Apologise lady
JF-Expert Member
- Sep 16, 2013
- 5,980
- 3,115
Ni hivi jirani yangu aliibiwa simu siku ya jumapili, wakati anafanya shughuli zake aliingia ndani akaacha sim nje kwa kuwa ni sehemu ambayo haina wizi wizi hakuwa na shaka, kuja kutoka nje kakuta sim ishapitiwa, ikatafutwa haikupatikana, mama yule akaondoka taratibu hadi kwa mganga siku hiyohiyo.
Yakafanyika yakufanyika mganga akamwambia rudi nyumbani ndani ya siku 7 utapata simu yako, mama yule akarudi kimya kama kaisahau simu yake, jambo la ajabu leo hii asubuhi mme wake anaamka kujiandaa kwenda kazini anakuta simu mlangoni, ndio kuita watu kwa furaha.
Sasa naomba mniunganishie dot, kuna connection gani ilifanyika kati ya mganga na mwizi hadi simu ikarudi? Bado nina mshangao wa ajabu, mara zote naamini waganga ni waongo na hutumia mchezo wa kisaikolojia zaidi kumwahadaa mtu.
Yakafanyika yakufanyika mganga akamwambia rudi nyumbani ndani ya siku 7 utapata simu yako, mama yule akarudi kimya kama kaisahau simu yake, jambo la ajabu leo hii asubuhi mme wake anaamka kujiandaa kwenda kazini anakuta simu mlangoni, ndio kuita watu kwa furaha.
Sasa naomba mniunganishie dot, kuna connection gani ilifanyika kati ya mganga na mwizi hadi simu ikarudi? Bado nina mshangao wa ajabu, mara zote naamini waganga ni waongo na hutumia mchezo wa kisaikolojia zaidi kumwahadaa mtu.