Nusu siku ndani ya jeneza

Nusu siku ndani ya jeneza

NUSU SIKU NDANI YA JENEZA - 9-

ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:
Kuna swali nilikuwa nalo nje kabisa na hayo, nikamuuliza:
“Eti, kuna viumbe wanaweza kupenya kuingia ndani ya nyumba hata kama imefungwa?”
“Wapo, hata mimi naweza.”
“Inakuwaje?”
“Sisi tuna miili ya moto, hatuna mifupa kama unavyodhani.”
“Kama ungekuwa hauna mfupa ungekuwa hai?”
“Uwezo wetu na wenu ni tofauti sana.”
SASA ENDELEA…


“Huwa inakuaje?”
“Mimi nikifika sehemu kwenye mlango naweza kupenya sehemu yenye nafasi ndogo sana, kwa sababu kinachokushinda wewe kupenya ni mifupa.
Viumbe wote wenye uwezo wa kujibadili wapo hivyo, hawana mifupa hata kama unawaona kama binadamu walivyo.”
“Nina swali jingine”
“Uliza.”
“Kuna peponi, mbinguni, duniani, jehanamu na wapi kwingine?”
“Tunavyojua sisi, kuna mbingu, kuna pepo na mahali tunapopaita bostinia, yaani mahali pa mapumziko. Hapa bostinia tunajua ni sehemu ambayo waliokufa wote wanakuwa hapo mpaka siku ya hukumu ya watu wote.”
“Kwa hiyo hakuna jehanamu?”
“Nani kasema ipo? Jehanamu lilikuwa ni eneo la kutolea adhabu kwa watu kule Israel. Unajua zamani mji wote wa Jerusalem ulizungukwa na ukuta mrefu wa kujihami kwa ajili ya uvamizi kutoka kwa maadui.
“Sasa jehanamu palikuwa nje ya ukuta ambapo takataka zote zilikuwa zikimwagwa huko. Kutokana na eneo hilo likaanza kufuka moshi na hatimaye kuzuka moto, hivyo hata watu waliofanya makosa makubwa walitupwa huko. Ilipotokea mtu amefanya kosa anaambiwa atatupwa jehanamu yaani kwenye lile eneo lao.
“Mbona katika mafundisho ya imani yangu niliambiwa nikitenda dhambi nitatupwa jehanamu?”
“Yule kiongozi wenu mkuu sana aliyesema vile alikuwa akiwatolea mfano watu wa Israel kwamba wakitenda dhambi kuna moto wa adhabu na wataweza kutupwa kwenye huo moto kama wao wanavyowatupa watenda dhambi pale jehanamu yao. Isingekuwa rahisi yule kiongozi wenu mkubwa atoe mfano ambao wale wasingeuelewa.”
“Sasa watenda dhambi wa duniani watatupwa wapi?”
“Kwenye ziwa la moto.”
“Nina swali jingine.”
“Uliza.”
“Nimekusikia ukisema yule kiongozi wenu mkubwa sana, kwa nini usimtaje jina?”
Nilimwona yule kiumbe anakunja ndita kama ishara ya kukasirika, nikaogopa sana. Nikakumbuka mambo ya nyuma nikiwa duniani, siku moja niliwahi kwenda kwenye mkutano wa Injili uliokuwa ukihubiriwa na Askofu Kakobe pale Jangwani, Dar es Salaam ambapo alisema:
“Mashetani huko waliko wanamjua Yesu ni nani? Ndiyo maana ukilitaja hilo jina wanakimbia, wenyewe pia hawawezi kulitaja jina la Yesu wanasema yule mtu mkubwa au yule kiongozi mkubwa.”
“Usije kuniuliza swali kama hilo tena na kama utarudia itakuwa mwisho wa uhai wako moja kwa moja. Sisi huku hatuogopi kulitaja hilo jina mbona Mungu tunamtaja?”
K
auli hiyo ilinitatiza sana kwamba ni kwa nini aliweza kulitaja jina la Mungu lakini akashindwa kulitaja jina la Yesu?
Nikiwa nafikiria nikasikia akili kichwani ikiniambia huyo anajua miungu wako wengi, lakini Mungu aliyeumba mbingu na nchi ni mmoja tu ndiyo maana analisema lakini hamaanishi Mungu wa m kubwa bali anamaanisha mungu wa m ndogo!
Nilimwomba radhi yule kiumbe kwamba sitarudia tena kutenda kosa hilo ambalo lilimkera sana.
“Nilitaka kuuliza swali moja la mwisho.”
“Uliza.”
“Ni amri gani ya Mungu aliyeumba mbingu na nchi ambayo ni kubwa kuliko zote?”
“Kwanza unapomtaja Mungu si lazima uyaseme hayo maneno ya mbele, sawa?”
“Sawa.”
“Amri kuu ni moja tu, ni upendo. Unajua ukiwa na upando huwezi kumfanyia jambo baya mwenzako. Upendo unatawala amri zote za duniani. Ukimpenda mwenzako huwezi kutembea na mke wake, huwezi kutembea na mume wake, huwezi kumwibia chochote, huwezi kumsengenya, yaani upendo ni amri kubwa sana na sisi huku tunapambana zaidi na upendo.”
“Mnapambana kivipi?”
Kabla hajanijibu aliniangalia kwanza kisha akaangalia pembeni kama anayeangalia kitu halafu akaniangalia tena.
“Unajua leo ngoja nikwambie sisi tunavyofanya kazi na binadamu. Sisi tuna uwezo wa kuingia kwenye akili au mawazo yenu tukafanya lolote. Tuna uwezo wa kumwamuru mtu asimame kama alikaa, yeye akaamini ni mawazo yake kumbe ameamriwa.
“Labda nikupe mfano mkubwa, kuna roho chafu za kila dhambi, yaani kuna roho chafu wa ngono, kuna roho chafu wa ugomvi, kuna roho chafu wa masengenyo, roho chafu wa pombe, roho chafu wa sigara, roho chafu wa wizi, yaani kila jambo baya lina roho wake mchafu.
“Sasa kila roho ina mtu wake. Mfano wewe una roho ya kupenda vya watu. Ukimwona mke wa mtu unamtaka, akiwa hajaolewa humtaki, ukiona gari la mtu unalitamani, ndiyo roho yako.
“Hawa roho wote hufanya kazi zao chini ya roho chafu moja ya kuamuru. Roho inayoamuru ndiyo inayoweza kumfanya mtu aamke usiku na kwenda kuiba mahali.
“Mfano, umekaa baa unakunywa pombe, roho ya ugomvi ikikujia inapamba na roho ya kuamuru. Mtu atapita mbele yako, halafu atakugusa lazima utawaka na kuanza kugombana kwa sababu tayari roho hiyo iko moyoni mwako.
“Mfano mwingine, roho mchafu wa ajali akikujia, hata kama umelala atakupa mawazo ya kutoka nyumbani kwako na kwenda mahali ilimradi upande chombo cha usafiri na kupata ajali.
“Hizi roho sasa hazikai kwa mtu wakati wote ndiyo maana kama ni mlevi inaweza kukujia jioni au usiku mpaka ukajikuta kulala bila kunywa pombe huwezi, lakini ikishakuingiza kwenye tendo ovu hutoka na kurudi kwenye makazi yake na kukuacha wewe katika majuto.
“Hebu fikiria kuhusu hili. Watu wengi wanapoingiwa na roho ya uzinzi huenda gesti wakiwa wameongozana hata kama ni saa sita mchana, lakini baada ya kumaliza dhambi hiyo wakati wa kutoka wanakuwa wenye aibu sana, ndiyo maana watatoka mmoja mmoja. Mara nyingi anaanza mwanaume kutoka. Ile ni aibu kwa sababu ujasiri wa lile pepo la ngono unakuwa umeshatoka, mtu anakuwa ana ufahamu wake mwenyewe.
Hapa naomba nifafanue kwamba ninaposema kila mtu ana pepo la dhambi moja ninamaanisha kufanya jambo kupita kiasi na lenye madhara.


Ili kujua zaidi usikose kusoma baadae
 
Last edited by a moderator:
MziziMkavuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu uniite ukiweka!!!
 
Last edited by a moderator:
Kuna tofauti nimezipata leo huk nyuma nilikuwa nazitumia ndivyo sivyo
1. Peponi na Mbinguni.
2. Bin Adamu (Binadamu) na Mtu.
3. Milele na Maisha.

SWALI SASA

"Mwanamke si mtu bali ni Kiumbe"

Waungwana naombeni tofauti kati ya mtu na kiumbe.
 
Kuna rafiki yangu anasemaga mwanamke ni kitu sio mtu! Linapikuja swala la mapenzi na mali
 
NUSU SIKU NDANI YA JENEZA - 10-


ILIPOISHIA JANA :
Mara nyingi anaanza mwanaume kutoka. Ile ni aibu kwa sababu ujasiri wa lile pepo la ngono unakuwa umeshatoka, mtu anakuwa ana ufahamu wake mwenyewe.
Hapa naomba nifafanue kwamba ninaposema kila mtu ana pepo la dhambi moja ninamaanisha kufanya jambo kupita kiasi na lenye madhara, binadamu anayevuta sigara kupitiliza ile ni roho chafu yake na binadamu huyo utamuona akikosa sigara hata nguvu zinamwishia au zinamtoka kabisa, kama alilala anatoka kwenda kununua na kuvuta ndiyo roho yake inatulia.
ENDELEA SASA


Si rahisi kwa binadamu wa kawaida kuishinda roho hii, mara nyingi inatanguliza uwezo wa mtu kutenda hilo kosa. Ndiyo maana mtu akizini, hawezi kufikiria kuzini tu lazima kuna muda ataisikia sauti nyingine ikimzuia kufanya tendo hilo kwamba ni dhambi.
Sisi tulishahukumiwa, yaani hatuna tena msamaha hata iweje, ndiyo maana tunakazana kila sekunde kuhakikisha wanadamu wanaopotea ni wengi kuliko wanaokwenda kwenye njia za Mungu wenu.
Kuna pepo la maafa na vilio, kazi yao ni kuhakikisha binadamu wanalia na kufa kila sekunde. Haya mapepo yapo kwa kitengo, mfano wapo wa ajali, wapo wa sumu, wa magonjwa, wa vifo vya ghafla, lakini mwisho wa kazi zao ni kuua na kusababisha vilio.
Napenda nikupe mfano mmoja, nyinyi binadamu mtu akifa mna kawaida ya kusema ni mapenzi ya Mungu au ni mipango ya Mungu, mnakosea sana kwa sababu hamjui lolote na tena hamjui maandiko.
Mungu alipanga binadamu azaliwe, akue, aishi mpaka miaka ya uwezo wake wa kimwili ndipo afe. Kwa sasa Mungu amesema mnatakiwa muishi miaka 75, kupita hapo ni lazima muwe na nguvu. Kwa hiyo mtu akifa mapema, yaani kabla ya miaka hiyo, mfano mtoto mdogo, kijana wa miaka 25 au mtu mzima wa miaka 45, hicho kifo si mpango wa Mungu, ni sisi.
Watumishi wote wa Mungu waliishi miaka mingi hadi uzeeni mwao, wakalala kwa mapenzi ya Mungu wenu. Kama umesoma kitabu cha Biblia utaona kizazi cha Adamu na Eva ambacho ni Kaini, Abeli, Enoko, Noa, Abrahamu, Sarah, Loti, Isaka na kuendelea walilala pale walipofikisha umri wa kufanya hivyo.
Sasa nitoe mfano wa pepo la ajali, hili pepo lina tabia ya kuwaangalia binadamu katika kundi moja tu, mkusanyiko. Mfano, pepo limeona basi limebeba watu wengi, hapohapo linaamua kuingilia kati na kuua.
"Kama unataka kuuliza kitu, uliza tu."
"Ina maana mtu akifa tunavyosema siku yake ilifika tunakosea?"
"Mnakosea sana, siku ya binadamu kufa ni kufika kwa umri alioupanga Mungu wenu. Wapo binadamu waliishi miaka mingi sana, kama sijakosea Methusela ndiye aliongoza, aliishi miaka 969 ndipo akafa. Baadaye Mungu wenu alipunguza umri wa kuishi, ilishuka polepole hadi kufikia miaka 75 ndiyo maana ajali nyingi haziwakuti wazee wenye miaka hiyo, we fuatilia utagundua hilo.

Kinachotuumiza sisi huku ni jinsi nyinyi mlivyojaaliwa kuwa na maandiko ili msome lakini hamfanyi hivyo ndiyo maana mnapitwa na utambuzi wa mambo mengi sana. Nyoka zamani alikuwa na miguu kama mjusi, kwenye maandiko yenu ipo lakini wengi hamjui.
"Kivipi? Si kweli," nilidakia.
"Si hilo tu, hivi mnajua kama mwanamke mwanzoni kabisa alikuwa akizaa bila uchungu?"
"Hamna bwana," nilidakia tena.
Sikiliza wewe, maandiko yenu wenyewe yanasema Mungu wenu alipoibaini dhambi iliyotendwa na Eva na mumewe Adam kwa kushawishiwa na mmoja wetu ambaye alijifanya nyoka, alitoa adhabu kali.
Katika adhabu hiyo, kila mmoja alipewa ya kwake. Adamu aliambiwa adhabu yake itakuwa kutoa jasho ili apate chakula ndiyo maana mpaka sasa kule duniani kwenu mwanaume ndiye anayelisha nyumba kwa kufanya kazi, tena wengine wanafanya kazi ngumu na nzito.
Mwanamke yeye kufanya kazi anapenda mwenyewe kwa sababu si adhabu yake. Yeye aliambiwa adhabu yake itakuwa kuzaa kwa uchungu. Pia akaambiwa atatawaliwa na mwanaume.
"Kwa hiyo ina maana wanawake wanaposema usawa wanakosea?" nilimuuliza.
Wanakosea sana kwani wanavunja maagizo ya Mungu wenu. Kwetu sisi wanawake ndiyo tunaowatumia kuuvunja utaratibu wa Mungu wenu, mifano ipo mingi sana.
Ukianzia na mwanzo kabisa wa maandiko kwenye kitabu chenu cha Agano la Kale ambacho kiliandikwa mwaka wa 1688 kabla ya kuzaliwa mkubwa wenu (Kabla ya Kristo).
Adamu alimkosea sana Mungu kwa kutumiwa na mke wake. Nyoka alimdanganya Eva kuhusu tunda akalila akampa na mumewe naye akalila, Mungu akakasirika.
Ukitoka kwa Adam utakutana na Samson yule mnadhiri wa Mungu wenu, naye alimkosea Mungu kwa kupitia kwa mwanamke ambaye ni Delila.
Ukiachana na Samson, Mfalme Suleiman naye alimkosea Mungu kupitia kwa wanawake. Kuna mtu alikuwa anaitwa Hamani, mfalme aliamuru akatwe kichwa kwa sababu ya mwanamke.
Yusufu kama unamkumbuka, alikwenda jela kwa sababu mke wa mfalme alimsingizia uongo kwamba alitaka kumbaka.
Kifupi kazi zetu nyingi za kwenda kinyume na mapenzi ya Mungu wenu sisi huwa tunazipitishia kwa wanawake kwa vile wao ni viumbe dhaifu sana lakini wana nguvu ya ushawishi. Majambazi wengi wanakamatwa kwa sababu ya kutegewa wanawake.
Nataka kuuliza swali, tangu umekuja huku kutoka duniani unadhani una muda gani?
"Mh! Kama wiki moja," nilimwona yule kiumbe akicheka, nikashangaa anacheka nini wakati ni kweli.
Haiko hivyo huku kwetu. Tunaishi kama watawala wakuu wa kwenye nguvu za giza. Siku moja kwetu kama miaka miaka kumi na miaka kumi pia inaweza kuwa siku moja.
Tangu umekuja huku, kule duniani leo ni siku ya pili tena asubuhi kumekucha lakini jua halijaanza kutoka. Kwaheri tutaonana siku nyingine kwani nimepewa amri ya kukuacha.
Nilitaka kusema kitu lakini kufumba na kufumbua sikumwona yule kiumbe mbele ya macho yangu, nikajikuta nimesimama mbele ya kiumbe mwingine aliyekaa kwenye kiti cheupe, pembeni yake walisimama viumbe wengine wanne, wawili kila upande.
"Karibu ukae," yule kiumbe aliniambia. Alionekana yeye ni bosi wa wote kwani eneo alilokaa ni zuri, mahali pazuri, panavutia na hali yake pia.
"Wapi?" nilimuuliza.
"Si ukae."
Niligeuka kuangalia pa kukaa, nikaona kiti kingine kidogo lakini kizuri sana, cheupe, nikakaa kwa kujiachia.


Ili kujua zaidi usikose kusoma leo jioni.....
 
Back
Top Bottom