NA MM NAPINGANA NA WEWE KWA NGUVU ZOTE kwani humjui Nyaisanga (Uncle J)
Si Waandishi wa habari tu waliomsaliti hata hao Matajiri wakubwa hawakumthamini kabisa hasa kwa vitu alivyobuni na kuliingizia shirika husika mamilioni ya pesa.
- Yeye ndiye aliyekuwa mtangazaji wa kwanza kabisa wa RTD kutangaza DISCO live kutoka BILLICANAS ilipofunguliwa kwa maray a kwanza enzi hizo na nakumbuka ilikuwa kila Ijumaa usiku
- Yeye ndiye aliyebuni kuziagiza bendi za DRC na za nje kuja kupiga muziki na kutangaza live kwenye redio lakini alipokuja kuliingiza Shirika fulani hasara ya mamilioni ALIFUKUZWA KAZI kwani Bendi hiyo haikuja, na lawama zikamuangukia
- Nyaisanga keshawahi tangaza mpaka Redio za Dodoma za kina Kifimbo FM na wakati huohuo jamaa yake majura akiwa na Redio hapahapa na asimsaidie
umenisikitisha sana unaposema uipanda bangi utavuna Bangi
Kumbuka binadamu ndio tulivyo,
- ukijitolea sana WANAFIKI MNAONA WIVU NA KUITA NI KIHEREHERE
- Mpango mzima ulioubuni ukifanikiwa WOTE MNAJIFANYA NI KAMATI NA MNAMFUNIKA KABISA MHUSIKA
Mauza uza jiulize Mkeo yupo na jeneza pale Leaders Club , na waliomdanganya kuwa MWILI usipelekwe kwanza tumuage hawaonekani na gharama ameachiwa wakati Morogoro walishazibeba ungevuta bangi au mahindi? na kutoka sandukuni huwezi
RIP NYAISANGA[/QUOTE
Mkuu nimekuelewa sana, ila hilo kosa la kamati ya mazishi la leaders hata mm sijapendezwa nalo limenisikitisha sana.mimi nalopinga ni pale mtu anaposema watu hawakumsaidia uncle J rip...umahiri wa uncle J ulikua ni kigezo tosha cha kumpeleka popote bila msaada wa mtu yeyote tatizo bongo wamezoea maisha ya whos know who?na hayo ndo yanawalemaza wengi.Mie nafikiri suala la kufanya kazi nje ni yeye tu labda hakupenda na si vingine...hilo suala la Majura mie sitaki kulijadili hapa but nafikiri labda Uncle J mwenyewe hakutaka kufanya kazi pale..anyway hii ni post yangu ya mwisho kuhusu hii issue tumuache apumzike kwa amani ndugu yetu na rafiki yetu mpendwa..amen.