Njombe: 50% ya Wanakijiji wa Utiriri wadaiwa kuwa Walevi

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
Asilimia 50 ya wakazi 1,200 wa kijiji cha Utiriri kilichopo kata ya Lupanga wilaya ya Ludewa mkoani Njombe wamedaiwa kuwa ni walevi hali ambayo inasababisha watoto wao kukosa lishe bora.

Afisa lishe halmashauri ya wilaya ya Ludewa John Kiusa ametoa taarifa hiyo kwenye kampeni ya lishe wilayani humo ambapo amesema kiwango cha udumavu kwa asilimia 46.2 katika wilaya hiyo na kushika nafasi ya pili kimkoa kunachagizwa na ulevi wa wazazi wengi katika maeneo mbalimbali wakiwemo wa kijiji cha Utiriri.

Mkuu wa mkoa wa Njombe,Anthony Mtaka amesema kutokana na jambo hilo ni lazima afike kwenye vijiji vyote vyenye walevi na kuzungumza nao ili kuwanusuru watoto na udumavu huku mganga mkuu wa mkoa huo Dkt. Juma Mfanga akionya tabia ya ulevi kwani inasababisha watoto wengi kukosa lishe bora.

20240126_213739.jpg
 
Mwaka jana nilikua na ziara njombe loh!!! kuanzia Havanga, ibiki, ibumila mpaka igongolo njia nzima unanuka ulanzi yani vitindi vimepangana kama behewa za treni, hawezi pona mtu
 
Asilimia 50 ya wakazi 1,200 wa kijiji cha Utiriri kilichopo kata ya Lupanga wilaya ya Ludewa mkoani Njombe wamedaiwa kuwa ni walevi hali ambayo inasababisha watoto wao kukosa lishe bora.

Afisa lishe halmashauri ya wilaya ya Ludewa John Kiusa ametoa taarifa hiyo kwenye kampeni ya lishe wilayani humo ambapo amesema kiwango cha udumavu kwa asilimia 46.2 katika wilaya hiyo na kushika nafasi ya pili kimkoa kunachagizwa na ulevi wa wazazi wengi katika maeneo mbalimbali wakiwemo wa kijiji cha Utiriri.

Mkuu wa mkoa wa Njombe,Anthony Mtaka amesema kutokana na jambo hilo ni lazima afike kwenye vijiji vyote vyenye walevi na kuzungumza nao ili kuwanusuru watoto na udumavu huku mganga mkuu wa mkoa huo Dkt. Juma Mfanga akionya tabia ya ulevi kwani inasababisha watoto wengi kukosa lishe bora.

View attachment 2883871
Actually,
ni sawa na Moscow tu kule Russia viwango vya baridi na Utitiri kule njombe vinalandanda sana na kwahivyo wananchi walio wengi hutumia pombe kali kupasha na kuupa mwili joto vinginevyo ni maumivu makali sana ya baridi...
 
mwaka jana nilikua na ziara njombe loh!!! kuanzia Havanga,ibiki,ibumila mpaka igongolo njia nzima unanuka ulanzi yani vitindi vimepangana kama behewa za treni,hawez pona mtu
Ni Mavanga sio Havanga.
 
Back
Top Bottom