huyu kaburu hakustahili. Yeye na Nyerere kuna tofauti kubwa sana. Nyerere alikuwa na mrengo wa kuikomboa kusini ya Afrika. Hao critics hawakujua kuwa mapigano yanahusisha mauaji pia? Obama anavyotuma ndege tupu nchi za watu kwenda kupeleleza na kushambulia hawaoni?
 
Ni nani awezaye kuuzawadia mkuki uliomjeruhi?Kila jambo na wakati wake angezawadiwa vipi wakati alikuwa mstari wa mbele kuondosha minyororo ya wakoloni? tena kwa kutumia mtutu wa bunduki!hapo amani inatoka wapi?
 
Ni nani awezaye kuuzawadia mkuki uliomjeruhi?Kila jambo na wakati wake angezawadiwa vipi wakati alikuwa mstari wa mbele kuondosha minyororo ya wakoloni? tena kwa kutumia mtutu wa bunduki!hapo amani inatoka wapi?


Ye mbona hapa hakutumia huo mtutu wa Bunduki matokeo yake tukapewa uhuru mdebwedo?
 
Nimesoma wasifu wa viongozi wote walopewa hiyo tuzo ya Nobel, mimi sioni kama nyerere anastahiki. Kwa sababu wote walopewa ukiona wasifu wao ni watu walotetea mazuri katika nchi zao NA SIO NJE YA NCHI ZAO!

Nyerere kipi kikubwa alikifanya hapa Tanganyika enzi hizo mpaka ikawa TAnzania apewe hiyo Tuzo! hebu naomba uniorodheshee nini alikifanya kwa nchi yake na wananchi wake wa TAnganyika na baadae TAnzania mpaka leo atunukiwe TUNU hiyo adhimu!

Nyerere alianzisha azimio la arusha na kutaifisha mali za wananchi wake na kuwaacha masikini na kusababisha uchumi wa nchi KUPOROMOKA!,
Akaona hiyo haitoshi akawalazimisha watu kuanzisha vijiji vya ujamaa kwa nguvu na kuwatoa watu katika makazi yao nakuwapeleka sehemu ambazo zilikuwa mapori na kusababisha wengine kuliwa na simba na kugongwa na nyoka wenye sumu kali na kuwaacha wanawake wakiwa wajane na watoto wakiwa yatima.
Upande wa Zanzibar (Ungaja na PEmba) akawaingiza katika muungano ambao unaonekana kabisa ni hauna tija kwa wa TAnganyika na wazanzibar na kuwaacha watu wakilalama mpaka leo !
Akaona haitoshi , akaingia katika vita isiyo yake kwa sababu tu ya kumsaidia swahiba wake Obote na kusababaisha UMASIKINI WA HALI YA JUU kwa nchi na wananchi wake kwa ujumla.

Watu walikuwa wanakula NJANO unga wa kulisha farasi kule marekani ambao sasa hivi ndio angalau una heshima! jamani

Mtu kwanza unaze na nyumbani kwako halafu ndio uende nje ! sasa kipi kikubwa babu nyerere alikifanya mpaka apate hiyo Nobel award! USINCHEKESHE FaizaFoxy anasema !
Hapo kwenye bold, hebu tujuze, mali zilitaifishwa kwa madhumuni gani, na baada ya kutaifishwa zilitumika kwa manufaa ya nani?
 
Back
Top Bottom