Nyama niliyokula sijui nitapike? Anyway, sikukusudia

cDNA

JF-Expert Member
Nov 10, 2016
353
348
Habari zenu wadau....
Napenda kushea nanyi kilichonikumba majuu.

Ni kawaida yangu kula menyu yoyote ile iwapo mbele yangu hasa nyama almuradi isiwe ya wanyama tunaokatazwa waislamu, haijalishi imechinjwa na muislamu au mkristo, mwanamke au mwanamme. Bongo wanyama waliwao na jamii kubwa ya TZ, pia waislamu hula isipokuwa wanyama wachache maarufu kama mbwa na Kitimoto. Pamoja na kuwepo kwa general formula (ktk uislamu) ya wanyama wasioliwa lakini mara nyingi hatutarajii waTZ kula wanyama kama paka na mfano wake.

Wakati fulani nilipokuwa moja ya nchi za Ulaya ktk shughui zangu nilienda kuwatembelea rafiki zangu wazungu. Waliniuliza vyakula gani ninakula...nikawajibu vyote kasoro nguruwe. Mbwa sikumtaja kwa kuwa Ulaya mbwa athaminiwa na kujaliwa mno na hawawezi kumchinja kama kitoweo. Safari mbili tofauti nilizokaribishwa kuwatembelea nilikula nyama za kawaida (ng'ombe, kuku). Safari ya tatu nikakuta wameandaa menyu kama kawaida na nilipoangalia kitoweo nikaona kama samaki mkubwa (mfano wa seewa) amekatwa vipande vingi (transversely).

Nilipokuwa naendelea kukamua...ni kawaida ya wazungu kuelezea aina ya chakula kilichomezani. Hapo wakataja nyama ile ni ya "Raccoon"...mbali ya classification yangu yote ya O' level na A' level hako kalikuwa kamsamiati kapya na kakanitoa jasho ila nikajipa moyo ni mnyama wa kawaida ambao kwetu ni halali kula...

Mi nikawajibu kuwa nilidhani ni samaki nyama imefanana mno na ya samaki. Wakasema ati nyama ile ni kutoka kwenye mkia.

Nilipomaliza makamuzi kikaletewa kitabu kikubwa kama BS wakijaribu kumdadavua huyo mnyama na kunionesha picha yake na kumpa sifa kede kede za akili n.k.

AYAA KUMBE MNYAMA MWENYEWE NDO HUYU! C KAMA PAKA TU...NILIJISIKIA VIBAYA KAMA KICHEFUCHEFU ILA KUTAPIKA CTAPIKI NIKAWA MNYONGE SANA BUT CKUWAONESHA HILO WENYEJI WANGU. Nikagundua kuwa nilipaswa niwape general formula ili wajue kuwa waislamu hatuli wanyama wenye sifa zipi kuliko kumtaja nguruwe pekee.

upload_2016-11-23_21-24-0.png

upload_2016-11-23_22-16-8.png
 

Attachments

  • upload_2016-11-23_21-20-17.png
    upload_2016-11-23_21-20-17.png
    60.7 KB · Views: 69
  • upload_2016-11-23_21-21-6.png
    upload_2016-11-23_21-21-6.png
    37.8 KB · Views: 66
  • upload_2016-11-23_21-22-53.png
    upload_2016-11-23_21-22-53.png
    37.8 KB · Views: 74
Umeyataka mwenyewe,wao walikuwa makini na ndiyo maana walikuuliza na ukawajibu Unakula Vyote isipokuwa Nguruwe.
 
Mi huwa sina miiko kwenye misosi. Konokono, mendw, farasi, punda, nyani, mbwa, kenge, huyo racoon wako, ngedere, ng'ombe, chair fire, bear na wengine unaowajua wewe kasoro nyau, wote ni chakula mradi wawe wameandaliwa vyema tu! Kichefuchefu kitakuua ugenini, talking from experience.
 
halafu wazungu wanapenda kujadili chakula wakati unakulaa...! Yani lazima wataulizana tu umechanganya nini na nini huku? Usitamani kusikia maana vingine kibongobongo hatuli!
 
ukome kuzamia zamia vya watu
Habari zenu wadau....
Napenda kushea nanyi kilichonikumba majuu.

Ni kawaida yangu kula menyu yoyote ile iwapo mbele yangu hasa nyama almuradi isiwe ya wanyama tunaokatazwa waislamu, haijalishi imechinjwa na muislamu au mkristo, mwanamke au mwanamme. Bongo wanyama waliwao na jamii kubwa ya TZ, pia waislamu hula isipokuwa wanyama wachache maarufu kama mbwa na Kitimoto. Pamoja na kuwepo kwa general formula (ktk uislamu) ya wanyama wasioliwa lakini mara nyingi hatutarajii waTZ kula wanyama kama paka na mfano wake.
Wakati fulani nilipokuwa moja ya nchi za Ulaya ktk shughui zangu nilienda kuwatembelea rafiki zangu wazungu. Waliniuliza vyakula gani ninakula...nikawajibu vyote kasoro nguruwe. Mbwa sikumtaja kwa kuwa Ulaya mbwa athaminiwa na kujaliwa mno na hawawezi kumchinja kama kitoweo. Safari mbili tofauti nilizokaribishwa kuwatembelea nilikula nyama za kawaida (ng'ombe, kuku). Safari ya tatu nikakuta wameandaa menyu kama kawaida na nilipoangalia kitoweo nikaona kama samaki mkubwa (mfano wa seewa) amekatwa vipande vingi (transversely). Nilipokuwa naendelea kukamua...ni kawaida ya wazungu kuelezea aina ya chakula kilichomezani. Hapo wakataja nyama ile ni ya "Raccoon"...mbali ya classification yangu yote ya O' level na A' level hako kalikuwa kamsamiati kapya na kakanitoa jasho ila nikajipa moyo ni mnyama wa kawaida ambao kwetu ni halali kula...Mi nikawajibu kuwa nilidhani ni samaki nyama imefanana mno na ya samaki. Wakasema ati nyama ile ni kutoka kwenye mkia. Nilipo maliza makamuzi kikaletewa kitabu kikubwa kama BS wakijaribu kumdadavua huyo mnyama na kunionesha picha yake na kumpa sifa kede kede za akili n.k. AYAA KUMBE MNYAMA MWENYEWE NDO HUYU! C KAMA PAKA TU...NILIJISIKIA VIBAYA KAMA KICHEFUCHEFU ILA KUTAPIKA CTAPIKI NIKAWA MNYONGE SANA BUT CKUWAONESHA HILO WENYEJI WANGU. Nikagundua kuwa nilipaswa niwape general formula ili wajue kuwa waislamu hatuli wanyama wenye sifa zipi kuliko kumtaja nguruwe pekee.
View attachment 438632
View attachment 438640
 
Mi huwa sina miiko kwenye misosi. Konokono, mendw, farasi, punda, nyani, mbwa, kenge, huyo racoon wako, ngedere, ng'ombe, chair fire, bear na wengine unaowajua wewe kasoro nyau, wote ni chakula mradi wawe wameandaliwa vyema tu! Kichefuchefu kitakuua ugenini, talking from experience.
Kasoro nyau tu kwahiyo hata binadamu ni Poa tu?
 
Umeyataka mwenyewe,wao walikuwa makini na ndiyo maana walikuuliza na ukawajibu Unakula Vyote isipokuwa Nguruwe.
Ni kweli mkuu...Wazungu nawakubali sana wapo wawazi na hawapendi kukulisha usichokipenda. Mimi ndiye niliyekosea ktk kutoa jibu lisilojitosheleza.
 
Ladha ya chakula ni mdomoni tu hasa kwenye ulimi. Tumbo na mwili unaohitaji hicho chakula havibagui alimradi tu chakula chenyewe kisiwe sumu
Philosophy ya chakula ni dawa na nishati ya mwili vinhine vyote mbwembwe tuu
Wabahili hutumia kanuni hiyo kujinyima kula vyakula bora vya gharama za juu.
 
Huyo raccoon hauzwi buchani ila ukibahatika kumla ujue aligongwa na gari motorway wakamuokota na kukukaribisha.
Naona hawakumalizia stori yote
 
Ni kweli mkuu...Wazungu nawakubali sana wapo wawazi na hawapendi kukulisha usichokipenda. Mimi ndiye niliyekosea ktk kutoa jibu lisilojitosheleza.
appreciation to that commet mkuu.....but haina mbaya kwani you did not before kuwa hukuruhusiwa kula as per your faith
 
Habari zenu wadau....
Napenda kushea nanyi kilichonikumba majuu.

Ni kawaida yangu kula menyu yoyote ile iwapo mbele yangu hasa nyama almuradi isiwe ya wanyama tunaokatazwa waislamu, haijalishi imechinjwa na muislamu au mkristo, mwanamke au mwanamme. Bongo wanyama waliwao na jamii kubwa ya TZ, pia waislamu hula isipokuwa wanyama wachache maarufu kama mbwa na Kitimoto. Pamoja na kuwepo kwa general formula (ktk uislamu) ya wanyama wasioliwa lakini mara nyingi hatutarajii waTZ kula wanyama kama paka na mfano wake.

Wakati fulani nilipokuwa moja ya nchi za Ulaya ktk shughui zangu nilienda kuwatembelea rafiki zangu wazungu. Waliniuliza vyakula gani ninakula...nikawajibu vyote kasoro nguruwe. Mbwa sikumtaja kwa kuwa Ulaya mbwa athaminiwa na kujaliwa mno na hawawezi kumchinja kama kitoweo. Safari mbili tofauti nilizokaribishwa kuwatembelea nilikula nyama za kawaida (ng'ombe, kuku). Safari ya tatu nikakuta wameandaa menyu kama kawaida na nilipoangalia kitoweo nikaona kama samaki mkubwa (mfano wa seewa) amekatwa vipande vingi (transversely).

Nilipokuwa naendelea kukamua...ni kawaida ya wazungu kuelezea aina ya chakula kilichomezani. Hapo wakataja nyama ile ni ya "Raccoon"...mbali ya classification yangu yote ya O' level na A' level hako kalikuwa kamsamiati kapya na kakanitoa jasho ila nikajipa moyo ni mnyama wa kawaida ambao kwetu ni halali kula...

Mi nikawajibu kuwa nilidhani ni samaki nyama imefanana mno na ya samaki. Wakasema ati nyama ile ni kutoka kwenye mkia.

Nilipomaliza makamuzi kikaletewa kitabu kikubwa kama BS wakijaribu kumdadavua huyo mnyama na kunionesha picha yake na kumpa sifa kede kede za akili n.k.

AYAA KUMBE MNYAMA MWENYEWE NDO HUYU! C KAMA PAKA TU...NILIJISIKIA VIBAYA KAMA KICHEFUCHEFU ILA KUTAPIKA CTAPIKI NIKAWA MNYONGE SANA BUT CKUWAONESHA HILO WENYEJI WANGU. Nikagundua kuwa nilipaswa niwape general formula ili wajue kuwa waislamu hatuli wanyama wenye sifa zipi kuliko kumtaja nguruwe pekee.

Mkuu Mkuu shushia na maji maisha yaendelee.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom