Sasa kwa nini wasiwakamate kama wamewaona wameingia nchini na wanawajua!? Au wanasubiri wafanye matukio ndio wawakamate!?
Ni kweli wizi umetokea, inasemekana ni vijana wadogo tu walikuwa na bunduki pamoja na vitu vinavyodhaniwa ni mabomu ambapo mashuhuda wanasema vilikuwa mithili ya simu za mkononi ambavyo walikuwa wakirusha wakati wanaondoka.
Jamaa hao walikuwa na Toyota Land Cruiser ya Kijani na walitoroka kuelekea njia ya Tandika. Kweli wamechota mihela maana inasemekana walikuwa na begi
"Rack Sack" kubwa tu lililokuwa limejaa mihela. Mhanga mmoja alisalimisha fedha zake TZS 2,000,000 alizokuwa akimtumia Baba Yake.
Majeruhi ni wengi, na inasemekana Askari Polisi wawili walipigwa risasi kabla jamaa hawajaingia ndani.
Polisi walifika eneo la tukio kama baada ya dakika kumi na tano.
Kweli ilikuwa kama action movie.
kazi ya simu za mkononi ni nini? nyingi zina kamera hamna watu wanaoweza kuchukua picha au video ya tukio??? tatizo wabongo simu ni sms,kubeep na zaidi ya mawasiliano......
heko kwa vijana kujiajiri
Kwenye matukio yanayohusisha silaha, polisi kwa makusudi husubiri wezi watokomee kwanza ili kukwepa confrontations, hasa nyakati za usiku.
Nasikia NMB headquarters hakuna camera hata moja (Nje na ndani). Temeke je?
Hizi benki kusogezwa karibu na wananchi inatakiwa na ulinzi pia kuongezwa. Ni risk kuweka benki Mbagala au Temeke
jamani hakuna mwenye taarifa kamili ya nini kimetokea na mauaji au watu gani wamejeruhiwa, ni wateja au wafanya kazi?
Hizi benki kusogezwa karibu na wananchi inatakiwa na ulinzi pia kuongezwa. Ni risk kuweka benki Mbagala au Temeke
dah! haya bana uhuru wa maoni unatumika ipasavyoMambo haya yataendelea sana kutokea kadri hali ya uchumi inavyozidi kuzama.Ajira hakuna ,Walinzi yaani polisi wamekata tamaa,wananchi wana hasira na serikali yao,Kwani haijakidhi matarajio yao.Maisha bora kwa kila Mtanzania.Sasa majambazi wameamua kujitwalia maisha bora mkononi.Nani alaumiwe????
Are you trying to stress the point kwamba huku majuu,majambazi never make a clean gateaway-you need to do your homework againHiyo Dar inahitaji Three 'D' satellite camare system. Inawezekana kwani itaonyesha mpaka njia hata kama wanaenda Moro hata kama wameingia shimoni. Huna haja ya kufukuzana nao.
Cha kufanya ni kukimbilia camera room na kuanza kutress ndiyo system inayo maliza uhalifu huku majuu.