NMB yalaumiwa kutoa siri ya Lipumba

NMB yalaumiwa kutoa siri ya Lipumba

Tuna safari ndefu sana wa Tz kufikia Au kupata wana mabadiliko wa kweli na siyo wachumia tumbo eehe mungu tuonyeshe wote wenge kututakia mabaya
 
Kwani CUF haikuwa Na Akaunti mpaka afungue nyingine? Wakaulaumiwa sio NMB Bali in Lipumba Kwa kufungua Akaunti kama wale wa Bukoba waliofungua Akaunti ya Maafa
 
SIRI kwamba Profesa Ibrahim Lipumba amefungua akaunti mpya yenye jina la chama cha Wananchi CUF imefichuka. Wanaolaumiwa kutokana na kufichuka kwa siri hiyo ni watumishi wa benki ya NMB tawi la Ilala.

Prof. Lipumba ni Mwenyekiti wa CUF, anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama Vya Siasa huku chama chake kikiwa tayari kimemfukuza uanachama.

Abdul Kambaya, Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano ya Umma anayetambulika na Msajili wa Vyama Vya Siasa pia huku Baraza Kuu la Uongozi la CUF likiwa limemsimamisha uanachama, amenukuliwa na gazeti la Tanzania Daima, akilaani kitendo cha benki ya NMB kuvujisha taarifa za akaunti mpya ya Prof. Lipumba.

“Aulizwe Meneja wa NMB Ilala, kutoa siri za wateja, hayo ndiyo maadili ya kazi yake? Uko wapi usiri kati ya mteja na benki?” alihoji Kambaya.

Hata hivyo, MwanaHALISI online ilipomtafuta Kambaya siku ya jana ili kufafanua uanzishwaji wa akaunti hiyo, matumizi yake na kama yamezingatia matakwa ya Katiba ya CUF na Sheria ya Vyama Vya Siasa, hakuwa tayari kufafanua akidai kuwa si wakati muafaka.

“Tutaeleza mambo hayo kwa wakati muafaka, kama kuna jambo tunakuwa accused (tunatuhumiwa), iulizeni ofisi ya msajili au benki husika, wao wana taarifa kamili,” amesema.

Ofisi ya Msajili wa Vyama Vya Siasa kupitia Sisty Nyahoza imenukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari ikikiri kumtambulisha Prof. Lipumba kwa benki ya NMB ili aweze kufungua akaunti hiyo, hata hivyo amedai kuwa ofisi ya msajili haijui matumizi ya akaunti hiyo.

Taarifa za kufunguliwa kwa akaunti mpya yenye jina la CUF kwa malengo yasiyojulikana zilianza kusambaa katika mitandao ya kijamii Alhamis ya tarehe 06 Septemba mwaka huu.

Uongozi wa CUF taifa kupitia kwa Mbarara Maharagande, Naibu Mkurugezi wa Uenezi na Mawasiliano ya Umma umesema kuwa, utatoa taarifa rasmi juu ya suala hilo siku ya kesho Jumatatu, tarehe 10 Oktoba.
Bila kusema hilo wange tumbuliwa km wale wa Mwanza kwamba wamesaidia kutenda uhalifu nani asiye jua CUF kuna mgogoro wa kijinga sana ambapo mtu ambaye hatunzi kauli zake anawasumbua na sasa tunapata jibu kumbe ndege karudi tunduni coz ya Ruzuku
 
Kwani CUF haikuwa Na Akaunti mpaka afungue nyingine? Wakaulaumiwa sio NMB Bali in Lipumba Kwa kufungua Akaunti kama wale wa Bukoba waliofungua Akaunti ya Maafa
hapa ishu sio kulaumu...ni kufikishwa mahakamani
 
Hapo hamna lawama wala dhambi.
Mhona yule mwalimu Ester wa Mbeya day aliyerusha video ya wanafunzi wa field wamkimpiga mwanafunzi wa kidato cha 3 hajalaumiwa?
Hamna lawama kwenye kufichua uovu
 
"...Katika nchi masikini mijadala mingi ya kisiasa ni kuhusiana na migogoro na ubadhilifu wa viongozi wa vyama nasio sera wala mipango. Hii ni sawa na kukumbatia umaskini kwa nguvu zote..."

Bill Clinton 1998
 
Kufungua akaunti mpya kwa ajili ya ruzuku wakati huu wa mgogoro yaweza kuwa njia ya kufanya matumizi mabaya ya pesa za chama.
Msajili anatakiwa kutumia busara hapa. Kama anaona Lipumba ana haki basi asubiri mgogoro umalizwe kisheria, hata kama itabidi kushikilia ruzuku kwa muda.
 
sasa mbna wale wa kule walificha siri ya mteja wao wakatumbuliwa? ina maana usir ni one way direction enhee
 
Hapo hamna lawama wala dhambi.
Mhona yule mwalimu Ester wa Mbeya day aliyerusha video ya wanafunzi wa field wamkimpiga mwanafunzi wa kidato cha 3 hajalaumiwa?
Hamna lawama kwenye kufichua uovu
Huyo mwalimu ukiwa unamgegeda unahakikisha unaficha simu zake zote, hakawii kuyafanya aliyoyafanya Mbeya day
 
Sasa kama hiyo Account ni halali wanailaumu vipi nmb kwani kufungua account ya bank ni siri?
 
Back
Top Bottom