Pagan Amum
JF-Expert Member
- Aug 28, 2015
- 1,930
- 4,409
Pamoja na mambo mengine kilichopelekea maboss wa NSSF kutenguliwa jana ni upendeleo katika ajira. Leo gazeti la Jamhuri limeonyesha jinsi Bunge linavyofanya upendeleo katika kutoa ajira.
Jana Bandari na BOT pia zililalamikiwa na taasisi ya SSRC, najua yatakuwa ni maamuzi magumu ila kwa manufaa ya taifa na kwa manufaa ya watoto wa masikini ambao hawana Godfathers katoka hizo taasisi ni sharti Rais pamoja na wizara ya utumishi itengue nafasi zote katika hizo taasisi ili ajira zitangazwe upya.
Najua kuna taratibu za kisheria ila katika hatua hii ya mpito kufata sheria sio muhimu sana la msingi ni kuhakikisha wananchi wote wanapata fursa na katika hili vijana wote watoto wa masikini na matajiri wapate fursa sawa.
Kama nchi tuko katika kipindi cha mpito. Tunamshukuru Mungu kutupa Rais Magufuli ambaye anafanya vyema sana. Tunamuomba katika hili la ajira aliangalie pia, kwenye taasisi za umma ajira zinatolewa kwa upendeleo kama njugu.
Jana Bandari na BOT pia zililalamikiwa na taasisi ya SSRC, najua yatakuwa ni maamuzi magumu ila kwa manufaa ya taifa na kwa manufaa ya watoto wa masikini ambao hawana Godfathers katoka hizo taasisi ni sharti Rais pamoja na wizara ya utumishi itengue nafasi zote katika hizo taasisi ili ajira zitangazwe upya.
Najua kuna taratibu za kisheria ila katika hatua hii ya mpito kufata sheria sio muhimu sana la msingi ni kuhakikisha wananchi wote wanapata fursa na katika hili vijana wote watoto wa masikini na matajiri wapate fursa sawa.
Kama nchi tuko katika kipindi cha mpito. Tunamshukuru Mungu kutupa Rais Magufuli ambaye anafanya vyema sana. Tunamuomba katika hili la ajira aliangalie pia, kwenye taasisi za umma ajira zinatolewa kwa upendeleo kama njugu.