lkn mbona hata wabunge wetu wanatakiwa wana sifa hizo. lkn soma kitabu ch mwembechai killingi
Kila ikijitokeza hoja ya inayohusu 'maslahi' ya waislamu, watu watakutaka ukasome Mwembechai Killings. Hawatakwambia kwamba kitabu hiki ni marufuku Tanzania na kwanini kilipigwa marufuku. Kwa kifupi, yaliyomo kwenye kitabu hiki hayana tofauti na ya Al nur, radio heri n.k. Mwembechai killings imejaa uchochezi, ambao kimsingi sio suluhu ya matatizo yanayowakabili waislamu.
Ushauri kwa ndugu waislamu:
Wakatoliki wanamiliki ardhi kubwa ukilinganisha na taasisi nyingi za kidini. Ishu hapa sio walipataje, muhimu ni kwamba hata nyie mkitaka mtapata. Tanzania hatuna shida ya ardhi kwa sasa, nunueni ardhi sasa-maana haitakuwepo milele kwa bei chee kama sasa. Nunueni ardhi ya kutosha kwa ajili ya kuwekeza ktk huduma za kiroho na kijamii (elimu, afya, n.k).
Wakatoliki wamewekeza sana kwenye huduma za jamii(recently, wamefungua chuo kikuu kishiriki Mtwara-ambako obviously wanawaumini wao wachache kuliko sehemu zingine. Huko kuna waislamu wengi). Nanyi pia mnaweza mkaongeza uwekezaji ktk eneo hili. Mna watu wanaoweza kuchangia pesa nyingi tu kwa ajili ya kuanzisha hospitali na vyuo vikuu vya hadhi ya kimataifa. Kwanini bilionea kama Bakhresa, Manji, Merey Balhabou n.k wasitumike kuchangia? Kinachohitajika ni central administration tu (sio BAKWATA-ambao inaonekana wameshindwa), je hili la kujiorganize kwa ajili ya maendeleo nalo ni gumu? Kuwekeza kwenye elimu ndio kila kitu ktk dunia ya sasa-waChina wanajua!
Prof. Njozi (aliyeandika Mwembechai Killings) amefanya nini kipya pale Muslim University Moro? Ameshafungua chuo kikuu kishiriki sehemu nyingine yeyote? Amekiimarisha chuo cha Morogoro au ndo ameridhika kwa kuzawadiwa cheo baada ya kuandika Mwembechai Killings? Kosa linalofanyika ni kutumia muda mwingi kusimuliana chakula cha jana, badala ya kujiuliza utakula nini kesho. Tunayo mifano ya kujifunza; kuna Rwanda ya Kagame-hata ukianza from scratch, unaweza kufanikiwa, kuna Botswana, kuna Wayahudi (nn wamefanya baada ya Hitler). Je waafrika tuendelee kulalamika kwa ajili ya biashara ya utumwa na ukoloni leo hii au tudhibiti mafisadi kama kina Chenge?