Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,796
- 11,959
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI
JESHI LA POLISI TANZANIA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KUKAMATWA KWA WATU 32 KWA TUHUMA ZA MABILIONI YA BENKI YA NMB JIJINI DSM.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam linawashikilia watu 32 kwa tuhuma za wizi wa fedha kiasi cha Tsh Tsh Bil 2.082.00WIZARA YA MAMBO YA NDANI
JESHI LA POLISI TANZANIA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KUKAMATWA KWA WATU 32 KWA TUHUMA ZA MABILIONI YA BENKI YA NMB JIJINI DSM.
Mnamo tarehe 08/06/2020 majira ya saa tisa mchana huko katika Benki ya NMB tawi la Mbezi
Beach wafanyakazi watano wa kampuni ya ulinzi ya SECURITY GROUP OF AFRICA @ SGASecurity Tanzania Limited wakiwa na gari namba T 853 DPX MITSUBISH CANTER walikabidhiwa kiasi cha fedha Tsh Tsh 2 /= kwa maelekezo ya kuzisafirisha kutoka NMB tawi la Mbezi Beach ili wazipeleke tawi la NMB Benki House - CASH CENTRE iliyopo maeneo ya Posta Mpya.
Mara baada ya kukabidhiwa fedha hizo wafanyakazi hao badala ya kuzipeleka walipoelekezwa, walitoweka na fedha hizo.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum DSM siku hiyo ya tarehe 08/06/2020 majira ya saa 12 jioni lilibaini kutelekezwa kwa gari hilo maeneo ya Mbagala rangi tatu jirani na Shule ya SAINT MARY.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum kupitia kikosi kazi chake cha kupambana na ujambazi lilianza ufuatiliaji mara moja ikiwa ni pamoja na kufika eneo lilipoonekana gari hilo na kubaini kuwa wafanyakazi hao watano wamekula njama na kuiba kiasi cha fedha Tsh kutoka kwenye sanduku moja la chuma kati ya masanduku manne waliyokabidhiwa.
Aidha, masanduku matatu yaliyokutwa katika gari hilo yalifunguliwa na kukutwa na kiasi cha fedha Tsh 1,302,000,000 /= pia katika gari hilo zilikutwa silaha mbili aina ya Short gun Pump Action yenye risasi 12 na Short gun Protector yenye risasi 05, pamoja na sare za kampuni hiyo.
Watuhumiwa hao walikamatwa Mkoa wa Mbeya na Kigoma wakiwa wamenunua vitu vifuatavyo:-
(i).Trckta Power Tiller aina ya TRA-Change Model 7C/15 lenye thamani ya Tsh 20,000,000/=
(ii),Pikipiki moja aina ya SANLG
(iii).TV flat screen moja aina SUNDA na vitu mbalimbali vya matumizi ya ndani kama kitanda, godoro,jiko la gesi,rnakochi n.k
Mpaka sasa katika shauri hili Jumla ya Tsh 1,497,680,000/= zimeokolewa, mbali na thamani ya vitu vilixyonunuliwa kutoka sehemu ya fedha zilizoibiwa.
Jumla ya "'atillnuniwa 32 wamekamatwa na kuendelea kuhojiwa juu ya ushiriki wao kuhusiana na tukio hili
Aidha Jeshi la Polisi linaendelea na msako mkali ili kuwakamata watuhumiwa wote waliohusika na tukio hili.
ONYO KUHUSU MAANDAMANO YANAYOHAMASISHWA KUPITIA MITANDAO YA KIJAMII
Jeshi la Polisi kanda Maalum Dar es salaam linatoa onyo kali kwa kikundi au mtu yeyote atakayeshiriki maandamano hayo batili tarehe 07/07/2020 kwa madai ya kudai Tume huru ya uchaguzi waaache mara moja vinginevyo watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.
LAZARO B. MAMBOSASA- SACP KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM DAR ES SALAM.
06/07/2020