Lihakanga
JF-Expert Member
- Dec 17, 2016
- 4,829
- 6,376
Nimepata taarifa za uhakika kutoka kijiji cha Lugarawa, wilaya ya Ludewa mkoani Njombe, kuwa kuna wakala wa NMB mmoja maarufu kwa jina la Deo, amewaibia wateja wake kupitia biashara yake ya uwakala huo.
Story iko hivi, mteja akifika kutoa fedha benki, anaingiza kadi kwenye mashine kisha anamwambia mteja wake kuwa mtandao umesumbua. Atamtaka mteja arudie tena.
Kinachotokea hapo ni kutoa kiasi kilekile cha fedha kama alivyoomba mteja, halafu mteja anakabidhiwa fedha ya muamala mmoja tu.
Kwa mfano, mteja ameomba kutoa sh. 3m, basi itatolewa 3m kisha atarudia 3m, kisha mteja anakabidhiwa 3m tu.
Tukio hilo lilimpata mteja mmoja ambaye baada ya kufuatilia alitulizwa ili wayamalize. Mteja huyo anafuatilia arejeshewe jumla ya sh9m alizoibiwa kwa awamu tatu. Ufuatiliaji huo uliwafumbua macho wateja wengine na kuwafanya wafuatilie mwenendo wa akaunti zao na baadhi yao kugundua kuwa wameibiwa pia.
NMB chukueni hatua kuwaondoa mawakala kama hawa kwa kuwa si tu wanawaibia wateja, bali pia wanapoteza image nzuri ya taasisi yenu.
Story iko hivi, mteja akifika kutoa fedha benki, anaingiza kadi kwenye mashine kisha anamwambia mteja wake kuwa mtandao umesumbua. Atamtaka mteja arudie tena.
Kinachotokea hapo ni kutoa kiasi kilekile cha fedha kama alivyoomba mteja, halafu mteja anakabidhiwa fedha ya muamala mmoja tu.
Kwa mfano, mteja ameomba kutoa sh. 3m, basi itatolewa 3m kisha atarudia 3m, kisha mteja anakabidhiwa 3m tu.
Tukio hilo lilimpata mteja mmoja ambaye baada ya kufuatilia alitulizwa ili wayamalize. Mteja huyo anafuatilia arejeshewe jumla ya sh9m alizoibiwa kwa awamu tatu. Ufuatiliaji huo uliwafumbua macho wateja wengine na kuwafanya wafuatilie mwenendo wa akaunti zao na baadhi yao kugundua kuwa wameibiwa pia.
NMB chukueni hatua kuwaondoa mawakala kama hawa kwa kuwa si tu wanawaibia wateja, bali pia wanapoteza image nzuri ya taasisi yenu.