Nyerere angewasikiliza Mtei na Kambona uchumi wa Tanzania ungekuwa mkubwa sana

Nyerere angewasikiliza Mtei na Kambona uchumi wa Tanzania ungekuwa mkubwa sana

Kamundu

Platinum Member
Joined
Nov 22, 2006
Posts
9,268
Reaction score
13,894
Nyere alishidwa sehemu moja tu kwenye uchumi. Wakati wa nyerere Tanzania ilikuwa masikini na hakufanikiwa kuja na suluhu ya maana.

Sera na maazimio yake hayakufanikiwa ndiyo maana hadi leo Kenya nchi ndogo zaidi imetuzidi uchumi. Kuna watu wawili ambao angewasikiliza tusingekuwa hapa Edwin Mtei na Oscar Kambona.

Mtei kwenye sera za uchumi na kambona kwenye mfumo wa demokrasia
 
Nyere alishidwa sehemu moja tu kwenye uchumi. Wakati wa nyerere Tanzania ilikuwa masikini na hakufanikiwa kuja na suluhu ya maana. Sera na maazimio yake hayakufanikiwa ndiyo maana hadi leo Kenya nchi ndogo zaidi imetuzidi uchumi. Kuna watu wawili ambao angewasikiliza tusingekuwa hapa Edwin Mtei na Oscar Kambona. Mtei kwenye sera za uchumi na kambona kwenye mfumo wa demokrasia
Huu upumbavu wa kujilinganisha na Kenya ambayo uchumi umeshikiliwa na familia chache hasa ya Kenyatta sijui utaisha lini!?? Wakenya wengi wana maisha magumu kupitiliza. Sera za baba wa taifa zimesaidia sana karibu kila mtu kufurahia keki ya taifa.
 
Nyere alishidwa sehemu moja tu kwenye uchumi. Wakati wa nyerere Tanzania ilikuwa masikini na hakufanikiwa kuja na suluhu ya maana. Sera na maazimio yake hayakufanikiwa ndiyo maana hadi leo Kenya nchi ndogo zaidi imetuzidi uchumi. Kuna watu wawili ambao angewasikiliza tusingekuwa hapa Edwin Mtei na Oscar Kambona. Mtei kwenye sera za uchumi na kambona kwenye mfumo wa demokrasia
Hapo nyumbani kwenu hawakuwepo Mtei na Kambona; mbona hakuna tofauti kubwa na hapa?
Mada nyingine mnajianzishia tu wakati hamjui chochote mnachokiwasilisha.

Kenyatta aliwafikisha mbinguni?

Ni miaka mingapi tokea Nyerere atoke madarakani; hawa wengine wooote waliofuata nao hawakuwa na uwezo waliokuwa nao Mtei na Kambona?
Sasa tutawatoa wapi hao unaowataka wewe?
 
Huu upumbavu wa kujilinganisha na Kenya ambayo uchumi umeshikiliwa na familia chache hasa ya Kenyatta sijui utaisha lini!?? Wakenya wengi wana maisha magumu kupitiliza. Sera za baba wa taifa zimesaidia sana karibu kila mtu kufurahia keki ya taifa.
Huyu ni mkikuyu aliyezamia Tanzania; lakini kila mara anaona hali ya huko kwao ndiyo bora. Sasa sijui hapa alikuja kufanya nini?
Alipandia mgongoni mwa Tanzania kwenda Marekani, lakini roho yake ipo nyumbani Kenya.
Sijui kwa nini yeye anatamani sana Tanzania igeuke kuwa Kenya; hili jambo silielewi litamsaidia nini yeye.
 
Sera na maazimio yake hayakufanikiwa ndiyo maana hadi leo Kenya nchi ndogo zaidi imetuzidi uchumi. Kuna watu wawili ambao angewasikiliza tusingekuwa hapa Edwin Mtei na Oscar Kambona.
Miaka zaidi ya 40 tangu alipoacha uongozi mmeshindwa kurekebisha hizo sera mbovu?

Unaandika as if Nyerere hakuna alichofanya kwenye uongozi wake.
 
Huu upumbavu wa kujilinganisha na Kenya ambayo uchumi umeshikiliwa na familia chache hasa ya Kenyatta sijui utaisha lini!?? Wakenya wengi wana maisha magumu kupitiliza. Sera za baba wa taifa zimesaidia sana karibu kila mtu kufurahia keki ya taifa.
Nyerere kwa kusisitizia ujamaa aliweza kupunguza matabaka ndani ya Tanzania. Kule kujitambua kuwa sisi ni watanzania imekuwa tunu moja muhimu sana.

Haya machafuko ya October 29 nyuma yake pia kuna vilio vya tofauti kati ya walionacho na wasionacho, hizi vurugu zingeweza kutokea miaka ya 2000 mapema ikiwa kile alichokiweka vichwani mwetu Mwalimu JKN kingeanza kupuuziwa tangu nyakati zile.
 
Nyere alishidwa sehemu moja tu kwenye uchumi. Wakati wa nyerere Tanzania ilikuwa masikini na hakufanikiwa kuja na suluhu ya maana.

Sera na maazimio yake hayakufanikiwa ndiyo maana hadi leo Kenya nchi ndogo zaidi imetuzidi uchumi. Kuna watu wawili ambao angewasikiliza tusingekuwa hapa Edwin Mtei na Oscar Kambona.

Mtei kwenye sera za uchumi na kambona kwenye mfumo wa demokrasia
Naunga mkono hoja
P
 
Mkuu, kwani hao wazee walisemaje kwa Mwl. Nyerere mpaka ashindwe kuwasikia ili nasi tusikie na tujuike pamoja nawe kumlaumu.

Hawa viongozi waliofata kabla yake nao walishindwa kuwasikiliza hao wazee ili kurekebisha makosa yaliyofanywa?
 
Nyerere aliendesha nchi akijua kuna migodi mingi ya dhahabu, chuma na madini mengineyo lakini nyinyi mnaochimba madini hadi kwenye mbuga bado mnakopakopa.
wakati wake kulikuwa na viwanda vingi vikubwa lakini hakukuwa na mgao wa umeme lakini pamoja na kuwa na gesi huku bidhaa nyingi zikiagizwa nje bado mna mgao wa umeme.
 
Ninachomlaumu Nyerere kuacha katiba mbaya ambayo alijua inaweza kuja kutuletea mambo mabaya ya kiongozi kama yaliyo tokea 29/10/2025.
Jambo la pili Muungano wa hovyo.
Nyerere alitukosea sana watanganyika na wazanzibar kwenye katiba na Muungano.
 
Nyerere aliendesha nchi akijua kuna migodi mingi ya dhahabu, chuma na madini mengineyo lakini nyinyi mnaochimba madini hadi kwenye mbuga bado mnakopakopa.
wakati wake kulikuwa na viwanda vingi vikubwa lakini hakukuwa na mgao wa umeme lakini pamoja na kuwa na gesi huku bidhaa nyingi zikiagizwa nje bado mna mgao wa umeme.
1990 tulikuwa milioni 20 2025 tupo milioni 64. Changamoto alizokutana nazo Mwalimu hazifanani na za Samia.
 
Nyerere kwa kusisitizia ujamaa aliweza kupunguza matabaka ndani ya Tanzania. Kule kujitambua kuwa sisi ni watanzania imekuwa tunu moja muhimu sana.

Haya machafuko ya October 29 nyuma yake pia kuna vilio vya tofauti kati ya walionacho na wasionacho, hizi vurugu zingeweza kutokea miaka ya 2000 mapema ikiwa kile alichokiweka vichwani mwetu Mwalimu JKN kingeanza kupuuziwa tangu nyakati zile.
Absolutely
 
Zaidi ya nusu ya umaskini wetu unatokana na sheria na policies zetu wenyewe, angalia kwenye mambo ya kodi, biashara mpaka haki zetu wenyewe, imagine mwanasiasa wa kuteuliwa anaweza kukuweka ndani bila mashtaka au kukuzuia kuuza mazao yako uliyolima mwenyewe, ukiangalia msururu wa kodi anayolipa mfanyabiashara inakula karibu nusu ya faida, mfano nasikia Rwanda ni biggest exporter wa gold na nyingi inatoka Tanzania, na sababu nasikia ni bad policies za Tanzania ndio maana watu wanaenda kuuza Rwanda kupata faida kubwa (nitaleta uzi kuonyesha Rwanda inavyotengeneza billions kwa dhahabu ya Tanzania, kwa sera nzuri walizojiwekea)
 
Nadhani kila kitu kina Faida na Hasara.
Faida ya sera za ujamaa za Nyerere, Moja wapo ni kwamba sasa hivi kijana akimaliza chuo, Anaweza kununua ardhi huko Morogoro kwa hela alizo zichanga za Boom.

Hii ni tofauti na kenya, Kutokana na Kushamiri kwa Ubepari, Sawa uchumi upo lakini uchumi wa kenya sio inclunsive.

Uchumi wetu ni kweli kabisa ni mdogo lakini ni Uchumi Inclusive kuliko wa kenye, na unakua taratibu kwa kadri uchumi wa mtu mmoja mmoja unavo kua, hii inasaidia kupunguza gape la wenye nacho na wasio nacho
 
Zaidi ya nusu ya umaskini wetu unatokana na sheria na policies zetu wenyewe, angalia kwenye mambo ya kodi, biashara mpaka haki zetu wenyewe, imagine mwanasiasa wa kuteuliwa anaweza kukuweka ndani bila mashtaka au kukuzuia kuuza mazao yako uliyolima mwenyewe, ukiangalia msururu wa kodi anayolipa mfanyabiashara inakula karibu nusu ya faida, mfano nasikia Rwanda ni biggest exporter wa gold na nyingi inatoka Tanzania, na sababu nasikia ni bad policies za Tanzania ndio maana watu wanaenda kuuza Rwanda kupata faida kubwa (nitaleta uzi kuonyesha Rwanda inavyotengeneza billions kwa dhahabu ya Tanzania, kwa sera nzuri walizojiwekea)

Tanzania ilitakiwa kununua Gold kutoka kwa Wafanyabiashara Without asking questions.

Maswali maswali, Watu waki smurge Gold wanaenda kuuza Rwanda tunajikuta Tunapoteza kila kitu.
 
Back
Top Bottom