Nusu siku ndani ya jeneza

Nusu siku ndani ya jeneza

Daah,haya mambo hua sipendagi,sasa mpka kesho tena saa kama hiyo..kumi na besenga ila kila baada ya dk 20 nachek ka umebadil mawazo
 
Nusu Siku Ndani ya Jeneza-20-


ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:

Kazi zao zenye kuwapa mafanikio ni uhusiano kataika jamii, ushauri wa masuala ya ndoa. Wengi

waliotaka kupeana talaka waliposuluhishwa na wenye nyota hii walirudiana na ndoa kudumu.

Pia ni wafanyabishara wakubwa sana hasa ya mambo ya sanaa, mambo ya sheria au uhakimu. Mtu

mwenye nyota hii akiwa wakili anashinda sana kesi na wateja kwake hawapungui. Kama atakuwa

hakimu atakuwa anatoa huku ya haki kwenye kesi ngumu.

SASA ENDELEA


Kwa wale wanaoamua kufanya biashara ya sanaa hufanikiwa sana, mfano ni kama wanamuziki akina Lil Wayne, Bella Thorne, Eminem, Kim Kardashian, Will Smith, Ushar Raymond na Snoop Dogg.
Wapo marais wenye nyota hii na waliongoza mataifa makaubwa, mfano ni Jimmy Carter wa Marekani. Marais wengi wenye nyota hii hufanya kazi zao kwa busara sana na utulivu, hawakurupuki, si wapenda vita wala udikteta.
Wanapoachia madaraka wengi huishi maisha ya heshima sana na jamii huwatambua miaka na miaka.
Wacheza mpira wenye nyota hii pia hung'ara sana ulimwenguni, kama akina George Opong Weah, Muset Ozil, Ibrahimovic, Vidoc, Defoe na wengine kibao ambao nyota zao ni Libra na wakafanya vizuri kwenye mpira wa miguu.
Ipo nyota inaitwa Nge, lugha ya kigeni inaitwa Scorpio. Hii ni nyota ya nane kati ya kumi na mbili za duniani. Hiii ni nyota yenye majukumu mengi sana, dunia imeendelea kupitia watu wenye nyota hii. Kama wanadamu wangejua wangefanya juu chini kuzaa kipindi cha nyota hii ya Scorpio.
Mtu mwenye nyota hii ili afinikiwe anatakuwa kufanya kazi za madawa, upelelezi na uchunguzi. Hata wavumbuzi wengi wa mambo ya kihistoria wapo kwenye kundi la nyota hii.
Watu waliogundua vitu vingi vya kisayansi, kama ndege, meli nakadhalika wanatoka kwenye nyota hii.
Lakini kuna binadamu wanasumbuliwa sana na mambo ya mapenzi, washauri wao wakubwa wanatakiwa watu wenye nyota hii.
Kuna nyota inaitwa Sagittarius au Mshale. Hii nyota inawafaa sana watu ambao watafanya kazi za kusafiri, kutoka sehemu moja kwenda nyingine kupeleka bidhaa au kuchukua, lakini wanasheria wazuri sana wanatokea kwenye nyota ya Mshale. Wakiwa waandishi wa habari wanakuwa mahiri zaidi na huvuma muda wote.
Ili wawe na mafanikio makubwa, wenye nyota hii wanatakuwa pia kufanya kazi ya ualimu, wachungaji wa makanisa wanaweza kujikuta wanavuta waumini wengi sana kama wana nyota ya Mshale. Wachungaji wenye nyota hii, wanakuwa na uwezo mkubwa sana wa kuponya wagonjwa, kufukuza mapepo na kutenda miujiza mingi ya kuwashangaza wengi.
Pia wenye nyota hii wana uwezo mkubwa wa akili, kufikiri na kukwamuka kutoka katika matatizo. Mwanamke yeyote, hata kama ana nyota ya Simba, akiolewa na mwenye nyota ya Mshale atakuwa chini yake tu.
Nizungumzie nyota ya Capricorn au Mbuzi kwa jina la kujulikana kule duniani mnakotokea nyinyi. Hii nyota huwa ya utajiri mkubwa kama wahusika watafanya shughuli zifuatazo:
Uinjinia, uchoraji wa ramani za majengo, watafiti wa ardhi, kuajiriwa serikalini. Mara nyingi mwenye nyota hii akiajiriwa serikalini hupanda cheo kwa kasi sana, anaweza kuanzia chini akapanda hadi kuwa waziri na watu wakamshangaa.
Lakini wanasiasa wengi mahiri mkiwachunguza kwa karibu wana nyota hii ya Mbuzi. Tena wengi wanapopanda majukwaani hupigiwa makofi sana, hushangiliwa. Wana uwezo wa kuwashawishi watu kufanya jambo fulani, mfano kupigiwa kura.
Mtu akiwa na nyota ya Mbuzi na akataka kugombea nafasi ya siasa huwashinda wenzake kwa kura nyingi sana, ni mahiri wa kujibu maswali ya watu kama ataulizwa.
Kabla sijaendelea napenda kuwaambia kuwa maskini wengi au fukara wengi ni wale wanaofanya shughuli ambazo nyota zao zinakataa. Mtu nyota yake anatakiwa kuwa mwalimu, anaamua kuwa mfugaji, huyu lazima atalia. Kama atakopa mkopo kwa ajili ya kununua ng'ombe ili afuge atajikuta ng'ombe wote wanakufa kwa sababu nyota yake inakataa.
Pia kuna jambo moja ambalo binadamu wengi linawaingiza katika umaskini bila wenyewe kujua. Mfano, ni vibaya sana mtu kuishi kwenye nyumba ambayo, ukienda kazini, jua linakupiga usoni, ukirudi nyumbani jioni pia jua linakupiga usoni.
Hapa sidhani kama kuna sababu ya kufafanua sana, ni uelewa mdogo tu. Ni vizuri mtu anapoishi iwe sehemu ambayo akienda kazini anapigwa na jua kisogoni, akirudi jioni hivyohivyo.
"Yule kiumbe aliposema hivyo tu mimi nikawaza kwamba, mfano mtu anaishi Kimara, kazi anafanyia Kariakoo, kwa hiyo asubuhi anapokwenda kazini jua linamuwakia usoni, jioni pia kwa sababu jua linakwenda kwenye kutua sasa.
"Nikamwelewa kuwa, ana faida sana mfano, mtu anayeishi Magomeni halafu kazi anafanyia Ubungo, akienda kazini jua linampiga kisogoni, akirudi jioni jua linakuwa limeshageuka, pia litampiga kisogoni.
Akaendelea kusema:
Pia watu waogope sana kulala kwenye vyumba ambavyo madirisha yake yanatazama upande unaotokea jua au mlango unaoingilia chumbani unatazamana na karo la maji au sehemu ya kuoshea vyombo.
Vyombo vya kupikia, wengi wanasema wamekula vyakula vibaya wameendesha, lakini ukweli ni kwamba kupika chakula halafu ukatoka jikoni huku umechukizwa na jambo fulani husababisha anayekula matumbo kuendesha.
Wapo binadamu wanakula sana lakini hawanenepeshwi na chakula hicho, sababu kubwa ni tabia ya kula chakula huku mtu anayekula shingo yake imepindia upande mmoja, uwe wa kulia au kushoto na si nyuma wala mbele.


Je, nini kiliendelea? Tuonane ujumamosi ijayo.................
 
Nusu Siku Ndani ya Jeneza-20-


ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:

Kazi zao zenye kuwapa mafanikio ni uhusiano kataika jamii, ushauri wa masuala ya ndoa. Wengi

waliotaka kupeana talaka waliposuluhishwa na wenye nyota hii walirudiana na ndoa kudumu.


Pia ni wafanyabishara wakubwa sana hasa ya mambo ya sanaa, mambo ya sheria au uhakimu. Mtu

mwenye nyota hii akiwa wakili anashinda sana kesi na wateja kwake hawapungui. Kama atakuwa

hakimu atakuwa anatoa huku ya haki kwenye kesi ngumu.


SASA ENDELEA


Kwa wale wanaoamua kufanya biashara ya sanaa hufanikiwa sana, mfano ni kama wanamuziki akina Lil Wayne, Bella Thorne, Eminem, Kim Kardashian, Will Smith, Ushar Raymond na Snoop Dogg.
Wapo marais wenye nyota hii na waliongoza mataifa makaubwa, mfano ni Jimmy Carter wa Marekani. Marais wengi wenye nyota hii hufanya kazi zao kwa busara sana na utulivu, hawakurupuki, si wapenda vita wala udikteta.

Wanapoachia madaraka wengi huishi maisha ya heshima sana na jamii huwatambua miaka na miaka.
Wacheza mpira wenye nyota hii pia hungara sana ulimwenguni, kama akina George Opong Weah, Muset Ozil, Ibrahimovic, Vidoc, Defoe na wengine kibao ambao nyota zao ni Libra na wakafanya vizuri kwenye mpira wa miguu.

Ipo nyota inaitwa Nge, lugha ya kigeni inaitwa Scorpio. Hii ni nyota ya nane kati ya kumi na mbili za duniani. Hiii ni nyota yenye majukumu mengi sana, dunia imeendelea kupitia watu wenye nyota hii. Kama wanadamu wangejua wangefanya juu chini kuzaa kipindi cha nyota hii ya Scorpio.
Mtu mwenye nyota hii ili afinikiwe anatakuwa kufanya kazi za madawa, upelelezi na uchunguzi. Hata wavumbuzi wengi wa mambo ya kihistoria wapo kwenye kundi la nyota hii.
Watu waliogundua vitu vingi vya kisayansi, kama ndege, meli nakadhalika wanatoka kwenye nyota hii.

Lakini kuna binadamu wanasumbuliwa sana na mambo ya mapenzi, washauri wao wakubwa wanatakiwa watu wenye nyota hii.
Kuna nyota inaitwa Sagittarius au Mshale. Hii nyota inawafaa sana watu ambao watafanya kazi za kusafiri, kutoka sehemu moja kwenda nyingine kupeleka bidhaa au kuchukua, lakini wanasheria wazuri sana wanatokea kwenye nyota ya Mshale. Wakiwa waandishi wa habari wanakuwa mahiri zaidi na huvuma muda wote.

Ili wawe na mafanikio makubwa, wenye nyota hii wanatakuwa pia kufanya kazi ya ualimu, wachungaji wa makanisa wanaweza kujikuta wanavuta waumini wengi sana kama wana nyota ya Mshale. Wachungaji wenye nyota hii, wanakuwa na uwezo mkubwa sana wa kuponya wagonjwa, kufukuza mapepo na kutenda miujiza mingi ya kuwashangaza wengi.
Pia wenye nyota hii wana uwezo mkubwa wa akili, kufikiri na kukwamuka kutoka katika matatizo. Mwanamke yeyote, hata kama ana nyota ya Simba, akiolewa na mwenye nyota ya Mshale atakuwa chini yake tu.
Nizungumzie nyota ya Capricorn au Mbuzi kwa jina la kujulikana kule duniani mnakotokea nyinyi. Hii nyota huwa ya utajiri mkubwa kama wahusika watafanya shughuli zifuatazo:

Uinjinia, uchoraji wa ramani za majengo, watafiti wa ardhi, kuajiriwa serikalini. Mara nyingi mwenye nyota hii akiajiriwa serikalini hupanda cheo kwa kasi sana, anaweza kuanzia chini akapanda hadi kuwa waziri na watu wakamshangaa.
Lakini wanasiasa wengi mahiri mkiwachunguza kwa karibu wana nyota hii ya Mbuzi. Tena wengi wanapopanda majukwaani hupigiwa makofi sana, hushangiliwa. Wana uwezo wa kuwashawishi watu kufanya jambo fulani, mfano kupigiwa kura.

Mtu akiwa na nyota ya Mbuzi na akataka kugombea nafasi ya siasa huwashinda wenzake kwa kura nyingi sana, ni mahiri wa kujibu maswali ya watu kama ataulizwa.
Kabla sijaendelea napenda kuwaambia kuwa maskini wengi au fukara wengi ni wale wanaofanya shughuli ambazo nyota zao zinakataa. Mtu nyota yake anatakiwa kuwa mwalimu, anaamua kuwa mfugaji, huyu lazima atalia. Kama atakopa mkopo kwa ajili ya kununua ngombe ili afuge atajikuta ngombe wote wanakufa kwa sababu nyota yake inakataa.

Pia kuna jambo moja ambalo binadamu wengi linawaingiza katika umaskini bila wenyewe kujua. Mfano, ni vibaya sana mtu kuishi kwenye nyumba ambayo, ukienda kazini, jua linakupiga usoni, ukirudi nyumbani jioni pia jua linakupiga usoni.
Hapa sidhani kama kuna sababu ya kufafanua sana, ni uelewa mdogo tu. Ni vizuri mtu anapoishi iwe sehemu ambayo akienda kazini anapigwa na jua kisogoni, akirudi jioni hivyohivyo.

Yule kiumbe aliposema hivyo tu mimi nikawaza kwamba, mfano mtu anaishi Kimara, kazi anafanyia Kariakoo, kwa hiyo asubuhi anapokwenda kazini jua linamuwakia usoni, jioni pia kwa sababu jua linakwenda kwenye kutua sasa.
Nikamwelewa kuwa, ana faida sana mfano, mtu anayeishi Magomeni halafu kazi anafanyia Ubungo, akienda kazini jua linampiga kisogoni, akirudi jioni jua linakuwa limeshageuka, pia litampiga kisogoni.

Akaendelea kusema:
Pia watu waogope sana kulala kwenye vyumba ambavyo madirisha yake yanatazama upande unaotokea jua au mlango unaoingilia chumbani unatazamana na karo la maji au sehemu ya kuoshea vyombo.
Vyombo vya kupikia, wengi wanasema wamekula vyakula vibaya wameendesha, lakini ukweli ni kwamba kupika chakula halafu ukatoka jikoni huku umechukizwa na jambo fulani husababisha anayekula matumbo kuendesha.

Wapo binadamu wanakula sana lakini hawanenepeshwi na chakula hicho, sababu kubwa ni tabia ya kula chakula huku mtu anayekula shingo yake imepindia upande mmoja, uwe wa kulia au kushoto na si nyuma wala mbele.

Je, nini kiliendelea? Tuonane ujumamosi ijayo.................

Daah! Saaf sana aise mkuu, em kwanza kula '5', kitufe cha 'Like' kwenye mchina wangu mi skionagi wala nini yan ....
Em kama vipi tudondoshee epidodes kama 13 hivi mfululizo watu tumsubirie mwali bila majasho .....
 
Nusu Siku Ndani ya Jeneza -21-

ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:
Wapo binadamu wanakula sana lakini hawanenepeshwi na chakula hicho, sababu kubwa ni tabia ya kula chakula huku mtu anayekula shingo yake imepindia upande mmoja, uwe wa kulia au kushoto na si nyuma wala mbele.
SASA ENDELEA


Hii tabia huku tulipo tunaichukulia kama ni kujinyima ndiyo maana mtu anakuwa hanenepi hata akila vipi kwa sababu kule kupindisha shingo ni sawa na kukilaumu chakula hiho hivyo unaondoa uwezo wake wa kufanya kazi vizuri mwilini!
Wengine, wengi tu wapo wanaokula chakula huku wana amani. Watu hawa hata wakila mboga za majani kila siku, watanenepa tu kwa sababu wanakipa chakula uwezo wa kufanya kazi vizuri mwilini.
Wengi wanaolaani chakula chao, utawaona wakiwa mfano baa au hata nyumbani, kikiwekwa tu mezani, anaanza kusema maneno ya kukilaani chakula, mfano kama ni kwa mgahawani a hotelini utamsikia mtu akisema:
&[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];Huu wali mbona kama una mabongemabonge, halafu nyama mchuzi mwepesi sana. He! Mboga za majani umeokota au. Mimi nitakuwa silipi hiki chakula. Ona nyama zilivyo ngumu.'
Hayo maneno ni ya laana kwa chakula, hata kama kipo vizuri lakini kwa maneno hayo lazima mtu huyo atakuwa kimbaumbau.
Kwa wale wanaoumwa, kila dawa ni dawa ndani ya mwili wa binadamu, ila akili au mawazo ya binadamu wenyewe ndiyo yanasababisha kuwepo na tofauti.
Mfano mzuri, utakuta binadamu anaumwa kichwa, lakini katika hizo dawa anachagua, kwamba dawa yenye jina fulani ndiyo inamponesha kuliko dawa nyingine.
Kusema ule ukweli hapo hamna ishu ya dawa, ila akili za mtu. Na mtu akizoea kusema hivyo maana yake ni kwamba hata ugonjwa wenyewe utakuwa wa kwake. Kuna binadamu wanaumwa halafu wakiulizwa wanajibu: &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];Huu ndiyo ugonjwa wangu mwenzio.'
Sasa turudi kwenye nyota kwanza, tumalize na kuendelea na mambo mengine. Nilikuwa naendelea kwenye nyota nyingine ambapo sasa tuiangalie nyota ya Ndoo au Aquaries kwa jina lingine.
Kama binadamu amezaliwa baada ya tarehe 22 ya mwezi Desemba mpaka Januari 21 nyota hii ni sawa kwake. Ili abadili maisha yake kuwa mazuri, atatakiwa kufanya kazi ya umeme, kama vile mashirika ya umeme ya nchi zao, wawe mafundi wa kampyuta, lakini pia watu wenye nyota hii watafanikiwa sana kama watafanya kazi ya uchunguzi wa kisayansi, kazi za kujua elimu ya anga, hasa sayari na kazi ya kutunza mazingira.
Hii kazi ya kutunza mazingira ina maana kwamba binadamu huyo hata kama ataamua kulima bustani za maua au mboga ataweza kuwa tajiri.
Nataka kusema kwamba wapo binadamu wanaokimbia kazi fulani kwa sababu wameshawaona wenzao wamefanya na hawajafanikiwa. Binadamu hatakiwi kutembelea nyota ya mwenzake.
Kuna binadamu ni waalimu na maisha yao ni mazuri, makubwa na yanavutia, lakini wengine wanaamini hakuna kazi haina fedha kama ualimu. Kumbe yule aliyefanikiwa ni nyota yake inamruhusu kuwa mwalimu, mwingine haimruhusu.
Kikubwa ni kila binadamu kufuata au kutafiti nyota yake ni nini na biashara gani afanye. Wengine wanakosa utajiri kwa sababu hawajui lolote. Unakuta binadamu anaanzisha
duka halafu fremu za duka lake zinaangalia kusini au kaskazini, nani atakuja kununua wakati uwazi wa duka unaangalia upande ambao unakinzana na mzunguko wa dunia.
Dunia yenu ipo na itaendelea kuwepo, maisha yenu duniani ni ya kubahatisha kwa sababu binadamu hawaombi au hawasali, ni kitu kibaya sana.
Kuhusu hili la kusali naomba msiende kuwaambia kwa sababu huku tulipo, pamoja na himaya hii kubwa mnayoiona lakini hakuna kitu tunakiogopa kwa binadamu mwombaji. Ni hatari sana kwetu.
Siku zote mwombaji ndiye anayetuumiza, anasababisha tunaungua, tunaingia vilema. Kwa kweli kila nikifikiria naumia sana. Hebu kwanza twendeni huku mkaone watenda kazi wetu walivyounguzwa, kupata ulemavu kwa sababu ya hao waombaji.
"Wakati yule kiumbe anasema hayo, alishatoka eneo alilosimama na kutembea akituangalia ili tumfuate.
"Tulitembea kama umbali wa dakika kumi tukafika kwenye banda moja la mabati, lakini si ya kuezekea nyumba. Tukaingia ndani na kusimama, kwa mbele yetu tuliweza kuwaona viumbe wa ajabu sana wakiwa wamelaliana, wengine wanalia, wengine wanaonesha sura zenye majonzi makubwa.
"Wengi wao walikuwa wakituangalia, kasoro wachache tu ambao walionekana kama wamelaliwa zaidi na wenzao. Yule kiumbe akasema:
"Hawa wote walikutwa na matatizo makubwa sana kutokana na wanadamu wanaojua kuomba au waombaji. Kuna yale maombi yenu mnamtaja jina bwana mmoja (akimaanisha Yesu). Lile jina linatuumiza sana sisi huku. Tena linatuumiza sana.
Ila na sisi kati ya mambo ambayo tunayakeshea huku na watu wanaoomba. Mpango wetu mkubwa ni kuwatupia mashile waombaji wote, iwe mchana, usiku au muda mwingine.
Kama mtakumbuka sana, mtu anayeomba huwa ananyemelewa sana na usingizi hasa kama ni usiku au lazima tutampa kibarua cha kuwaza jambo lolote ambalo halihusiani na yale maombi anayofanya.
Mfano mdogo, kama mmewahi kuchunguza ni kwamba, mara nyingi binadamu anaposali kwa kumaanisha, huwa anafuumba macho dakika chache baada ya kuanza sala.
Kinachotokea ni kwamba, anaposali amefumbua macho sisi tunamwelekeza kuangalia kitu chochote pale alipo. Kama ni sebuleni tunaweza kumwelekeza aangalie hata picha za siku ya harusi yake ukutani.


Itaendelea wiki ijayo. Jumamosi kama hii ya leo
 
Samahani mzee ningependa kujua kila nyota na mwezi wake kama yawezekana. Mfn nyota ya simba ni mwezi wa ngap,mshale ni mwezi wangap n.k
 
Samahani mzee ningependa kujua kila nyota na mwezi wake kama yawezekana. Mfn nyota ya simba ni mwezi wa ngap,mshale ni mwezi wangap n.k

Kwa Mtu Mwenye nyota ya Punda Tabia yake ni moto ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( ARIES - The Aggressive

(March 21 to April 19)

Kwa Mtu Mwenye nyota ya Ng'ombe Tabia yake ni Udongo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( TAURUS - The Tramp

(April 20 to May 20)


Kwa Mtu Mwenye nyota ya Mapacha Tabia yake ni upepo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( GEMINI - The Twin

(May 21 to June 20)


Kwa Mtu Mwenye nyota ya Kaa Tabia yake ni maji ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( CANCER - The Beauty (June 21 to July 22)



Kwa Mtu Mwenye nyota ya Simba Tabia yake ni Moto ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( LEO - The Lion (July 23 to August 22)


Kwa Mtu Mwenye nyota ya Mashuke Tabia yake ni udongo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( VIRGO - The One

that Waits (August 23 to September 22)


Kwa Mtu Mwenye nyota ya Mizani Tabia yake ni Upepo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa (LIBRA - The Lame One

(September 23 to October 22)


Kwa Mtu Mwenye nyota ya N'ge Tabia yake ni maji ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( SCORPIO - The Addict

(October 23 to November 21)


Kwa Mtu Mwenye nyota ya Mshale tabia yake ni moto ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( SAGITTARIUS - The

Promiscuous One (November 22 to December 21)



Kwa Mtu Mwenye nyota ya Mbuzi tabia yake ni udongo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( CAPRICORN - The

Passionate Lover (December 22 to January 19)


Kwa Mtu Mwenye nyota ya Ndoo Tabia yake ni Upepo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa (

AQUARIUS - Does It in the Water (January 20 to February 18)


Kwa Mtu Mwenye nyota ya Samaki Tabia yake ni Maji ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( PISCES - The Partner

for Life (February 19 to March 20)
 
Kwa Mtu Mwenye nyota ya Punda Tabia yake ni moto ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( ARIES - The Aggressive

(March 21 to April 19)

Kwa Mtu Mwenye nyota ya Ng'ombe Tabia yake ni Udongo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( TAURUS - The Tramp

(April 20 to May 20)


Kwa Mtu Mwenye nyota ya Mapacha Tabia yake ni upepo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( GEMINI - The Twin

(May 21 to June 20)


Kwa Mtu Mwenye nyota ya Kaa Tabia yake ni maji ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( CANCER - The Beauty (June 21 to July 22)



Kwa Mtu Mwenye nyota ya Simba Tabia yake ni Moto ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( LEO - The Lion (July 23 to August 22)


Kwa Mtu Mwenye nyota ya Mashuke Tabia yake ni udongo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( VIRGO - The One

that Waits (August 23 to September 22)


Kwa Mtu Mwenye nyota ya Mizani Tabia yake ni Upepo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa (LIBRA - The Lame One

(September 23 to October 22)


Kwa Mtu Mwenye nyota ya N'ge Tabia yake ni maji ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( SCORPIO - The Addict

(October 23 to November 21)


Kwa Mtu Mwenye nyota ya Mshale tabia yake ni moto ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( SAGITTARIUS - The

Promiscuous One (November 22 to December 21)



Kwa Mtu Mwenye nyota ya Mbuzi tabia yake ni udongo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( CAPRICORN - The

Passionate Lover (December 22 to January 19)


Kwa Mtu Mwenye nyota ya Ndoo Tabia yake ni Upepo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa (

AQUARIUS - Does It in the Water (January 20 to February 18)


Kwa Mtu Mwenye nyota ya Samaki Tabia yake ni Maji ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( PISCES - The Partner

for Life (February 19 to March 20)

vp kwamtu aliezaliwa march 12 nyota yake ni ipi na huwa anatabia gani? PLEASE NAOMBA MSAADA WAKO.
 
vp kwamtu aliezaliwa march 12 nyota yake ni ipi na huwa anatabia gani? PLEASE NAOMBA MSAADA WAKO.

Kwa Mtu Mwenye nyota ya Samaki Tabia yake ni Maji ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa (PISCES - The Partner

for Life (February 19 to March 20)



NYOTA YA SAMAKI (PISCES)

  • Hii ni nyota ya 12 katika mlolongo wa nyota 12
  • Wenye nyota hii ni wale waliozaliwa kati ya tarehe 19 February na tarehe 20 Machi.
  • Sayari yao ni JUPITER (MUSHTARA)
  • Siku yao ya Bahati ni Alhamisi.
  • Namba yao ya Bahati ni 8.
  • Rangi yao ya Bahati ni Zambarau au Kahawia iliyochangamka.
  • Asili ya nyota yao ni Maji.

VIPAJI VYA SAMAKI (VISIONARY)

Wenye nyota hii wana kipaji cha kufikiria jambo na kuliunda na likawa vile walivyotaka wao.

TABIA ZA SAMAKI


Watu wenye nyota ya Samaki ni wenye huruma, wapole na wenye moyo mzuri na hawawezi kukubali kumuona binaadamu mwingine akipata taabu au uchungu. Kwa hakika ni watu ambao wana hisia kati kwa

wengine ni watu ambao hawajipendelei na wako tayari wakati wowote kujitoa mhanga ili watu wanufaike, mapenzi yao au huruma kwa binadamu wengine hayana masharti yeyote.


Nafsi zao zimegawanyika katika nafsi ndogo ndogo kama vile muathiriwa mwenye kujitoa mhanga, mwokozi, na mkombozi.


Hayo yote yaliyotajwa wanaweza kuyatekeleza inapohitajiwa na ikiwa mwenye nyota hii akishatumbukia katika moja ya mambo hayo huwezi kumtoa.


Kwa ujumla nafsi za wenye nyota ya Samaki siyo za kidunia, ni watu wabunifu na wenye ndoto za kufikiri mambo ya baadaye na katika maisha yao wanaona raha sana kuwa na mawazo ambayo yatawaepusha na ugumu wa maisha.

Ikiwa wamekwama katika jambo lolote basi wataitafuta faraja au watajituliza kwa ulimwengu wao wa mawazo.

TABIA YA SAMAKI KATIKA FEDHA


Ni vigumu sana kukadiria tabia za wenye nyota hii katika fedha kwa sababau wote waliozaliwa katika nyota huwa wanachanganyikiwa kwa sababu huwa wanashindwa kutafautisha kati ya matumizi na thamani ya fedha.


Hii ni kwa sababu wanashindwa au hawakubali vikwazo kati ya muda na nafasi au za kwako na zangu, kwao kila kitu ni sawa sawa.


Pamoja na kwamba wana uroho wa pesa, uwezo na matamanio lakini wanajichukulia mambo kadri yanavyokuja. Kwao wakiwa na fedha sawa wakiwa hawana sawa vile vile kwao uwezo wa kubuni au kutunga taswira ni muhimu kuliko fedha.


Mara nyingi huwa wanajishughulisha na masuala ya kutatua matatizo ya watu wengine kuliko masuala ya kifedha. Wakati wote wako tayari kupoteza fedha kuliko kuibiwa ndoto zao.


TABIA YA SAMAKI KATIKA MAPENZI


Wenye nyota ya Samaki ni wenye kukamilika na Mahaba mengi na wanapenda sana kujitumbukiza na kuzama kwenye dimbwi la mapenzi.


Kuwa katika mapenzi ni kitu wanachokipenda na kukifurahia sana. Ni waangalifu wazuri kwa wapenzi wao wana huruma nyingi.

Ni watu wenye hisia kali za kimapenzi na ni wepesi kuathirika.

Mara nyingi huwa waoga wa vitu vya kimapenzi kwa sababu ya kuogopa kuvurugika kwa mipango yao ya baadaye.


Ni watu wenye kuyachukulia mapenzi kama ua la waridi na wanawaona wapenzi wao kama binaadamu wasio wa kawaida.


Tatizo lao kubwa la kimapenzi ni kwamba wanawaamini sana wapenzi wao na wanakuwa na mawazo au firika za kimapenzi ambazohazipo katika dunia hii.


Kwa ujumla wenye nyota hii wanapokuwa katika mapenzi wanakuwa wamejawa na shauku na mifano ya kuvutia na wanapenda wapwnzi wao waishi kiroho. Mategemeo yao yanakuwa makubwa na yaispotimia huwa wanavunjika moyo.

{mospagebreak}

MAVAZI YA SAMAKI


Wenye nyota ya Samaki wanatakiwa wavae nguo za michezo kama vile fulana au za kiasili na zilizoongezwa madoido na vimbwanga vingi.


Nguo zao ziwe za rangi ya Zambarau au Kahawia iliyochangamka na rangi ya bluu.

Kitambaa kiwe cha sufu (tweed)
Wanawake wapendelee sana kuvaa sketi, ikiambatana na mikanda na viatu vyao viwe vya bati.

MATATIZO YA KIAFYA


Nyota hii inatawala nyayo na vidole vya miguu.

Matatizo yao ya kiafya yanakuja pale wanaposhindwa kutekeleza ndoto zao au mipangilio yao kimaisha au wanapokorofishana na wapenzi wao.

Wanapoathirika na hayo yaliyotajwa hukimbilia kwenye ulevi na utumiaji vidonge uliokithiri.

Tatizo lingine ni maradhi ya nyayo za miguu, uvimbe unaotokana na baridi kali hasa katika vidole vya miguu.

KAZI ZA SAMAKI


Kugunuda muelekeo wa kimaisha kwa wenye nyota hii wakati mwingine huwa ni matatizo.

Tabia yao ya kushughulikia sana binaadamu wengine huwafanya wasiwe na muelekeo.
Wenye nyota hii wanatakiwa wasifanye ubaguzi katika kazi.

Wanatakiwa wafanye kazi ambazo zinazohusiana na kusaidia watu. Kipaji cha kutafsiri mambo huwasaidia vile vile kufanya kazi za sanaa kama vile kupiga picha na kazi za muziki au maigizo.

Kazi zingine zinazowafaa ni za kuhudumia wagonjwa, kucheza shoo, uaskari wa majini (Navy) kazi za dini au kazi za kutoa ushauri nasaha (Counselling).

FAMILIA ZA SAMAKI


Wenye nyota hii ni wazazi wenye hisia, wanaopenda watoto wao na wanahuruma hasa watoto wanapowasikiliza.


Pamoja na hayo wazazi wa Samaki wana matatizo ya kukubali kwamba watoto wanaweza kuwa tofauti na wao, hata mwishowe wanapokubaliana na hilo huwa wanawachukulia watoto wao kama wageni kuliko ndugu.


Mtoto akiwa anapenda kusoma na mwenye kujituma au akiwa na tabia ya kutumia sana akili kuliko moyo huwa hapendwi na mzazi wa Samaki.


Wazazi wenye nyota hii wana mipangilio mibovu ya nidhamu na muelekeo, hivyo watoto wakorofi huwa wanatumia mwanya huo kufanya mambo yao.


Hiyo ina maana kwamba watoto wa wazazi wa Samaki wanaweza kuharibika au kutumiwa kutokana na udhaifu wa wazazi wao.

{mospagebreak}

(MADINI YA SAMAKI)


Wenye nyota hii wanashauriwa wavae madini yanayoitwa.

Madini haya yanasaidia kupunguza hisia na kumuepusha mvaaji na ulevi.

UHUSIANO WA KIMAPENZI


(SAMAKI NA MASHUKE)

Tabia ya Samaki ya kuwa na mbinu na mawazo ya mambo ya baadaye huenda sambamba na tabia ya Mashuke ya utekelezaji na kujishughulisha bila kuchoka.

VYAKULA VYA SAMAKI


Wenye nyota ya Samaki wanashauriwa wapenda kula matunda au vyakula vifuatavyo.

Matunda ya Kunazi, Nyama mwitu kama Swala,nyati na kadhalika.
Vile vile wapendelee kula maboga.

NCHI ZA SAMAKI


Ili kupata mafanikio ya kinyota kwa wale wenye uwezo wanashauriwa aidha waishi au watembelee nchi au miji ifuatayo ambayo inatawaliwa na nyota yao.

Nchi hizo ni Tonga na Tanzania na miji ni Alexandria (Misri) na Seville (Ufaransa).

RANGI ZA SAMAKI

Wenye nyota ya Samaki wanatakiwa wapake nyumba zao au magari yao au sehemu zao za biashara rangi ambayo haijakoza ya Bluu au Kijani au Urujuani (violet).
 
Kwa Mtu Mwenye nyota ya Samaki Tabia yake ni Maji ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa (PISCES - The Partner

for Life (February 19 to March 20)



NYOTA YA SAMAKI (PISCES)

  • Hii ni nyota ya 12 katika mlolongo wa nyota 12
  • Wenye nyota hii ni wale waliozaliwa kati ya tarehe 19 February na tarehe 20 Machi.
  • Sayari yao ni JUPITER (MUSHTARA)
  • Siku yao ya Bahati ni Alhamisi.
  • Namba yao ya Bahati ni 8.
  • Rangi yao ya Bahati ni Zambarau au Kahawia iliyochangamka.
  • Asili ya nyota yao ni Maji.

VIPAJI VYA SAMAKI (VISIONARY)

Wenye nyota hii wana kipaji cha kufikiria jambo na kuliunda na likawa vile walivyotaka wao.

TABIA ZA SAMAKI


Watu wenye nyota ya Samaki ni wenye huruma, wapole na wenye moyo mzuri na hawawezi kukubali kumuona binaadamu mwingine akipata taabu au uchungu. Kwa hakika ni watu ambao wana hisia kati kwa

wengine ni watu ambao hawajipendelei na wako tayari wakati wowote kujitoa mhanga ili watu wanufaike, mapenzi yao au huruma kwa binadamu wengine hayana masharti yeyote.


Nafsi zao zimegawanyika katika nafsi ndogo ndogo kama vile muathiriwa mwenye kujitoa mhanga, mwokozi, na mkombozi.


Hayo yote yaliyotajwa wanaweza kuyatekeleza inapohitajiwa na ikiwa mwenye nyota hii akishatumbukia katika moja ya mambo hayo huwezi kumtoa.


Kwa ujumla nafsi za wenye nyota ya Samaki siyo za kidunia, ni watu wabunifu na wenye ndoto za kufikiri mambo ya baadaye na katika maisha yao wanaona raha sana kuwa na mawazo ambayo yatawaepusha na ugumu wa maisha.

Ikiwa wamekwama katika jambo lolote basi wataitafuta faraja au watajituliza kwa ulimwengu wao wa mawazo.

TABIA YA SAMAKI KATIKA FEDHA


Ni vigumu sana kukadiria tabia za wenye nyota hii katika fedha kwa sababau wote waliozaliwa katika nyota huwa wanachanganyikiwa kwa sababu huwa wanashindwa kutafautisha kati ya matumizi na thamani ya fedha.


Hii ni kwa sababu wanashindwa au hawakubali vikwazo kati ya muda na nafasi au za kwako na zangu, kwao kila kitu ni sawa sawa.


Pamoja na kwamba wana uroho wa pesa, uwezo na matamanio lakini wanajichukulia mambo kadri yanavyokuja. Kwao wakiwa na fedha sawa wakiwa hawana sawa vile vile kwao uwezo wa kubuni au kutunga taswira ni muhimu kuliko fedha.


Mara nyingi huwa wanajishughulisha na masuala ya kutatua matatizo ya watu wengine kuliko masuala ya kifedha. Wakati wote wako tayari kupoteza fedha kuliko kuibiwa ndoto zao.


TABIA YA SAMAKI KATIKA MAPENZI


Wenye nyota ya Samaki ni wenye kukamilika na Mahaba mengi na wanapenda sana kujitumbukiza na kuzama kwenye dimbwi la mapenzi.


Kuwa katika mapenzi ni kitu wanachokipenda na kukifurahia sana. Ni waangalifu wazuri kwa wapenzi wao wana huruma nyingi.

Ni watu wenye hisia kali za kimapenzi na ni wepesi kuathirika.

Mara nyingi huwa waoga wa vitu vya kimapenzi kwa sababu ya kuogopa kuvurugika kwa mipango yao ya baadaye.


Ni watu wenye kuyachukulia mapenzi kama ua la waridi na wanawaona wapenzi wao kama binaadamu wasio wa kawaida.


Tatizo lao kubwa la kimapenzi ni kwamba wanawaamini sana wapenzi wao na wanakuwa na mawazo au firika za kimapenzi ambazohazipo katika dunia hii.


Kwa ujumla wenye nyota hii wanapokuwa katika mapenzi wanakuwa wamejawa na shauku na mifano ya kuvutia na wanapenda wapwnzi wao waishi kiroho. Mategemeo yao yanakuwa makubwa na yaispotimia huwa wanavunjika moyo.

{mospagebreak}

MAVAZI YA SAMAKI


Wenye nyota ya Samaki wanatakiwa wavae nguo za michezo kama vile fulana au za kiasili na zilizoongezwa madoido na vimbwanga vingi.


Nguo zao ziwe za rangi ya Zambarau au Kahawia iliyochangamka na rangi ya bluu.

Kitambaa kiwe cha sufu (tweed)
Wanawake wapendelee sana kuvaa sketi, ikiambatana na mikanda na viatu vyao viwe vya bati.

MATATIZO YA KIAFYA


Nyota hii inatawala nyayo na vidole vya miguu.

Matatizo yao ya kiafya yanakuja pale wanaposhindwa kutekeleza ndoto zao au mipangilio yao kimaisha au wanapokorofishana na wapenzi wao.

Wanapoathirika na hayo yaliyotajwa hukimbilia kwenye ulevi na utumiaji vidonge uliokithiri.

Tatizo lingine ni maradhi ya nyayo za miguu, uvimbe unaotokana na baridi kali hasa katika vidole vya miguu.

KAZI ZA SAMAKI


Kugunuda muelekeo wa kimaisha kwa wenye nyota hii wakati mwingine huwa ni matatizo.

Tabia yao ya kushughulikia sana binaadamu wengine huwafanya wasiwe na muelekeo.
Wenye nyota hii wanatakiwa wasifanye ubaguzi katika kazi.

Wanatakiwa wafanye kazi ambazo zinazohusiana na kusaidia watu. Kipaji cha kutafsiri mambo huwasaidia vile vile kufanya kazi za sanaa kama vile kupiga picha na kazi za muziki au maigizo.

Kazi zingine zinazowafaa ni za kuhudumia wagonjwa, kucheza shoo, uaskari wa majini (Navy) kazi za dini au kazi za kutoa ushauri nasaha (Counselling).

FAMILIA ZA SAMAKI


Wenye nyota hii ni wazazi wenye hisia, wanaopenda watoto wao na wanahuruma hasa watoto wanapowasikiliza.


Pamoja na hayo wazazi wa Samaki wana matatizo ya kukubali kwamba watoto wanaweza kuwa tofauti na wao, hata mwishowe wanapokubaliana na hilo huwa wanawachukulia watoto wao kama wageni kuliko ndugu.


Mtoto akiwa anapenda kusoma na mwenye kujituma au akiwa na tabia ya kutumia sana akili kuliko moyo huwa hapendwi na mzazi wa Samaki.


Wazazi wenye nyota hii wana mipangilio mibovu ya nidhamu na muelekeo, hivyo watoto wakorofi huwa wanatumia mwanya huo kufanya mambo yao.


Hiyo ina maana kwamba watoto wa wazazi wa Samaki wanaweza kuharibika au kutumiwa kutokana na udhaifu wa wazazi wao.

{mospagebreak}

(MADINI YA SAMAKI)


Wenye nyota hii wanashauriwa wavae madini yanayoitwa.

Madini haya yanasaidia kupunguza hisia na kumuepusha mvaaji na ulevi.

UHUSIANO WA KIMAPENZI


(SAMAKI NA MASHUKE)

Tabia ya Samaki ya kuwa na mbinu na mawazo ya mambo ya baadaye huenda sambamba na tabia ya Mashuke ya utekelezaji na kujishughulisha bila kuchoka.

VYAKULA VYA SAMAKI


Wenye nyota ya Samaki wanashauriwa wapenda kula matunda au vyakula vifuatavyo.

Matunda ya Kunazi, Nyama mwitu kama Swala,nyati na kadhalika.
Vile vile wapendelee kula maboga.

NCHI ZA SAMAKI


Ili kupata mafanikio ya kinyota kwa wale wenye uwezo wanashauriwa aidha waishi au watembelee nchi au miji ifuatayo ambayo inatawaliwa na nyota yao.

Nchi hizo ni Tonga na Tanzania na miji ni Alexandria (Misri) na Seville (Ufaransa).

RANGI ZA SAMAKI

Wenye nyota ya Samaki wanatakiwa wapake nyumba zao au magari yao au sehemu zao za biashara rangi ambayo haijakoza ya Bluu au Kijani au Urujuani (violet).


Kama mimi sijui tarehe yangu ya kuzaliwa, na majina yangu yanaanza na herufi M, M, N N hayo ni majina manne… je siku yangu ya kuzaliwa ni ipi na nyota yangu ni nini?
 
..................

Kwa Mtu Mwenye nyota ya Ndoo Tabia yake ni Upepo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa (

AQUARIUS - Does It in the Water (January 20 to February 18)............

mkuu mm nimezaliwa katika ya hzo trh hapo juu vp tabia za watu wenye nyota hyo na wafanye kazi ya dizain gan au biashara ya dizain gani na pia pia wanatakiwa wawe na marafiki wa aina gani na vp mahusiano yao ya kimapenzi huwa wanakuweje




 
Kama mimi sijui tarehe yangu ya kuzaliwa, na majina yangu yanaanza na herufi M, M, N N hayo ni majina manne… je siku yangu ya kuzaliwa ni ipi na nyota yangu ni nini?

MAANA YA HERUFI YA JINA LAKO LA KWANZA

HERUFI A

Mwenye jina linaloanziana na herufi A ni mtu anayependa mambo makubwa, anajiamini na mwenye uwezo wa kutimiza malengo yake. Ni mtu mwenye tahadhari, mchangamfu na mpenda matukio. Anapenda Kuheshimiwa, anapenda Mamlaka, na ana kiburi, na hasira. Herufi A inawakilisha Nyota ya Punda,

HERUFI B
Mwenye jina linaloanziana na herufi B ni mtu, mkarimu, muam
inifu, na hupenda kazi. Ni Jasiri, shujaa na mkatili katika vita au pale anapotaka kulinda vilivyo katika himaya yake. Herufi B inawakilisha Nyota ya Ngombe,

HERUFI C
Mwenye jina linaloanziana na herufi C ni mtu wa kukubadilika badilika, mshindani na hupenda kupigania malengo yao wanayopenda. Ni watu wa wabunifu na wanaopenda mawasiliano Herufi C inawakilisha Nyota ya Mapacha,

HERUFI D
Mwenye jina linaloanziana na herufi D ni mtu anayependa usawa, Biashara. Ni watu wanaopenda kuamrisha na mwenye kupenda usafi. Ni jeuri na wenye msimamo. Herufi C inawakilisha Nyota ya Kaa,

HERUFI E
Mwenye jina linaloanzia na herufi E ni mtu mwenye roho nzuri ,yenye mapenzi na huruma. mwenye kupenda uhuru katika mapenzi na mchangamfu. Kinyume na hivyo atakuwa ni mtu asiotegemewa na kigeugeu. Herufi E inawakilisha Nyota ya Simba,

HERUFI F
Mwenye jina linaloanzia na herufi F ni mtu mwenye mapenzi,huruma , roho nzuri na ana uwezo wa kuwafariji watu. Ni mtetezi wa watu na mwenye huzuni lakini ni mzito wa kufanya maamuzi. Herufi F inawakilisha Nyota ya Mashuke,

HERUFI G
Mwenye jina linaloanzia na herufi G ni mtu mwenye mwenye imani ya kidini na nguvu za kiroho. Ana kipaji cha kubuni na uwezo wa kutatua matatizo ya watu. ni mtu mwenye hisia kali,msomi, mpweke na mkaidi wa kukubali ushauri wa kutoka kwa watu. Herufi G inawakilisha Nyota ya Mizani,

HERUFI H
Mwenye jina linaloanzia na herufi H ni mtu mwenye ubunifu na nguvu katika biashara, hupata faida kubwa kutokana na jitihada na bidii zake. ni mwenye mawazo mengi, mchoyo na mbinafsi. Herufi H inawakilisha Nyota ya Nge,

HERUFI I
Mwenye jina linaloanzia na herufi I ni mtu mwenye kupenda sheria, ana huruma na utu. Wakati mwingi hajiamini na ni mwenye hasira za haraka. Herufi I inawakilisha Nyota ya Mshale,

HERUFI J
Mwenye jina linaloanzia na herufi J ni mtu mwenye matamanio,mkweli, mkarimu na muerevu. asiyekubali kushindwa na hupata mafanikio makubwa. Wakati mwingine anakuwa ni mtu mvivu na aliyekosa mwelekeo. Herufi J inawakilisha Nyota ya Mbuzi,

HERUFI K
Mwenye jina linaloanzia na herufi K ni mtu mwenye jeuri. mwenye msimamo thabiti,mashuhuri na mwenye uwezo wa kushawishi na kuamsha hisia za watu wana uwezo wa utambuzi ambao watu wengi hawana. ni mtu asioridhika na hali ya kimaisha. Herufi K inawakilisha Nyota ya Ndoo,

HERUFI L
Mwenye jina linaloanzia na herufi L ni mtu wa vitendo, mwenye hisani na aliyejipanga vizuri kimaisha. Huwa wanapata ajali mara kwa mara. Herufi L inawakilisha Nyota ya Samaki,

HERUFI M
Mwenye jina linaloanzia na herufi M ni mtu mwenye kujiamini sana, mchapakazi na hupata mafanikio. ni mtu mropokaji,mwenye haraka na mwepesi kukasirika. Herufi M inawakilisha Nyota ya Punda

HERUFI N
Mwenye jina linaloanzia na herufi N ni mtu mwenye ubunifu, hisia kali na hupenda kuwasiliana lakini ana wivu sana. Herufi N inawakilisha Nyota ya Ngombe

HERUFI O
Mwenye jina linaloanzia na herufi O ni mtu mwenye subra, mvumilivu na mwenye bidii ya kusoma. Ni mtu mwenye kupenda kutumikia jamii na mwenye uwezo mkubwa wa kudhibiti hisia. Herufi O inawakilisha Nyota ya Mapacha

HERUFI P
Mwenye jina linaloanzia na herufi P ni mtu mwenye uwezo wa kuamrisha na hekima kubwa. Ana nguvu za kiroho lakini anapenda sana kujitumbukiza kwenye mambo ya watu. Herufi P inawakilisha Nyota ya Kaa

HERUFI Q
Mwenye jina linaloanzia na herufi Q ni mtu mwenye kupenda mambo ya asili. Ni watu wasiyoelezeka nawana uwezo wa kuonyesha vitu visivyojulikana hata hivyo ni mtu aliyepooza sana. Herufi Q inawakilisha Nyota ya Simba

HERUFI R
Mwenye jina linaloanzia na herufi R ni mtu mwenye uvumilivu, wenye huruma lakini ana hasira za haraka. Muda wote anakuwa mpenda amani. Herufi R inawakilisha Nyota ya Mashuke

HERUFI S
Mwenye jina linaloanzia na herufi S ni mtu mwenye mvuto mkali wa kuleta utajiri. Ni watu wenye maamuzi ya ghafla na hupenda mageuzi makubwa. Herufi S inawakilisha Nyota ya Mizani

HERUFI T
Mwenye jina linaloanzia na herufi T ni mtu mwenye kupenda ushauri wa kiroho, anatumia nguvu za ziada kusaidia watu na hupata mafanikio baada ya muda mrefu. Ni watu wenye hisia kali sana na ni wepesi kushawishika. Herufi S inawakilisha Nyota ya Nge

HERUFI U
Mwenye jina linaloanzia na herufi U ni mtu mwenye bahati kubwa kwa ujumla. Anapenda uhuru katika mapenzi. Lakini ni mtu mbinafsi, mwenye tamaa na aliyekosa maamuzi. Herufi U inawakilisha Nyota ya Mshale.

HERUFI V
Mwenye jina linaloanzia na herufi V ni mtu Mchapakazi, wenye bidii na asie choka. Hata hivyo ni watu wasiotabirika. Herufi U inawakilisha Nyota ya Mbuzi.

HERUFI W
Mwenye jina linaloanzia na herufi W ni mtu muwazi, wachangamfuu kupita kiasi na mwenye uwezo wa kutambua mtu mwema na mbaya. Ni watu wenye tamaa na hufanya mambo ya hatari. Herufi W inawakilisha Nyota ya Ndoo.

HERUFI X
Mwenye jina linaloanzia na herufi X ni mtu asiyependa kuwekewa vizuizi katika kwenye anasa na ni rahisi kujiingiza kwenye uzinzi na kujitoa uaminifu. Herufi X inawakilisha Nyota ya Samaki.

HERUFI Y
Mwenye jina linaloanzia na herufi Y ni mtu mwenye kupenda Uhuru na hawapendi kupingwa jambo lao lolote. Ni watu wanaokosa uamuzi na husababishia kupoteza bahati katika maisha. Herufi Y inawakilisha Nyota ya Punda

HERUFI Z
Mwenye jina linaloanzia na herufi Z ni mtu mwenye kupenda matumaini na amani. Ni wenye msimamo mkali ila wanashauriwa kufikiria kabla ya kuamua jambo. Herufi Z inawakilisha Nyota ya Ng’ombe.


Herufi M inawakilisha Nyota ya Punda

KWA HIYO ANGALIA NYOTA YAKO YA PUNDA KWA HERUFI YA M.

NYOTA YA PUNDA AU KONDOO (ARIES)


Hii ni nyota ya kwanza katika mlolongo wa nyota 12.
Wenye nyota hii ni wale waliozaliwa kati ya tarehe 21st March na tarehe 19 April ya mwaka wowote.


Sayari yao ni Mars (Mariikh)
Siku yao ya bahati ni Jumanne
Namba yao ya bahati ni 9
Rangi yao ya Bahati ni Nyekundu.
Asili yao ni Moto.


NYOTA YA PUNDA AU KONDOO KATIKA MAPENZI NA MAHABA


Kwa vile wao ni wenye nyota ya kwanza mara nyingi wenye nyota hii wanapenda kuwa mbele. Wanakuwa wakarimu na wenye pendo kwa wapenzi wao.
Ni watu wenye kupenda kushirikiana na watu wengine, wanapenda mikusanyiko ya jamii na wacheshi. Ni watu wazuri kuwa nao karibu na mara nyingi wao wanakuwa ndio maisha na roho ya kundi wanalojihusisha nalo. Hivyo inatokana na tabia zao za asili za uchangamfu. Hata hivyo wakiudhiwa huwa ni viumbe wenye hasira kali.


Wenye nyota hii ni wepesi sana kuvunjika moyo na hii inatokea wakati wapenzi wao wanapowaangusha au kuwadharau katika mapenzi ambayo wao wanayachukulia kwa uzito mkubwa.
Pamoja na uchangamfu walio nao wenye nyota ya Punda wana moyo dhaifu usiovumilia matatizo na wanaweza kudhuriwa kirahisi katika mapenzi.


Wanaingia katika mapenzi na kupenda kirahisi. Mara nyingi wanawafanya wapenzi wao ndio nguzo au kiegemezo na hapo ndipo matatizo yanapoanza.
Wasipopata njia ya kutatua matatizo ya kimapenzi huwa wanachanganyikiwa na wanafadhaika sana hasa wanapogundua kwamba wapenzi wao ni binadamu kinyume na walivyofikira wao.


Kwao wazo la kuwa waaminifu kwa mpenzi mmoja milele linapewa kipaumbele katika mambo ya mahaba, lakini wakiona mambo yanaenda kombo basi ni mwepesi sana kuondoka kwenda kutatufa mpenzi mpya sehemu nyingineyo.
Kwa ujumla wenye nyota ya Punda ni watu wenye mapenzi motomoto, tatizo lao kuwa hawapendi kusikiliza ushauri wa kimapenzi, na hawakubaliani na mambo nusu nusu. Ni watu wenye kutegemea mazuri wakati wote na hawakubali kushindwa. Hupenda kukimbilia katika mapenzi bila kufikiri wanapohisi wamepata mpenzi wa kweli. Ni wepesi kuvutwa katika mapenzi na ni wenye miamko ya ghafla au misukumo ya kiwazimu ambayo wakati mwingine inawafanya waonekane wapumbavu.


NYOTA YA PUNDA KATIKA FEDHA
Wenye nyota hii wanapenda sana kutumia nguvu au kulazimisha na siyo waoga. Mipango yao ya kifedha wanayoipanga inakuwa na ubora wa hali ya juu inayopendeza na inayowavutia watu wengine. Hii inatokana na uwezo wao, shauku na vipaji vya kiakili kuhusiana na masuala ya fedha.
Hakuna sehemu yeyote ambayo mwenye nyota ya Punda atafanya shughuli yeyote bila watu kupendezwa na mipango yao. muda wote wako tayari kuchukua majukumu bila kujali chochote na mwisho wake mafaniko yanakuwa makubwa. Suala la kujiliza ni kuwa je wanaweza kufanya hivyo kwa muda mrefu?


Jibu ni hapana watu wa Punda wanatambulika kwa tabia yao ya ufuatiliaji wa mambo, bila kuchoka lakini tabia yao ya kiburi katika mambo madogo madogo ya kibiashara na kikazi wakati mwingine huhatarisha mradi au kazi zao zote.
Wanapenda kutumia fedha kiholela bila kupata uhakika kwamba zitarudi au zipo. Hulka yao ya kuwa mbele na kupenda kuishi kiuaminifu huwafanya wakose kinga kwa wajanja wanao penda kuwatapeli.


Kitu kimoja ni kwamba Mungu amewapa uwezo wa kufanya kazi vizuri wanapokuwa wao viongozi au wasimamizi. Wanakuwa na nia na moyo wa kufanya mambo mapya, lakini ajabu ni kwamba hawana subira wala mbinu za utawala hasa katika masuala ya fedha.
Papara zao za kujua mambo zaidi mara nyingi husababisha utatanishi kwa watu wote wanaowazunguka na wanao wakilisha.


Kimaisha wenye nyota ya Punda wanapenda sifa na kuonyesha matunda ya kazi zao au uwezo wao kifedha kwa kununua magari mazuri, nguo zenye thamani kubwa na vito vya thamani ili waonekane pamoja na ukarimu wao wakati mwingine hubadilika na kuwa wabinafsi na wachoyo.
Kwa ujumla wenye nyota hii ni watu wenye ari na uwezo wa kuanzisha mambo na wanapenda kupata maendeleo ya kimaisha na kuwa na miradi mipya. “NATAKA” ndio neno lao kubwa. Wanahitaji sana fedha, uwezo na uvutio ni wakati mchache sana huangalia maslahi ya watu wengine. Huwa wanakabiliwa na tatizo la kuchagua fedha au mamlaka, hata hivyo mapenzi yao ya kuwa na uwezo huwa yanashinda.
{mospagebreak}


NYOTA YA PUNDA (AFYA ZAO)


Wenye nyota hii ni watu wenye nguvu na afya nzuri. Wakati wote wao wanakuwa hawana subira ya kungoja kufanya shughuli zinazowahusu. Ni watu ambao hawapendi kabisa kuugua au kupata maradhi. Mara nyingi wanakuwa na uwezo wa ajabu wa kupona maradhi yanyaosumbua.
Kwa vile nyota hii ya Punda inatwala kichwa maradhi yao mengi yanahusiana na kuumwa kichwa na homa za mara kwa mara ambazo hupotea kama zilivyokuja.


Tatizo lao kubwa la kiafya ni la “Adrenalini” (Hii ni Homoni inayotoka ndani ya mwili wakati mtu anaposhtushwa au kukasirika, ambayo inafanya moyo upige haraka na kuutayarisha mwili kupambana na khatari). Watu hawa wanafanya kazi bila kuchoka na inatakiwa nguvu zao zielekezwe sehemu inayohusika, ikitokea vinginevyo huwa wanakosa raha na kuwa na wasiwasi.
Wasiwasi huo unasababisha “Adrenalini” kumwagika kwa wingi wanakuwa wepesi kuudhika na kukasirishwa na kuwa na Hamaki au ghadhabu za haraka ambazo huwaletea matatizo ya mzunguko wa damu katika Ubongo na macho.


Watu wa Punda wanahitaji kufahamu kwamba wao hawana kinga hivyo mapumziko ni muhimu kwao. Wanatakiwa wapendelee kutembea kwa miguu au wajihusishe na michezo ili kuondoa mzigo wa uchokozi, hakami na hasira walionao.
Utaratibu maalum wa kula chakula vile vile ni muhimu, na wenye nyota hii wanashauriwa kukiepusha na kahawa na sukari nyeupe ambao inaongeza mfadhaiko katka mfumo wa neva na tezi za “Adrenalini”. Ni wachache sana wenye nyota hii ambao wana matatizo ya uzito kwa sababu wanajishughuoisha sana na shughuli mbalimabli.
Kwa ujumla wenye nyota hii wanapokata tamaa huwa wanaathirika, na tbaia yao ya haraka haraka inawafanya wawe katika vita na miili yao wenyewe. Matokeo yake ni kuathirika kiafya. Wanatakiwa wajifunze tabia ya nyota ya Mizani ya ushirikiano. Tabia hii pamoja na kwamba itawapunguza kasi zoa katika utendaji lakini itawasaidia kudhibiti matatizo yao ya kiafya.


NYOTA YA PUNDA (MAISHA YAO)


Punda wanapenda sana kujihusisha na masuala ya kuwafanya waishi vizuri kama binaadamu wengine. Wanapenda sana vitu vyenye msisimko vya pekee na utaona hivyo katika nyumba zao.
Kuweka makazi ya kudumu kwa mtu wa Punda ni moja ya mitihani mikubwa ambayo ana lazima atekeleze lakini kwa watu wengine jambo hili wanalichukulia kama mojawapo ya mambo mengi ya kimaisha ambayo wakipata fedha anataka watekeleze.


Moja ya hulka za Punda ni kuthibiti namna nyumba zao zinavyoendeshwa. Hivyo inamaanisha kwamba wanahitaji kupata mwenzi mwaminifu ambaye atatekeleza yote atakayoagizwa kuyafanya hapo nyumbani. Vinginevyo tabia zao za kutokupumzika na tamaa ya kufanya mambo mapya itawafanya wapoteze hamu ya maisha yao ya nyumbani.
Wanapokuwa tayari wameweka mizizi yao wanakuwa waaminifu kwa familia zao. Hata hivyo kuna hatari kwamba wasipoweza kupata wanachokitaka hapo nyumbani wanaweza kusimama na kuondoka.


Hawawezi kuficha hisia zao kwa yeyote wanayemualika katika nyumba zao ukikosa atakuambia na hawategemei hata walioalikwa nao kuficha hisia zao vile vile.
Kutokana na shauku na hamu kubwa ya kuthitisha maisha yao, ni vizuri Punda wakawa waangalifu, wasiwe wajeuri au wakandamizaji katika nyumba zao.


Ni watu wanaozipenda familia zao na mara nyingi wanatumia nyumba zao kama sehemu ya kufanyia kazi badala ya mapumziko.
{mospagebreak}


NYOTA YA PUNDA (LIKIZO NA SAFARI)


Nyota ya Punda ni nyota yenye asili ya moto, maana yake ni watu wenye ari na nguvu zisizo na mipaka, na mara nyingi wanatatufa vitu vinavyowafurahisha. Wanapenda sana kusafiri aidha katika biashara au kwa kujifurahisha.
Wenye nyota hii wana tabia ya kujenga uhusiano mkubwa katika tabia fulani. Hii inapotokea wanapenda kutumia muda wao mwingi katika mazingira hayo ili wayaelewe vizuri. Wanajua kabisa sehemu au mji ambao watajisikia wako nyumbani.


Muda mwingi huwa wanapenda mazingira mapya na hii inawafanya kupata uzoefu mkubwa mara nyingi wanakuwa ni waalimu wazuri sana. Ukweli wa mambo ni kwamba walimu wengi wa shule wanaowaongoza wanafunzi katika safari za nje ni wenye nyota ya Punda.
Punda ni wasafiri majasiri na wanapenda vyombo vinavyokwenda kasi. Kwao ni bora kusafiri kwa ndege kuliko kupanda basi linaloenda polepole. Huwa wanapenda kusafiri daraja la kwanza kama wakikosa kabisa basi watasafiri daraja la pili.


Ukiwa katika likizo pamoja na mwenye nyota hii unaweza ukaudhika kwa sababu wao mara nyingi wanatafuta mambo mapya na wanakuwa hawatulii sehemu moja kwa kutegemea ujasiri wao.
Kwa ujumla kwa vile wenye nyota ya Punda ni watu wasiokuwa na subira kwa rafiki zao wa duniani hawapendi kungoja watu wakubaliane na mipango yao ya safari ambayo wanaweza kubadilisha bila taarifa. Kwa sababu hiyo mara nyingi wanasafiri peke yao, au wanaweza kujitenga mbali na walio karibu nao. Hivyo watu wa Punda wanashauriwa kuwa na subira ya kuwangoja wenzi wao katika likizo au safari zao.


NYOTA YA PUNDA (TABIA ZAO)


Tabia ya wenye nyota ya Punda ni wakali na wachangamfu, wenye hisi na wanaoweza kujieleza wakiwa na ari ya kufanya chochote. “SASA HIVI” hivyo ndio mambo wanayotaka kusikia.
Ni watu wasiokuwa na surbira, kila kitu kinafanyika kwa msukumo na haraka haraka. Wenye nyota hii ni viongozi majasiri ambao hawaoni karaha kuchukua majukumu. Wao wakati wote wanajiona kwamba “Wanajua sana”.


Pamoja na kwamba wanakuwa wa kwanza kukamata mambo ya msingi ya jambo lolote wao wanakuwa wa mwisho kuliacha na ni wafuatiliaji wazuri.
Kwa upande mwingine watu hawa wewe wape njia ya kutatua tatizo au ya kufanya jambo jipya, utashangaa jinsi watakavyolichambua na kulitekeleza jambo lenyewe.


Jambo la kushangaza kwa wenye nyota hii ni kwamba tatizo lao kubwa linakuwa kusitasita au kuchelewesha jambo. Pamoja na kwamba wao wanapenda mambo ya haraka lakini yakiwa hayawavutii basi huwa hawana haraka nayo.
Vile vile wanaweza kuwa butu. Mara nyingine hufanya makosa makusudi au kuwachokoza wafanyakazi wenzao kuonyesha ubinafsi wao ili wafanikiwe.


Kwa ujumla wenye nyota hii ni watu ambao wanajipendelea. Ni watu ambao “MIMI KWANZA” ndio tabia yao wanapenda waonekane kwamba wao ndio wanajua zaidi na tabia hiyo inawasaidia, ukweli wa mambo ni kwamba wenye nyota ya punda kila walitakalo wanalipata.
{mospagebreak}


TABIA YA PUNDA (KATIKA NGONO)


Wanapokuwa chumbani, tatizo kubwa la wenye nyota hii ni ubinafsi. Watu wa Punda huwa wanapenda kujishughulisha sana na mambo ya ngono na wanategemea kwamba wapenzi wao nao wajihusishe kikamilifu katika tendo hilo. Wakiona kwamba wapenzi wao hawako makini wakati wa ngono basi hujihisi kwamba hawapendwi na hawatakiwi.
Wenye nyota hii ni watu wenye bashashi na wacheshi na hiyo inawafanya wawe ni watu wenye hisia kali na haraka, hivyo inakuwa vigumu kwao kufanya mambo kwa mpangilioi na pole pole. Hivyo inawafanya wasiweze kuwachezea wapenzi wao kabla ya ngono.


Hisia zao kubwa ni kufanya tendo la ndoa na ni wakati huo huo bila kungoja.
Kutokana na ubinafsi huwa wanasahau kabisa hisia za wapenzi wao. Kwa kweli ni watu ambao wanajipendelea sana katika tendo la ndoa na hiyo huwa inawaletea matatizo katika uhusiano wao wa kimapenzi.


Wakati wanapochagua mpenzi Punda wanashauriwa wahakikishe kabisa wanapata wapenzi ambao wana ashiki au nyege za haraka haraka kama wao.
Katika kipindi cha kubembeleza pendo (kutongoza) watu wa Punda wanatakiwa waonyehse tabia ya asili ya ukarimu na mahaba ili wapendeke na vile vile wajaribu kuachana na tabia yao ya asili ya hisia kali na ukali.
Wanaume wa nyota hii wanapenda sana kujiona kwamba wao ni mabingwa na mashujaa katika ngono.


Kwa ujumla watu wa nyota hii ni wenye kuhitaji sana ngono. Ni watu ambao hawataki kukataliwa. Wanaume wa nyota hii wana ashiki na hamasa za kufanya ngono kuliko kupenda na wanaliangalia hilo wanapotafufa wapenzi kwa wanawake nao wana hamu kubwa ya kufanya tendo la ndoa.
Hakika wenye nyota hii wanaweza kuwa wapenzi wazuri.


NYOTA YA PUNDA (KAZI ZAO)


Wote wake kwa waume waliozaliwa katika nyota hii wana kipaji cha asili cha uongozi na wasiwasi wa kushindwa katika utekelezaji.
Kwao kitu cha pili au wao wenyewe kuwa namba mbili. Wanawake katika hali ya ushindani ambapo wanaweza kutekeleza kazi zao katika spidi au haraka wanayoitaka ambayo mara nyingi inakuwa mara mbili ya spidi ya kawaida, kila kitu kitakuwa sawa.


Wenye nyota hii huwa wanafanya vizuri shughuli zao za kazi au taaluma, mradi shughuli hizo ziwe zinazoleta athari. Hawapendi kuburuzwa wala kuishi bila kupata ushindani ni kawaida mara nyingi katika kazi zao hutokea migongano kati yao na wale wenye mamlaka juu yao. Wanapenda sana kupambana na hali ya ushindani wa kikazi na mara nyingi huwa wakiasisi shughuli mpya au kutoa mawazo mapya. Vile vile wanapenda sana ushindani wa kutafuata kitu kilichopotea.
Watu wa Punda ni watu ambao wanaweza kuhisi jambo lolote, ni watu wanaopenda kutumia nguvu katika kazi na wakifanya kazi yoyote wanaifanya kwa moyo mmoja. Wakiwa katika kazi, hupenda kufanya kazi peke yao au katika kazi hiyo wawe ni wasimamizi.


Kwa ujumla kwa vile watu wa Punda wanafanikiwa katika ushindani wanafurahi sana wanapofanya kazi ambazo zenye vipingamizi na ambazo utekelezaji wake unahitaji akili nyingi na nguvu.
Watu wa aina hii wakishindwa kutekeleza majukumu yao huwa wanavunjika moyo vibaya sana. Wanapenda sana kufanya kazi katika mazingira ambayo yanahitaji muda maalum kutekeleza mambo fulani.
{mospagebreak}


NYOTA YA PUNDA (FAMILIA ZAO)


Wazazi wenye nyota ya Punda wanakuwa wakarimu sana kwa watotowacheshi watafanya kila njia kuwahimiza wawe huru na watawaruhusu wafanye majaribio mbali mbali ya kimaisha na kuwahimiza kuchukua majukumu makubwa kwa gharama yeyote. vile vile watawahimiza watoto wao wawe na tabia ya ushindani badala ya kuwafundisha michezo.
Wazazi wenye nyota hii watawapa watoto wao nafasi kujisimamia wenyewe katika mambo yao. tatizo lao moja ni kuwa hawapendi watoto ambao ni ving’ang’anizi na wanaohofia usalama wao.


Watoto ambao ni waangalifu waoge na wanaofanya mambo kwa kufikiria wanakuwa hawaendani sana na wazazi wenye nyota ya Punda kwa sababu Punda hawapendi watoto wenye haya, waoga na wepesi kutishwa.
Wazazi wa nyota hii wanaweza kuwa wakali, wasiokuwa na mbinu na wenye kauli za ukali ambazo zinaweza kuudhi mtoto yeyote mwenye moyo mdogo. Tabia hii mara nyingi inasababisha migongano kati ya mzazi na mtoto na kutokuelewena kunakuwa kukubwa.


Wazazi wa Punda wanashauriwa kujilinda katika kuwashinikiza watoto wao kwa nguvu na haraka na kuwaruhusu watoto hao wakue na wafanye vitu katika njia za kawaida.
Kwa ujumla wazazi wa Punda ni wenye msukumo lakini wanajivunia sana watoto wao ni wazazi wenye makaka na wanapenda sana utani kwa vile hata wao mioyo yao ni ya kitoto. Mzazi wa kike anapenda ushindani hasa katika mausuala ya maisha na kuishi lakini hata yeye anapenda utani hasa anapokuwa nyumbani.


NYOTA YA PUNDA (MAUMBO YAO)


Wenye nyota ya Punda ni wenye uso mrefu mpana paji lao la uso hutanuka likiambatana na fuvu lililokaa vizuri. Macho yao ni makali na yenye kuonyesha uzima na uhai na yaliyotumbukia kwa ndani.
Nyusi zao ni nyeusi zenye kuonekana wazi au zilizo dhahiri kama zimepakwa wanja. Pua zao ni za bapa na midomo yao ni mipana.


Unapozungumza na wenye nyota hii naye atakusimamia wima mbele yako na kukuangalia moja kwa moja kwenye macho yako.
Tabia yao hiyo inawafanya waonekane wao ni wenye tabia za kigomvi au ushauri lakini ukiangalia kwa undani utagundua kwamba ni wakweli na wanaoweza kuaminiwa.


Hata hivyo kipindi cha kukusimamia wima inakuwa kifupi hasa anapokuona mpuuzi.
Kimaumbile ni watu wepesi na mwendo wao ni wa madaha. Miili yao kidogo imeinamia mbele ya misuli yao inaonekana imekakamaa, hiyo ni kwa sababu ya kujishughulisha sana bila kupumzika.


Sifa za wanaume wa Punda ni kwamba wako makini na wenye msimamo. Ni wembamba na miili yao ni yenye misuli iliyojikunja kunja.
Wanawake nao ni wembamba na maumbile yao siyo ya kupendeza sana, mikono yao na miguu yao ni yenye nguvu. Matamanio yao na uwezo wao huwa inawafanya wawe wanawake wenye tabia za kiume.
Kwa ujumla alama ya Kondoo ni pembe zake na mambo yote yanayohusiana na pembe hizo. Wenye nyota hii wanapenda kupambana na maisha. Kimaumbile athari zao huonekana mara moja. Kama vile kujiamini, namna wanavyosalimia watu na vicheko vyao. Vitendo vyao hivyo vinakujulisha kwamba huyu ni Punda.


{mospagebreak}


NYOTA YA PUNDA (VYAKULA VYAO)
Kama ilivyo katika tabia zao wenye nyota ya Punda vile vile wanapenda vyakula vya haraka haraka.
Ukweli ni kwamba mawazo yao mara nyingi yanakuwa katika maisha kuliko chakula pamoja na kwamba wanakuwa na hamu na uwezo mkubwa wa kula. Wanapenda chakula kizuri lakini kiwe cha haraka na rahisi kutayarisha.


Wanapenda sana kufanya karamu tafrija ambazo wana kipaji kikubwa cha kuzitayarisha na wanazifurahia. Katika karamu hizo vyakula vyao vinakuwa vya haraka ambavyo vinagawiwa wima wima bila kucheleweshwa.
Wakati wanapokuwa hawafanyi karamu au tafrija wanapenda chakula chochote kinachotayarishwa upensi na ambacho kinaweza kulika huko wanatembea, kama vile asusa na vyakula vyepesi kama biskuti, chipsi n.k.


Wanapenda ladha iwe nyepesi na viwe na pili pili na viungo vingi. wanapenda sana vyakula vinavyopooza au kutuliza njaa kama viazi, tambi na maziwa.
Huwa wanapenda sana ladha za uchachu kama limao limao au ndimu ndimu au mbilimbili vile vile wanapenda sana mkate na Jibini au vyakula vilivyo kaangwa kama nyama.


Wanatakiwa wawe waangalifu katika kula mafuta hasa vyakula vya kipuuzi puuzi ambavyo vinaweza kuwaletea madhara.
Kwa ujumla wenye nyota hii wanapenda sana tafrija, na vyakula wanapenda viwe vile vinavyotayarishwa mbele ya wageni na viwe vilivyokaangwa na vyenye ladha nzuri. Vyakula hivyo viwe ni vyepesi kutayarisha visivyopoteza muda.


NYOTA YA PUNDA (VIPAJI VYAO)


Wenye nyota hii wanapenda sana kupambana na maisha na wanakuwa na mambo mengi sana vichwani mwao kiasi kwamba wakati mwingine wanasahau vipaji vyao vya asili.
Tabia hiyo waliyo nayo haiwapi muda wa kufanya mambo mengine kama ya ubunifu. Kwa asili, wao ni watu wabunifu na wakati mwingine wanapata wasiwasi katika ubunifu wao.


Kuna wakati wenye nyota hii wanashindwa kutofautisha kati ya vipaji vyao na matakwa yao. ambayo yanakuwa makubwa na yenye shinikizo. Watapata msaada katika hili iwapo watafanya jitihada za maksudi za kuwasiliana na busara zao za asili kuwa kupata mapumziko na kufanya taamuli (Meditation).
Kipaji cha wenye nyota hii kinahusiana na kichwa ambacho ndio nyota yao inapotawala hivyo “Frenologia” (Ujuzi wa tabia ya mtu kwa umbo la kichwa chake iko chini ya nyota hii.


Kwa kuongezea wenye nyota hii wana kipaji cha kutafsiri ndoto na kipaji cha kusikia sauti ndani ya kichwa.
Kwa ujumla watu wa Punda wanapenda njia ya utabiri ambazo zinatoa matokeo ya haraka kama vile kutumia karata , dhumna, au dadu (dice).
Taamuli (meditation) ni jina au mbinu nzuri kwa wenye nyota hii kuongeza kipaji chao. Ikiwa watafanya taamuli kwa dakika ishirini wakati wa usiku au kitu cha kwanza wanapoamka asubuhi, akili na miili yao itatuliza. Hivyo itawafanya wawe na uwezo wa kutumia nguvu zao za kimwili na kiakili pamoja na kuendeleza au kukuza vipaji vyao.
{mospagebreak}


NYOTA YA PUNDA (BAHATI ZAO)


Watu wa nyota hii wana tabia ya kitoto ya kuamini kwamba mazuri yatatokea kwa amri ya Mungu. Kwa hiyo inawawia vigumu kufikiria uwezekano wa kushindwa katika jambo lolote.
Wakiwa ni waliozaliwa katika nyota yenye kuasisi mambo, wengi wao hudharau kutopata matumaini katika jambo moja na kurukia jambo lingine.


Kwa sababu shauku yao ni ya kuambukiza mara nyingi hufanikiwa kuwashawishi wengine wakubali kuongozwa nao hata kama kuna khatari.
Mara nyingi hawana muda wa kutoa mashitaka wala kuwaza makosa yaliyofanyika mwanzoni, wao wanaamini kwamba wakati wote mafankii yapo na kwa vile wamezaliw ana roho ya ujasiri wa kupenda vituko wako tayari wakati wowote kuyaweka maisha yao katika hatari ili wafanikiwe.


Tabia yao ya kutojali na misukumo au mihemko ya ghafla inawafanya wawe na sifa zilizokithiri za kubahatisha mambo.
Hakimu kwa bahati, hii kwao inakuw asiyo tatizo kwa sababu hawafanya kitu kimoja kwa muda mrefu, ghafla huwa wanarukia katika jambo lingine.


Watu wa Punda wana moyo wa ujasiri wa ushindani na wanafanya vizuri iwapo katika hali hiyo kutakuwa na uadui hasa mtu na mtu.
Katika michezo ya karata ua kupimana nguvu au kuwekeana dau watu wa Punda wana pata bahati sana.
Kwa ujumla watu wa nyota hii wanapenda kubahatika na wanachukia sana kukosa pamoja na kwamba faida zoa wanazopata zinalingana na hasara zinazowafika.

NYOTA YA PUNDA (URAFIKI)


Wenye nyota ya Punda ni wachangamfu, wanaosema kweli na wenye uwazi katika urafiki wao. Kama walivyo katika kila kitu kwenye maisha yao.
Ni wazuri katika kuanzisha urafiki, wakati mwingine wanakuwa wawazi sana katika mazungumzo yao na vitendo vyao kiasi kwamba huwaogopesha baadhi ya marafiki.
Kwa upande mwingine wao wanapendwa kwa sababu ya uaminifu wao na kusema kweli.


Watu wa Punda wanathamini sana uhuru wao na wanapenda kufanya vitu katika njia zao wanachukia sana kufugika au kuogopa watu kwa hiyo urafiki sio kitu muhimu kwa wenye nyota hii . wakati mwingine huwa wanajisikia furaha wanapokuwa katika kundi la watu wanaopenda vituko na mambo ya ajabu.
Watu wa Punda wako katika kundi moja na wale wenye nyota zenye asili ya moto na tabia zao zinafanana. Mfano wale wenye nyota ya Mshale wanakuwa marafiki wao wazuri ambao wanachangia tabia ya kupenda vituko.


Hata hivyo huwa hawapendi au hawaoni umuhimu wa kuwa na rafiki mwenye nyota ya Mapacha. Kwa wenye nyota ya Ndoo kwa vile wanathamini uhuru wao basi wao wanaweza kuelewana nao.
Watu wenye nyota zenye asili ya udongo Mbuzi, Ng’ombe na Mashuke wanakuwa marafiki wazuri wa Punda kwa Sababu wanamsaidia kutekeleza mipango yake kivitendo, pamoja na kwamba madhari na akili za hao Ngo’ombe, Mbuzi na Mashuke kupunguza nguvu ya urafiki wa kudumu.


{mospagebreak}
Kwa ujumla wote wenye nyota zenye asili ya moto mara kwa mara wanakuwa na tofauti na wenye nyota ya Punda hasa katika masuala ya ushindani mfano ni nyota ya simba na Punda wote huwa wananeemeka kutokana na uadui usioepukika katika urafiki wao, kama ikiwa katika kazi au nyumbani au kwenye starehe au wanapokuwa pamoja katika michezo.


NYOTA YA PUNDA (MITINDO)


Mitindo ya Punda ni yenye kuchangamka na nguo zisizo na madoido. Wanapenda wawe wanavaa kulingana na wakati. Mavazi yao huwa yanaambatana na mabegi, saa nzuri au mikufu na vito vyenye kupendeza.
Hata hivyo watu wa Punda hawapendi kupanga kununua au kushona nguo. Wanapendeza sana wakiwa katika mavazi ambayo ni mepesi kuliko nguo zile zilizosanifiwa na zenye madaha.


Suti zilizotafauti yaani suruali na koti tofauti, zikiambatana na buti pamoja na skafu na glavu ndio mavazi hasa na nyota ya Punda. Mavazi hayo yanaendana hasa na tabia yao ya ujasiri na mambo ya ajabu.
Wengi wenye nyota hii huwa wanapenda kuvaa suti za michezo ambazo pia zinaendana na namna yao ya maisha.


Wanapoamua kuvaa nguo, waume kwa wake wanakuwa wavaaji wazuri. Wanapenda nguo zilizoshonwa vizuri na zinazoeleweka.
Rangi zao zinakuwa Nyekundu na Njano na mara nyingi hupendelea nguo zisizo na nakshi.


Wanapenda mitindo thabiti na vitambaa ambavyo ni vyepesi kuvitunza. Wanawake wanapenda sana mikufu ya dhahabu na hereni za kuning’inia.
Kwa ujumla watu wa punda wanapenda kuvaa kulingana na mitindo na wanapenda nguo ambazo zinawafanya watu wakiwaona washituke wakiamua kuvaa nguo maalum basi mavazi hayo yataambatana na vitu vya ziada kama mikufu. Pete, saa visivyo ghali. Hiyo huwainawafanya waonekane na wakati katika mavazi ya aina yeyote.


NYOTA YA PUNDA (TASWIRA YA UMBO)


Inapofikia hali ya kuweka miili katika hali bora wenye nyota hii wana bahati kubwa kutokana na hali halisi ya maisha yao ya kujishughulisha. Kwa kuongezea labda wawe wanapenda kula lakini kama ilivyoanishwa na nyota yao ni watu ambao hawapendi sana vyakula vinavyoweza kuwaletea unene.
Hata hivyo wanafurahia chakula na wanapenda vyakula vyepesi. Kama ikiwa Kalori zinazoingia mwilini zinazidi zinazotoka basi uzito wao huongezeka.


Inapofikia hali ya kupunguza uzito wenye nyota hii wanakuwa hawana subira, wanapenda mlo ambao utapunguza uzito wao upesi na katika muda mfupi inavyowezekana ikiwa ni pamoja na kujiadhibu wenyewe kwa kujimyima chakula kwa muda mfupi wakiwa na imani yakupata matokeo.
Kwa wenye nyota hii muda wa siku chache au hata wiki moja ni muda tosha wa kujinyima chakula ili kupunguza unene.


Baada ya hapo ni juu yao kuwa na ratiba maalum ya ulaji wao ikiambatana na mazoezi ya kila siku, kama kuongelea, kukimbia, au kutembea kwa nguvu kwa muda mrefu wenye nyota hii wanahitaji mazoezi ya kila siku ili waweze kupunguza uzito. Vinginevyo itawawia vigumu baadaye.
{mospagebreak}


Kwa ujumla wenye nyota hii huwa wanapata uzito mkubwa kwa sababu huwa wanajishughulisha sana kula milo ya kawaida ikiambatana na vitu vitamu vilivyojaa Kalori wanapokuwa wamechoka.
Wanashauriwa kutumia muda wao kula tu milo ya kawaida hiyo itawasaidia kuondoa au kupunguza unene na kuboresha afya zao.


NYOTA YA PUNDA (USHINDANI NA UADUI)


Wenye nyota hii wanapenda sana ushindani na kuonyesha madaraka na uwezo wao, kwa sababu hii wanachukiwa na watu wengi. Wanapenda sana wawe wa kwanza na watatumia mbinu zozote ili wafanikiwe.
Punda wako wazi na waaminifu katika malengo yao ni watu wenye kusema ukweli na haamini visingizio, ulaghai wala kuficha siri.


Wanapenda kufanya mipango yao moja kwa moja na mtu yeyote akiingilia huwa unazuka ugomvi. Ikitokea hivi watu wa Punda huwaeleza wagomvi wao bila kuficha kinachoendelea.
Kutokana na ukweli na uwazi wao wenye nyota hii huwaudhi sana watu wengine kwa maneno yao na vitendo vyao.


Ni tabia yao kutojali hisia za watu na wala hawana muda wa kufikiri, maneno wanayosema au vitendo vyao vitawaathiri vipi wenzao.
Mara nyingi watu wa Punda, hushinda vita vyao kutokana na uwezo wao na nguvu zao za ukatili lakini ikitokea pakatakiwa kujieleza au kutoa hoja au diplomasia huwa wanashindwa kujieleza.


Wakiwa katika siasa hali ya uadui huibuka kutoka kila upande, wao huneemeka sana Kisiasa kutokana na upinzani na uadui mkali uliopo duniani ambao wao hufurahia.
Kwa ujumla watu wa Punda ni washindani katika sehehmu zote, ni madereva wanaopenda kwenda kasi hivyo wanapenda mashindnao ya magari. Mara nyingi watu wa nyota hii wanapenda michezo yenye ushindani au kutumia nguvu ikiwa kama jambo la kupitisha muda au kazi yake, na hii inawapa changamoto katika kuendeleza ushindani wao wa Asili.


NYOTA YA PUNDA (MANUNUZI)


Kama tulivyoona tangu mwanzo wenye nyota hii wanapenda ushindani, kushughulika na vitendo na hawapendi kabisa kufuata utaratibu kwa hivyo kununua vitu ni mojawapo wa mambo wanayoyapenda sana.
Vile vile wanapenda kupungua na kupanda kwa manunuzi au msisimko wa kwenda dukani katika mitaa inayopendeza au katika nchi za nje.


Wenye nyota hii wanapokwenda kufanya ununuzi hufanya juhudi ya kuamka mapema ili wawakwepe watu, na manunuzi yao wanayafanya haraka haraka.
Huwa wanakwenda kutoka duka moja hadi jingine wakizunguka kiuerevu kufanya manunuzi.


Wanapenda kununua vitu vya wiki nzima na orodha yao lazima vitakuwepo vyakula vya kupikwa kwa haraka au vya kuliwa papo kwa papo kama nyama za kopo au Samaki wa Kopo. Mara nyingi hawana muda wa kupika na hawapendi kutumia muda wao mwingi jikoni.
Kwa hiyo kitu ambacho hawa watu wa Punda wanapenda kununua. Jibu ni kwamba wanunue chochote ambacho kitaharakisha mwendo wa maisha yao.


Mfano wanapenda magari yanayo kwenda kasi au vitu ambavyo wanaviota, kama ramani, glavu za kuendesha gari na viatu.
Kwa ujumla watu wa Punda huwa hawapendi kwenda dukani kila siku lakini wanaona raha ikiwa kwa kufanya hivyo watapata ushindani.
Wanapenda kushindana na rafiki zao ili kuonyesha nani atanunua mwanzo na kitu kizuri au kubishana katika bei ya kitu fulani, hiyo inawafanya wajisikie raha sana.


 
Back
Top Bottom