MAKANJAMNA
JF-Expert Member
- Aug 8, 2013
- 1,138
- 1,515
uEMMANUEL Muhuge Magende, mkazi wa Wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam anasimulia kisa alichowahi kukumbana nacho miaka mitatu (2010) nyuma baada ya kugongwa na gari dogo akiwa
anavuka barabara ya Kawawa eneo la Mkwajuni, jirani na msikiti.
Anasema: Nakumbuka ilikuwa tarehe kumi na tisa, mwezi wa saba, nilipanda daladala pale sokoni
Kariakoo. Hili daladala lilikuwa likienda Mwenge kupitia Kinondoni kisha kupita Morocco na kuunga Barabara ya Ali Hassan Mwinyi.
Nilikaa kwenye siti ya kwanza mlangoni. Wakati naingia, kwenye siti hiyo alikaa mzee mmoja kwa makadirio ya umri alikuwa kama ana miaka sabini hivi.
Huyu mzee mimi nilipoingia tu, akasimama na kuniambia nikae pale ambapo pembeni yake palikuwa na abiria. Nilimkatalia kwa sababu daladala lenyewe lilijaa, sasa mzee kama yeye akiniachia siti mimi ambaye wakati huo nilikuwa na miaka 45 nilihisi si sawa.
Cha ajabu huyu mzee alilazimisha sana akisema yeye anakwenda kukaa siti ya nyuma. Ilifika mahali nilimkubalia, nikakaa yeye akatoka kuelekea nyuma lakini sikumfuatilia hadi kukaa kwake.
Muda huohuo, daladala liliondoka, likapita njia yake hadi Faya ambapo halikusimama kwa sababu nafasi haikuwepo. Kufika Magomeni ya Hospitali, daladala lilisimama, abiria walishuka wengi tu hadi nafasi ya kukaa watu wengine ikabaki. Wakati abiria wakishuka nilikuwa namwangalia mmoja baada ya mwingine ili kama kuna yule mzee nimwambie namlipia nauli, lakini hakuwepo, nikajua bado yupo ndani.
Daladala lilipoondoka hapo halikusimama Kituo cha Morocco Hotel mpaka Mkwajuni ambapo mimi nilikuwa nashuka. Kwa kuwa nilikuwa jirani na kondakta nilimwambia shusha hapo Mkwajuni, akagonga daladala likasimama. Nilisimama huku nikimwangalia yule mzee ili nimwambie namlipia, lakini sikumwona!
Nilishuka, kufika chini nikasimama ili kuvuka barabara maana nilikuwa naishi upande wa pili wa kituo hicho.
Cha ajabu sana nikamwona yule mzee kwa ngambo akiwa anatembea kwenda uelekeo uleule ninaokwenda mimi.
Nilivuka barabara haraka ili nimuwahi, lakini nikiwa katikati ya barabara hiyo gari dogo, jekundu, lilitokea upande wa Kinondoni Studio na kunifuata kwa kasi. Nilifanya jitihada zote kulikwepa lakini ilishindikana, likanigonga! Sikujua kilichoendelea.
***
Mbele yangu kulikuwa na jumba kubwa la kifahari, sikujua kama wanaishi wanadamu au la! Nilitembea kuelekea kwenye ile nyumba. Ilijengwa si kwa matofali wala simenti, ilionekana kama vioo vya kujitazamia ndivyo vilitumika sana.
Nilikuwa katika hali ya kuogopa sana, hivyo kufika kwangu kwenye nyumba ile kulikuwa na maana ya kuomba msaada. Kuogopa kulisababishwa na mazingira, sikuona jua, sikuona mawingu wala sikuona ardhi, nilitembea juu ya vioo.
Ili uingie mlangoni kulikuwa na ngazi tatu. Nilikanyaga ya kwanza na ya pili, nilipotaka kukanyaga ya tatu, mlango ulifunguka wenyewe nikaingia kama kwa kulazimishwa.
Ndani niliwakuta watu wengi weupe, naweza kusema walikuwa Wazungu pia naweza kusema walikuwa Waarabu, lakini hakukuwa na mtu mweusi hata mmoja.
Watu wote waliniangalia nilipokuwa naingia, wakanishangilia sana huku wengine wakiwa wanapiga vigelegele. Lakini pamoja na vigelegele hakukuwa na mwanamke.
Walikuwa wanaume wenye midevu mingi, warefu mfano wa watu warefu wakiwa wawili kwa kwenda juu hivyo mimi nilikuwa nawaangalia kwa juu.
Mmoja alinifuata na kunishika mkono. Akatembea na mimi hadi kwa wenzake, mmoja akanipokea hapo akanipeleka mbele ya jumba hilo ambako pia kulikuwa na mlango mkubwa kama niliouingia.
Unajua uko wapi hapa? aliniuliza.
Niko ugenini.
Ni ugenini ndiyo, ni wapi?
Mimi sijui.
Ngoja nikuoneshe ulikotoka, alisema yule mtu na kunitoa nje, tulitoka na yeye, akanyoosha mkono kuangalia juu huku akisema:
Unakuona kule?
Niliinua macho na kuangalia juu, nikaona dude kubwa likiwaka kama mwanga wa taa za kisasa.
Umeona kule? yule mtu aliniuliza.
Ndiyo, nilimjibu.
Ni nini?
Dude.
Siyo dude, wewe umetoka kule.
Ina maana ile ni dunia?
Ile ni dunia, na pembeni yake unachokiona kidogo ni mwezi.
Huku sasa ni wapi?
Huku sasa ndiko wanakokuja watu waliokufa wakisubiri kupewa adhabu.
Ina maana mimi nimekufa? nilimuuliza, akacheka sana kuonesha kwamba mimi ni mjinga sana kama sijui kama nimekufa.
Unataka kujua kama umekufa au la!
Ndiyo, nataka kujua.
Alinirudisha ndani ambapo hakukuwa na mtu hata mmoja, tukatembea kuelekea upande wa mashariki mwa jumba hilo hadi kwenye mlango mwingine mkubwa sana, ukafunguka wenyewe. Tuliingia ndani ambako tulikuta watu mchanganyiko, wengine weusi kama mimi wengine weupe.
Walikuwa wamekaa wakiangalia skrini moja kubwa sana. Ndani ya skrini hiyo kulikuwa na watu wanafanya mambo mbalimbali. Wengine walikuwa wanafanya zinaa, wengine wanaiba, wengine wanapigana, wengine wanachinja binadamu wenzao.
Kifupi ni kwamba watu walikuwa wakifanya madhambi ndicho nilichokibaini mimi.
Watu wote walikuwa wamekodolea macho ile skrini, lakini tulipoingia sisi wakageuka kutuangalia. Mmoja akauliza:
Huyo naye haamini kama amekufa?
Yule niliyekuwa naye akajibu:
Ndiyo.
Nilikaribishwa kiti nikakaa halafu skrini ikazimwa. Baada ya muda ikaanza kuonesha picha yangu. Nilionekana napanda daladala Kariakoo. Picha hiyo ikanionesha nikiwa nazungumza na yule mzee akisema anipishe kwenye kiti chake.
Cha ajabu, huyo mzee awali alionekana kama nilivyomwona mimi lakini ghafla akageuka, akawa mweupe kama watu niliowakuta kwenye lile jumba.
Tukio zima lilionekana, daladala likipita Magomeni, likakata kona kwenda Hospitali na kupita Hoteli ya Morocco hadi Mkwajuni.
Nilimwona yule mzee akitoka kwenye daladala kwa kupitia kioo cha mbele cha dereva kisha akavuka barabara kabla hata daladala halijasimama.
Nilionekana nashuka, natembea kwenda kuvuka barabara. Lile gari jekundu lilizuka tu palepale jirani yangu na kunigonga.
Je, kiliendelea nini? Tuonane jioni ...
Kwa Mtu Mwenye nyota ya Punda Tabia yake ni moto ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( ARIES - The Aggressive
(March 21 to April 19)
Kwa Mtu Mwenye nyota ya Ng'ombe Tabia yake ni Udongo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( TAURUS - The Tramp
(April 20 to May 20)
Kwa Mtu Mwenye nyota ya Mapacha Tabia yake ni upepo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( GEMINI - The Twin
(May 21 to June 20)
Kwa Mtu Mwenye nyota ya Kaa Tabia yake ni maji ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( CANCER - The Beauty (June 21 to July 22)
Kwa Mtu Mwenye nyota ya Simba Tabia yake ni Moto ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( LEO - The Lion (July 23 to August 22)
Kwa Mtu Mwenye nyota ya Mashuke Tabia yake ni udongo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( VIRGO - The One
that Waits (August 23 to September 22)
Kwa Mtu Mwenye nyota ya Mizani Tabia yake ni Upepo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa (LIBRA - The Lame One
(September 23 to October 22)
Kwa Mtu Mwenye nyota ya N'ge Tabia yake ni maji ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( SCORPIO - The Addict
(October 23 to November 21)
Kwa Mtu Mwenye nyota ya Mshale tabia yake ni moto ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( SAGITTARIUS - The
Promiscuous One (November 22 to December 21)
Kwa Mtu Mwenye nyota ya Mbuzi tabia yake ni udongo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( CAPRICORN - The
Passionate Lover (December 22 to January 19)
Kwa Mtu Mwenye nyota ya Ndoo Tabia yake ni Upepo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa (
AQUARIUS - Does It in the Water (January 20 to February 18)
Kwa Mtu Mwenye nyota ya Samaki Tabia yake ni Maji ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa ( PISCES - The Partner
for Life (February 19 to March 20)
Hadithi si za ukweli ni za kutunga tu mkuu.Kaka mzizi mkavu,nilitaka kujua kuhusu nyota ya mapacha(gemin) na kama kuna hadith nyengine link tofauti na malkia wa gorl na hii ,za ukweli sana,mungu akupe maisha marefu,uzi zako zaukweli
Heshima kwako. MziziMkavu kwa kweli unazidi kutupevusha akili zetu,ubarikiwe kwa kujitolea kufanya hivyo.
Tungefurahi na sisi wa nyota ya Mizani(libra) kama ungetujuza kuhusu Tabia,biashara,kazi,Uhusiano wa mapenzi,maradhi,madini,namba ya bahati na vingne vingi kama ulivyodadavulia wenye nyota ya Mapacha na Ng'ombe.
Huwezi kuwa na nyota mbili ukiwa unajuwa Tarehe yako ya kuzaliwa huna haja ya kuangalia herufi . Ukiwa hujuwi tarehe yako ya kuzaliwa ndio waweza kuangalia herufi sasa wewe chaguwa moja usinichanganye akili yangu wewe unajuwa tarehe ya kuzaliwa kwanini unaangalia herufi?Kwa Mtu Mwenye nyota ya Ndoo Tabia yake ni Upepo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa (AQUARIUS - Does It in the Water (January 20 to February 18) na kisha tena umetoa maana ya herufi ya kwanza katika nyota jina langu linaanza na herufi ''z''
HERUFI Z
Mwenye jina linaloanzia na herufi Z ni mtu mwenye kupenda matumaini na amani. Ni wenye msimamo mkali ila wanashauriwa kufikiria kabla ya kuamua jambo. Herufi Z inawakilisha Nyota ya Ng'ombe.
MASWALI YANGU NI HAYA
1: m2 unaweza kuwa na nyota mbili maana hapo kwa maelezo yuako tiyali ni nanyota mbili
2: Kwa Mtu Mwenye nyota ya Ndoo Tabia yake ni Upepo ni yule aliyezaliwa Tarehe hizi hapa (
AQUARIUS - Does It in the Water (January 20 to February 18)............
mkuu mm nimezaliwa katika ya hzo trh hapo juu NA linaanza na herufi Z vp tabia za watu wenye nyota hyo na wafanye kazi ya dizain gan au biashara ya dizain gani na pia pia wanatakiwa wawe na marafiki wa aina gani na vp mahusiano yao ya kimapenzi huwa wanakuweje ?
Heshima kwako. MziziMkavu kwa kweli unazidi kutupevusha akili zetu,ubarikiwe kwa kujitolea kufanya hivyo.
Tungefurahi na sisi wa nyota ya Mizani(libra) kama ungetujuza kuhusu Tabia,biashara,kazi,Uhusiano wa mapenzi,maradhi,madini,namba ya bahati na vingne vingi kama ulivyodadavulia wenye nyota ya Mapacha na Ng'ombe.
Niambie jina lako la kwanza linaanzia na herufi gani? na pia niambie umezaliwa tarehe gani? kwanza ndio ninaweza kukujibu swali lako asante.Mzizi, nashukuru sana kwa ufafanuzi wa nyota ya Punda... Hii ndo nyota yangu kwa mujibu wa maelezo yako, na nilivyofuatilia tabia za nyota hii na kulinganisha na tabia zangu, zinafanana kwa asilimia 98%, pengine asilimia 2% zilizobaki sijajichunguza. Ila nimefurahi sana tena sana... Mkuu una uwezo mkubwa sana ambao awali sikuufikiria kuwa ungekuwa nao.. Wakati napitia maelezo yako juu ya nyota ya punda nilikuwa nashituka mara kadhaa nikidhani unaniona au unanijua vema. Mungu akuzidishie... Nina SWALI: mimi natakiwa kuoa mwanamke wa nyota gani? Je mwanamke mwenye jina linaloanzia G au A au W anaweza kuwa mke wangu? BIG LIKE 
Hadithi si za ukweli ni za kutunga tu mkuu.
NYOTA YA MAPACHA (GEMINI)
- Hii ni nyota ya tatu katika mlolongo wa nyota 12.
- Wenye nyota hii ni wale waliozaliwa kati ya tarehe 21 Mei na 20 Juni ya mwaka wowote.
- Sayari yao ni Mercury (Attarid).
- Siku yao ya bahati ni Jumatano.
- Namba yao ya bahati ni 5.
- Rangi yao ya bahati ni njano na bluu isiyoiva.
- Asili ya nyota yao ni upepo.
KIPAJI CHA MAPACHA: (TELEPATHIC):
Wenye nyota hii wana kipaji kikubwa cha kuwasiliana na watu ambao wako mbali kwa kutumia akili zao au hisia walizokuwa nazo.
TABIA ZA MAPACHA:
Watu wenye nyota hii ni watu wenye hisia kali sana ambao wanakasirika upesi, ni watu wasiotulia na wenye uwezo mkubwa wa kujieleza na kuzungumza na wanaweza sana kushawishi watu.
Ni watu ambao wanapenda sana mabadiliko na tofauti na wanapenda sana kujua mambo, wanapenda watu na wanapenda kujumuika na watu lakini wakati mwingine hawaeleweki. Wanapenda kusafiri sana.
TABIA YA MAPACHA KATIKA MAPENZI:
Watu wenye nyota ya Mapacha wanajulikana sana kwa hadhi yao ya kuwa na sura mbili. Kuna wakati wanakuwa na hisia tofauti na muda si muda wamebadilika.
Pamoja na kwamba hawapendi kubanwa sana , ni watu wachamgamfu na wenye mahaba mazuri.
Ni watu wenye asili ya mawasiliano na ni vigumu sana kuwafanya wajinga hivyo basi wakishampenda mtu wanahakikisha kwamba hawamchoshi huyo mpenzi. Watatumia muda mrefu kuzungumza maneno mazuri na wapenzi wao ili kuhakikisha kuwa uhusiano unazidi kuwepo.
Katika mapenzi, wao wanapenda vitu tofauti tofauti na wanahisi wamechoshwa basi huwa wa kwanza kuondoka aidha kwa muda au moja kwa moja.
Uaminifu ni kitu kigumu kwa watu wenye nyota hii na wanahisi kwamba kuna kitu wanakikosa nje hivyo basi wanatoka sana nje hata kama wakiwa wana ndoa yenye furaha.
Wengi wao wanafikia hatua ya kuishi maisha ya sehemu mbili; mke na bwana au bwana na mke.
{mospagebreak}
MATATIZO YA KIAFYA:
Nyota hii inatawala mabega, mikono, viganja na sehemu ya juu ya mbavu.
Tatizo la kutopumzika kwa sababu ya kutafuta mambo mapya ndio yanayosababisha maradhi kwa wenye nyota hii. Wanafikia mpaka hali ya kuisahau miili yao na mara nyingi wanapata matatizo ya neva kutokana na uchovu kwa mishughuliko mingi.
Matatizo yanayotokana na nyota hii ni mgonjwa kukosa pumzi (bronchitis), pumu (asthma), matatizo ya kifua, mafua, flu, ajali za mara kwa mara kwenye mikono na mabega.
KAZI ZA WENYE NYOTA YA MAPACHA:
Kwa vile wenye nyota hii asili yao ni upepo na wao ni wenye kuzaliwa kwenye mawasiliano na uhusiano, wanapenda sana uhuru na uwazi katika kazi zao.
Wanapenda sana kazi ambazo zinawashughulisha na kufanya akili zao zisipumzike lakini siyo jambo hilo hilo kwa muda mrefu. Kuwa na mawasiliano na watu wengi kwa wakati mmoja ndio jambo linalopendwa na wenye nyota hii. Kazi zao hasa ni zile zinazohusiana na mambo ya utangazaji wa radio na televisheni.
Kazi ambazo zinahusika na mambo ya vitabu au uchapishaji vitabu. Kazi za kufundisha na kazi za ushauri nasaha.
Vilevile wenye nyota hii wanatakiwa wafanye kazi za ukalimani au kazi za biashara lakini zinazohusiana na safari za nje.
FAMILIA ZA MAPACHA:
Watu wa nyota ya Mapacha ni waliochangamka na wenye hiari na wazazi wa Mapacha huingia katika msisimko wa watoto wao kwa raha.
Ni wazazi wenye furaha muda wote katika kutekeleza shughuli zao za nyumbani pamoja na kupenda kucheza na watoto wao na wana mipango mizuri na wanajua wapi wakiwapeleka watoto watafurahi.
wenye nyota hii wanathamini sana elimu na hawawezi kuishi bila mawasiliano na habari, hivyo huwa wanapenda kuwanunulia watoto wao vitabu vingi.
Tatizo linalotokea iwapo mtoto ataonyesha kwamba hapendi kusoma na watajaribu kila njia kumuweka katika njia wanayoitaka wao. Wakishindwa wanaacha.
Wazazi wa Mapacha hawawezi kuelezea jambo na hawana uvumilivu wa kun'gan'gania kwa mtoto asiyeelewa mambo.
MADINI YA MAPACHA:
Wenye nyota ya Mapacha wanatakiwa wavae madini ya Agata au kito chochote chenye rangi ya njano. Kito hicho inasemekana kinamuwezesha mvaaji awe na uwezo wa mawasiliano na ufahamu.
UHUSIANO WA KIMAPENZI:
(MAPACHA NA MSHALE)
Tabia ya Mapacha ya kupenda kufahamu na kuelewa mambo hutulizwa na tabia ya Mshale ambao ni wasomi na wenye kuelewa mambo mengi.
VYAKULA VYA MAPACHA:
Wenye nyota hii wanashauriwa wapende kula vyakula vifuatavyo ambavyo ndio vinavyotawaliwa na nyota yao. Vyakula vyenyewe ni kuku, rasiberi, karoti na uduvi.
NCHI ZA MAPACHA:
Ili kupata mafanikio ya kinyota wenye nyota hii wanashauriwa watembelee au waishi katika nchi au miji ifuatayo inayotawaliwa na nyota yao. Nchi hizo ni Ubelgiji na Wales, na baadhi ya miji ni London (Uingereza) na San Fransisco (Marekani).
RANGI ZA MAPACHA:
Wenye nyota hii wanashauriwa kinyota wapake au watumie rangi za njano au bluu isiyoiva ambayo inapendeza ikipakwa ndani ya nyumba.
Ukitaka kujuwa Pete ya Bahati yako au Pete ya kinga yako dhidi ya maaduwi zako wasiliana na mimi kwa njia ya Email nitumie baruwa ya pepe Email yangu hii hapa fewgoodman@hotmail.com
Yani kufundishwa ushirikina ndio kupevushwa akili?