Bila NRNE na hivyo bila Lissu kuwa mbele ya Pilato tungeonana wapi, ana kwa ana na kina Polepole au Gwajima?
Hatimaye leo imefika, ile siku ya ahadi, na ahadi iliyopo ni kumwagwa kwa mboga, baada ya ugali kutangulizwa!
Kumbe basi, nani atakereka na labda kusikia waliko wenzetu kina Ben, Azory, Mdude, Kipanya, Soka na wengine wote? Mungu mkubwa wakarejeshwa makwao salama? Ni mkata switch au nani? Labda yeye kama ndiye ibilisi mwenyewe!
Nani atakereka kusikia kama kuna rasilimali zetu fulani kwamba labda kuna genge linalozifuja kwa maslahi yake binafsi?
Nani atakereka labda kusikia kama kuna Futungo mahali, tukawaweka panapo wastahili?
Au kuwa ni nani atakareka labda kusikia kama kunachofanyika mahali kitu fulani kinyume cha maslahi ya taifa hili? Hapa sasa si ndipo palipokuwa pa kupiga kambi kwa kila mpambana na maovu ili kupata pa kuanzia?
Huku hatimaye si ndiko kungekuwa kufufuka kwa zile zama pendwa za: "tuambie, yuko wapi, kajificha wapi na anafanya nini kuhujumu uchumi," zilizohakikisha uwepo wa fursa sawa kwa wote?
Ashukuriwe bwana wa majeshi, ama kwa hakika NRNE ni mpango wa Mungu!
Hatimaye leo imefika, ile siku ya ahadi, na ahadi iliyopo ni kumwagwa kwa mboga, baada ya ugali kutangulizwa!
Kumbe basi, nani atakereka na labda kusikia waliko wenzetu kina Ben, Azory, Mdude, Kipanya, Soka na wengine wote? Mungu mkubwa wakarejeshwa makwao salama? Ni mkata switch au nani? Labda yeye kama ndiye ibilisi mwenyewe!
Nani atakereka kusikia kama kuna rasilimali zetu fulani kwamba labda kuna genge linalozifuja kwa maslahi yake binafsi?
Nani atakereka labda kusikia kama kuna Futungo mahali, tukawaweka panapo wastahili?
Au kuwa ni nani atakareka labda kusikia kama kunachofanyika mahali kitu fulani kinyume cha maslahi ya taifa hili? Hapa sasa si ndipo palipokuwa pa kupiga kambi kwa kila mpambana na maovu ili kupata pa kuanzia?
Huku hatimaye si ndiko kungekuwa kufufuka kwa zile zama pendwa za: "tuambie, yuko wapi, kajificha wapi na anafanya nini kuhujumu uchumi," zilizohakikisha uwepo wa fursa sawa kwa wote?
Ashukuriwe bwana wa majeshi, ama kwa hakika NRNE ni mpango wa Mungu!