Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,286
- 10,831
Hayo ni maneno ya mwanangu, akitaka ninunue gari kali, means hajaridhika na nilililonalo. Matokeo ya kidato cha pili yametoka na amefaulu kidogo nikaona nimtembeze mjini kuangalia vitu mbali mbali.
Mtoto wangu akataka tuende Mlimani City, kama mnavyojua jana pale Mlimani kulikuwa na watu wazito wana sherehe. Basi nikazurura nae madukani, tulivyotoka nikasema twende upande wa sherehe (tupite karibu na ukumbi kwenda kwenye lile duka lingine la wachina kula upande wa pili). Basi nikapita na mwanangu pale, nje kulikuwa na askari kibao wakiona gari halihusiki wanakuelekeza kupita kwa haraka. Nikawaza kunanini hapa? Maana ukumbi ulipambwa hadi nje.
Mwanangu akaona magari makali yamepaki nje, akaniambia "enhee kama hili". Nikasema sawa mwanangu tutanunua. Oya yeyote aliyefanya sherehe jana pale Mlimani City hall ni tajiri haswa maana nje pale waliweka Fountains za kutosha kwa sample. Halafu ukumbi mzima ulininginizwa taa kwa nje. Wale walinzi as if ni mkutano wa kitaifa. Gari ya bei rahisi zilizopaki nje pale ni la milioni 100 nadhani.
Anyway, nimekuwa inspired na mimi kuwa na maisha ya vile, na nitafika kwa dua za mwanangu maana amesema anaendelea kupiga dua ili mashavu yafunguke nimiliki gari kali na ghorofa. Nikasema Amen!
Mtoto wangu akataka tuende Mlimani City, kama mnavyojua jana pale Mlimani kulikuwa na watu wazito wana sherehe. Basi nikazurura nae madukani, tulivyotoka nikasema twende upande wa sherehe (tupite karibu na ukumbi kwenda kwenye lile duka lingine la wachina kula upande wa pili). Basi nikapita na mwanangu pale, nje kulikuwa na askari kibao wakiona gari halihusiki wanakuelekeza kupita kwa haraka. Nikawaza kunanini hapa? Maana ukumbi ulipambwa hadi nje.
Mwanangu akaona magari makali yamepaki nje, akaniambia "enhee kama hili". Nikasema sawa mwanangu tutanunua. Oya yeyote aliyefanya sherehe jana pale Mlimani City hall ni tajiri haswa maana nje pale waliweka Fountains za kutosha kwa sample. Halafu ukumbi mzima ulininginizwa taa kwa nje. Wale walinzi as if ni mkutano wa kitaifa. Gari ya bei rahisi zilizopaki nje pale ni la milioni 100 nadhani.
Anyway, nimekuwa inspired na mimi kuwa na maisha ya vile, na nitafika kwa dua za mwanangu maana amesema anaendelea kupiga dua ili mashavu yafunguke nimiliki gari kali na ghorofa. Nikasema Amen!