BARDIZBAH
JF-Expert Member
- Jan 11, 2017
- 6,417
- 12,987
Msanii wa Bongo Fleva, Selemani Mvamba maarufu kama Spack, amefariki dunia leo Aprili 27, 2026 nyumbani kwake Chanika jijini Dar es Salaam.
Spack alijipatia umaarufu mkubwa kupitia kundi la Tip Top Connection, pamoja na nyimbo ya Nipe Ripoti aliyoshikiana na Tundaman.
Akizungumza na Mwananchi leo Jumatatu, Aprili 27, 2026, Meneja wa msanii huyo Abdulrahman Hassan maarufu Malefti amesema jana alizungumza na msanii huyo kuhusu mpango wao wa ‘kushoot’ video ya wimbo mpya.
"Ni kweli amefariki mara ya mwisho nimezungumza nae saa saba usiku. Akaaga akaenda kulala sasa asubuhi alienda kugongewa kwa ajili ya kutoa nauli za watoto kwenda shule akawa haamki,”
“Jana tulivyozungumza alikuwa mzima alinitumia wimbo akasema niusikilize kwa sababu leo tulikuwa tunaenda Sinza kukutana na director Lenzo kwa ajili ya kuandika script za video ya wimbo wake mpya," amesema meneja.
Spack alijipatia umaarufu mkubwa kupitia kundi la Tip Top Connection, pamoja na nyimbo ya Nipe Ripoti aliyoshikiana na Tundaman.
Akizungumza na Mwananchi leo Jumatatu, Aprili 27, 2026, Meneja wa msanii huyo Abdulrahman Hassan maarufu Malefti amesema jana alizungumza na msanii huyo kuhusu mpango wao wa ‘kushoot’ video ya wimbo mpya.
"Ni kweli amefariki mara ya mwisho nimezungumza nae saa saba usiku. Akaaga akaenda kulala sasa asubuhi alienda kugongewa kwa ajili ya kutoa nauli za watoto kwenda shule akawa haamki,”
“Jana tulivyozungumza alikuwa mzima alinitumia wimbo akasema niusikilize kwa sababu leo tulikuwa tunaenda Sinza kukutana na director Lenzo kwa ajili ya kuandika script za video ya wimbo wake mpya," amesema meneja.